AAMIIN.HARUFU umenikumbusha mbali sheikh Wangu.
Mwenye EZ Mungu akuzidishie Elmu Na Akuruzuku Hekma ili utufundishe Na sisi.
Kwa kweli nalifurahia Hilo darsa la dadaFaiza foxy Na wachangiaji wote.
AAMIIN.
Labda kwa kukazia nikazie kwa hivi,
QAALA RASUULULLAHI SWALLA LLAHU A'LAYHI WASALLAM:-
Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (Amani iwe juu yake).
IDHAA MAA TAA IBNU AADAMA INQATWA'A AMALUHU ILLAA MIN THALAATH,
Pindi Akifa/Anapokufa Mwanaadam, Amali zake zote zinapotea isipokuwa mambo matatu.
Ambayo,
1. SWADAQATUN JAARIYA.
2.AW ILMUN YAN TAFIUBIH.
3.AW WALADUN SWAALIHUN YAD'ULAH.
Nikiwa na maana,
1.SADAKA inayoendelea/ya kuendelea. Yaani kiuchache ni kama vile, Kumfundisha Mtu Swallah/Sala, Kumfundisha Mtu QUR'AAN, Kumuelekeza Mtu kutoa ZAKA. Haya machache niliyoyataja nikisema niyachambue, DARSA lake ni kubwa mno na ni refu mno, nimejatihidi kutaja kiufupi ili nieleweke.
2.ILMU yenye kunufaisha/Manufaa. Kivipi? ILMU ambayo imewawezesha Watu. Na hapa napo DARSA lake ni kubwa pia, najitahidi kufupisha.
3.Au Mtoto Mwema ambae anakuombea DUA. Kivipi? Nikiwa na maana, Mtoto mwenye kujua/kuijua DINI.
Yule Mtoto ambae atakuwa Mwema, atakuwa anamuombea/anawaombea DUA Mzazi wake/Wazazi wake.
Hapa napo pana DARSA lake ila najitahidi kufupisha.
Kiufupi Sheikh wangu mgogoone, lengo langu hapa ni kukumbusha na kutiliana mkazo kwenye ILMU, ikiwemo Vizazi vyetu. Kumbuka Mimi na Wewe tusipokuwepo hapa Ulimwenguni, Watoto wetu, wao ndio watakaotukumbuka Sisi (Watakaotuombea SISI) Muhimu tuwaandalie mazingira mema na bora ya ILMU.
Kwa mfano hai wa hapa Bibie FAIZA, ILMU anayoitoa anajiwekea Akiba mbeleni, kwa watakaoifanyia kazi itawasaidia, na hapo kipengele namba Mbili, kipengele cha Pili kinamuhusu Bibie FAIZA, ambacho kinasema:-
AW ILMUN YAN TAFIUBIH
Mama unawatambuaje WAHHAB ni waislam halisi na itikadi zao Zinamashiko kwenye dini.? Hata kwa dondoo fupi .
Jazakallah kheyraAAMIIN.
Labda kwa kukazia nikazie kwa hivi,
QAALA RASUULULLAHI SWALLA LLAHU A'LAYHI WASALLAM:-
Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (Amani iwe juu yake).
IDHAA MAA TAA IBNU AADAMA INQATWA'A AMALUHU ILLAA MIN THALAATH,
Pindi Akifa/Anapokufa Mwanaadam, Amali zake zote zinapotea isipokuwa mambo matatu.
Ambayo,
1. SWADAQATUN JAARIYA.
2.AW ILMUN YAN TAFIUBIH.
3.AW WALADUN SWAALIHUN YAD'ULAH.
Nikiwa na maana,
1.SADAKA inayoendelea/ya kuendelea. Yaani kiuchache ni kama vile, Kumfundisha Mtu Swallah/Sala, Kumfundisha Mtu QUR'AAN, Kumuelekeza Mtu kutoa ZAKA. Haya machache niliyoyataja nikisema niyachambue, DARSA lake ni kubwa mno na ni refu mno, nimejatihidi kutaja kiufupi ili nieleweke.
2.ILMU yenye kunufaisha/Manufaa. Kivipi? ILMU ambayo imewawezesha Watu. Na hapa napo DARSA lake ni kubwa pia, najitahidi kufupisha.
3.Au Mtoto Mwema ambae anakuombea DUA. Kivipi? Nikiwa na maana, Mtoto mwenye kujua/kuijua DINI.
Yule Mtoto ambae atakuwa Mwema, atakuwa anamuombea/anawaombea DUA Mzazi wake/Wazazi wake.
Hapa napo pana DARSA lake ila najitahidi kufupisha.
Kiufupi Sheikh wangu mgogoone, lengo langu hapa ni kukumbusha na kutiliana mkazo kwenye ILMU, ikiwemo Vizazi vyetu. Kumbuka Mimi na Wewe tusipokuwepo hapa Ulimwenguni, Watoto wetu, wao ndio watakaotukumbuka Sisi (Watakaotuombea SISI) Muhimu tuwaandalie mazingira mema na bora ya ILMU.
Kwa mfano hai wa hapa Bibie FAIZA, ILMU anayoitoa anajiwekea Akiba mbeleni, kwa watakaoifanyia kazi itawasaidia, na hapo kipengele namba Mbili, kipengele cha Pili kinamuhusu Bibie FAIZA, ambacho kinasema:-
AW ILMUN YAN TAFIUBIH
Ahsante sana Sheikh wangu.Akhsante sheikh HARUFU Kwa darsa Na Kwa kuongezea kuhusu sadak ya Tabasamu maana hiyo NI sadak ambayo unatoa nabado unayo.
Kila la kheri
Tatizo lako unataka ujibiwe unavyotaka wewe na si kwa mujibu wa swali lako. Mungu ana mipango yake na taratibu zake za utekelezaji malengo yake, na hayakufuatisha unavyotaka wewe, bali wewe ndo ufuate anavyotaka yeye. Alipotaka wanadamu wote walione jua kwa wakati alioupanga, amefanya hivyo, huku jua linawaka na huku wengine wako gizani, angelitaka watu wote wapate jua kwa wakati mmoja pia angeweza, lakini hakutaka hivyo. Kwenye imani ya kiroho, pia angetaka watu wote wapate ujumbe mmoja kwa wakati mmoja (kama unavyotaka wewe), pia angeweza, lakini hakutaka hivyo unavyotaka wewe (wewe sio muumba na wala si muweza) amefanya vile anavyotaka yeye (kwakuwa yeye ni muumba na muweza wa kila jambo) Ametuma Wajumbe wake kuleta ujumbe wake katika zama tofauti, tofauti ya karne nyingi tu, na wala hakuwalazimisha wajumbe wake kuzunguka dunia nzima na kuonana na kila nwanadamu (kama unavyotaka wewe) bali alitaka ujumbe wake uendelee kusambaa hata baada ya wajumbe wake hao kuondoka duniani, na hivyo ndivyo ilivyo sasa, ujumbe unaendelea kusambaa na utaendelea kusambaa hadi siku ya kiyama ndipo utakapokoma kusambaa, hivyo ndivyo alivyotaka. Kuhusu wale walioishi hadi kufa bila kupata ujumbe, imeelezwa katika maandiko nini itakuwa hatima yao, na walikuwepo hata wakati wa uhai wa Wajumbe hao, wengine waliweza hata kukutana nao, lakini kwa sababu mbalimbali hawakuweza kupata ujumbe huo (viziwi, vichaa, uzee wa kiwango cha kupoteza ufahamu nk) hukumu yao anaijua mwenyewe, maandiko yanabainisha hali hii, lakini kwakuwa huyaamini maandiko, pamoja na kubainishiwa, basi haina maana yoyote kuhangaika na "...wana masikio lakini hawasikii, wana macho lakini hawaoni (na wala hawataona), ...wamekuwa kama wamefungwa makongwa ya shingoni, shingo zao haziwezi kugeuka kulia wala kushoto!"
Habar zenu wakubwa, mm ni mgeni humu naomba mnifahamishe how to creat and posting thread. Najua kua hapa sio mahali pake nisaidieGeneral Knowledge.
Naam, kama kichwa cha habari kinavyojieleza.
Natumia fursa hii ya mtandao adhyim wa JF kuwapa fursa wanamtandao wote wapate fursa ya kuuliza kuhusu mada au jambo lolote ambalo unataka upatiwe majibu.
Si majibu yote yatatoka kwangu binafsi, bali nitajitahidi iwezekenavyo kukupatia majibu murwa na yanayolingana na swali lako na ambapo sina jibu itakuwa fursa kwa wengine kutoa majibu.
Hapa ni kwa ajili ya kuelimishana na kujuzana bila kikomo, iwe swali lolote liwalo.
Update 1:
Tafadhalini tuulize maswali kiheshima . Heshima ni kitu cha bure na hii JF yetu pendwa inasomwa na wengi, tujiheshimu.
Update 2:
Siku kadhaa zimepita toka tuanzishe uzi huu na nimesikitishwa na aina ya maswali yanayoulizwa kwenye huu uzi.
Tumetowa fursa ya kuulizana na kila niwezapo kujibu au kutafuta majibu muafaka kutokana na hayo maswali na fursa ya wachangiaji kujibu maswali yatakayojitokeza ya "general knowledge" lakini hadi hii leo ni maswali machache sana yenye faida kwa wengi yameulizwa. Maswali yaliyojaa ni amma ya kutaka kuanzisha ubishi "ligi" na amma yamelenga mtu binafsi, hususan amelengwa mleta mada. Ni masikitiko makubwa sana.
Nnawashauri wote waliouliza maswali yenye kulenga binafsi na wale waliouliza maswali yenye kubomoa badala ya kujenga wabadilike na waanze kuuliza maswali yenye kujenga, kuelimisha, kutujaza hekima na maarifa.
Nilipoweka aina ya elimu niliyoisomea nilidhani ntakumbana na kibano kikali kuhusu hilo na nijibu ili iwe faida kwa wengi lakini kwa bahati mbaya au nzuri hakuna hata mmoja aliyeuliza swali lolote kuhusu hilo.
Isitoshe, mna fursa ya kuuliza kuhusu chochote. Ndege, mimea, dunia, sayari, nyota, maajabu, maswali yasiyokuwa na majibu, viumbe kwa ujumla vinavyojulikana na visivyojulikana, maajabu ya duniani, elimu na vitu vingi kama hivyo na vinginevyo.
Nnauhakika wale walioleta maswali ya kiajabu ajabu ya ubishi wana mengi sana ya kuuliza yanayoweza kuwapa faida wengi na kuna wengi kati yao wana mengi wanayajuwa na wanaweza kuchangia kwenye majibu kwa faida ya wengi.
Ombi langu kwa wote ni tuboreshe aina ya maswali na majibu.
Karibuni.
Kuna tofauti kati ya kujibu/kuwajibu na kujaza.kwa hiyo wewe kwenye form za kiofisi ambazo wanauliza date of birth unawajibugi hivi ulivyojibu hapa?
Unajuaje kama anakuangalia?Kuna demu hakiniona anapenda kuniangalia
Sababu wewe ni bwana mchungaji.Napataje mtoto wa kiume
[emoji120] [emoji120] [emoji120]Naam, nimerudi kama nilivyokuahidi, nnaona hujazileta hizo aya kama nilivyokutaka lakini si kitu.
Aya ya za 2:191-193 ukitaka uzipate kwa "context" yake anzia aya ya 2:190 - 195, soma:
190. Na piganeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanao kupigeni, wala msianze uadui. Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi waanzao uadui. Maelezo
Na maelezo yake ni haya:
190. Na katika kumcha Mwenyezi Mungu ni kustahamili mashaka katika kumt'ii Yeye, na mashaka makubwa kabisa juu ya nafsi ni kuwapiga vita maadui wa Mwenyezi Mungu. Lakini wakikuvamieni, basi piganeni na hao wavamizi. Na mmepewa ruhusa kuurudi uvamizi wao, lakini nyinyi msivamie kwa kuanza nyinyi, au kwa kumuuwa asiye kupigeni vita wala hana mahusiano na vita; kwani Mwenyezi Mungu hawapendi wavamizi.
191. Na wauweni popote mwakutapo, na muwatoe popote walipo kutoeni; kwani fitina ni mbaya zaidi kuliko kuuwa. Wala msipigane nao kwenye Msikiti Mtakatifu mpaka wakupigeni huko. Wakikupigeni huko basi nanyi pia wapigeni. Na hivi ndivyo yalivyo malipo ya makafiri.Maelezo
Maelezo yake:
191. Wauweni walio kuanzeni vita popote mnapowakuta, na watoeni Makka, wat'ani wenu ambao wamekulazimisheni kuutoka. Wala msione vibaya, kwani walio kufanyieni nyinyi ni maovu zaidi kuliko kuuwa msikitini, nako ni kuwafitini Waumini katika Dini yao kwa kuwaadhibu huko Makka mpaka wakauacha mji wao kuhifadhi Dini yao. Na huu Msikiti Mtakatifu una utakatifu wake, basi msiuvunje kwa kupigana ndani yake. Lakini wakikupigeni vita ndani yake basi nanyi pia wauweni, na nyinyi kwa fadhila ya Mwenyezi Mungu, mtashinda. Na malipo ya makafiri ni kufanyiwa wanayo wafanyia watu.
192. Lakini wakiacha basi Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu. Maelezo
Maelezo yake:
192. Wakirejea wakaacha ukafiri, wakafuata Uislamu basi Uislamu humuitikia anaye uelekea. Na Mwenyezi Mungu atawasamehe ule ukafiri wao wa zamani kwa fadhila yake na rehema yake.
193. Na piganeni nao mpaka pasiwepo fitina, na Dini iwe ya Mwenyezi Mungu tu. Na kama wakiacha basi usiweko uadui ila kwa wenye kudhulumu. Maelezo
193. Wapigeni vita walio taka kukuuweni na kukugeuzeni muache Dini yenu kwa maudhi na mateso mpaka ing'oke mizizi ya fitina na isafike Dini iwe ya Mwenyezi Mungu tu. Wakiuacha ukafiri wao basi wamejiokoa nafsi zao na wataepukana na adhabu. Hapo basi haifai kuwafanyia uadui. Uadui hufanyiwa mwenye kuidhulumu nafsi yake akaiteketeza kwa maasi na akaacha uadilifu kwa maneno na vitendo.
194. Mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu. Na vitu vitakatifu vimeekewa kisasi. Anaye kushambulieni nanyi mshambulieni, kwa kadiri alivyo kushambulieni. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu yu pamoja na wachamngu. Maelezo
194. Na pindi wakikushambulieni katika mwezi mtukufu msiache kupigana nao, kwani huo ni mtukufu kwao kama ulivyo kuwa mtukufu kwenu. Ikiwa wao watauvunja utukufu wake basi nanyi wakabilini kwa kuzilinda nafsi zenu katika huo mwezi. Na katika mambo matukufu na matakatifu pana sharia ya kisasi na kutendeana mfano kwa mfano. Anaye kushambulieni katika matakatifu yenu nanyi jilindeni na uadui huo kwa mfano wake. Na mcheni Mwenyezi Mungu, msikiuke mipaka katika kulipiza kisasi. Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwanusuru wachamngu.
195. Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala msijitie kwa mikono yenu katika maangamizo. Na fanyeni wema. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema. Maelezo
195. Kupambana na makafiri kunahitaji kutoa roho kama ilivyo kutoa mali. Basi toeni kwa kuandaa vita, na jueni kuwa kupigana na hawa ni kupigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Basi msikae tu. Toeni mali kwa ajili yake, kwani mkitofanya na mkafanya ubakhili adui atakupandeni na atakudhilini. Hapo itakuwa kama mlio jitokomeza wenyewe kwenye maangamio. Tendeni lilio kuwajibikieni kwa uzuri na vilivyo, kwani Mwenyezi Mungu hupenda anapo fanya jambo mtu alifanye vizuri.
Aya 190 mpaka 195 zinaeleza sharia ya vita katika Uislamu. Nazo zinaeleza kwa matamshi yalio wazi haya yafuatayo:
*1. Ruhusa ya kupigana imetolewa kwa ajili ya kujilinda na uvamizi wa vita wa vitendo khasa, au zikidhihiri dalili kuwa maadui wanataka vita. Vita havikulazimishwa kwa ajili ya vita wala kwa sababu ya kutaka kuwasilimisha watu kwa kuwauwa na kuwapiga vita.
*2. Kunakatazwa kuvamia au kuanza uadui kwa njia yoyote ile. Basi hapana ruhusa kufanyiwa uadui asiye pigana, wala hapana ruhusa kuvuka mipaka ya uadui wakati wa vita: basi hauliwi asiye chukua silaha, wala hakhusiani na vita bali ni mwenye kukumbwa tu na vita. Wala hauliwi mwenye kusalimu amri na akatupa silaha. Wala hapana ruhusa kuwavunjia watu nyumba zao, huko ni kupita mpaka.
*3. Mzingatie fadhila iliyo onyeshwa kwa kuamrishwa kuchamngu. Basi msivunje heshima ya wanawake kuwanajisi, hata washirikina wakifanya hayo. Wala msiwakatekate walio uwawa hata ikiwa makafiri wakiwafanyia hayo Waumini. Washirikina walimfanyia hayo Bwana wa Mashahidi, Hamza, wala Mtume s.a.w. hakutoa ruhusa kumfanyia hayo maiti yeyote, bali alikataza akasema:"Tahadharini msiwakatekate maiti".
*4. Vita vinakwisha wakiacha washirikina kuwafitini Waumini katika Dini yao, na Dini inakuwa inataka akili na nyoyo zimwelekee Mwenyezi Mungu kwa uhuru.
*5. Hapana vita katika mwezi mtukufu, nayo ni miezi ya Hija na Umra. Ikiwa washirikina watapigana katika miezi hiyo, basi Waumini nao yawapasa wapigane.
*6. Kuacha kutoka kwenda pigana na maadui wanauwa pasina nasi kupigana nao ni kuipoteza kheri na wema. Kwa haya inadhihiri kuwa vita vya Islamu vina fadhila katika sababu zinazo pelekea kuanza kwake, na vina uadilifu katika kuviendesha. Viwapi hivi na vita vya mataifa mengine ya zamani na ya sasa! Vita vyao hao ni vya uchafu, na vita vya Islamu ni vya Haki na vyenye fadhila.
semper saratoga
Nnaona mpaka hapo utagunduwa kuwa ulipozitowa hizo aya zilikuwa si kwa "context" yake.
Jee, kuna tatizo katika hayo mafundisho mema kabisa?