Fanya haya kuifanya sound system yako idumu kwa muda mrefu

Fanya haya kuifanya sound system yako idumu kwa muda mrefu

Nje ya mada kidogo mkuu Kuna subufa nimeifungia mp3 lakin inakoroma/inavuma Sana solution nini hapa
Chukua waya nene mfano wa 4mm
Unga kwenye ground ya power supply na pale kwenye ki bati cha frash(ground!)
 
Chukua waya nene mfano wa 4mm
Unga kwenye ground ya power supply na pale kwenye ki bati cha frash(ground!)
Mkuu nashukuru nimefanya hivyo nimefanikiwa kwa kiasi japo bado sound sio quality Kama mwanzo

Kama Kuna mbinu zaidi naomba tafadhali

Pia nifunge kifaa gani ili kupunguza kidogo bass
 
Mkuu nashukuru nimefanya hivyo nimefanikiwa kwa kiasi japo bado sound sio quality Kama mwanzo

Kama Kuna mbinu zaidi naomba tafadhali

Pia nifunge kifaa gani ili kupunguza kidogo bass
Ntumi namba zako dm mkuu
 
Mkuu nashukuru nimefanya hivyo nimefanikiwa kwa kiasi japo bado sound sio quality Kama mwanzo

Kama Kuna mbinu zaidi naomba tafadhali

Pia nifunge kifaa gani ili kupunguza kidogo bass
Sio quality kama mwanzo kwa maana gani?
Yaan baada au kabla ya kuweka hiyo mp3
 
Naishi fresh JBL flip 5 yangu

Mungu akijalia niivute Charge 5

Nikitoka nichukue JBL soundbar Dolby Atmos sound
 
Habari ya wakati
Natumaini tuko salama

Fanya haya ili subwoofer yako na sound system yako idumu kwa muda mrefu
[emoji1314] usichajie simu sehemu ya kuchomeka frash disk

Sababu hi imekua ndio sababu kuu ya kuuwa system ya frash ya watu wengi zaidi Ile haikutengenzwa kwajiri ya kuchajia bali kuchomeka frash peke. Na hi sio kwenye subwoofer pekee bali hata DVD players
[emoji1314] usiongeze speaker nyingine zaidi ya zile zilizokuja na system yako

Mara zote redio inapotengenezwa hua inatengenezwa kusukuma speaker za kiwango husika
Unapoongeza za kwako bila ya kua na kipimo maalumu au kiwango cha ukinzani wa coil ya speaker yako (ohms) KUNAUWEZEKANO wa kusababisha uharibifu wa system yako.

Sikukatazi kufanya hivyo ila kwanza elewa kiwango cha ohms kinachotakiwa na system yako kisha elewa kiwango cha ohms cha speaker zako zote kabla ya kuziunganisha na sound system yako
[emoji1314] usipende kuweka sauti kubwa sana kwa muda mrefu na mara kwa mara.

Hii inawahusu zaidi wenye subwoofer za mchina.

Hii itakusaidia kuifanya subwoofer yako iishi kwa muda mrefu zaidi.

Hii inawahusu wenzangu na mimi wa birthday na vipaimala[emoji16].

Kwa faida yako tu ni kuwa.

Unapoongeza sauti kwenye redio yako tafsiri yake ni kua unaruhusu umeme mwingi kutoka kwenye amplify yako na kwenda kwenye speaker.

Hivyo ongezeko la joto hupanda zaidi kwenye baadhi ya components zinazounda circuit za subwoofer yako (components zinazounda circuit ni vitu vote kiujumla vinavyounda ramani, kadi, mashine ya system yako).

Hivyo unapoifungua kwa sauti kubwa kwa muda mrefu zaidi ni kua ile joto inakuwepo humo kwa muda mrefu.

Kumbuka kua subwoofer nyingi kama sio zote hazina mfumo mzuri wa kupooza (feni)

[emoji1314] Kwa namna yoyote jitahidi mende, panya wasiingie ndani ya system yako
Sababu mkojo wao huweza kutengeneza short ya components.

Hii ni kwa wale wanaotumia home theater na subwoofer hizi za kisasa

Pia panya hula waya na speaker.

Hivyo unatakiwa kuzilinda kwa namna yoyote utakayoiweza

[emoji1314]tumia voltages stabilizer kulinda vifaa vyako vya kielecronic.

Hii sio kwenye sound system pekee.

Bali vifaa vyako vyote vinatakiwa kulindwa na stabilizer.

Stabilizer za kisasa huweza kujizima zenyewe pindi umeme unapokua juu au chini ya kiwango.

Na zipo nyingine zinabalance bila ya kuleta hitilafu ya vifaa vyako

Kwa leo ni hayo tu

For additional
Ili kupata sound safi (bass nzuri) usiweke subwoofer yako juu ya meza au stool au sehemu itakayoitenga mbali na floor

Itakupa good sound ikiwa on floor

View attachment 2368030


K’phin.
Unapoongeza spika ni lazima pia uongeze amplifier kwa sababu ya hizo spika za ziada.
 
Back
Top Bottom