Familia ya Rais Magufuli mkiliachia hili jambo lipite bila ya kumburuza mahakamani Kabendera itakuwa ni usaliti wa karne!

Ndo maana nikasema wakiliacha hili suala bila kuchukua hatua, tuhuma zitaaminika!
Hizi tuhuma zipo siku nyingi sana tangu mwenyewe akiwa hai na wengi tumeziamini kutokana na hulka ya Magufuli ya ukatili. Huko mahakamani yanaweza kuibuliwa makubwa zaidi ya hili,busara ni kukaa kimya tu.
 
Hili ni kweli kabisa huyu amempita kwa mbali sana Magufuli kwa uovu,yaani hii awamu ya sita ya mchongo tunaweza kabisa kuibatiza na kuiita awamu ya "ubaya ubwela".
Mnauana wenyewe kwa wenyewe halafu mnawatuhumu watu wasiohusika kwa kisingizio ndio marais
Acha bhangi mbichi..!
 
Napata wakati mgumu sana kuamini kuwa Rais Magufuli anaweza kumuua kijana wa Kitanzania, ambaye ni mtu mdogo sana, in the grand scheme of things, kwa mikono yake mwenyewe tena kwenye nyumba ya wananchi, Ikulu.
Kwa Wakristo Kisasi ni jambo baya sana. Ninachokiona kutoka kwa Kabendera ni Kisasi dhidi ya Mpendwa Magufuli. Hizi ni serious accusations ambazo zinahitaji tangible evidence na sio evidence zinazotokana na hearsay! Pia inashangaza kusoma moja miongoni mwa sources zake ni Viongozi wa Upinzani! Hao viongozi wa upinzani walikuwa wapi hadi wakashuhudia Ben akiingizwa Ikulu ambako Mh Magufuli alikuwa na pistol?!

Naona Kibendera anatafuta Ukimbizi wa Kisiasa!
 
Nina uhakika kuna watu wanatamani na kuomba hili suala liende mahakamani!
Katika watu hao mimi niko msitari wa mbele kabisa. Kwa bahati mbaya sidhani kama yuko mwenye ujasiri wa kufanya hivyo!

Eti kumshtaki Kabendera, thubutu! Nasubiri kwa hamu kubwa kuona Serikali itakavyovuliwa nguo mbele ya ulimwengu!

Barua za Ben Saanane kwa polisi na vyombo vya dola si zipo? Na je vipi kuhusu tukio la Lissu mwaka moja baadaye? Serikali ile ile na viongozi wale wale!
 
Wakati mwi Ng Wewe nawe, umeanza kuwa kituko. Unafikiri Familia haijui kwamba Jpm alikuwa muuaji? Wewe ndio umekuwa family advisor?
 
kwa hiyo unaamini waliopo wameamua tu kuachia hicho kitabu kimkakati kisomwe, japo wanaweza kukipiga marufuku lakini ujumbe utakuwa umesambaa na hauwezi kufutwa! Kwani kuna nini januari hii mapema tu kitabu msisimko kinaachiwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…