Fanani wa Hard Blasters apelekwa Sober House Bagamoyo

Fanani wa Hard Blasters apelekwa Sober House Bagamoyo

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,515
Reaction score
28,506
Rapper wa kundi la zamani la muziki wa Hip Hop, Hard Blaster Crew ‘HBC’ Terry Fanani apelekwa sober house Ijumaa hii ili kuachana na matumizi ya Madawa ya kulevya.

Rapper Kalapina ambaye ni mmoja kati ya wanaharakati wa kupambana na Matumizi ya madawa ya kulevya, jana alipost picha akiwa sober house na kuandika:

Jana baada ya kumfikisha sober house mkongwe katika Hip Hop, Terry Fanani wa kundi la HBC tumuombee kwa Mungu amjaalie aweze kupona na kurudi katika hali yake kama zamani ni harakati umaarufu bila dawa za kulevya inawezekana.

Baada ya kumfikisha Terry Fanani Sober House jana muasisi wa kundi la Hard Blaster Crew ‘HBC’ ni harakati zinaendelea kuhakikisha ndugu zetu wanapona maradhi ya kuwa utegemezi dhidi ya dawa za kulevya mungu mkubwa na mjuzi na mwenye hekima #kalapinafoundation.

Fanani ni mmoja wa waasisi wa kundi la HBC ambalo lilimtoa pia Professor Jay enzi hizo akijiita Nigger Jay.
xFanani-Witness-pamoja-na-Kalapina-wakiwa-Snnober-House.jpg.pagespeed.ic.ifZKd7vfZA.jpg
 
Tatizo la uteja... haina dawa, labda miungu na mizimu iingilie kati. Akitoka sober house... miezi 3 mingi anarudia. Kwa wewe ambaye hujaanza kutumia... please.... USITHUBUTU kujaribu for whatever reason.
 
Terry aliacha madawa muda Mrefu na alikuwa muumini pale kwa kakobe sijajua karudia madawa au ni kiki
All in all goodluck
Mnaosema jay anamjali hamjui mnachosema tery anakuwa maskani kigogo mwisho Mara nyingi anadaka kutoka kwa makonda Wa daladala
 
Clouds FM ni jipu lisipotumbuliwa litaleta madhara makubwa daz baba mbona hawampeleki na dullayo nae ndo anakoelekea stress za music zinawaumiza Sana hawa wasanii
 
Clouds FM ni jipu lisipotumbuliwa litaleta madhara makubwa daz baba mbona hawampeleki na dullayo nae ndo anakoelekea stress za music zinawaumiza Sana hawa wasanii
Clouds Fm wanaingiaje hapa?
 
Clouds FM ni jipu lisipotumbuliwa litaleta madhara makubwa daz baba mbona hawampeleki na dullayo nae ndo anakoelekea stress za music zinawaumiza Sana hawa wasanii
Mzee wa naumia rho nae kaingia kwenye unga?[emoji26][emoji26][emoji26][emoji26]
 
Back
Top Bottom