magnifico
JF-Expert Member
- Jan 14, 2013
- 11,075
- 24,634
Nimekuwa karibu na Waarabu na Wahindi. Baadhi wana ubaguzi japo wanajitahidi kuuficha na baadhi wako poa sana na wana upendo pia. Nilipataga homa kipindi nasoma mkuu wa shule akaja kuniona nyumbani kabisa na zawadi za mgonjwa.Hao watu poa sio Wahindi... Huwajui wahindi we mtoto. Ulifananisha kimuonekano ukadhania ni muhindi. Tulia!
Baadhi yetu mfano mleta mada kakutana na maswaibu hayo kipindi anafanya nao kazi, ni kweli yanatokea hata huku nakoishi nayaona pia. Najaribu kuongelea upande wangu.
Hadi leo hii nina marafiki Waarabu na Wahindi pia, naheshimu tamaduni zao na mimi nawahimiza waheshimu zangu pia. Huwa sipendi kupandwa kichwani asee. Nimeshawahi timua baadhi ofisini kwangu kama masihara.
Pole kwa waliowahi kuwakuta ingekua mimi hali ingeweza kuwa mbaya kwa pande zote mbili nina hasira sana nikidharauliwa au kubaguliwa. Naomba Mungu aniponye hii hali.
Fanya yote hata kama una pesa ila linda heshima yako.
Ila siamini kama ameleta huu uzi kwajili ya kutaja mabaya yao tu, hapana.
Kuna kitu nilijifunza kwenye maisha, unapopita mahali ukakuta mtu unayemjua anasemwa kwa mabaya jitahidi uwaambie hata jema lake moja tu utabarikiwa pia.