Familia na vyanzo mbalimbali vya mapato

Familia na vyanzo mbalimbali vya mapato

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Wengi huwa tunapenda kuanzisha familia ikiwa lengo kuu ni kupeana faraja tu, bila kufikiria ili familia iwe na amani na utulivu uchumi unatakiwa uwe umetulia.

Si vema kwa mtu mwenye familia kuwa na chanzo kimoja cha mapato, mfano mshahara; mshahara siku zote huwa hautoshi na huwa unapatikana mara moja kwa mwezi.

Na unapokuwa na familia kunaweza kutokea baadhi ya changamoto na kupelekea familia kuhangaika kutafuta suluhu ya kifedha kwa ndugu, jamaa, na marafiki; na wakati mwingine kutokufanikisha kabisa.

Kama umeamua kuanzisha familia, hakikisha umeanzisha vyanzo vingine vya mapato ambavyo vitakufanya uwe huru pamoja na kufurahia familia yako.

Sio unakuwa na chanzo kimoja cha mapato, ambapo bosi wako akikukoromea tu, na familia pia inaathirika kutokana na msongo wa mawazo utakao kuwa nao kutokana na kutokuwa na mbadala.

Ni vizuri kuwa na vibiashara vidogo vidogo kutokana na uwezo wako, mfano viduka vidogo vidogo, vigenge, vibustani, vishamba, mifugo n.k.

Na si lazima uanze na mtaji mkubwa, unaweza ukajiwekea malengo ya kuanzisha vigenge labda 10, vya laki tatu tatu n.k Kuwa na mifugo itakayo kuwezesha muda wowote kupata nyama n.k

Nimeona familia nyingi wanaoishi kwa chanzo kimoja hasa mshahara (ajira), huwa wana msongo wa mawazo sana, na wakati mwingine familia zao hazina amani; jumatatu mpaka jumamamosi wako bize kazini, na asipoenda familia inateketea kwa hiyo inabidi kujilazimisha hivyo hivyo.

Muhimu, tuwe na vyanzo mbalimbali vya mapato, ili kuboresha furaha, malezi na kuwa karibu na familia zetu​
 
Nimeona familia nyingi wanaoishi kwa chanzo kimoja hasa mshahara (ajira), huwa wana msongo wa mawazo sana, na wakati mwingine familia zao hazina amani; jumatatu mpaka jumamamosi wako bize kazini, na asipoenda familia inateketea kwa hiyo inabidi kujilazimisha hivyo hivyo.


Yaani ikitokea (muajiriwa) akaugua ghafla familia inaugua kwa ukubwa sana


Umenena kwa lugha ya kufikirisha sana mkuu.
 
Nimeona familia nyingi wanaoishi kwa chanzo kimoja hasa mshahara (ajira), huwa wana msongo wa mawazo sana, na wakati mwingine familia zao hazina amani; jumatatu mpaka jumamamosi wako bize kazini, na asipoenda familia inateketea kwa hiyo inabidi kujilazimisha hivyo hivyo.


Yaani ikitokea (muajiriwa) akaugua ghafla familia inaugua kwa ukubwa sana


Umenena kwa lugha ya kufikirisha sana mkuu.
Wanasema ni bora ushtuke mapema na uanze kufanya maamuzi, na muda wa kufanya maamuzi ni sasa
 
Uzi wako unaonyesha jinsi gani Jamii kwa ujumla wake imeoza...

Watu Ujira wao hautoshi (Yaani hakuna disposable income) Nini kinatokea

Traffic anakuwa anawaza kupiga rushwa na sio kufanya kazi yake kwa uhakika) Daktari badala ya kuweka nguvu zake kutizama wateja anawaza atoke hapo aende kwenye kibarua kingine au ni vipi wale kuku wake na mbuzi wake anaweza kuwaongeza...

Mwalimu badala ya kutumia jioni kuwaza ni vipi atamfanya yule John aweze kusikiliza na ni vipi atamwingia ili apende kusoma anawaza huyu mkata majani ya ng'ombe aliyetoroka atapata wapi mwingine...

Tatizo watu mshazoea na mnaona kwamba hii ndio the norm na hakuna any other way.... In short kama Jamii tumekuwa watu wa kubangaiza na wote tupo kwenye Rat Race....

Things have fallen apart na kama jamii inabidi tu-press a reset button - Kunahitajika revamption ambayo ni inclusive kwa majority na sio solutions za mtu mmoja mmoja...

That said, You need to Bite what you can Chew..., kabla hamjatotoa offprings wa kutosha kwanza mjiulize kama mataweza kuwa-afford... (zamani watoto walikuwa nguvu kazi - the more you have, the more farmers you get)
 
Kama wapo watu wanasomesha, wanaishi kwa biashara ya laki 2; kwa nini wengine washindwe, unapata mshahara labda milioni, kwa nini usiwe hata na kagenge?​
Kama mtu hayajakukuta au hujayaona kwa mtu wako wa karibu huwezi kuwa na hiyo akili ya kufungua genge au kuwa na mbadala.

Unakuwa na akili za hovyo sana.
 
Uzi wako unaonyesha jinsi gani Jamii kwa ujumla wake imeoza...

Watu Ujira wao hautoshi (Yaani hakuna disposable income) Nini kinatokea

Traffic anakuwa anawaza kupiga rushwa na sio kufanya kazi yake kwa uhakika) Daktari badala ya kuweka nguvu zake kutizama wateja anawaza atoke hapo aende kwenye kibarua kingine au ni vipi wale kuku wake na mbuzi wake anaweza kuwaongeza...

Mwalimu badala ya kutumia jioni kuwaza ni vipi atamfanya yule John aweze kusikiliza na ni vipi atamwingia ili apende kusoma anawaza huyu mkata majani ya ng'ombe aliyetoroka atapata wapi mwingine...

Tatizo watu mshazoea na mnaona kwamba hii ndio the norm na hakuna any other way.... In short kama Jamii tumekuwa watu wa kubangaiza na wote tupo kwenye Rat Race....

Things have fallen apart na kama jamii inabidi tu-press a reset button - Kunahitajika revamption ambayo ni inclusive kwa majority na sio solutions za mtu mmoja mmoja...

That said, You need to Bite what you can Chew..., kabla hamjatotoa offprings wa kutosha kwanza mjiulize kama mataweza kuwa-afford... (zamani watoto walikuwa nguvu kazi - the more you have, the more farmers you get)
Nakubaliana na hoja yako; ghafla umeugua na unatakiwa upelekwe India, na inatakiwa milioni 100, utafanyaje?
 
Back
Top Bottom