Faraja: Matokeo Ya Ufugaji Wa Kuku

Faraja: Matokeo Ya Ufugaji Wa Kuku

nashukuru Jana nimefanikiwa kuanza ufugaji,nimeanza na vifaranga 10 vya wiki 3.

Hongera sana Kuku wa Kabanga, Nakutakia kila la Kheri Ndugu. Sijui kwanini imekuwa ngumu kupata ramani ya mabanda ya kuku. Ila nitajitahidi nitafute wahusika ili wanielekeze.
 
kulea vifaranga wala si tatizo. kwahao kuku wako banda la bati 3 za mita 3 au 2.5 litakutosha. PM namba yako nikuelekeze cha kufanya dhidi ya vifaranga na kama utakuwa karibu na nilipo naweza kukutumia kitabu (bule) bila malipo nilicho toa SUA

Habari za majukumu Mkuu,

Ukipata nafasi tufanyie ule mpango wa kitabu.
 
Hongera sana Kuku wa Kabanga, Nakutakia kila la Kheri Ndugu. Sijui kwanini imekuwa ngumu kupata ramani ya mabanda ya kuku. Ila nitajitahidi nitafute wahusika ili wanielekeze.

sielewi mnaposema mnataka ramani mbona sample zipo umu nyingi tu. Mfano unaweza google chicken huts/house pia kwa kiswahili utapata local. Kuna uzi uliwekwa na picha hadi cost, ni wewe kuwa mbunifu ukitumia nafasi, vifaa ulivyonavyo na idadi na aina ya kuku. Hakuna formula maana kila mtu ni unique ingawa kuna vitu muhimu kama hewa, sakafu na paa lisilovuja vingine unajazia vyako
 
sielewi mnaposema mnataka ramani mbona sample zipo umu nyingi tu. Mfano unaweza google chicken huts/house pia kwa kiswahili utapata local. Kuna uzi uliwekwa na picha hadi cost, ni wewe kuwa mbunifu ukitumia nafasi, vifaa ulivyonavyo na idadi na aina ya kuku. Hakuna formula maana kila mtu ni unique ingawa kuna vitu muhimu kama hewa, sakafu na paa lisilovuja vingine unajazia vyako


Mama Joe upo Best??? Tumepotezana Sana ILA hakika Ni Mimi ndiyo mwa.na mpotevu hapa jukwaani.....wapi Ndugu yetu Kubota?
 
Last edited by a moderator:
Mama Joe upo Best??? Tumepotezana Sana ILA hakika Ni Mimi ndiyo mwa.na mpotevu hapa jukwaani.....wapi Ndugu yetu Kubota?

dah ulipotelea wapi best? Bunge la katiba? Maana naona ufugaji ulitupa kule hahaa. Sisi tupo bado tunapambana sasaivi nina Kenbro wa Reti wanakaribia kutaga. Karibu tena kundini. Kubota anazama na kuibuka mara chache sana sijui yuko wapi.
 
Last edited by a moderator:
dah ulipotelea wapi best? Bunge la katiba? Maana naona ufugaji ulitupa kule hahaa. Sisi tupo bado tunapambana sasaivi nina Kenbro wa Reti wanakaribia kutaga. Karibu tena kundini. Kubota anazama na kuibuka mara chache sana sijui yuko wapi.

Nakumbuka uzi wa Kubota ni moa wapo ya nyuzi zilizo nivutia kanza ufugaji wa kuku.
 
Nakumbuka uzi wa Kubota ni moa wapo ya nyuzi zilizo nivutia kanza ufugaji wa kuku.

ni kweli hata mimi uzi ule ndo ulinihamisha kutoka kuku wa kisasa kuja kwa chotara. Na sintarudi ni investment nzuri
 
Habari Mkuu!

Yaan leo hawa kuku nimeshindwa cha kuwafanya. Niliamka asubuhi sana kuenda kusafisha banda ile naingia Paaa... Hamad!! nakuta ndio wanaalizia yai nimeangalia banda Zima sijakuta hata masalia ya ute wa yai. Hapa ndipo nilipo pata jibu la Kwanini wiki hii sijapata mayai ya kutosha japokuwa kuna kuku wengine wawili wenye dalili kuwa wameanza kutaga.

Hapa najipanga kutengeneza chakula chenye choka ya kutosha tu, sijui kama itasaidia!

Kama kuna mbinu nyingine naombeni jamani maana wameniweza hawa viumbe wiki hii.Yaani mayai 8 kwa wiki!

Pole sana ni chokaa itakuwa pia madini ya chuma hivi, mi wangu huwa nawapa masaa kama matatu tu kila wiki wale nyasi. Nimepanda nyasi kibao kwa kweli sina mgogoro kabisa na ulaji wa mayai.
 
Njia nzuri ya kulea vifaranga ni IPI? Nimetengeneza sehemu ya kuwantunzia ila kuku mlezi niliyemchagua anawadonoa sasa.
Vipo 21,naweza wawekea taa? Mama Joe Malila GAZETI
 
Last edited by a moderator:
Njia nzuri ya kulea vifaranga ni IPI? Nimetengeneza sehemu ya kuwantunzia ila kuku mlezi niliyemchagua anawadonoa sasa.
Vipo 21,naweza wawekea taa? Mama Joe Malila GAZETI

Sikia, inaonekana wakati unampa awalee alikuwa anakuona. Majuzi mie kuku wangu alitotoa vifaranga sita akaacha mayai nane. Mie nikamchekiii nikaona sio kesi. Nikamuweka kwenye kachumba kadogo nikaweka msosi na maji.

Yale mayai nane nikamuwekea mwingine alikuwa na mayai 16 na ambaye alikuwa analalia karibu muda sawa na huyu wa kwanza. Mungu akajaalia juzi huyu wa pili ambaye alikuwa na mayai 24 sasa akatotoa vifaranga sita. Nikavibeba vyote nikamfata yule wa kwanza nikamchapa na ufagio akakimbia nje nikaweka vifaranga sita puu. Nikamfata nje namtolea macho kwa hasira nikamkimbiza atokomee mbali ili vifaranga wamlilie apate mzuka na kweli nikawasha fegi navuta pafu moja ya pili mara na yeye kacharuka kaja mbio balaa nikawa nacheka tu. Karuka hadi kwenye kakibanda kake akawakumbatia vifaranga wake mie kikuu na njia nawahi bar.

Jana tena nikaenda kwa yule aliyebakiza mayai 18 sasa nikakuta katotoa vifaranga 7 nikabeba kama kawaida, mie siwabembelezi na wao washajua wakiniona na mfagio wanakuwa wapole sana. Nikamfata yule wa kwanza tena kama kawaida kala wa mgongo paa kaona atakufa kakimbia nje, nikaweka tena vifaranga halafu nikamsikilizia nikaona anakuja spidi mie nikaenda zangu kuvuta fegi. Sasa hivi nina vifaranga hao 19 na huyu wa pili ana mayai 11. Asubuhi wakati nawapa matikiti na dagaa nimeona yule wa kwanza anaishi kwa amani kabisa na wanae.

Kamwe usimpe kuku vifaranga akiwa anakuona ataua wote. Na pia kaza sura wajue muda wa kazi ni kazi.

Pangu Pakavu.
 
Last edited by a moderator:
ni kweli hata mimi uzi ule ndo ulinihamisha kutoka kuku wa kisasa kuja kwa chotara. Na sintarudi ni investment nzuri

Mama Joe, Usiniambie umeachana na kuku wa kisasa! Nini tatizo/changamoto au faida ya chotara inazidi wale wa kisasa?
 
Pole sana ni chokaa itakuwa pia madini ya chuma hivi, mi wangu huwa nawapa masaa kama matatu tu kila wiki wale nyasi. Nimepanda nyasi kibao kwa kweli sina mgogoro kabisa na ulaji wa mayai.

Ahsante Mkuu, Nitapanda majani na bustani pindi nitakapo maliza ujenzi wa mabanda kwenye site yangu. Ila kwa sasa huwa nimeweka order ya mchicha siku tatu za wiki wanapata. Sijui kama nipo sahihi katika hilila siku tatu.
 
Sikia, inaonekana wakati unampa awalee alikuwa anakuona. Majuzi mie kuku wangu alitotoa vifaranga sita akaacha mayai nane. Mie nikamchekiii nikaona sio kesi. Nikamuweka kwenye kachumba kadogo nikaweka msosi na maji.

Yale mayai nane nikamuwekea mwingine alikuwa na mayai 16 na ambaye alikuwa analalia karibu muda sawa na huyu wa kwanza. Mungu akajaalia juzi huyu wa pili ambaye alikuwa na mayai 24 sasa akatotoa vifaranga sita. Nikavibeba vyote nikamfata yule wa kwanza nikamchapa na ufagio akakimbia nje nikaweka vifaranga sita puu. Nikamfata nje namtolea macho kwa hasira nikamkimbiza atokomee mbali ili vifaranga wamlilie apate mzuka na kweli nikawasha fegi navuta pafu moja ya pili mara na yeye kacharuka kaja mbio balaa nikawa nacheka tu. Karuka hadi kwenye kakibanda kake akawakumbatia vifaranga wake mie kikuu na njia nawahi bar.

Jana tena nikaenda kwa yule aliyebakiza mayai 18 sasa nikakuta katotoa vifaranga 7 nikabeba kama kawaida, mie siwabembelezi na wao washajua wakiniona na mfagio wanakuwa wapole sana. Nikamfata yule wa kwanza tena kama kawaida kala wa mgongo paa kaona atakufa kakimbia nje, nikaweka tena vifaranga halafu nikamsikilizia nikaona anakuja spidi mie nikaenda zangu kuvuta fegi. Sasa hivi nina vifaranga hao 19 na huyu wa pili ana mayai 11. Asubuhi wakati nawapa matikiti na dagaa nimeona yule wa kwanza anaishi kwa amani kabisa na wanae.

Kamwe usimpe kuku vifaranga akiwa anakuona ataua wote. Na pia kaza sura wajue muda wa kazi ni kazi.

Pangu Pakavu.

Mkuu Hossam, You Made my Day. Kumbe ufagio ni zaidi ya jela kwa kuku. Ha ha ha ha...
 
Njia nzuri ya kulea vifaranga ni IPI? Nimetengeneza sehemu ya kuwantunzia ila kuku mlezi niliyemchagua anawadonoa sasa.
Vipo 21,naweza wawekea taa? Mama Joe Malila GAZETI

kama mama keshajua sio wake itakuwa ngumu kuwafunika baridi usiku hivyo waweza kuwasha gai karibu au weka dumu au ndoo yenye maji moto ili wakilizunguka wanapata joto. Huyo mama umtoe tu huwa wanawaletea magonjwa
 
Last edited by a moderator:
Mama Joe, Usiniambie umeachana na kuku wa kisasa! Nini tatizo/changamoto au faida ya chotara inazidi wale wa kisasa?

changamoto ya kuku ni chakula na soko. Wale kisasa wanakula sana na hivyo faida yao wawe wengi, sasa tena kuwa wengi kama soko niliko limekuwa sio zuri na hiyo kula yao ni risk. Pili ikitokea umepata hasara waweza anguka mtaji maana unaanza moja na vifaranga wa kununua. Chotara ni dual purpose kama soko sio zuri waweza subiri huku unauza mayai pia hawali sana kama broiler. Pia waweza totolesha mayai yako kupata batch mpya. Broiler ukikosa soko unahesabu hasara kwa siku
 
changamoto ya kuku ni chakula na soko. Wale kisasa wanakula sana na hivyo faida yao wawe wengi, sasa tena kuwa wengi kama soko niliko limekuwa sio zuri na hiyo kula yao ni risk. Pili ikitokea umepata hasara waweza anguka mtaji maana unaanza moja na vifaranga wa kununua. Chotara ni dual purpose kama soko sio zuri waweza subiri huku unauza mayai pia hawali sana kama broiler. Pia waweza totolesha mayai yako kupata batch mpya. Broiler ukikosa soko unahesabu hasara kwa siku

Shukran Mama Joe,
Nimekupata vizuri, Ngoja nikomae kidogo nikikaa sawa nitainvest kikamilifu tu.
 
mi nilianza kufuga mwezi wa tano mwaka huu nikiwa na majike 8 na jogoo 1. Kwa sasa nina kuku 63 na majike matatu wanalalia jumla ya mayai 38 natarajia kupata vifaranga vipya mwezi ujao mapema. Nina plan ya kufikisha kuku 200 by december. Eneo no dogo so nina plan ya kununua ekari 2 nipanue business. Siri ya kuwa na kuku wengi ni kuwanyang'anya vifaranga majike wanaototoa kwa pamoja na kuwatia jela siku mbili wakitoka huko ni msosi tu. Baada ya wiki 2 anaanza kazi tena.

mpendwa mungu awabariki sana kwa kuthubutu, na mimi nipo nyuma yenu, nina eneo langu limekaatu sasa nafikiria kuliwekeza kwenye kilimo cha shamba kuku. Mbarikiwe sana kutoka ni malengo na mipango ndugu zangu. Mungu atupe uzima na hekima ya kutenda kwa maarifa yake.
 
Back
Top Bottom