Familia ya Ulomi yakubali ndugu yao amefariki kwa ajali

Familia ya Ulomi yakubali ndugu yao amefariki kwa ajali

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Hatimaye familia ya mfanyabishara Daisle Ulomi aliyefariki na mwili wake kukutwa mochwari ya Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, imesema kuwa ndugu yao ni kweli alifariki kwa ajali.
IMG_1735.jpeg
Akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 17, 2024, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema ajali hiyo ilitokea Ubungo Extenal Makuburi mchana na walitokea wasamaria wema waliosaidia kumpeleka mwili huo hospitali.

"Tukio lile lilitokea mchana kweupe na wasamaria wema waliojitolea wenye ubinadamu na utu licha ya kwamba ilikuwa ajali mbaya ambayo kama ukiona ule mwili utajua ni kwa nini hata ndugu walipopita mochwari walishindwa kumtambua," amesema.
IMG_1736.jpeg

Akizungumza na wanahabari leo Mikocheni ambako familia imeweka msiba, msemaji wa familia hiyo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hassan Bomboko amesema baada ya mwili kupatikana Mwananyala walipigiwa simu kisha baadhi ya ndugu walienda kuangalia na kuutambua.

"Tupo kwenye taratibu za maombolezo ya kwenda kumstiri ndugu yetu ambaye alipata ajali Desemba 11, 2024 saa 7:55 mchana katika maeneo ya Gereji akiwa anatokea Barabara ya Mandela baada ya kutokea ajali watu wema walimpeleka kituo cha afya Makuburi," amesema.

Soma, Pia:
 
"Tukio lile lilitokea mchana kweupe na wasamaria wema waliojitolea wenye ubinadamu na utu licha ya kwamba ilikuwa ajali mbaya ambayo kama ukiona ule mwili utajua ni kwa nini hata ndugu walipopita mochwari walishindwa kumtambua," amesema.
Kutoka Sinza, kwenda Makuburi wakati safari yake ni Mbagala, meaning alifika Shekilango akakunja kuelekea Ubungo, binafsi naona alitengeneza mzunguko
 
Bodaboda ni hatari wakuu. Asieamini kuwa kafa kwa ajili awake ushahidi wake kwamba huu late Ulomi hakufa kwa ajali.
Huyo jamaa ni muongo hata ukiangalia facial expression yake unaona kabisa anadanganya ni maneno yakubumba tu.

Hawa watu ni waongo hawaaminiki. Hayo aliyoongea sio genuine.
 
Ninani wa kuwatenganisha wachaga pesa? Je! ni kifo,shida,au adha au njaa au uchi au hatari au upanga?


Aliwahi kusema mtume paul katika kitabu cha Warumi 8:35.

Msemaji wa familia kasawazisha dk za jioni sana kama mtoto wa mfalme price Dube
 
Msemaji Wa Familia Tambua Kuwa Mungu Yupo Na Mungu Anabaki Kuwa Mungu.

Je Katika Sakata la Kumtafuta Marehemu alipopotea, Wewe Ndo Ulikuwa Msemaji Wa Familia toka mwanzo? Au Umejipachika sasa usemaji wa familia?
 
Hatimaye familia ya mfanyabishara Daisle Ulomi aliyefariki na mwili wake kukutwa mochwari ya Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, imesema kuwa ndugu yao ni kweli alifariki kwa ajali.
View attachment 3178956Akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 17, 2024, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema ajali hiyo ilitokea Ubungo Extenal Makuburi mchana na walitokea wasamaria wema waliosaidia kumpeleka mwili huo hospitali.

"Tukio lile lilitokea mchana kweupe na wasamaria wema waliojitolea wenye ubinadamu na utu licha ya kwamba ilikuwa ajali mbaya ambayo kama ukiona ule mwili utajua ni kwa nini hata ndugu walipopita mochwari walishindwa kumtambua," amesema.
View attachment 3178957
Akizungumza na wanahabari leo Mikocheni ambako familia imeweka msiba, msemaji wa familia hiyo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hassan Bomboko amesema baada ya mwili kupatikana Mwananyala walipigiwa simu kisha baadhi ya ndugu walienda kuangalia na kuutambua.

"Tupo kwenye taratibu za maombolezo ya kwenda kumstiri ndugu yetu ambaye alipata ajali Desemba 11, 2024 saa 7:55 mchana katika maeneo ya Gereji akiwa anatokea Barabara ya Mandela baada ya kutokea ajali watu wema walimpeleka kituo cha afya Makuburi," amesema.

Soma, Pia:
Aligongwa/aligongana na nani?
 
Back
Top Bottom