wazee husema ujana maji ya moto
na wataalamu wanasema,ukitaka kuishi vizuri,
yatazame maisha yako kuanzia mwishoni kuja mwanzoni...
weka picha siku unayokufa,nini umeacha,nani atakulilia?
halafu rudi taratiibu mpaka leo ulipo
...na ulichotanguliza pia,...maana tuendako giza! Tunasikia tu kuna moto...!
Anyway, nahisi sie wabantu tulio wengi hasa huku kusini mwa jangwa la sahara
tunaulemavu wa kutokuwa na upeo wa kuona mbali na kujipangia maisha yetu.
Kabla hamjaanza kunitwanga 'mawe,' ...jiulize umeupangilia vipi muda wako kuanzia leo mpaka
Ijumaa ijayo? ...au ndio mmemuachia Mungu? LOL!
mkuu hatukupigi mawe
but siri nyingine ya maisha ya furaha ni kutoyapaanga saana
acha nature pia ifuate mkondo
ndo maana watu wasio na elimu na kipato cha chini huwa na furaha zaidi
kuliko matajiri na maprofesa....
kumbuka tulivyokuwa watoto,
kitu kama pilau kinakupa furaha ya wiki nzima lol
...lol, no wonder sisi kama taifa tunakaribia miaka 50 baada ya uhuru na matatizo yanatuzidi. Umeme tabu, maji safi tabu, magonjwa, umasikini, ujinga, njaa, ufisadi, mismanagement ya viwanda na mashirika ya umma, mmomonyoko wa maadili, yaani kila kitu tabu, tabu, tabu...
Kama umri, taifa limepoteza dira. Taifa bila watu ni pori tu au kisiwa. Kama wenyewe hatuna discipline ya kujipangia maisha, lawama za nini kwa hao wanaoendesha serikali? Tatizo sugu hili, tatizo la taifa, aka "ujinga wa mwafrika"..
Kujiandaa ni muhimu ili usijeaibika baadae.
Ila ukweli ni kwamba waAfrika wengi bado tunaamini kwamba jukumu la kumlea MTOTO ni la WAZAZI na jukumu la kulea WAZAZI kipindi cha uzee ni la WATOTO.
Hamna ubaya wowote wenye kujiwekea akiba....ila tujaribu na sisi tusije tukaishia kuwa kama hawa ndugu zetu ambao wanawakimbia wazee wao kipindi ambacho wanawahitaji zaidi maishani mwao.Kama hawakukupeleka wewe kwenye nyumba ya watoto wakati huishi usumbufu usichukulie uzee wao kama usumbufu kwao.
Mi naona tulifunge tu hili sredi kwakuwa halina kuchakachua wala maofu topiki..........Hii inaashiria watu wanaogopa sana uzee.
Kwangu mimi uzee ni kama nchi ya "kusadikika"..... Uzee ni maandalizi ya kufa, ni kulipigia kaburi hodi. Of which kila mtu lazima mauti yamkute. Mie hapa naamini katika "hapa na karibu na hapa" zaidi kuliko "mbali kule". Maadam sijampigia Mungu simu anihakikishie ntakufa lini, nimedhamiria kujitosheleza kwa sasa zaidi badala ya kufikiria kusikokuwa na uhakika.
Leo mwanangu anakula nini na kesho kuna cha kumpa?
Leo mke wangu ntampa nini ntamfurahisha na nini na kesho je itakuwaje?
Leo naishi wapi navaa nini najitoshelezaje, na je kesho napo itakuwaje
Sasa biashara ya keshokutwa mtondo na mtondogoo inategemea kesho imekuwaje siyo? Kama kesho itakuwa poa, eventually mipango ya mtondo na mtondogoo itaendelea kutaradidi..... Ila sasa kama hata hiyo kesho hakieleweki itakuwaje uanze kupanga ya mtondogoo? Si waweza kufa kesho?
Ndo maana nlimuuliza mbu uzee anaozungumzia hapa ni umri gani hasa?
Kwa mtu mwenye miaka 20 atahisi uzee ni miaka 50. Na wa miaka hamsini anaona uzee ni miaka 70 huko..... Sijui kama naeleweka lakini kwangu mie kwa kijana wa miaka 22 kuanza kupanga mikakati ya namna atakayoishi baada ya miaka 65+(2) ni kutojitendea haki na kujizeesha kabla ya muda.... Wa miaka 22 anapaswa kufikiria maisha yatakuwaje atakapotimiza lets say 40. Ntakuwa nimeoa? na watoto? Ntawamudu? Ntakuwa na kagari kangu? je ka kiwanja au kakibanda?
Tuacheni sisi wenye miaka 60 tuwaze namna tutakavyoishi tukifikisha 70+...Hatuna cha kupoteza tena na muda ndo ushatamalaki....
Ushauri wa babu ODM ni huu:
Vijana wadogo fikirieni na kuwaza maisha yenu yatakavyokuwa mtakapofikisha umri wa makamo..... say 41+
Watu wa makamo fikirieni mlipokosea kwa kuyakosa yale mliyoyawaza kuwa mgekuwa nayo katika umri huu.... Bado hamjachelewa....pambaneni.... Maisha haya ya 41+ ndo kioo cha hali halisi utakayokuwa nayo utakapoingia kwenye uzee (60+)
Ukishaingia kwenye umri wetu huu ...60+ ndo muda sasa wa kuyafurahia/kusononeka kwa kuyafikia/kushindwa kuyafikia yale malengo ambayo ulipaswa kuyawazia na kuyafanyia kazi ukiwa na 41+.
Otherwise......karibuni kitandani huku, babu nimepumzika.
Samahani kwa ambao hawajanielewa, babu na ungwini wapi na wapi bana?
Uzee ni noma sana, na hasa kama hukukumbuka kujiwekea hazina yako....wako wengi tunawaona wanaadhirika mtaania tu, wamebaki kulalamikia watoto wao oooo mmetutupa, hamtutunzi, sababu walisahau kujiwekea akiba uzeeni, thanx mbu umefanya jambo la busara kutukumbushia hili
Jamani muacheni Mungu aitwe Mungu. kwa akili zetu sisi hatuwezi lolote!
Wifi ungefafanua kidogo hapa ingeleta utamu!!
Kaka hajambo?
.... Sijui kama naeleweka lakini kwangu mie kwa kijana wa miaka 22 kuanza kupanga mikakati ya namna atakayoishi baada ya miaka 65+(2) ni kutojitendea haki na kujizeesha kabla ya muda.... Wa miaka 22 anapaswa kufikiria maisha yatakuwaje atakapotimiza lets say 40. Ntakuwa nimeoa? na watoto? Ntawamudu? Ntakuwa na kagari kangu? je ka kiwanja au kakibanda?
Tuacheni sisi wenye miaka 60 tuwaze namna tutakavyoishi tukifikisha 70+...Hatuna cha kupoteza tena na muda ndo ushatamalaki....
Ushauri wa babu ODM ni huu:
Vijana wadogo fikirieni na kuwaza maisha yenu yatakavyokuwa mtakapofikisha umri wa makamo..... say 41+
Watu wa makamo fikirieni mlipokosea kwa kuyakosa yale mliyoyawaza kuwa mgekuwa nayo katika umri huu.... Bado hamjachelewa....pambaneni.... Maisha haya ya 41+ ndo kioo cha hali halisi utakayokuwa nayo utakapoingia kwenye uzee (60+)
Ukishaingia kwenye umri wetu huu ...60+ ndo muda sasa wa kuyafurahia/kusononeka kwa kuyafikia/kushindwa kuyafikia yale malengo ambayo ulipaswa kuyawazia na kuyafanyia kazi ukiwa na 41+.
Otherwise......karibuni kitandani huku, babu nimepumzika.
Samahani kwa ambao hawajanielewa, babu na ungwini wapi na wapi bana?
...60+ ndo muda sasa wa kuyafurahia/kusononeka kwa kuyafikia/kushindwa kuyafikia yale malengo ambayo ulipaswa kuyawazia na kuyafanyia kazi ukiwa na 41+.
sote hatujambo kabisa mpendwa, tunamshukuru Mungu.
hoja yangu ni kwamba kufunga ndoa na mtu sio mwisho wa kujenga mahusiano. tuna kazi ya kuendelea kujenga mahusiano na watu wote wakiwemo wenzi wetu siku zote hata mwisho wa maisha yetu. unaweza kuchagua mke/mume ambaye wa maoni ya baadhi ataonekana si match wako lakini kadiri mnavyoishi, mnaweza kuzoeana taratibu na kufahamiana zaidi na hivyo hofu ya kukimbiwa uzeeni au kuwa mpweke kwa namna nyingine haina nguvu.
kwangu mimi, fainali ni LEO! iwe ujanani au uzeeni. uzeeni kuna maisha kama yalivyo ujanani ama utotoni. kuna vijana wengi wapweke kama ilivyo kwamba kuna wazee wengi vilevile wapweke. vilevile kuna hata watoto amabo ni wapweke pia. kwa hiyo, tusipomtegemea Mungu, kila siku tutakuwa tunajiandaa na maisha ambayo hatutakuja kuyafikia na ambayo Mungu kwa rehema zake tayari kishatuandalia na daima hutuwazia mambo mema na makubwa akitupa tumaini katika siku zetu za mwisho.
kwa majaliwa yetu wanadamu ni ngumu sana kufahamu kwa hakika yatakayotokea hata kesho tu, sembuse huko uzeeni? tunaweza kuwa makini kuchagua wenzi wa maisha, tukaridhika na assessment zetu za kibinadam tukiongozwa na macho na akili za nyama laini mwisho wake hatuwezi kuujua lolote na kwa kweli hatuwezi kitu!
nakubaliana na wanaosema akiba itakayotufaa uzeeni na huduma kwa watoto wetu ni muhmu ili kuwajengea uwezo wa kuyamudu maisha, lakini zaidi sana kumtumaini Mungu ndio muhimu zaidi kwani yeye ajua tunachohitaji hata kabla hatujaomba. kama tunataka kuziona siku njema za uzeeni, basi tuzuie ndimi zetu zisinene hila na mioyo yetu isitawaliwe na tamaa. huku tumkumiomba Mungu bila kukoma tukiamini kuwa sisi tu watumishi tu na kondoo wa malisho yake.
tukifaya hayo tutashukuru daima kwa kila jambo kwa maana yote (mazuri kwa mabaya, matamu kwa machungu nk) ni mapenzi ya Mungu na tukisimama kwa imani katika yote hata mwisho, ndipo tutakapopata kushinda na zaidi ya kushinda kwake yeye atutiaye nguvu na Mungu atajipatia utukufu
nawatakieni wote baaka za Bwana
Jina la Bwana libarikiwe