FC Barcelona (Barça or Blaugrana) | Special Thread

Pole sana kwa kushindwa kunielewa na nitarudia kusema kile niaminicho.
1. Unaposema Pep filosofi yake ni tiki taka naweza nikakubalia ila tambua mimi nimesema pep ameonesha udhaifu mkubwa kuipeleka tiki taka Bayern. Bayern ndo timu ya taifa ya German, ni sawa na Barca pale Spain. Amepeleka Tiki Taka Bayern, amevuna nini UEFA!!?? Unaweza ukaiweka level moja Bayern Pep na ya Heynkess!!??
Kama unatazama kwa makini utaona hata Style wanayocheza ni tofauti, Bayern ilikuw nzuri ktk nafasi ya Kiungo, Winga, Beki mpaka Mshambuliaji. Miaka ya hivi karibuni Pep kapeleka Tiki Taka, angalia Game zote alizotolewa UEFA amefungwa kwa style ipi. Anza na Game za Real Madrid alizomchapa nje ndani, angalia hata ile aliyompiga 4 kwake. Bayern ilikuwa ni weak ktk kukaba, na ndo hata Barca yake ilikuwa ni hivyo. Barca na Madrid wameifunga Bayern kwa pasi zisizozidi hata 8.
----Ukweli ni kwamba mashabiki wengi wa German hawakupendezwa na Tiki Taka, wajerumani hawataki soka la pasi nyingi, yaani mchezaji akipata nafasi ya kupiga mbali hawezi kupiga mpaka aingie ndani ya 18.
-----Wajerumani wamezoea kuona soka la kupiga pasi kadhaa kisha mpira unapelekwa golini, hawataki kuona timu inamiliki mpira mda mwingi bila kushambulia.

2. Huwezi kusema kushinda makombe ni bahati wakati una timu nzuri na kila kitu, bahati hii ilidondoka kwa Chelsea tuu na ndo maana mpaka leo hawajafika tena final. Mpira ni kujipanga, andaa wachezaji wazuri na mbinu nzuri makombe yatafata. Kama mpira ni bahati mbona Tanzania haijawahi hata kushirik World Cup au Arsenal kubeba UEFA. Pep alikuwa ana wachezaji wazuri sana pale Barca akiwemo Messi, Xavi na Iniesta ambalo walikuwa moto kipindi kile huku mfumo wa tiki taka uliosisiwa na Johan Cruyff ulikuwa ukisumbua sana timu pinzani.
-Zamani Barca magoli yake mengi alipenda afunge kwa move nzuri, yaani pasi zinaanzia kwa mabeki mpaka viungo, na viungo mpaka kwa Washambuliaji. Leo hii Soka linachezwa kwa viungo na mabeki na ikifika kwa washambuliaji basi mpira kwa viungo, kazi ya viungo wa sasa ni kudondosha mpira kwa MSN popote ilipo hata kama wamecheza pasi 3 ilimradi tu MSN imekaa sehemu nzuri basi pasi inadondoshwa, hii ni tofauti na zamani ambapo ni lazima wafate miiko ya tiki taka.

3. Ninasema na ninarudia kusema, Pep ni kocha wa kawaida tuu, sitashangaa kama Man City nao wakafundishwa tiki taka. Na endapo ikakutana na timu yenye wachezaji wenye kasi basi tutegemee mengine kwa Man City, mbali na hapo wachezaji waokoe jahazi maana Man City wana wachezaji wazuri wenye vipaji.
 
mkuu aleyn hapa kidogo na mimi nataka niingie unaposema pep ni kocha wa kawaida tu unamaanisha kwamba pep ndo hana kitu na hana mpya na hayo mataji aliyoshinda ni kwa ajili ya masupastaa alokua nao kama messi, xavi and iniesta . is ok hapa umesema eti ancelot unamkubali zaidi kuliko pep wakati anceloti huyo huyo ametimuliwa pale madrid na kama pep alikua anashinda mataji kwa ajili ya xavi . messi na iniesta mbona kocha kama tata martino alipokuja barca alimaliza season yote ya mwaka 2013/2014 bila hata kikombe cha mbuzi wakati palikua na xavi. messi . neymar na iniesta hapa utasema kua xavi alishapungua kasi mbona kaja lius enrique kaendeleza style ile ya barca ya tikitaka na xavi ndani na iniesta na uengezeko wa suarez na neymar kawatumia vizuri tumeona matunda yake big up kwa enrique na hapo utasema enrique sio kocha ila kapata wachezaji wazuri tu .
mourihno ma fan wa chelsea walimsifu sana na hata media za uk zikampamba sana kua ni bonge la kocha yoote kwa sababu kawaletea kombe la epl juzi tumeona walivyo muadhirisha ni kwa sababu tu ya matokeo mabaya . nataka nikuambiye tu mkuu hii ndo soka unapofanya vizuri ndipo utaambiwa wee ni bora ukiboronga huna kitu sasa wee jiulize huyu pep kila timu inamtaka kuanzia psg . cheslea . man u n.k. jiulize kama sio kocha mzuri kwanini wanamtaka mourinho mpaka leo hajapata kibarua pep anaachiya tawi anakamata tawi
 
-Tunaposema wa kawaida haina maana kwamba tunamuweka level moja na makocha akina Maximo. Ninasema wa kawaida kwa kile ambacho alichofanikiwa, huwezi kumuweka Pep level moja na akina Mourinho ama Anceloti unless kwamba mpira umeanza kushabikia 2008.

-Suala la Pep Guardiola kutakiwa na timu kubwa haimaanishi kwamba yeye ni bora, mpira ni biashara kubwa sana ambayo inalipa kuliko maelezo. Unaposikia mtu kama Messi mkataba mpya ambao ataingia atalipwa 1.2 Bilion za kitanzania kwa wiki basi ujue kwenye mpira kuna pesa nyingi sana. Unapoambiwa Cristiano Ronaldo anamiliki magali zaidi ya 20 ya kifahali basi tambua mpira ulipa. Unapoambiwa John Terry anamzidi kwa pesa Wazir wao Mkuu wa Uingereza basi tambua mpira ni biashara kubwa mno.
Kwa waliosoma Biashara kuna kitu kinaitwa Brand, Brand inasehemu kubwa sana ya kuincrease sales ktk biashara. Kwanini Pep ni Brand kubwa!?
1. Mashabiki wengi wanatambua Pep ni mtu wa mafanikio, kuja kwa Pep kunavuta attention kwa mashabiki kuifatilia Man City.
2. Pep ataleta soka la tofauti EPL, tangu EPL ianzishwe, sidhani kama kuna timu itacheza soka la kuvutia kama ambalo Pep atalipeleka EPL na ndo maana hata Abramovic alikiri kuwa anamtaka Pep ili aje alete soka la tofauti Chelsea, HAKUSEMA ILI ALETE MAKOMBE ILA ALISEMA ILI ALETE SOKA LENYE BURUDANI.
3. Man City wanatumaini kumpata Neymar au Messi kwa miaka ya hivi karibuni, kumchukua Pep wanaamini kutaleta matumaini ya kuwapata hao nyota. Ukitaka kuamini hili angalia Club zote ambazo zinawawinda Messi na Neymar zimetangaza dau juu ya Pep ila Man City ndo imeshinda hapa majuzi.
4. Wachezaji wataweka imani kwa Pep, wachezaji wa Man City lazima watamheshimu sana Pep. Unapokuwa na kocha mwenye jina kubwa huwa inapelekea kuwa na heshima kubwa ndani ya club pamoja na wachezaji kumheshimu kocha. Ukiwa na kocha ambaye anaonekana ana mafanikio wachezaji watacheza kwa umakini mkubwa uwanjani, timu ikiyumba itaonekana ni wao wachezaji na si kocha ila kocha akiwa akiishiwa mbinu au akiwa mbovu huwa tunaona hali ya uchezaji itakavyobadilika.

-Mafanikio aliyoyapata Pep pale Barca kwa asilimia kubwa yalichangiwa na mfumo pamoja na wachezaji hao watatu. Ule mfumo miaka ya 2009-2010 hususani Mourinho alivyoenda Madrid mfumo wa Barca ulipata shida sana. Na kama unakumbuka kipindi kile Barca alikuwa anasemwa sana kwamba anabebwa. Binafsi suala la Barca kubebwa nalipinga kiasi na nalikubali kiasi kwa miaka ile. Barca ilikuwa ikikutana na Madrid ilikuwa ikishinda kwa tabu sana tangu alipokuja Mourinho, Mourinho amechangia kiasi kikubwa sana kudhibiti mfumo wa Barca. Rejea 3-1 tulizopigwa Milan, style ya magoli yalivyopatikana na ndo tukawa tunafungwa hivyo hivyo na Madrid na timu zingine na mpaka leo Bayern anafungwa hivyo hivyo, walau Barca amejirekebisha.

-Sitaweza kusema hasa kwanini Tata kashindwa kubeba Makombe Barca ila nachodhani ni kwamba Geraldo Tata ni msimu wake wa kwanza pale Barca na sidhani kama alishawahi kufundisha Ulaya. Ila nikukumbushe tu kuwa Tata alikosa kombe la ligi ktk mechi ya mwishi kabisa ya Ligi pia alikosa kombe la Mfalme ktk fainali, so unaweza ukasema jamaa hakuwa na bahati tuu pia ilichangiwa na Barca kukosa namba 9. Kumbuka kipindi kile Messi alikuwa anacheza winga wa kulia huku namba 9 akicheza Cesc Fabregas na ndo maana msimu ulivyoisha akasajiliwa Suarez.

-Carlo Ancelot katimuliwa Madrid sababu tu ya utahira na sifa za kijinga za Perez, Carlo ni kocha mzuri na ni kocha mwenye CV kubwa sana kwa sasa sawasawa na Jose Mourinho na Sir Alex.
 
Messi and Iniesta have more cup semi-final experience than anybody. The Copa del Rey has been all about FC Barcelona in recent years, and the facts are there to prove it. The team has made it as at least as far as the semi-finals in all but one of the last ten editions, and Andrés Iniesta and Leo Messi have been there to see it happen every time

That’s a humungous eight cup semi-final appearances in nine years for the Barça duo, and more than 2,000 minutes of football between them. The only game in which neither appeared was the second leg at Almeria in the 2010/11 season. But that was something of a formality after Barça had already won the first leg 5-0, so they were both rested.

Barça have gone on to appear in five of the last nine finals, and have won the trophy three times.



Semi-final goals
Iniesta scored in the first leg of last season’s semi-final against Villarreal, while Messi has scored in seven of the different encounters: 2006/07 (Getafe), 2008/09 (Mallorca), 2010/11 (Almería), 2013/14 (Real Sociedad) and 2014/15 (Villarreal).

The most famous of those was probably the one against Getafe at the Camp Nou. That was the almost exact replica of Diego Maradona’s goal against England at the 1986 World Cup, and which is often hailed as the greatest goal ever. Here’s a video reminder of one of the goals that confirmed the name of Messi among the all-time elite of world football.

 
ahsante kwa uchambuzi wako maridadi ila naomba unitake radhi kunambia nimeanza kushabikia mpira 2008
 
...kuna baadhi ya team hazikupi mawazo kabisa. Ni vigumu kuamini kama hii ni valencia wanavyopigishwa nusu uwanja! Na ndio kwanza first half. Huyo Neymar sasa na showboats zake

la 3 hilooooo messi
 
...messi kagonga mwamba kwenye open play, messi akafanyiwa foul -> penalty ambayo neymar kaipiga kibishoo kama kawa ikagonga mwamba. Valencia watarudi wakiwa pungufu baada ya kadi nyekundu. Tutarajie magoli mengine labda mawili hivi! Mechi ishakuwa nyepesi zaidi, ila itaboa kwa vile valencia wako pungufu!!!
 
....nishachoka sasa...7. This is too much, anyways walideserve kupigwa 5 wakiwa kamili, hii saba ni bile wako pungufu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…