FARAGHA: Waziri amwagiza Mganga Mkuu wa Serikali kufuatilia suala la Taarifa Binafsi za Mgonjwa kuanikwa Mtandaoni

FARAGHA: Waziri amwagiza Mganga Mkuu wa Serikali kufuatilia suala la Taarifa Binafsi za Mgonjwa kuanikwa Mtandaoni

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Kufuatia tukio la mwanaume mmoja anaesemekana kuwa na mataizo ya akili kukata uume wake, ambapo toka tukio hilo limetokea mpaka baada ya matibabu waandishi wametoa taarifa zote juu ya hali yake, ikiwemo jina, umri, jinsia, makazi na ugonjwa wenyewe.

mgonjwa.jpg
mgonjwaa.jpg

Wadau mbalimbali wamelalamikia kitendo cha Taarifa Binafsi za mgonjwa huyo kuanikwa mtandaoni kwa kukiuka Sheria na miongozo ya taaluma za afya ambapo Faragha ya mgonjwa inatakiwa kulindwa na kuheshimiwa, lakini pia inaenda kinyume na Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ambayo imeanza kutumika tangu Mei 1, 2023

Kwa mujibu wa Kifungu cha 25, Kifungu kidogo cha 2 cha Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kinaeleza jinsi uchakataji wa Taarifa Binafsi unavyotakiwa kufanywa endapo taarifa hizo zitatumiwa kwa madhumuni mengine tofauti na madhumuni yalilokusudiwa, ambapo kifungu kidogo 2 (d) kinasema mchakataji ataweza kutumia Taarifa Binafsi kwa matumizi mengine kwa namna ambayo muhusika hatambuliki.

Screenshot 2023-07-13 104754.png

Wachakati wa Taarifa Binafsi wanatakiwa kuelewa Sheria vizuri, na ndio maana Serikali inatakiwa kutoa kipindi cha mpito kwa taasisi, makampuni na watu binafsi wanaoathiriwa na Sheria hii kuelewa vizuri kabla ya matumizi rasmi kuanza.

Kutokana na madhara yanayoweza kutokea, Wadau walipendekeza Serikali itoe Kipindi cha Mpito kwa wote wanaoathiriwa na Sheria hii ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ili kuendana na mabadiliko yaliyokuja na sheria hii.
 
Habari wakuu,

Nimeona taarifa mahali kuwa yule daktari aliyetoa taarifa ya mgonjwa kukiona.

Hii ni baada ya habari hizi kumfikia Waziri wa Afya Ummy Mwalimu na kutoa tamko kuwa afuatiliwe.

Pia amesema achukuliwe hatua stahiki za kisheria...


Nb: Je, taarifa zetu wagonjwa zipo salama kwa madaktari?
 
Watu bhn hizo taarifa zimeanza kutolewa na waandishi wenyewe tangu tukio lilipotokea,wangeanza na waandishi wa habari kwanza.Sijaona kosa la daktari,tafuteni mambo ya muhimu ya kufanya
 
Wewe huelewi miiko ya kitaaluma ya Madaktari!
Jina, umri, ugonjwa vyote vinajulikana kutoka mtaani, ama kosa la Dr ni kusema hawezi tomber tena ? Kwan hii inahitaji elimu ya chuo kujua? maana mtu kajikata uume na wote umetoka nani asiyejua kwamba hakuna uwezekano wa kushiriki tena tendo la ndoa?
 
Watu bhn hizo taarifa zimeanza kutolewa na waandishi wenyewe tangu tukio lilipotokea,wangeanza na waandishi wa habari kwanza.Sijaona kosa la daktari,tafuteni mambo ya muhimu ya kufanya
Kosa lake kuelezea mambo ya mashine yake kutofunction tena hapo ndo alipoharibu angesema mgonjwa anaendelea vizuri ingetosha
 
Wameshuhudia wachache waliomuona baharini lakini taarifa zake zimetangazwa nchi nzima tumezijua
Ndio leno la waandishi wa habar kwaabarusha raia, sasa ww ulitaka tusijue? Kwan Kuna matukio mangapi umehabarishwa na hao hao waandishi wa habar?
 
Jina, umri, ugonjwa vyote vinajulikana kutoka mtaani, ama kosa la Dr ni kusema hawezi tomber tena ? Kwan hii inahitaji elimu ya chuo kujua? maana mtu kajikata uume na wote umetoka nani asiyejua kwamba hakuna uwezekano wa kushiriki tena tendo la ndoa?
Kenge wa kijani
 
Back
Top Bottom