Father Dkt. Kitima: Tunakubaliana na Rais Magufuli kwamba tumuombe Mungu na tuchukue tahadhari za kisayansi dhidi ya Covid 19

Acha mawazo mfu, ugonjwa huu anaweza kukuletea mtoto wako kutoka huko shuleni alipochangamana na watoto wenzie kutoka familia zisizojilinda.

Vita ya Taifa zima haiwezi kupiganwa kwa mafanikio kama hakuna jitihada ya pamoja. Sasa uadhani nani ana power na resources za kucoordinate jitihada hizo zaidi ya serikali?
 

Dk. Charles Kitima ni padre na mwalimu wa sheria na Katiba aliye na elimu ya uzamivu.

Akisema kuwa "ni vema wananchi wakachukua tahadhari zote za kisayansi dhidi ya ugonjwa wa Corona huku wakimtanguliza Mungu mbele" ni sawa. Anacho kibali cha kikatiba cha kuyasema hayo.

Lakini kauli yake kwamba wao "wanakubaliana na tamko la Rais Magufuli kwamba wananchi wamwombe Mungu bila kuacha kuchukua tahadhari za kisayansi dhidi ya ugonjwa wa Corona" inayo dosari kubwa kisheria.

Rais wa nchi ambayo inaongozwa na Katibu isiyofungamana na dini yoyote hana kibali cha kikatiba cha kumruhusu kutoa tamko kwamba "wananchi wamwombe Mungu."

Kwa kauli hii Rais anakuwa anavunja Katiba ya nchi. Na kina Kitima wakisema kuwa "wanakubaliana na tamko la Rais" wanakuwa wanakubaliana na uvunjaji wa Katiba ya nchi.

Kwa hiyo, Dk. Charles Kitima anataka tuamini kuwa sasa Kanisa Katoliki limeachana na tabia yake ya kuheshimu Katiba ya nchi?

Ni swali la udadisi tu.
 
Mungu hana dini binadamu ndio wenye dini.

Tunaimba katika wimbo wa taifa " Mungu ibariki Tanzania "

" Mungu wabariki viongozi wetu"
 
Mungu hana dini binadamu ndio wenye dini.

Tunaimba katika wimbo wa taifa " Mungu ibariki Tanzania "

" Mungu wabariki viongozi wetu"

Maswali matatu:

1. Mungu yupi asiye na dini? Yehova? Allah? Luhanga? Ng'ombe wa Wahindi?

2. Wimbo wa Taifa ni sehemu ya Katiba na sheria za nchi?

3. Maneno MUNGU, SALA, MAOMBI, MAOMBEZI, MISA na IBADA ni misamiati ya kiserikali hapa Tanzania?
 
Kosa kubwa lililofanywa na utawala ni kushindwa kutoa tamko kitaifa la kurudi kwa corona wakiamini watu wata hofu. Watu wengi wanajua, lakini pia kuna kundi la watu wengi zaidi (mbumbumbu) ambao bila kusikia kiongozi katamka, hawaamini. Nao ndio wapokea na wasambazaji wakubwa. Ndio wanao sombwa kwenye malori kufikisha nyomi ya mikutano ya waheshimiwa.
 
Kama TAG wameshatupa tuzo ya kuishinda corona kupitia maombi matamko ya nini tena
Uelewa wetu ndio kikomo hapo. Watashindwaje kutoa tuzo ilhali juzi ndugu zao wametoka kwa sangoma na maiti ya mwenzao aliekufa kwa kushindwa 'kupumua' na sangoma akawambia alikabwa na jini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…