Underthesea
JF-Expert Member
- Jul 8, 2021
- 327
- 882
The Radford Family
Noel (50) na Sue (46) Radford walikuwa mayatima na walikutana wakiwa wadogo.
Sue alipata mimba akiwa na umri wa miaka 14 huku Noel akiwa na 18. Walikaa bila kongeza mtoto hadi walipooana binti akiwa na miaka 17.
Tangia wakati huo karibu kila mwaka Sue huwa na ujauzito hadi leo hii 2021 ana mtoto wa 22 aliyezaliwa 2020, wavulana 11 na wasichana 11.
Mimba yake ya 17 iliharibika ikiwa imeishakuwa kubwa, walimzika mtoto na kila mwaka humpelekea zawadi kwenye kaburi lake na huwa wanasafiri na picha yake kila wakisafiri. Bado wanamuhesabu kama mwanafamilia (asingehesabiwa wangesema wana watoto 21 tu).
Kwa sasa Wana wajukuu 6.
Watoto wanne wakubwa (mkubwa 32years) wanaishi kwao na familia zao ambapo sio mbali na nyumbani. Wengine 18 bado wapo wanachangamsha jumba lao lenye vyumba 10.
Unaambiwa kelele za watoto wakiwa wanacheza nje ya nyumba ni kama shule wakati wa break.
Baba alikuwa akifanya kazi kama Baker kwenye bakeries mbalimbali na sasa anamiliki Bakery yake akisaidiwa kazi na wanawe wawili anaowalipa.
Bakery ndo inayoendesha maisha yao, watoto wanasoma private schools, wamenunua jumba lao, watoto wana afya na furaha. Wanaweza kwenda "vacation" familia nzima.
Kuna kiasi fulani cha pesa huwa wanapewa na serikali kama familia zingine zote huko Uingereza wanazopewa kulingana na idadi ya watoto (child benefits).
Wanakwambia watu wanafikiri wao wanazaa tu kwakuwa ni wavivu na wanategemea misaada lakini wao wana familia kubwa kwasababu wanapenda kuwa na familia kubwa na wanafanya kazi kwa bidii na wala hawategemei misaada ya watu wasiojiweza.
Reality shows, interviews wanazopata na YouTube channel yao zitakuwa zimewasaidia ku boost maisha. Kwakweli ukiwaangalia huwezi kusema ni "maskini".
Wanatumia kama 350 pounds sawa na Tsh. 1,123,000/= kila wiki kwa ajili ya chakula pekee. Inabidi mama aende shopping Kila siku kununua vyakula. Wanasema kipindi watoto wamefunga shule ndo balaa, watoto wanakula kama nzige (locusts).
Baba ndio mpishi mkuu wa familia. Mama mara nyingi ana deal na watoto na usafi.
Wanakwambia karibu kila wiki kuna birthday ya mtu, na kama desturi lazima wakate keki. Mama mwenyewe kasema ana "birthday fatigue". Baba anasema hata hakumbuki tarehe za wanawe za kuzaliwa.
Bila kusahau sherehe kubwa ya Krismas ambapo watoto wote hununuliwa zawadi.
Wanasema wao sio matajri, hawanywi pombe, hawavuti sigara, hawatoki kula out, hawanunui magari ya kifahari. Hela yote wanayopata inarudi kwa watoto wao.
Wameshazoea kila wakienda vacation lazima watu wawanyoshee vidole na kuwahesabu.
Mtoto mmoja alisema kwenye interview Moja kuwa kuna tendency ya kuchelewa kuondoka nyumbani kwa watoto hao kwani wanapapenda nyumbani kwao hawatamani kuondoka.
Noel (50) na Sue (46) Radford walikuwa mayatima na walikutana wakiwa wadogo.
Sue alipata mimba akiwa na umri wa miaka 14 huku Noel akiwa na 18. Walikaa bila kongeza mtoto hadi walipooana binti akiwa na miaka 17.
Tangia wakati huo karibu kila mwaka Sue huwa na ujauzito hadi leo hii 2021 ana mtoto wa 22 aliyezaliwa 2020, wavulana 11 na wasichana 11.
Mimba yake ya 17 iliharibika ikiwa imeishakuwa kubwa, walimzika mtoto na kila mwaka humpelekea zawadi kwenye kaburi lake na huwa wanasafiri na picha yake kila wakisafiri. Bado wanamuhesabu kama mwanafamilia (asingehesabiwa wangesema wana watoto 21 tu).
Kwa sasa Wana wajukuu 6.
Watoto wanne wakubwa (mkubwa 32years) wanaishi kwao na familia zao ambapo sio mbali na nyumbani. Wengine 18 bado wapo wanachangamsha jumba lao lenye vyumba 10.
Unaambiwa kelele za watoto wakiwa wanacheza nje ya nyumba ni kama shule wakati wa break.
Baba alikuwa akifanya kazi kama Baker kwenye bakeries mbalimbali na sasa anamiliki Bakery yake akisaidiwa kazi na wanawe wawili anaowalipa.
Bakery ndo inayoendesha maisha yao, watoto wanasoma private schools, wamenunua jumba lao, watoto wana afya na furaha. Wanaweza kwenda "vacation" familia nzima.
Kuna kiasi fulani cha pesa huwa wanapewa na serikali kama familia zingine zote huko Uingereza wanazopewa kulingana na idadi ya watoto (child benefits).
Wanakwambia watu wanafikiri wao wanazaa tu kwakuwa ni wavivu na wanategemea misaada lakini wao wana familia kubwa kwasababu wanapenda kuwa na familia kubwa na wanafanya kazi kwa bidii na wala hawategemei misaada ya watu wasiojiweza.
Reality shows, interviews wanazopata na YouTube channel yao zitakuwa zimewasaidia ku boost maisha. Kwakweli ukiwaangalia huwezi kusema ni "maskini".
Wanatumia kama 350 pounds sawa na Tsh. 1,123,000/= kila wiki kwa ajili ya chakula pekee. Inabidi mama aende shopping Kila siku kununua vyakula. Wanasema kipindi watoto wamefunga shule ndo balaa, watoto wanakula kama nzige (locusts).
Baba ndio mpishi mkuu wa familia. Mama mara nyingi ana deal na watoto na usafi.
Wanakwambia karibu kila wiki kuna birthday ya mtu, na kama desturi lazima wakate keki. Mama mwenyewe kasema ana "birthday fatigue". Baba anasema hata hakumbuki tarehe za wanawe za kuzaliwa.
Bila kusahau sherehe kubwa ya Krismas ambapo watoto wote hununuliwa zawadi.
Wanasema wao sio matajri, hawanywi pombe, hawavuti sigara, hawatoki kula out, hawanunui magari ya kifahari. Hela yote wanayopata inarudi kwa watoto wao.
Wameshazoea kila wakienda vacation lazima watu wawanyoshee vidole na kuwahesabu.
Mtoto mmoja alisema kwenye interview Moja kuwa kuna tendency ya kuchelewa kuondoka nyumbani kwa watoto hao kwani wanapapenda nyumbani kwao hawatamani kuondoka.