Fainali Uzeeni!....

Fainali Uzeeni!....

Duh sasa nyie mnaosema si rahisi kufikia 'uzee'? Mnataka kusema tukate tamaa?

MJ1,

Uzee (kwa kipimo cha serikali ya JMT) ni miaka 65 (+2) na kuendelea.. Nikitizama kwa undani hii jamii inayonizunguuka wale wenye miaka 60 ni wachache sana! Unaweza kufanya utafiti mwenyewe hapo mtaani kwako, kijijini kwako, wilayani kwako.. tafuta idadi ya wazee wenye miaka 67 na kuendelea na ukishapata idadi waweza kufanya ile tunaita partial conclusion - Kufikisha miaka umri wa miaka 65 kwa kizazi hiki ni vigumu sana!

Hii rate ya watu kwenda kutibiwa India imeongezeka sana - cancer, figo, sukari, pressure, AIDS, e.t.c

Sishawishi vijana waziwekeze kwa ajili ya uzee wao, ila ningependa wawekeze kwa ajili ya WATOTO na WAJUKUU wao - Uzee hatutaufikia - Mechi za siku hizi hazina fainali! - Refa anamaliza mchezo wakati Ligi inaendelea - strange!?
 
...baba enock, iwapo mzee wako alivusha 60yrs, nawe andaa safari. Hayo ya magonjwa, ajali nk ni matokeo tu, hakuna anayeombea.

Nikisema fainali uzeeni ni pamoja na afya yako, ndugu jamaa na marafiki, kazi uifanyayo, uwezo wa kusomesha na kuhudumia familia nk...it's a whole life package.
 
Mbu hii habari ya kufikiria uzee saa hizi...dau unaweza kuzeeeka kesho boira kula maisha tu..
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
lakini mkuu kuna wazee wengine ... uzeeni ndio mwanzo wao .. ona hii picha


262340_201803149866905_100001116631088_494850_5890824_n.jpg
attachment.php
 
Mbu hii habari ya kufikiria uzee saa hizi...dau unaweza kuzeeeka kesho boira kula maisha tu..

...kaizer, kuna DNA test kuonyesha mwili wako ushafikia umri gani. Nitakuja na more info later. Mtaani jamaa kibao wa umri wangu tayari wanaonekana wazee kuliko umri wao...sasa sijui tatizo ni matokeo ya miaka 50 tangu uhuru wa Tanganyika, au ni genes...

Mimi nishajiamulia liwalo na liwe, almuradi hawatapitisha ujenzi wa barabara kuu kati kati ya kibanda changu, am safe for the time being. Chumba cha pili napangisha, maisha yanaendelea.
 
lakini mkuu kuna wazee wengine ... uzeeni ndio mwanzo wao .. ona hii picha View attachment 33551
attachment.php

...lol, wewe mwenyewe umemuona kituko...

kuna umri ukifika, inabidi ui control akili na maamuzi yako badala kuachia akili iamue. Ndio utakuta akili inakwambia "kojoa!" nawe unaachia kwenye suruali mbele ya wajukuu!
 
kuna mtu kaniambia life expectancy yetu hairuhusu uzee niache uoga
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
...lol, wewe mwenyewe umemuona kituko...kuna umri ukifika, inabidi ui control akili na maamuzi yako badala kuachia akili iamue...ndio utakuta akili inakwambia "kojoa" nawe unaachia kwenye suruali mbele ya wajukuu!

Hahahaha wenyewe wajiita vijana wazamani (wengi wao utakuta bado fedha wanayo ) ... walikosa hekima wakati wa ujana wao basi waendeleza hadi uzeeni ...
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mh Mbu hii kwa kweli inatia huruma kwa jinsi wazee wetu wengi wanavyoishi! Nakumbuka kulikuwa na mkutano mmoja ulioandaliwa na HelpAge International ambao waliainisha kuwa katika wazee wote nchini ni asilimia 4 tu ya waliokuwa covered na hizo pension zao!

But najiuliza hii fainali uzeeni kwa mkulima wa kijijini!! Mbona tutakuwa tunamwonea? Tukumbuke hiyo asilimia 4 ni wale waliokuwa wanafanya kazi za kuajiriwa!! Ambao wanastahili pension!!

....4%?!!! SHOCKING STATISTICS!...


Asante Mbu, sasa hapa wazazi wetu ambao ni wakulima tuwasaidie je?

...LD na Mwj1, naomba niwajibu maswali yenu ya nyongeza kwamba...uzee hauchagui muajiriwa wa serikali, mkulima,
mvuvi au mfanyabiashara... uzee (kama kifo) hauna ubaguzi bana, iwe mwanamke, iwe mwanaume...umri ukifika utazeeka tu utake usitake.

Bahati nzuri/mbaya...life expectancy ya wazee wetu vijijini ninasemekana ni fupi kulikoni ya wazee wetu wa mijini. Sina uhakika na hili, maana wa mjini pamoja na huduma za afya, maji safi ya bomba, nk...bado kule vijijini utakutana na vizee vilivyokula chumvi nyingi...nadhani mazao asilia, ambayo hayajachakachuliwa kwenye supermarkets zinawasaidia sana.

Anyway, kuna msemo...mtaji wa masikini ni nguvu yake mwenyewe... wa vijijini kama hatakuwa na shamba, basi atakuwa na mifugo. Hiyo ni pensheni tosha kabisa. Kuna yale makabila through mfumo wao wa maisha ilibidi mume aoe wake wengi apate watoto wa kumtosha wamsaidie kilimo/ufugaji......---ndio pensheni yenyewe hiyo, japo miaka ya kisasa vijana hawachelewi kuwakimbia wazee wao kuja kuwa wamachinga mjini.

Sijui nimewajibu?


kuna mtu kaniambia life expectancy yetu hairuhusu uzee niache uoga

kaka, ...hapa naangalia Atlantis shuttle launch,....countdown ilikuwa tayari ishafikia 00:00:31 ikatokea delay....
wakasimamisha kwa dakika mbili tatu.,...sasa nawe jaribu ku delay siku yako kwa sekunde mbili tatu ukione cha moto...

Kila unaposherehekea siku ya kjuzaliwa, ujue ndio kibano kinakaribia...
Waswahili sie kwa kutafuta unafuu, wengi wetu insurance tunakata 3rd party, (fire and theft)
Ukija kwenye health insurance, house insurance, travel insurance nk kila mtu anazitolea nje... siku ya siku yakifika ya kufika utaona mtu kawa mkaaali!...Haya mambo bana sikiza mwenyewe roho yako inavyokwambia,..

...kuna wengine weshakata tamaa ya maisha...bahati mbaya watu wa aina hiyo (waliodata na mapema!) nao hawafi mapema! akijitundika ajinyonge, either tawi au kamba inakatika, ....akijitupa ghorofani anaishia kuvunja uti wa mgongo na paralysis, maisha yote kitandani (bed ridden)...kufa hafi cha moto anakiona!
 
...kaizer, kuna DNA test kuonyesha mwili wako ushafikia umri gani. Nitakuja na more info later. Mtaani jamaa kibao wa umri wangu tayari wanaonekana wazee kuliko umri wao...sasa sijui tatizo ni matokeo ya miaka 50 tangu uhuru wa Tanganyika, au ni genes...

Mimi nishajiamulia liwalo na liwe, almuradi hawatapitisha ujenzi wa barabara kuu kati kati ya kibanda changu, am safe for the time being. Chumba cha pili napangisha, maisha yanaendelea.

now thats what am talking about...
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Jamani kwa post chache nilizosoma ninaona kama watu wanatishwa na life expectancy lakini nadhani ni vema tukajiandaa tu hakuna ubaya tukiwaachia hata vizazi vyetu makazi mazuri!

Ni kweli wengi wetu siku hizi hatuchomoi magonjwa chungu mbovu so nadhani pamoja na kuwa lengo ni kuwa safe uzeeni nadhan ni vema tukaapply ile slogan ya Andaa Chako Mapema kwani huwezijua lini utaondoka.

Vijana wengi siku hizi naona wanaamka Mbu, ingawa kuamka kwao ni kwa mlengo nyuma, wengi wakipata kazi anakuwa na malengo ingawa malengo yenyewe mara nyingi si endelevu! Mtu anawAza kwanza gari zuri, kisha kujenga heshma bar.

Tuwaangalie wazee wetu ambao hawana watoto wa kuwatunza huku wakiwa wameachiwa wajukuu wawalee as a result of UKIMWI n.k
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mbu ni kweli nakubali kuwa uzee hauna ajira nakubali ila sasa ajira pia inamatter katika kukuwezesha kujiandaa na kuangalia unajiandaaandaaje!
Naangalia mkulima kijijini ambaye kipato chake ni cha tumbo na mahitaji ya lazima, haimruhusu kusave au kuwekeza for the future, yeye ni jembe, jembe ni yeye. The only matumaini ktk kuwekeza ni elimu duni kwa watoto wake (hii ni kilio kingine) sasa mtu kama huyu ambaye miaka yote amekuwa akitumika pasipo faida ya kujiandaa na uzee, fainali yake inakuwaje?

Na isitoshe katiba ya nchi inasema wazee wote wako entitled to be protected ambap tunaamini ingekuwa ahueni kwa hawa wa vijijini au wasiojiweza but bayo ni kilio kingine tu!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mada za Mbu ni kiboko ya akili!!Ilibidi niinakili kisha niwatumie watu wote walio karibu nami. Nimepokea majibu ya ajabu sana nilipouliza miwshowe: Je umejiandaa vipi kwa fainali uzeeni: Nilijibiwa:
  • Nimesomesha watoto kwa bei mbaya sana!
  • Nimewekeza kwenye stocks
  • Nimejenga na kusomesha
Hakuna hata mmoja aliyeonyesha kuwekeza kwenye mahusiano na mwenza wake au hata watoto.

Good one Mbu, good one.........

when i was getting married (over seven years ago) i wanted a woman who was attractive, smart, a mother to my kids, a lover, a friend, sweetheart.... you name it!! i never factored issue ya maisha yetu after 70 years

Most of us (i believe) marry for the happy moments we dream of and sometimes we forget this important life after 60's

I only started to think of such scenarios last year when i watched a certain movie... and to be honest, so far i am too deep on investing for the kids and quality time

Kids are always a very good energy when couples get old

Inabidi kwa kweli tuwekeze sana kwenye MAHUSIANO NA WAUME/WAKE ZETU na hata watoto, au hata wale tulio nao karibu kimaisha.Usipofanya hivi utajikuta uko mpweke sana. Wazungu ambao wana nyumba za kutunzia wazee wanao msemo kabisa " be nice to your children because they are the ones to choose your old people's home"!!Ukiwa mtu mbaya kwao, watakuchagulia mahali pabaya sana na utakuwa huna usemi.Watakuwa hawaji hata kukutembelea Christmas!! Kwa sisi huku nchi za dunia ya tatu, kama watoto wako ulikuwa unawalisha kauzu na ugali wakati wewe ukila kuku na mishkaki ukiteremshia na bia, ujue uzee wako utakuwa reverse ya hiyo.... maana unapozeeka unageuka mtoto na watoto wako wanageuka "walezi" wako! Ukitaka waje kukujali kwa matunzo bora, basi waonyeshe matunzo mazuri ni yepi kimalazi, chakula na mavazi maana utakuwa umewaonyesha kwa mfano!

Sasa nimejua kwa nini vibinti vidogo vinang'ang'ania vibabu

Vibabu Fidel vinakuwa havikuwekeza kwa wenzi wao, hivyo kwa vile vinakuwa havina company home, bas vinafurukuta huko je na kudakwa na "dakadaka".Usiombe uone kibabu kimeishiwa kinarudi home kufa!! Utaona huruma sana. Mara nyingi wakina mama hupata kampani ya watoto wao uzeeni kwa sababu wao walishikana na watoto enzi baba anakesha viti virefu!! Payback time chungu!

Inside Every Old Man there is a Young Man Wondering, What the Hell Happened....

But for those who were prepared materially and socially, they age gracefully with respect

Mambo ya mafao dah wanawake bana muwage na huruma jamani kababu kanataka kufaidi mafao nyie ndo mnakachuna mpaka ngozi

Fundisho ni kwamba jiandae ujanani usijeangukia "dakadaka" uzeeni.

Fidel sasa unataka Fainali waende na nani?? Lol!!!

Wataenda na wale vijana wa zamani wenzao.

...baba enock, iwapo mzee wako alivusha 60yrs, nawe andaa safari. Hayo ya magonjwa, ajali nk ni matokeo tu, hakuna anayeombea.

Nikisema
fainali uzeeni ni pamoja na afya yako, ndugu jamaa na marafiki, kazi uifanyayo, uwezo wa kusomesha na kuhudumia familia nk...it's a whole life package.

Hiyo ndio summary y akila kitu ndugu yangu!! Asante sana kwa mchango wako na kutukumbusha kuhusu quality life.
 
Mbu ni kweli nakubali kuwa uzee hauna ajira nakubali ila sasa ajira pia inamatter katika kukuwezesha kujiandaa na kuangalia unajiandaaandaaje!
Naangalia mkulima kijijini ambaye kipato chake ni cha tumbo na mahitaji ya lazima, haimruhusu kusave au kuwekeza for the future, yeye ni jembe, jembe ni yeye. The only matumaini ktk kuwekeza ni elimu duni kwa watoto wake (hii ni kilio kingine) sasa mtu kama huyu ambaye miaka yote amekuwa akitumika pasipo faida ya kujiandaa na uzee, fainali yake inakuwaje?

Na isitoshe katiba ya nchi inasema wazee wote wako entitled to be protected ambap tunaamini ingekuwa ahueni kwa hawa wa vijijini au wasiojiweza but bayo ni kilio kingine tu!

...hapana, hapana, hapana Mwj1 jamani, hapana, uuuuwwwwiiiiiiiiiii!......unless nimekusoma vibaya, lakini kuwekeza kwenye elimu ya mtoto/watoto (ili waje wakufae baadae) hiyo mimi siiafiki hata kidogo!...Ni wajibu wetu wazazi kuhakikisha mwanao unamsomesha na kumpatia kila aina ya msaada ili kumsaidia aweze naye huko mbele ya safari aje ajitegemee na apate na ahueni ya maisha yake, FULL STOP!

Kumsomesha mtoto ili iwe ni deni la kuja kukusaidia binafsi sikubaliani nalo kabisa jamani, hapa mpaka roho inaniuma nikifikiria eti nitakuja gombana na wanangu kisa hawataki kunisaidia. Hiyo ni hiari yao (kunisaidia),...kuwasomesha natimiza wajibu wangu kama mzazi. Wakiamua kutusaidia, nitashukuru Mungu, wakiamua kuuchuna, nitashukuru mungu..,.almuradi niliwapa msingi mzuri wa maisha, inatosha.

Jamani ee...Ole wenu mnaodhani eti kuwasomesha watoto wenu ndio investments za uzeeni hizo,...wao kuwasaidia uzeeni ni hiari, sio lazima.
Mwj1 wewe tutamalizana kwa wakati wetu, lol...!
 





elderly-couple.jpg


"When marrying, ask yourself this question: Do you believe that you will be able to converse well with this person into your old age?
Everything else in marriage is transitory."

anza sasa kujijengea mahusiano mazuri na mkeo uwe na mtu wa kujifariji nae miaka hiyo ya ukiwa, ....fainali uzeeni!

........Sasa Mbu tukitoka kule kwenye generals......nadhani hili ulilooanisha hapa ni la msingi kuliko kuwekeza kwenye majumba na mashamba na elimu za watoto....Mwenzi wako!! Unawekezaje kwa mwenzi wako kwa maisha ya pamoja uzeeni?........nafikiri tukiliwaza hili na kulitilia maanani hata maumivu ndani ya ndoa huwenda yajapungua...maana wajiandalia list ya vitu au matendo ya uwekezaji. Mie nawekeza kwa spouse wangu kipenzi ili hata tukizeeka basi atazeeka nami kwa furaha na memories njema nyingi zaidi ya zile mbaya......... !!

Mbu ninaomba msaada wa list ya vitu ambavyo one can use/do tu invest for uzee na mwenzi wake!!
Baba/Mama anapokuwa na nyumba ndogo/kidumu hadharani, huwa anakuwa na mawazo ya who's going to be with him/her uzeeni?
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mada za Mbu ni kiboko ya akili!!Ilibidi niinakili kisha niwatumie watu wote walio karibu nami. Nimepokea majibu ya ajabu sana nilipouliza miwshowe: Je umejiandaa vipi kwa fainali uzeeni: Nilijibiwa:
  • Nimesomesha watoto kwa bei mbaya sana!
  • Nimewekeza kwenye stocks
  • Nimejenga na kusomesha
Hakuna hata mmoja aliyeonyesha kuwekeza kwenye mahusiano na mwenza wake au hata watoto.

Inabidi kwa kweli tuwekeze sana kwenye MAHUSIANO NA WAUME/WAKE ZETU na hata watoto, au hata wale tulio nao karibu kimaisha.Usipofanya hivi utajikuta uko mpweke sana. Wazungu ambao wana nyumba za kutunzia wazee wanao msemo kabisa " be nice to your children because they are the ones to choose your old people's home"!!Ukiwa mtu mbaya kwao, watakuchagulia mahali pabaya sana na utakuwa huna usemi.Watakuwa hawaji hata kukutembelea Christmas!! Kwa sisi huku nchi za dunia ya tatu, kama watoto wako ulikuwa unawalisha kauzu na ugali wakati wewe ukila kuku na mishkaki ukiteremshia na bia, ujue uzee wako utakuwa reverse ya hiyo.... maana unapozeeka unageuka mtoto na watoto wako wanageuka "walezi" wako! Ukitaka waje kukujali kwa matunzo bora, basi waonyeshe matunzo mazuri ni yepi kimalazi, chakula na mavazi maana utakuwa umewaonyesha kwa mfano!

Vibabu Fidel vinakuwa havikuwekeza kwa wenzi wao, hivyo kwa vile vinakuwa havina company home, bas vinafurukuta huko je na kudakwa na "dakadaka".Usiombe uone kibabu kimeishiwa kinarudi home kufa!! Utaona huruma sana. Mara nyingi wakina mama hupata kampani ya watoto wao uzeeni kwa sababu wao walishikana na watoto enzi baba anakesha viti virefu!! Payback time chungu!

But for those who were prepared materially and socially, they age gracefully with respect

Fundisho ni kwamba jiandae ujanani usijeangukia "dakadaka" uzeeni.

Wataenda na wale vijana wa zamani wenzao.

Hiyo ndio summary y akila kitu ndugu yangu!! Asante sana kwa mchango wako na kutukumbusha kuhusu quality life.

...WoS, umezungumzia suala la maana sana sana sana mydear...ni ukweli usiopingika katika post zote humu ndani, ni MTM pekee aliyegusia suala la ndoa na maisha ya uzeeni,...very strange!....

Tatizo ni nini? wachangiaji walilifumbia macho hili;
elderly-couple.jpg

"When marrying, ask yourself this question: Do you believe that you will be able to converse well with this person into your old age?
Everything else in marriage is transitory."
...anza sasa kujijengea mahusiano mazuri na mkeo uwe na mtu wa kujifariji nae miaka hiyo ya ukiwa, ....fainali uzeeni!

...au huu ni uthibitisho mwingine ndoa za miaka hii kila mtu akili kichwani mwake?...
watu wanaishi kwa kuviziana?....ama kuna haja kubwa ku invest mapenzi kwa mke/mume jamani...
Ni Mke/Mume pekee atayekustiri uzeeni!
 
...hapana, hapana, hapana Mwj1 jamani, hapana, uuuuwwwwiiiiiiiiiii!......unless nimekusoma vibaya, lakini kuwekeza kwenye elimu ya mtoto/watoto (ili waje wakufae baadae) hiyo mimi siiafiki hata kidogo!...Ni wajibu wetu wazazi kuhakikisha mwanao unamsomesha na kumpatia kila aina ya msaada ili kumsaidia aweze naye huko mbele ya safari aje ajitegemee na apate na ahueni ya maisha yake, FULL STOP!

Kumsomesha mtoto ili iwe ni deni la kuja kukusaidia binafsi sikubaliani nalo kabisa jamani, hapa mpaka roho inaniuma nikifikiria eti nitakuja gombana na wanangu kisa hawataki kunisaidia. Hiyo ni hiari yao (kunisaidia),...kuwasomesha natimiza wajibu wangu kama mzazi. Wakiamua kutusaidia, nitashukuru Mungu, wakiamua kuuchuna, nitashukuru mungu..,.almuradi niliwapa msingi mzuri wa maisha, inatosha.

Jamani ee...Ole wenu mnaodhani eti kuwasomesha watoto wenu ndio investments za uzeeni hizo,...wao kuwasaidia uzeeni ni hiari, sio lazima.
Mwj1 wewe tutamalizana kwa wakati wetu, lol...!

Hata hujakosea kunisoma mydia....amini usiamini mawazo ya wazee wetu walio wengi ni hayo..namsomesha mtoto aje anitunze uzeeni......... mimi nilishawahiambiwa nimekusomesha na sasa ni jukumu lako kunitunza na kusomesha wadogo zako' na huyo si mzazi ambaye hajenda shule! Nakubali wapo walel ambao dhana ya kusomesha kwa faida ya uzeeni ishatoka but kwa waliowengi bado ipo na ndio kilio kikuu kwa wale ambao wamesomesha na bahati mbaya watoto wakafariki either kwa maradhi au lah......wengi wanalia mwanangu ameondoka hata matunda yake sijayafaidi!!

Ni wachache wenye kuamini kumsomesha mtoto kwa faida ya mtoto mwenyewe.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Back
Top Bottom