Familia nyingi hazijawahi kubadili kitanda na godoro hadi UZEENI

Familia nyingi hazijawahi kubadili kitanda na godoro hadi UZEENI

Mleta mada vitanda kama hivi inatakiwa kubadilishwa baada ya muda gani
0e775061c95ca5b89fa6fcff9e5d34fe.jpg
072ac82754865fb4c42ba5eeb4b45768.jpg
 
Vitanda na magodoro katika familia nyingi za Kiafrika vimetumika kuzalishia watoto, wajukuu na hata vitukuu. Vitanda hivi vimeshuhudia mmiliki akiwa kijana au watu wakiwa wachumba, wakaoana, wakapata watoto ,wajukuu na kushuhudia wanavyozeeka hadi kufa. Pia mtu tangu aanze kazi hadi anastaafu amekuwa na Kitanda alichonunua kwa mshahara wake wa kwanza.
Bahati mbaya sana kitanda kilichotumika kukuzaa unakuta umerithishwa na wewe umekitumia kupata watoto wako. Nadhani ni kutokana na hali ya Maisha ILA MIMI NINGETAFUTA CHANGU KUPATA WATOTO NA SIO CHA WAZEE WANGU.

Anyway Nadhani sina issue nimejiandikia tu maana sina pa kwenda leo.

Kuna watu wakinunua Kitanda, godoro na kabati yaani ndio HADAIWI TENA MAISHANI , NI KAMA NYUMBA TU KWAKE.

Legendary ambaye hulalii kitanda cha urithi na ambaye umebadilisha kitanda cha kwanza na kununua godoro jipya JIPIGE KIFUANI MARA TATU UJIPONGEZE
Ninafuata ushauri wa TanForm, alianza babu, baba mpaka mjukuu na kitukuu.
 
😂😂😂😂Mtoa mada as long as watu wanakoroma mengine hayo ni ya ziada
 
😂😂😂😂Mtoa mada as long as watu wanakoroma mengine hayo ni ya ziada
Ni kweli ila kuna godoro lina mkojo likaanikwa weeee miaka hadi kijana naye kapata mtoto ambaye naye analikojolea. Cha kufurahisha huwa linatolewa kuanikwa sehemu ileile lilipokuwa likianikwa baba wa mtoto alipolikojolea akiwa mtoto.
 
Godoro la tanfoam lile orijino linalodumu mpaka mjukuu analitumia kwann ulibadili
Kama hali ya maisha hairuhusu sawa, lakini kama hali ni njema ifike sehemu kila uzao wako(mtoto) apatikane kwenye godoro lake. Na kama umeshamaliza kuzaa basi angalau badili godoro kila baada ya miaka mitano na kitanda baada ya miaka 10. Pia nguo za kuvaa isifike watu kukukariri kwa vazi lako ambalo hutaki kuliacha hadi lichanike kabisa.
 
Ninaamini mtu kama Baba Levo kule kigoma godoro lake amezaliwa kalikuta na hajui limeanzia wapi. Amshukuru Diamond kumleta Dar angalau analalia godoro jipya sasa
 
Ishu sio hali ya uchumi ni mazoea tu Sasa kitanda cha mninga kinachakaaje.hata miaka 1000 kinakaa.
Tena ukitaka kiwe kipya unamuita fundi anakisugua kwa msasa laini kisha anapaka vanish, kinawaka ile mbaya 😄!.
 
Tena ukitaka kiwe kipya unamuita fundi anakisugua kwa msasa laini kisha anapaka vanish, kinawaka ile mbaya 😄!.
Me nilibadili godoro tu lakini kitanda kile kile kilichobeba mabehewa ya treni nabadili tu godoro jipya kwa mtoto mpya akizaliwa.
Mama Yao anakilalia toka enzi zile za wizi hadi Sasa zama za uhalali.
Ngojaa nilibadili sikuwa na wazo hilo
 
Wengi wanaogopa kununua godoro mpya wakidhani labda ni bei sana zipo mpaka za laki moja na nusu karibuni mzipate kwetu bei ni poaaaa
 
Kwanza kiafya unashauriwa ulale chini achana na vitanda na sababu wa Japan wanaishi maisha marefu na yenye afya they must be doing something right....

1719816129874.png


to each their own...
 
Back
Top Bottom