Familia yangu Mke na Mtoto wangu Mkubwa wamepata tatizo la Akili naomba ushauri wakuu

Familia yangu Mke na Mtoto wangu Mkubwa wamepata tatizo la Akili naomba ushauri wakuu

Mungu niguse

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2024
Posts
272
Reaction score
729
Habari wanaJF .

Kiufupi Mimi Baba wa watoto watatu ambao wote ni wa kike.

Naishi nao pamoja na Mama yao .

Tumefanikiwa kuishi miaka 12 mpaka sasa katika ndoa yetu.

Changamoto kubwa ambayo ninaipitia ni hii hapa.

Mimi kazi yangu kubwa ambayo huwa nafanya ni kuuza mazao , kuku wa kienyeji huwa naenda kijijini naangalia bei ndogo ya bidhaa Kama mahindi au kuku nanunua na kuja kuuza mjini.

Kiufupi Mimi ni mjasiriamali wa kiwango cha chini ambaye bado napambana.

Jambo Ambalo limenifanya nije ni changamoto iliyompata mke wangu na watoto.

Familia yangu ilikuwa vizuri Ila ilianza kuingia changamoto ambazo zimeniumiza Sana Akili na kunipa mawazo.


Mwezi wa kumi Mke wangu alianza kuumwa kawaida kabisa nikampeleka hosptali kumpima ikaonekana hana tatizo .

Ila nikikaa nae usiku halali anaongea mambo Kama ya kuchizika Anapasua vitu ndani .

Sasa nikaona hii hali itakuwa mbaya nimempeleka hosptali zote za mkoa Government na private Ila tatizo lipo pale pale .

Napoandika hapa mke wangu amefungiwa ndani , sasa hii hali Kama ya Mke wangu imeanza kumungia mtoto wangu wa kwanza Ana umri wa miaka 10 anaongea peke yake anaharibu vitu ndani .

Akikaa kidogo na wadogo zake wanapigwa kipigo kikali Sana hivyo mtoto na mama yao ambaye ni mke wangu ni Kama wanaumwa ugonjwa unaofanana.

Nimefatilia Sana katika familia zetu kujua Kama kuna mtu amewahi kupitia hali Kama hii sijafanikiwa kupata majibu.

Baada ya yote haya nimeamua nisafiri nimpeleke hosptali inaitwa milembe ipo Dodoma nimpeleke Mama na mtoto wawafanyie uchunguzi.

Wakuu naumia Sana Kazi haziendi mtaji umekata .

Ikiwa kuna wadau wanaweza nisaidia 400K nikapata nauli na kumsafirisha huyu Mama na binti yetu nitashukuru , Endapo nikifika Dodoma gharama zikahitajika zaidi nafikiria pia kuuza kiwanja ambacho nilikinunua Kwa ajili ya ujenzi.

Mrejesho

Wakuu nashukuru Kwa ushauri wenu mpaka sasa niseme nitaufanyia Kazi kadri nitakavyojaliwa.


Pia nimeona nianze na hii hatua ya maandalizi ya kumpeleka mgonjwa Dodoma yeye na Binti yetu pale Milembe , nitafanya huduma za hosptalini Ila pia sitoacha kumuombea kila siku.

Ikiwa unataka kuwasiliana na Mimi au Kwa chochote Ni-PM.

Pia nina kiwanja Heka moja ni kiwanja kipo katika muundo wa shamba ninakiuza ili pia kinisaidie katika hiki kipindi .

Gharama ya kiwanja ni maelewano kipo Katoro Bukoba Vijijini (Kagera)

Mungu awabariki nyote.🙏🏽

Mrejesho:
- Mrejesho changamoto ya Mke wangu ambaye alionekana kuwa na shida ya ugonjwa wa akili yeye na binti yetu mkubwa
 
Back
Top Bottom