Familia yangu Mke na Mtoto wangu Mkubwa wamepata tatizo la Akili naomba ushauri wakuu

Pole sana


Elekea kwenye MAOMBI.

NA PIA
Je, umechepuka popote pale au niulize na umemchezea mwanamke ukamuumiza

Au pia kudhulumu mtu kwenye BIASHARA?

Nauliza tu kutokana na kujifunza kusoma ya humu JF ya wadau.
Lakini inaweza kuwa vise versa, kwamba mke amechepuka na mme wa mtu (ingawa hakuna mme wa mbwa), sasa aliyenyang'anywa mme akaamua kulilipia! Dunia hii ni hatari sana!
 
Pole sana! Hayo ni mapepo. Tafuta Padre wa Kikatoliki atakusaidia Bure
 
Sio Kazi Yake Jamaa Kasema Anajitolea Kumpeleka Bure Wasiwasi Wa Nini?

Ninachohofia Isije Jamaa Anataka michango Badala Ya Tiba.
Sasa kama sio jukumu lake kumpeleka sehemu sahihi huko kujitolea kumpeleka kutakuwa na maana gani wakati siku hizi waganga wamejaa kila kona wapo hadi mitandaoni.
 
Mnaongea tu uwepo wa So called mungu na shetani ila hamna uwezo wa kuthibitisha uwepo wake zaidi ya porojo tu .
Sio lazima kuthibitisha mkuu, unamthibitishia nani na ili iweje? Mtu unaishi na watu unawaita wazazi na hujawahi kutaka uthibitishe kama wazazi wako kweli waliyo kuzaa ila maisha yanaendelea sasa huku kutaka kuthibitishiana Mungu sijui majini ndio ili iweje?
 
Pole sana mkuu, nimeumia utafikiri limenipata mm, jamani matatizo yaskie tu kwa mwenzie acha kabisa.
 
Sasa kama sio jukumu lake kumpeleka sehemu sahihi huko kujitolea kumpeleka kutakuwa na maana gani wakati siku hizi waganga wamejaa kila kona wapo hadi mitandaoni.
Sijakuelewa.
 
Sasa kama sio jukumu lake kumpeleka sehemu sahihi huko kujitolea kumpeleka kutakuwa na maana gani wakati siku hizi waganga wamejaa kila kona wapo hadi mitandaoni.
Sijakuelewa.
 
Uishipo tambua utepe mwembamba utenganishao utabibu na ulozi.Kabla ya kwenda Milembe tembelea wataalam wa tiba asili wafanye vipimo.Hii itakuongoza hatua ya pili.
 
Unaposema jambo hili ni kweli na hakika mimi binafsi nitaomba uthibitisho wa huo uhakika na kweli.
 
Sijakuelewa.
Yani waganga wako wengi sana siku hizi wapo hadi mitandaoni hivyo ukiona mtu anakwambia akupeleke kwa mganga basi maana yake anamjua huyo mganga si tapeli na fundi hasa.
 
Unaposema jambo hili ni kweli na hakika mimi binafsi nitaomba uthibitisho wa huo uhakika na kweli.
Ushawahi kumuomba mtu akupe uthibitisho wa watu anaowaita kuwa ni wazazi wake waliyomzaa? Au huo uthibitisho unaudai kwa wenye kusema kuna Mungu tu?
 
Ushawahi kumuomba mtu akupe uthibitisho wa watu anaowaita kuwa ni wazazi wake waliyomzaa? Au huo uthibitisho unaudai kwa wenye kusema kuna Mungu tu?
Uthibitisho wa namna hiyo uombe wewe mkuu mimi naomba Uthibitisho wa uwepo wa Mungu
 
Hali kama hiyo imemtokea mwinjilist flani
West kilimanjaro
Mke na mtoto wa pili nadhani wa kike
Mpaka wa leo
 
Unahitaji maombi na hayo yote yatakwisha.
Karibu sana kanisani kwetu.
 
Uthibitisho wa namna hiyo uombe wewe mkuu mimi naomba Uthibitisho wa uwepo wa Mungu
Umesema mtu akidai jambo fulani ni kweli na uhakika unamdai uthibitisho, sasa ajabu unadai uthibitisho wa Mungu na majini tu mbona hudai uthibitisho kwa vitu vyengine ambavyo watu hudai ni kweli na uhakika ila bila uthibitisho?

Ndio maana nasema hakuna haja ya kuthibitisha uwepo wa Mungu kama ambavyo ilivyo kwa mambo mengine hatuoni watu kudai uthibitisho na maisha yanaendelea. Sasa kwa sababu wewe una mtazamo wako wa kudai hakuna Mungu ndio maana unashughulishwa na kudai uthibitisho wa kuwepo Mungu.

Vitu vyengine simple tu wewe kama haukubaliani na habari za uwepo wa Mungu unaachana nazo haina haja ya kutaka kulazimisha watu et wathibitishe.
 
Mkuu pole sana hiyo n mitihani ya dunia na hujafa hujaumbika mimi mwaka 2017 nilipia mtihani kama kama huu mdogo wangu akiwa form three alianza kama kuwehuka hivi tukahisi labda balehe lakni hali ikawa mbaya zaidi alianza kukimbia hovyo na hata kuanza kusalua nguo zake.
Baada ya hapo tulimpeleka hospital zaid n zaidi alikuwa anapigwa sindan za usingz n minyororo asee narudia huu usemi usemao.
"CHIZI ANACHEKESHA KAMA SIO NDUGU YAKO" kwa hali aliyokuwa nayo mdg wangu kila nkimuona na minyororo niliishia kutokwa na machozi.
Katika kuongea na watu nikakutana na mtu kutoka rorya akanambia kuhusu dhehebu moja linalopatikana huko wanaitwa ROHO hawa wanasali jumamos na wanavaa majoho meupe. Akanambia wanaweza nisaidia nili safiri kutoka moro tena ndani ndani huko mpka rorya sehm moja unashukia mika sijui nyasoro kama sijakosea
Mdg wang akaanza kuombewa hawa wanaomba kwa kilugha.
Asee pale n maombi saa tisa alasir maomb saa sita mchana saa tisa alasiri na saa tatu mpka akapona kabsa na sasa yupo kwake .
Ushauri wang kuna hali fulani ukiona jarbu kuangalia njia mbadala sema kupata wa kweli ndio ishu na lazima uwe vizur kiuchumi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…