Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kabisa.Washindwe walegee
Wakumbuke Kuna Familia za akina Ben saananeMmoja wa wandani wa familia ya aliyekuwa rais wa tano wa Tanzania hayati Magufuli amepenyeza taarifa kuwa mara baada ya kumaliza msiba walikaa kikao na kuamua kuwa familia hiyo haitamjibu mtu yoyote anayetukana au kukebehi legacy ya Magufuli kwenye nchi hii, badala yake watauachia muda ujibu maana siku zote muongo mpe muda na uongo wake utabaki hadharani.
Na ni kweli baada ya miaka 3 ya kifo cha mpendwa wao muda umeendelea kuwajibu wale wanafiki na waongo hasa kutokea Chadema. Baada ya miaka 3 bado familia ya Lisu inalishwa na wazungu na hajadhubutu kabisa kuirudisha nyumbani, Godbless Lema pia bado mke wake na watoto wanaishi kama wakimbizi Canada!
Baada ya miaka 3 wale wabunge 19 akina Mdee wameendelea na ubunge wao licha ya Mbowe kuahidi kuwatoa bungeni!
Baada ya miaka 3 ununuzi wa ndege unaendelea, ujenzi wa bwawa la mwl Nyerere na SGR unaendelea kwa kasi licha ya kupingwa na Chadema!
Baada ya miaka 3 ya kifo cha Magufuli, CCM imeendelea kushinda na kuzoa viti vyote vya udiwani hadi Pemba, Mbowe na Zito hawajaambulia chochote kwenye hizi chaguzi ndogo.
Baada ya miaka 3 , Lengai Ole Sabaya yuko huru anakula maisha uraiani baada ya mahakama kumkuta hana hatia na kesi zake zote zilikuwa za uongo. Paul Makonda ni mkuu wa mkoa wa Arusha licha ya Chadema kuahidi kumpoteza.
Baada ya miaka mitatu Mange na Kigogo wamegeuka wachochezi,wakosa adabu kwa Rais na Nape Nnauye ndiyo anahusika kuwafungia akaunti zao kwenye mitandao ya kijamii! Kumbuka Nape alikuwa mlilia uhuru wa kutoa maoni nchini. Kutoka kuitwa mashujaa wa taifa hadi kufungiwa Instagram zao, karma is karma na bado.
Baadhi ya vigogo walioshangilia kifo chake, tayari walishamfuata na kusahaulika kama walishawahi kuwa viongozi wa nchi hii kwa miaka mingi. Eg Rondo
Ama hakika muongo mpe muda na muda unaendelea kujibu na tutaona na kujifunza mengi ndani ya muda.
Mbowe yupo anadunda yule dhalimu kafaMuda ulishajibu tayari, mara ya mwisho Ben saanane alitumwa na mbowe
Mmoja wa wandani wa familia ya aliyekuwa rais wa tano wa Tanzania hayati Magufuli amepenyeza taarifa kuwa mara baada ya kumaliza msiba walikaa kikao na kuamua kuwa familia hiyo haitamjibu mtu yoyote anayetukana au kukebehi legacy ya Magufuli kwenye nchi hii, badala yake watauachia muda ujibu maana siku zote muongo mpe muda na uongo wake utabaki hadharani.
Na ni kweli baada ya miaka 3 ya kifo cha mpendwa wao muda umeendelea kuwajibu wale wanafiki na waongo hasa kutokea Chadema. Baada ya miaka 3 bado familia ya Lisu inalishwa na wazungu na hajadhubutu kabisa kuirudisha nyumbani, Godbless Lema pia bado mke wake na watoto wanaishi kama wakimbizi Canada!
Baada ya miaka 3 wale wabunge 19 akina Mdee wameendelea na ubunge wao licha ya Mbowe kuahidi kuwatoa bungeni!
Baada ya miaka 3 ununuzi wa ndege unaendelea, ujenzi wa bwawa la mwl Nyerere na SGR unaendelea kwa kasi licha ya kupingwa na Chadema!
Baada ya miaka 3 ya kifo cha Magufuli, CCM imeendelea kushinda na kuzoa viti vyote vya udiwani hadi Pemba, Mbowe na Zito hawajaambulia chochote kwenye hizi chaguzi ndogo.
Baada ya miaka 3 , Lengai Ole Sabaya yuko huru anakula maisha uraiani baada ya mahakama kumkuta hana hatia na kesi zake zote zilikuwa za uongo. Paul Makonda ni mkuu wa mkoa wa Arusha licha ya Chadema kuahidi kumpoteza.
Baada ya miaka mitatu Mange na Kigogo wamegeuka wachochezi,wakosa adabu kwa Rais na Nape Nnauye ndiyo anahusika kuwafungia akaunti zao kwenye mitandao ya kijamii! Kumbuka Nape alikuwa mlilia uhuru wa kutoa maoni nchini. Kutoka kuitwa mashujaa wa taifa hadi kufungiwa Instagram zao, karma is karma na bado.
Baadhi ya vigogo walioshangilia kifo chake, tayari walishamfuata na kusahaulika kama walishawahi kuwa viongozi wa nchi hii kwa miaka mingi. Eg Rondo
Ama hakika muongo mpe muda na muda unaendelea kujibu na tutaona na kujifunza mengi ndani ya muda.
Lowassa alivyohamia Chadema alinunuliwa na nanNa mchungaji Msigwa amenunuliwa na nani?
Familia iendelee kunyamaza hvy hvy na muda utaongea wnyw.
1. Saliva kutekwa: Enzi za JPM Chadema wangesema ni yeye amehusika.
2. Msigwa kuhama chadema: Chadema wangesema n muendelezo wa michezo michafu ya JPM kununua wapinzani huku wangesahau hao Chadema walivomnunuaa Lowassa [emoji23]
Bado kuna uuzaji wa mali za nchi [emoji23]
Not only wrong, but irrelevant...Wangekaa kimya tu.
Ukishasema humjibu mtu pia ni jibu.