Faisal aliweza kulipa mil.110 za kuvunja mkataba, anakosaje mil.50?

Faisal aliweza kulipa mil.110 za kuvunja mkataba, anakosaje mil.50?

Kwa Sasa ata Feitoto akienda CAS mpaka shauri lake lipangiwe ma jaji, lianze kusikilizwa, wahusika waletewe ujumbe Ili Kwa maandishi, uwakilishi, au wahusika wafike kwenye usikilizwaji wa shauri,
Haitapungua miezi mitatu.

Najua hii ya kuchangiashana mitandaoni ni kutafuta huruma tu kwakua aliye nyuma ya hili ni mtu mwenye fedha ndugu Yusufu Bakresa.
Baada ya muda upo uwezekano mkubwa wa kumpatia iyo fedha.

Baada ya kusikilizwa ilo shauri Kuna muda wa kusubiri hukumu nao haupungui wiki mbili mpaka mwezi kwakua alisikilizwi swala la Feisal pekeyake, uwa yanafika mpaka mashauri kumi tofauti Kwa wakati mmoja.
Mpaka swala lake liishe itakua mwakani na itategemea uharaka wa kulipeleka CAS na kama ameshinda au ameshindwa.

Kama angekwenda Yanga upo uwezekano mkubwa swala lake lingeisha ndani ya wiki Moja.
Kupanga ni kuchagua, kiburi Cha Fei kinaletwa na Yusufu Bakresa.
Hapo Yanga ameshaenda, wamegoma kuvunja mkataba, wanataka fei abakie wamuongezee mkataba na kuboresha maslai, kitu ambacho fei hakitaki, mnataka aende wapi? Kama si CAS
 
Eti wadau mi sielewi sijui Faisal anatuchukuliaje wenzake. Km aliweza kulipa zaida ya mil 100 ili avunje mkataba wake sasa anakosaje mil.50? Hii taarifa ni changanya bwege.Wale wale waliompa ile mil.110 ndo hao hao wanaenda kumlipia CAS. Hii ya kuomba kuchangiwa ni kichaka cha kuonekana Watanzania tumemchangia ila mzigo wote tayari anao. Sisi tuliosoma Cuba tushaelewa.
Huenda hata hizo mil 100 alichangiwa au alikopeshwa, hivyo sio mbaya kuomba msaada.
 
86EF44AB-8884-4082-9AA5-854260D11991.jpeg

Mchangienii
 
Wanafahamu dhahiri kwenda CAS ni kupoteza pesa..

Hivyo hawako tayari kupata hasara,

Ndio maana wanawachangisha wasakatonge ili ziwe zimepotea za wasakatonge na sio za feisali
Hakika, hakuna kesi hapo
 
Fei ni MHUJUMU, anaihujumu Yanga na soka la Tanzania kwa ujumla.

Hii itamtafuna maisha yake yote na kizazi chake
 
Huhitaji 50M kupeleka kesi CAS. CAS unalipa processing fees tu ambayo ni cheap otherwise CAS ingekua ya players wenye uwezo tu. Msuva katoka CAS juzi juzi wakati alikua hajalipwa miezi na alienda mwenyewe. Huyu feisal anataka achangiwe 50M ya nini?
 
Back
Top Bottom