Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 9,836
- 7,231
Shida kweli maana hii inaathiri pia hata viongozi wao kama Wasira anayelilia ubunge toka kwa Bulaya kila uchwao. Mara amtishie kumwachisha na jamaa yake mara akimuona anamvunja miguu na kumwagia tindikali ili tu mtoto wa watu aachie ubunge.Shida kubwa ni ubabe watu hawataki kuelekezwa na kukubali kutii.
Ni kweli unaweza kuona hapo tu ni mfano mmoja,watu wana viburi hatari,Pro.mmoja wa kutoka huko alikuwa anatukana, anabeza anavyojisikia kisa amesoma.Shida kweli maana hii inaathiri pia hata viongozi wao kama Wasira anayelilia ubunge toka kwa Bulaya kila uchwao. Mara amtishie kumwachisha na jamaa yake mara akimuona anamvunja miguu na kumwagia tindikali ili tu mtoto wa watu aachie ubunge.
Ni nyingi sana ndg.Nafikiri sheria tu haitoshi , jamii ipewe elimu na wajue madhara ya ndoa changa. Hiyo imeshikwa jamii imejua. Tunafikiri ni ndoa ngapi za namna hiyo zimefanyika kimya kimya ?
Siyo wote wako hivyo japo wengi wanaamini mwanamke ni kiumbe dhaifu. Omba usimkute ni mwenye hasira.Hawa ndio wale kina Vita ni Vita Muraaaa.Jaman kuna mura mmoja hapa mjin nishaingia mkenge nina mimba yake basi km mambo yenyewe ndio haya nijipange tu.
Sherehe gani ilkkosa hata mpigapicha wa simu, isijekuwa wamebambikiwa kesi haoJeshi la Polisi Mkoa wa Mara linawashikilia watu saba, wakiwamo wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi Kitarungu Wilayani Sereni kwa tuhuma za kuhusika kufanikisha ndoa ya wanafunzi hao wenye umri wa miaka 12 na 16 kinyume cha sheria.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Longinus Tibushubwamu alisema watu hao wamekamatwa cha Getarungu baada ya polisi kupata taarifa za kiintelijensia.
Alisema nyumbani kwa wazazi wa bwana harusi' kulikokuwa na sherehe za ndoa. Aliwataja katika tukio hilo lililotokea wilayani Seren katika Kijiji polisi walifika wanaoshikiliwa Aprili 2 kuwa ni Nyang'ombe Magere (50) na Ghati Masero (38) ambao ni wazazi wa mtoto wa kiume aliyekuwa anaozwa.
Mwingine anayeshikiliwa ni Kibaki Rioba (23) mkazi wa Sirari Wilaya ya Tarime pamoja na watoto wenye umri wa miaka 12 na 16 waliokuwa wanaoana.
Polisi pia inamshikilia msimamizi wa ndoa hiyo batili kwa upande wa mwanamume ambaye pia ni mtoto mwenye umri wa miaka 10 (jina limahifadhiwa), darasa la pili Shule ya Msinggi Kitarungu," alisema Kamanda Tibushubwamu.
Akizungumza kwa sharti la kuhifadhiwa jina lake, mkazi mwanafunzi wa Kijiji cha Kitarungu alisema wazazi wa mtoto wa kike (16) anayesoma darasa la saba walipokea mahari ya ng'ombe Sita kutoka upande wa mwanamume ambaye ni mwanafunzi (12) wa darasa la nne.
Alisema baada ya wazazi wa mtoto wa kike kupokea mahari, walimkabidhi binti yao kwa mume wake mtarajiwa, maandalizi ya sherehe yakaanza nyumbami kwao mwanamume.
"Baada ya taarifa hizo kufika polisi, askari walivamia sherehe hiyo na kuwatia mbaroni watuhumiwa," alisema mtopa taarifa huyo.
Juliana Kobiro ambaye ni mdau wa haki za watoto mjini Musoma alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kuchukua hatua za haraka kudhibiti uvunjifu wa sheria na haki za watoto ulio karibia kufanyika, huku akiomba wahusika wote wachukuliwe hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine.
Chanzo: Mwananchi
Esther Bulaya ana kazi ya kuwafunda wananchi wake.Ni kweli unaweza kuona hapo tu ni mfano mmoja,watu wana viburi hatari,Pro.mmoja wa kutoka huko alikuwa anatukana, anabeza anavyojisikia kisa amesoma.
Miradi mingi inakwama si kwasababu hakuna watendaji bali ni ushirikiano hafifu kutoka kwa jamii.
Kuna sehemu nimeona wamechimbiwa kisima cha maji masafi wakajenga miundombinu mizuri, utaratibu ukawekwa kwamba walipie ndoo shs 50 ili wapate pesa ya kununulia luku.
Cha ajabu baadhi ya akina mama wakakataa eti hawajazoea kuchota maji kwa kulipia bora waende wachote maji ya madimbwi tena wanayasafiria mbali.
Serikali na asasi za kiraia zijikite kutoa elimu jamii ili kuwakomboa hawa. Vitendo vya ukeketaji navyo vimeshamiri katika jamii zinazokeketa kama siyo wanaongoza hapa Tanzania basi ni miongoni mwa mikoa iliyo na idadi kubwa ya wanawake wanaokeketwa.
Muraaa acheni ubabe kwenye vitu vya kuleta maendeleo, nyinyi ni wachapakazi wazuri , mkoa wenu mzuri sana mtaufanya watu wasiwe wanakuja kwenu kwa kuogopa kupewa vitasa na sime.
Kabisa mkuu!Esther Bulaya ana kazi ya kuwafunda wananchi wake.
warudi kwenye sheria ya ndoa,halafu waje ktk sheria inayomlinda mwanafunzi.ItafahamikaJeshi la Polisi Mkoa wa Mara linawashikilia watu saba, wakiwamo wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi Kitarungu Wilayani Sereni kwa tuhuma za kuhusika kufanikisha ndoa ya wanafunzi hao wenye umri wa miaka 12 na 16 kinyume cha sheria.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Longinus Tibushubwamu alisema watu hao wamekamatwa cha Getarungu baada ya polisi kupata taarifa za kiintelijensia.
Alisema nyumbani kwa wazazi wa bwana harusi' kulikokuwa na sherehe za ndoa. Aliwataja katika tukio hilo lililotokea wilayani Seren katika Kijiji polisi walifika wanaoshikiliwa Aprili 2 kuwa ni Nyang'ombe Magere (50) na Ghati Masero (38) ambao ni wazazi wa mtoto wa kiume aliyekuwa anaozwa.
Mwingine anayeshikiliwa ni Kibaki Rioba (23) mkazi wa Sirari Wilaya ya Tarime pamoja na watoto wenye umri wa miaka 12 na 16 waliokuwa wanaoana.
Polisi pia inamshikilia msimamizi wa ndoa hiyo batili kwa upande wa mwanamume ambaye pia ni mtoto mwenye umri wa miaka 10 (jina limahifadhiwa), darasa la pili Shule ya Msinggi Kitarungu," alisema Kamanda Tibushubwamu.
Akizungumza kwa sharti la kuhifadhiwa jina lake, mkazi mwanafunzi wa Kijiji cha Kitarungu alisema wazazi wa mtoto wa kike (16) anayesoma darasa la saba walipokea mahari ya ng'ombe Sita kutoka upande wa mwanamume ambaye ni mwanafunzi (12) wa darasa la nne.
Alisema baada ya wazazi wa mtoto wa kike kupokea mahari, walimkabidhi binti yao kwa mume wake mtarajiwa, maandalizi ya sherehe yakaanza nyumbami kwao mwanamume.
"Baada ya taarifa hizo kufika polisi, askari walivamia sherehe hiyo na kuwatia mbaroni watuhumiwa," alisema mtopa taarifa huyo.
Juliana Kobiro ambaye ni mdau wa haki za watoto mjini Musoma alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kuchukua hatua za haraka kudhibiti uvunjifu wa sheria na haki za watoto ulio karibia kufanyika, huku akiomba wahusika wote wachukuliwe hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine.
Chanzo: Mwananchi