Familia ya Gwajima imemkosea Waziri wa Afya, kiungwana wamtafute wamuombe radhi

Familia ya Gwajima imemkosea Waziri wa Afya, kiungwana wamtafute wamuombe radhi

msovero

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2019
Posts
863
Reaction score
1,534
Askofu gwajima huku akijua kwamba shemeji yake ndiye amepewa dhamana ya kusiamamia mambo ya chanjo. kiungwana tu hata kama hakubaliani na chanjo kwa kumheshimu shemeji yake angeweza kusema natumia hiari kutochanjwa basi akaishia hapo ili kuepusha migogoro ya kifamilia isiyokuwa ya lazima na pengine kumharibia shemeji yake kazi.

Lakini badala yake askofu gwajima amegeuza suala la chanjo kuwa mahubiri yake ya kila siku kanisani kwake huku akihamasisha na watu wengine kutochanjwa.

Si hivyo tu, pia kwenye mahubiri yake, askofu gwajima amekuwa akitumia mahubiri hayo kumshambulia shemeji yake na kuvuruga jitihada anazofanya kuhamasisha wananchi kuchanjwa chanjo ya UVIKO-19.

Kwa sababu ya busara ndogo ya askofu gwajima na kwa sababu ya kusaka umaarufu wa kisiasa amepelekea kuwepo kwa mzozo wa kifamilia na hata kuhatarisha ndoa ya mdogo wake.

Licha ya ndoa ya mdogo wake kuwa mashakani, pia anamharibia shemeji yake kwani mwitiko mdogo wa zoezi la chanjo unatokana na kauli zake anazozitoa akiwa madhabahuni.

Kwenye ibada ya leo, askofu gwajima ndio kaharibu kabisa kwani inaonyesha ameamua kumvunjia heshima na kumdhalilisha shemeji yake wazi wazi kwamba yeye kuolewa na mdogo wake ni hasara kwa familia yao na kwamba wamekuwa hawaelewani kwa sababu yake.

Mbaya zaidi mzee gwajima naye pamoja na uzee wake inaonyesha hana hekima wala busara kwa sababu alipaswa kuwa sehemu ya usuluhishi kwa kumshauri mwanaye 'askofu' kuacha kulumbana na shemeji yake hadharani lakini naye amezidi kukoleza moto kwa kumpa go ahead ya kumdhalilisha dorothy ambaye ni 'mwenga' wake.

Kwakweli kitendo kilichofanywa na askofu gwajima pamoja na mzee wake kumtweza Dorothy ni kitendo cha aibu na kiungwana wamtafute wamuombe radhi hili jambo walimalize kifamilia kwani msingi wa matatizo yote haya bila kupepesa macho ni Askofu Gwajima.
 
Hawa wahutu waliojivika usukuma ni waongo sana
Screenshot_20210822-192501.jpg
 
Kama Dorothy asingemjibu na kumshambulia Askofu kwa maneno ya kuudhi (hata kama mengine ni kweli) bila shaka Askofu Rashid asingechomoa battery

Huna haja ya kumuonea huruma Dorothy. She is old enough to deal with whatever is thrown at her. Alijiingiza kwenye mabishano huku akijua nini kitafuata. Acha tu waonyeshane makali.

Askofu Rashid sio muumini wa “ukinitandika kofi shavu hili, nitageuza upige na huku”. Yeye ni mzee wa tit-for-tat, jino kwa jino.
 
Askofu gwajima huku akijua kwamba shemeji yake ndiye amepewa dhamana ya kusiamamia mambo ya chanjo. kiungwana tu hata kama hakubaliani na chanjo kwa kumheshimu shemeji yake angeweza kusema natumia hiari kutochanjwa basi akaishia hapo ili kuepusha migogoro ya kifamilia isiyokuwa ya lazima na pengine kumharibia shemeji yake kazi...
Hivi mnapata wapi muda wa kumsikiliza huyo Gwajima? Mimi hata mahubiri yake siyaelewi
 
Back
Top Bottom