Fainali ipi ya 'UEFA Champions League' ilikuvutia kwa miaka 10 iliyopita?

Man city bingwa

Man city vs chelsea ..

ilikuwa bonge la final aisee
 
Uliingalia fainali ya man utd na chelsea???

Bonge moja la fainali 50/50 ilee
 
Hivi ndo kusema mtiti wa 2011/12 Bayern Munich Vs Chelsea mmeusahau? Au ni hasira zenu na chuki tu dhidi ya Chelsea?[emoji12]

Ngoma imeenda hadi 120 kwa header la kiroho mbaya lililotandikwa na mmatumbi, Robben ananoa penalti ndani ya extra time, watu wanahema vya hatari, game inaisha kwa mbinde la matuta, wanaume wamepambana hadi mwisho ndo bingwa anapatikana!

Mnatuletea habari za game ambazo mtu anakufa 4-1! Fainali unapigwa mabao manne? Imekuwa rede? Fainali tamu mchezee kwenye 1-0, 2-1, 3-2 mwisho, zaidi ya hapo ni NBA.

Mada yenyewe inasema within 10yrs, mnafosi kwenda hadi 1990's huko ili tu msiisifu hii burudani[emoji16]

Semeni kiliumana!!!!
 
Binafsi fainali timu ikifungwa zaidi ya goli mbili naona sio fainali nzuri
 
Barcelona walikuwa katika ubora wa aina yake!

Sir Alex miaka kadhaa baadae alihojiwa kuhusu Fainali ile akasema alirudia kutazama zaidi ya mara mbili fainali ile akagundua Man Utd hamna sehemu walikosea ila walikutana na timu bora sana!
Hapa Fergie aliamua kulinda heshima yake.
 
UEFA 2018/2019 ilikuwa bora sana kwangu. Kuingiza timu zote za premier league
fainali kimiujiza ujiza kwangu ndo iliishia pale. Kwenye fainali nikasema liwalo na liwe na sikutegemea kuona maajabu yoyote.
 
Hakuna fainali iliyoboa watu kama ile ya Liverpool vs Spurs
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…