Mad Max
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 26,961
- 77,890
Wanasemaga "niende na maini mazima mbinguni ya nini?"baada mafigo,na maini yakianza kufa mje kusifia tena
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wanasemaga "niende na maini mazima mbinguni ya nini?"baada mafigo,na maini yakianza kufa mje kusifia tena
Kwenye mafunzo ya udereva.kuna somo linaitwa MADHARA YA POMBE.ukifundishwa utaogopa hata kugusa chupa ya pombe.Wanasemaga "niende na maini mazima mbinguni ya nini?"
Suala " nikumwagilia moyo kiafya " unakula kitimoto kilo mbili na nusu!! Kwanza ukimaliza unaingia kumwagilia moyo taratibu ,sio unakunywa Kama kunajamaa kakununulia .Hapana mkuu ivi kweli mtu ambaye nashika zaidi ya million na nusu kwa mwezi unaamin kweli nitakuwa nashindia zakienyeji..sisemi kwamba sijawahi kunywa za kienyeji hapana NImewahi Ila sio Sana kbs kupitiliza..na hata navyokwambia sijiskii kula sio zamani ni juzi juzi Tena niliamua kuitoa cash laki Tisa baada ya kuona tozo nyingi kuchomoa Chomoa kila siku...nikajiuliza hv Mimi nimjinga namna hii yaani pesa zote nashindwa kula vzr mpk naumwa kwa sababu ya sumu hizi.NIMEPUMZIKA BWANA YESU ANIPONYE
Kifupi ni kwamba, kwa sisi watumiaji wa vilevi vya aina mbalimbali huwa inakuwa ni sehemu ya kustarehesha ubongo na pia kupeana mawili matatu katika changamoto za kila siku.
Kumwagilia moyo kunaendana na muziki huku ukiwa unatikisa mwili na vyombo ndio vinashuka.
Tujuane wazee wakumwagilia moyo
Sawa kaka nimekuelewa.Sio kwamba hakuna misosi mingine isipokuwa tatizo NI kichefuchefu btw Niko mikoa ya pwani samaki wapo wengi tu hamu ya kula ndo Nilikuwa sipati just imagine nakuwekea picha ya screenshot ya bank statement kwa miezi mitatu ya nyuma NImeshika zaidi ya millioni sita kweli uniambie nikose hela ya kula vizuri??ishu kubwa mi pombe zilikuwa nyingi mpaka ubwabwa kuku nikila kile kijiko cha kwanza nakuwa Kama nataka kutapika labda option Nilikuwa nayo ilikuwa NI kula na maji yaani naweka chakula mdomoni nasukumia na maji...pombe NI mateso dada yangu wengi tu hawasemi wanavumilia hasa wanywaji kupita kiasi...thanks God Nina siku mbili sijaona leo nimekula kamchemsho Cha samaki japo mdogo mdogo View attachment 2346904View attachment 2346914
Sawa kaka nimekuelewa.
Pole kwa yaliyokukuta. Mimi nipo tofauti...pombe itanifanya nile nitake nisitake...na bahati nzuri sichagui chakula....naweza nikanywa sana na nikala wali kitu ambacho wengi hawawezi.
Ikitokea nimeshindwa kula ni ile imetokea mara moja moja nimelewa kupitiliza napata kichefuchrefu na hali hurudi kawaida baada ya siku moja au mbili.
Huyo ni mlevi😀Wewe haunywi kila siku huyo ni mnywaji wa kila siku
Unywaji wa kila siku sio mzuri tena kila siku unamaliza konyagi sio poa
naomba detail kidogoKwenye mafunzo ya udereva.kuna somo linaitwa MADHARA YA POMBE.ukifundishwa utaogopa hata kugusa chupa ya pombe.
Ina madhara ya Figo,moyo,maini. Nakusababisha presha na kisukariItnaomba detail kidogo
Hatukatai ,mimi nilipata shida mwaka 2014 aisee pombe za kunywa kila siku sio nzuri nilikunywa kwa miezi 11 bila kupumzika ni mwendo wa gambe asubuhi lazima na mchana na jioni kama dawa. nashukuru sana niliamua kujikana nikaona hapa nitakufaa..
saizi sheria yangu ni moja tu kula nashiba na lala kidogo naamka nakunywa maji ndo naenda kunywa na nikirudi kulala ni msosi tena na maji ya uvuguvugu basi nikiamka asubuhi kiroho safi.
kwanza kuna muonekano wa kuchakaa na kuonekana cha pombe (hii ni kama sio mtu wa mazoezi na chakula kwa wingi)- kupoteza umakini (hii watu wanaweza kubisha ila ndo ukweli yani hata kama unafanya kazi ofisini/kazi/biashara kama una kunywa makali huo ndo ukweli
- Hangover ya 5G
Pole ndugu.Mkuu kunywa ila pombe sio nzuri zimenipa matatizo ya kiafya sitayasema hapa coz sijapimwa Bado ila..nahisi ninayo.
Achilia mbali kutoheshimika na jamii