Fatma Karume: Kelele, ubabe na mabavu siyo ushahidi kwamba Dkt. Tulia Ackson ni jasiri

Uyu Mama vile baba yake alimuingiza tiss ndio anajiona anajua kila kitu kuliko wengine..

Laana ya kumtukana Magufuli itamuandama daima..

Yaani uwa haelewi nini anataka!!
Huyu Fatma ni great brain. Hakika alichokisema ndiyo uhalisia. Wasioliona hilo lazima kichwani kumeyumba.

Tulia alikosa hekima kabisa katika kujibu alichoulizwa. Kipindi chake kikiisha atatupiliwa mbali na hataweza kuigusa nafasi yoyote ya kimataifa labda iwe ya kuteuliwa na Tanzania. Alijisahau, akadhani anaongoza lile bunge lake uchwara, la akina kibajaji na musukuma.
 
Nimependa mfano wa panya. Tunasubiria hapa paka afanye yake.
 
Kuna kaujinga fulani kanawaandama wateule wa.mama.eti wanaweza bila hao majamaa wakati wao wenyewe hawawezi!

Aloewaweza mabeberu ni jpm tu,coz alikua IQ kubwa sana halafu alikua natural reader!

..Jpm aliwaweza vipi mabeberu wakati wao ndio waliomtengenezea kidubwasha cha mapigo ya moyo?

..Na ilivyoshindikana kukibadilisha unafahamu nini kilimtokea?
 
I am no fan of Tulia.

Ila napata hisia za Fatuma za wivu juu ya Tulia.

Hapo anataka ni yeye ndie angekuwa hapo.
 
πŸ’―
 
Waliuliza maswali ya kipumbavu na kashfa, naye akawajibu kibabe hivyohivyo...sio kila wakati utaweka ustaarabu mbele, maswali waliyouliza walijua majibu yake - itakuwa walifikiri akili yake ni ndogo sana asiwaelewe..dawa na moto ni moto.
 
Waliuliza maswali ya kipumbavu na kashfa, naye akawajibu kibabe hivyohivyo...sio kila wakati utaweka ustaarabu mbele, maswali waliyouliza walijua majibu yake - itakuwa walifikiri akili yake ni ndogo sana asiwaelewe..dawa na moto ni moto.
Dawa ya πŸ”₯ ni πŸ”₯
 
Wivu tu kwa mwanamke mwenzake. Yeye hata hayo makelele mbona hajawahi kuyafanya.? Mwanasheria wa mitandaoni tu hana cha maana.
 
Heheheh nimependa sana nikweli na amesha haribu picha keep cool mtasikia
 
Tulia ni msomi ambaye hajaelimika na anayetegemea uchawa ili aendelee kula . Hata tofauti na wale machawa wengine ambao hawajawahi kanyaga darasani. Ni tofauti sana na Prof. Ndalichako.
 
Sio sawa amewafokea wabunge jambo sio sawa kwa maadili yake. Mbaya kuliko yote usifikiri wazungu hawajuwi habari zake nakile anakifanya ndio maana aka panic tulia muone aibu hii
 
Acha ujinga, kwani hao wazungu wa America wanajikuta wao kina nani wasiambiwe ukweli?

Unadhani Tulia bila cheyo cha IPU maisha hawezi?

Kawachana vema sana, sasa wewe na huyo mzungu pori fatuma wako, endeleeni kuwaabudu hao wazungu wenzenu
Nyie mbona mnamuabudu chura kiziwi ambaye hana hata darasa Moja na hajui hata anchokifanya zaidi ya utekaji na kuua!?
 
Uyu Mama vile baba yake alimuingiza tiss ndio anajiona anajua kila kitu kuliko wengine..

Laana ya kumtukana Magufuli itamuandama daima..

Yaani uwa haelewi nini anataka!!
Hakuna atakayelaaniwa kwa kumtukana Magufuli!!! Sanasana atabarikiwa tu. Lile DUBWASHA dhulumati na liuaji halina utukufu wowote wa kutoa laana
 
Sio sawa amewafokea wabunge jambo sio sawa kwa maadili yake. Mbaya kuliko yote usifikiri wazungu hawajuwi habari zake nakile anakifanya ndio maana aka panic tulia muone aibu hii
Mbona wabunge na wazungu hapohapo wamempigia makofi kwa wingi!?,au nyie ndo mnajua kutathmini alichosema kuliko alikuwa nao ukumbini waliompigia makofi!?
 
Nakubaliana na Fatma kwa kua simpendi Tulia. Sio kwa sababu sawa na za Fatma. Namuona sio mzalendo na ni mnafiki, msaliti na mbinafsi kwa jinsi alivyoshiriki lile tukio la kuwapa bandari zetu zote dubai wamiliki kama mali yao. Sitokaa nimsamehe kwa tukio hilo.
 
Nyie mbona mnamuabudu chura kiziwi ambaye hana hata darasa Moja na hajui hata anchokifanya zaidi ya utekaji na kuua!?
mkuu. Mi na huyo uliyemtaja wapi na wapi
 
I am no fan of Tulia.

Ila napata hisia za Fatuma za wivu juu ya Tulia.

Hapo anataka ni yeye ndie angekuwa hapo.
Wewe ni hisia ΕΌako tu. Fatma anakosa nini? Hivi kumsikliza Fatma au Tulia nani ana bore? Weka merit mezani Fatma Vs Tulia nani atakuwa kidedea? Obviously Fatma.

Merit, siyo kubebana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…