Mshambuliaji wa Barcelona Luis Suarez amekiri kuwa maumivu yamemzuia kucheza katika ubora wake mapema msimu huu
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 sasa amefunga mara sita katika mechi 18 alizoichezea Barcelona msimu huu, lakini bado hajafanikiwa katika mechi tano za Ligi ya Mabingwa katika kampeni za 2017-18.
Suarez amekuwa akipambana dhidi ya majeraha yake ya goti, hata hivyo, Mchezaji huyo wa Kimataifa wa Uruguay amebainisha kuwa jeraha hilo limeharibu kiwango chake wiki za awali za msimu huu.
"Naam, lakini sasa najisikia vizuri. Nilihitaji matibabu ya kina na sasa naimarika. Sitaki kuendelea kuhisi maumivu, ni lazima niyazuie kujirudia tena," Marca lilimnukuu Suarez akisema.
Suarez amefanikiwa kufunga magoli 59 katika mechi 53 katika msimu wake wa pili Barcelona, na pia alifunga magoli 37 katika mechi 51 msimu uliopita akiwa na Lionel Messi na Neymar katika safu ya mbele ya mashambulizi.