Familia ya Gwajima imemkosea Waziri wa Afya, kiungwana wamtafute wamuombe radhi

Tumejua yafuatayo.

Kumbe Dada Doro alishavunja ndoa zingine huko nyuma kabla ya hii.

Kumbe kina Gwajima ni Wahutu.

Kumbe Gwajima Ni kweli alikua na binti gesti wakati anandoa.

Kumbe Dada Doro amewavuruga ndugu wa mume hawasikilizani.

Acha waendelee kuvuana chupi tunaweza hata kujua mengi zaidi
 
Kwani Yesu alivunja ndoa za watu hadharani??!
 
Askofu Rashid sio muumini wa “ukinitandika kofi shavu hili, nitageuza upige na huku”. Yeye ni mzee wa tit-for-tat, jino kwa jino.
Kwahiyo hamfuati Yesu!!, sasa anamfuata nani??
 
Ni kama vile wewe hujui usemalo..

Dr Dorothy Gwajima na naibu wake ndiyo walioanza kumkashfu Mch. Gwajima na kutukana zaidi ya watanzania 70% wasiotaka kuchanja chanjo hii kwa usalama wao. Walifikia hatua ya kuwaita hawa 70% wote ni wajinga...
Sio lazima atokee mlango huo huo, anaweza kutokea mlango wa nyuma.
 
Hivi inakuwaje mabifu ya familia watuletee Hadi huku na wananchi tunalazimishwa kuyaingia mabifu yao ya siyo hata na kichwa Wala miguu
 
Askofu piga sapana achana na wapiga debe wa chanjo. Waziri who!
 
Naunga mkono hoja, na huu ni udhalilishaji sio tuu kwa Doro, bali kwa kabila zima la Wanyiramba, katakako shusha rate ya kuolewa kwa mabinti wa Wanyiramba.

Wanyiramba msikubali udhalilishaji huu, simameni m demands public apology.
P
 
Nasikia yule mzee sio baba wa mume wa Dorothy ila Ni baba yake ye Gwajima.Mkwewe Dorothy alishafariki.
Licha ya kuwa Dorothy kuwa alianza kumdharirisha Gwajima lkn alichofanya Leo Gwajima Ni upuuzi zaidi
Ndg yangu Steve,siku zote tambua kua dhuluma haina kiwango, ukimdhulumu Mtu elfu kumi,alafu yeye kesho yake akakudhulumu laki moja,huwezi sema eti akurudishie elfu 90 kisa wwe ulimdhulumu elfu kumi tu, hiyo inakua isha kula kwako!

Ni sawa na kumkashifu Mtu,nae akiamuwa kukukashifu huwezi kumchagulia Maneno ya kukukashifu,wwe pokea lolote lile litakalo toka kwake!! Dorothy ndiyo kachokoza Moto kwa Shemeji yake,Sasa nae zamu yake kupokea Moto,haijalishi Moto ni Mkubwa au ni mdogo, tunasema Moto ni Moto tu!!
 
Ok lakini kauli za waziri Gwajima Zina tatizo
 
Wewe acha ujinga wa kuangalia upande mmoja tu.

Kama kuna kampeni ya kuhamasisha watu wachanjwe pia lazima na watu wasiokubaliana na chanjo nao wafanye kampeni yao .
 
Kaka Mtu tena Askofu Mtumishi wa Bwana amepataje Hekima ya kudhalilisha Mke wa Nduguye hadharani?? Inaingia akilini kweli Askofu anahesabu idadi ya Ndoa za Shemeji?

Kwa kweli nimemtoa anayejiita Askofu thamani na ningekuwa muumini wake Leo ningekuwa Mpagani.
 
Nimekuelewa na upo sahihi,lakini Mimi namlaumu Gwajima kwa sababu ya nafasi yake ya Uaskofu.Laiti Kama Gwajima angekuwa mwanasiasa Basi Kama ilivyo kwa Dorothy nisingeshangaaa Wala nisingemlaumu maana Mambo ya kejeli alianza Dorothy.Nampa Lawama Gwajima kwa sababu ya nafasi yake ya Uaskofu.Kesho atafundisha Nini kanisani kuhusu upendo,msamaha kutokuwa na kiasi.Kuna sehemu kapigia debe uzinzi,hapo anamaanisha Nini? Sera ya jino kwa jino ndio anayohubiri Gwajima.Huyu kesho akikufundisha kuhusu kuwasamehe madui zetu kwa vile hawajui watendalo utamuelewa?
 
Ahahaha mama anajuta kumchokoza kifaru! Mama naye alizidi,huwezi kiwa waziri ukajibizana kijinga vile!

Siku zote ukiwa kiongozi HEKIMA HUTANGULIA JAZIBA sasa Dorothy(simuiti Gwajima tena maana kakatazwa na wenye jina) angejiengue fasta kwenye uwaziri-ova
 
Halafu Kuna mtu anaaga nyumbani kuwa naenda kanisani kusikiliza neno la Mungu.Hivi pale neno la Mungu Ni lipi?
 
Waziri wa afya kajidharirisha mwenyewe.

Kwa mfano alipomtuhumu askofu kuwa alidai atamfufua Amina chifupa ,Sijui mara akaja akafumwa na mrembo huku akijua huyo ni shemeji yake au ni mkwe wake hiyo ni adabu?Halafu hayo yanauhusiano gani na mambo ya chanjo? Halafu wewe unatetea huo ujinga!

Kwa mfano angejibu hoja tena bila hata kumtaja jina shemeji yake huyo askofu, angepungukiwa na nini? Si angesema naomba nijibu hoja za wananchi ambao wamekuwa wakipotosha kuhusu chanjo.Kisha akajibu hizo hoja bila kumtaja jina bila kutaja mambo ya msukule,Mrembo au mambo ya ushemeji.Kwani hapo anapozungumza anazungumza akiwa kwenye kikao cha familia yao au anazungumza akiwa waziri?Halafu unaibuka mtu kama wewe unatetea ujinga.!
 
Aliyeanza vita ni askofu gwajima. Kwa sababu baada ya serikali kuleta chanjo yeye akageuza hilo suala kuwa mahubiri yake ya kila siku kanisani huku akimzodoa waziri wa afya 'Dorothy' kwamba ni kigeugeu na hafai kuwa kwenye uwaziri. Dorothy baada ya kuona vichambo vimezidi ikabidi naye ajitetee kwa hayo ya kumfufua amina chifupa, mkono wa baunsa na mengine mengine.

Kwahiyo kiini cha tatizo ni askofu kwa sababu yeye asingetumia suala la chanjo na kumshambulia 'dorothy' kila jumapili kwenye mahubiri yake haya yote yasingetokea
 
Kichaa akikwapua wiki lako sokoni ukaanza kumkimbiza wewe ndio unakuwa kichaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…