Feitoto agoma kurudi Uto, ataka review ya hukumu ya TFF

Feitoto agoma kurudi Uto, ataka review ya hukumu ya TFF

Kama mlishindwa na muhuni kutoka ghana sembuse watoto wa tajiri la Afrika mashariki ya kati.
Makolokolo Yanga hii ya sasa ni tofauti na ya kipindi cha Kocha Mkuu Mwinyi Zahera, kipindi kile Yanga haikuwa kampuni kama sasa hivi ilivyo chini ya GSM.

Mtatapatapa hadi mtakaa maana sasa hivi Yanga FC ina mapesa na ina wenye mamlaka tofauti na yule Msanii aliyeweka mkataba feki wa B 26 kwenye jezi badala ya kwenye mkataba halisi kama wa Yanga [emoji23]
 
Utopolo ni kikundi cha wachawi ndo kilicho sababisha mpaka sasa ngasa ni masikini baada ya kuharibu dili ambalo linge mpatia milion 300
Makolokolo mlikula pesa za Mchezaji wenu Marehemu Mafisango na kupiga kimya lakini mmeamua kujitoa ufahamu kama vile haziwatoshi?

Au ndiyo nyani huwa haoni kundule?
 
Watu tunajadili mambo ya msingi, wewe unaleta story za uchawi! Huku ukisahau ni mwaka wa jana tu timu yako ya simba ilipigwa faini ya dola elfu 10 na CAF kutokana na vitendo vyake vya kishirikina uwanjani kule Afrika ya Kusini.

Halafu aliyekuambia Mrisho Ngasa ni maskini ni nani? Na kuna uhusiano gani wa huo umaskini wake na hilo dili la milioni 300?

Yaani mtu achezee Kagera Sugar, Yanga, Azam, simba, Afrika ya Kusini, Ndanda, nk tangu 2004 huko! Halafu from nowhere tu awe maskini kwa sababu alibaniwa dili la milioni 300!

Kweli Rage alikuwa sahihi kuwaita mbumbumbu.
Nakazia ni Mbumbumbu wote na hata hao waliompa LIKES [emoji38]
 
Hakuna raha wanaojiita wananchi wataipata kama Fei akikaa benchi. Watahalalisha furaha yao kwa sababu kama dogo hana nidhamu, dogo kadanganywa, dogo msaliti. Hii haitajalisha alichokifanya kwenye club, kiwango chake, umuhimu wake kwenye timu ya taifa, uvumilivu wake wa kuona kina morison wakipokea mshahara mara saba yake huku yeye akitakiwa asubiri na avumilie.

V/S

Hakuna raha Wananchi halisi wa TZ tutaipata kama Fei akifanikiwa na kuendeleza kipaji chake nje ya mkataba wa kinyonyaji na tukawa na wachezaji ndani ya nchi mwenye kiwango kizuri na mwenye kipato kizuri. Binafsi sijali hata kama ni hao Yanga wakimpa mshahara mzuri kama kina Aziz K.

NGOJA TUONE WANANCHI WAPI WATAIBUKA NA FURAHA.
 
Umetuchokoa na kutuchokonoa, umetuparura utopolo mpaka nimeamua nikujibu kirefu sana kama mkojo wa mwanzo asubuhi maana mikia wote nyie wote nchi nzima ni mbumbumbu.

Kaka sidhani kama we unajua boli! We itakuwa unaJua sana pool table au bao tu!

Pia nadhani una defect kwenye ubongo na unafeli kufikiri vizuri kuhusu mambo ya mpira! Nakiri Sijui uwezo wako wako wa kufikiri mambo mengine!

Mpira ni bizness kama bizness zingine kuuza mkaa, maji, unga, magari nk. Kwakuwa nadhani wewe umetoka familia ya wakulima na sio wafanyabiashara kama Mimi naamini hutaelewa kuhusu ishu ya Feitoto maana Si Kilimo ni biashara kwenye boli!! Mchezaji akipanda kiwango anapanda thamani anauzwa bei kubwa club iliyomkuza nayo Ina benefit!

Yanga haimuhitaji Tena Feitoto Wala haimng'ang'anii . Aziz Ki na Mudathir sijui Sureboy , Bigirimana, Yusuph Athumani, Clement, Morisson na Farid mara Huku Kuna Zawadi Mauya na Denis Nkane tayari wote hawa amewapa chance waoneshe viwango. Yanga imeziba pengo lake tayari si unaona unbeaten ziko pale pale na Feitoto Yuko JKU kule mchambawima ? Au umejitoa ufahamu Mkuu?

Yanga haimng'ang'anii Feitoto Bali timu inataka kupiga pesa zake tu maana Feitoto ni Mtoto wetu inapaswa auzwe kihalali mezani sio kihuni kihuni under influence ya shisha au whiskey!!

Inatakiwa tu Feitoto awe mpole alete matajiri uchwara wake mezani utopoloni tuwalipue dau lake la uhamisho ni one billion thamani yake, dogo aende!

Mkataba wake Feitoto waliuweka hapa JF nikausoma taratibu nikaona unasema akitaka kuvunja Feitoto atalipa ada ya usajili na mishahara Mitatu mkataba ukaongeza Katika hicho kifungu "Feisal avunje mkataba ikiwa tu kukiwa na sababu za maana kufanya hivyo" na bahati mbaya sababu hizo za maana kuvunja mkataba hazikutajwa kwenye mkataba. Maana yake ni kuwa

1. Kipengele alichotumia Feitoto Ili kuvunja mkataba na Yanga hakukielewa maana hatakiwi kuishia tu kuweka mzigo mezani Bali pia akae Mezani kuongea na uongozi na kuwaeleza "sababu za maana" za kuvunja mkataba na uongozi uzielewe na uzikubali!

2.Yanga na TFF Wana loophole ya kukataa sababu zote atakazosema Feitoto kwa kusema "si za maana" na watakuwa sahihi mbele ya sheria maana sababu za maana za kuvunja mkataba hazijulikani!

3. Feitoto alipiga zake shisha tu likakolea akaweka mzigo mezani akaandika barua kutuaga mashabiki wa utopolo akatimka Wala hakusema sababu za kuvunja mkataba na hakuongea na uongozi. Uhuni asilimia mia plus!

4. Feitoto Hana sababu ya maana ya kuvunja mkataba. Tukifikiria sababu hizo ni kama kutolipwa mishahara, kutotibiwa akiumia au kutopangwa!! Dogo Hana sababu ya maana ya kuvunja mkataba.

Kwa wanasimba wote habari njema ni kuwa maana yake Feitoto atasalia utopoloni mpaka apate "sababu ya maana" ya kuvunja mkataba na waliodhani Feisal ndo moyo wa Yanga wamekosea sana Yanga imejaza vipaji milioni hatufeli makombe yako pale pale hata mkimvuruga Feitoto amerudi JKU!

Mimi Zuga nilianza kubeba viatu vya wachezaji Ili kuingia uwanjani kucheki ligi kuu miaka 50 iliyopita nikiwa Mtoto mdogo sana nisikilize vizuri nimeona kwa macho yangu timu za ligi kuu zikiroga klabuni kabla ya kwenda uwanjani nakwambia laivu Ngoma ya kitoto haikeshi, Feisal Simba sijui Azam wamemrubuni kwa pesa kwa vile yeye mwenyewe ameona vipaji na vigimbi vya wenzake na ameingia baridi na kushindwa kuhimili presha ya kugombania namba , Bado ana akili za kitoto.

Utopolo tunajua mikia mnakaribia kufa kwa presha na wivu na kurubuni wachezaji wetu Ili mtuharibie sherehe kwa vile tu kinawauma sana sie utopolo tuna possess boli , tumeingia makundi shirikisho CAF kwa kuwafunga waarabu kwao, tunaongoza ligi tukisubiri Simba mpigwe mechi moja ambayo hamtapewa penati na timu pinzani kucheza pungufu!! Kombe la NBC mmeona mmelikosa mmeamua kumwaga mboga na ugali!!

Utopolo tunajua Simba mnakaribia kufa kwa kihoro kwa kuudukua mpango wa Yanga kubeba makombe yote ya bara kwa misimu mitano na utaratibu wetu wa kuhesabu unbeaten 100 maana pale tulipopanga sherehe ya kugawa keki 50 uwanjani kwa kufikisha unbeaten 50 Mikia mlienda Mbeya kabla ya mechi na mkafanikiwa kuharibu sherehe japo msichokijua ni kuwa mliongeza petrol kwenye moto Na kubadili hesabu ya unbeaten 50 kuwa unbeaten 100!

Feisal akae tu home hadi 2024 mkataba utaisha ataenda huko Azam sijui Simba. Nyie la Saba B Endeleeni kumpotosha Feitoto tu sie wenye madigirii yetu tumebukua ishu ya Feikubwa tunawafafanulia alichokosea hamuelewi!
Shikamoo Baba [emoji119][emoji2]
 
Hakuna raha wanaojiita wananchi wataipata kama Fei akikaa benchi. Watahalalisha furaha yao kwa sababu kama dogo hana nidhamu, dogo kadanganywa, dogo msaliti. Hii haitajalisha alichokifanya kwenye club, kiwango chake, umuhimu wake kwenye timu ya taifa, uvumilivu wake wa kuona kina morison wakipokea mshahara mara saba yake huku yeye akitakiwa asubiri na avumilie.

V/S

Hakuna raha Wananchi halisi wa TZ tutaipata kama Fei akifanikiwa na kuendeleza kipaji chake nje ya mkataba wa kinyonyaji na tukawa na wachezaji ndani ya nchi mwenye kiwango kizuri na mwenye kipato kizuri. Binafsi sijali hata kama ni hao Yanga wakimpa mshahara mzuri kama kina Aziz K.

NGOJA TUONE WANANCHI WAPI WATAIBUKA NA FURAHA.
Wewe ni Msemaji Mkuu wa Wananchi hadi uwasemee badala ya kujisemea we mwenyewe?
 
Wewe ni Msemaji Mkuu wa Wananchi hadi uwasemee badala ya kujisemea we mwenyewe?
Ww ni yule wa akae benchi hana adabu dogo? Au ni yule wa Apewe maslahi ya maana kama haiwezekani aachwe aende?
 
Roho mbaya ya viongozi iliyomfikisha hapo Feisal.

Morrison naskia anapokea 23M halafu kwa mwezi anacheza mechi mbili nazo hizo anatokea sub hachezi dakika 60

Aziz Ki inadaiwa anapokea 26M ila at least huyu anacheza mechi nyingi japokuwa kihalisia yeye na Feisal kwenye ubora sioni utofauti.

Hao wote wamemzidi Feisal mara 7 mshahara, is that fair?
Mshahara huja baada ya negotiations
 
Kitaka kuthibitisha kwa 100% kile alichokisema Rage ni sahihi kuhusu mashabiki wa makolo basi soma huu uzi kisha comments zilizomo
 
Roho mbaya ya viongozi iliyomfikisha hapo Feisal.

Morrison naskia anapokea 23M halafu kwa mwezi anacheza mechi mbili nazo hizo anatokea sub hachezi dakika 60

Aziz Ki inadaiwa anapokea 26M ila at least huyu anacheza mechi nyingi japokuwa kihalisia yeye na Feisal kwenye ubora sioni utofauti.

Hao wote wamemzidi Feisal mara 7 mshahara, is that fair?
Unataka nikujuze Eden Hazard anapokea kiasi gani pale Madrid? Imani yangu unafahamu kwahiyo sitakujuza

Nikikuuliza amecheza mechi ngapi msimu huu nadhani utazihesabu

Kwa hiyo haifanyi kazi namna hiyo unayoiweka, Fei amesaini 2020.. hawa wamesaini 2022, kuna factor nyingi sana hapa zimeingia

Nikikuuliza Okwa amecheza mechi ngapi hapo Dunduka naimani utabaki unatoa macho tuu.. Nikikuuliza kwa nini pia kua kwa nini Okwa analipwa pesa nyingi kuliko Mzamiru Yanis utabaki unakodoa bila jibu.
 
Ww ni yule wa akae benchi hana adabu dogo? Au ni yule wa Apewe maslahi ya maana kama haiwezekani aachwe aende?
Nilikuwa juzi kati hapa naangalia mkeka wa mshahara wa klabu ya Man City; mchezaji kama Julian Alvarez aliyeisaidia timu yake ya Argentina kuchukua ubingwa wa kombe la Dunia 2022, anapokea paundi 50,000/= tu kwa wiki! Huku Kelvin De Bruyne akiwa ndiye kinara kwa kupokea zaidi ya paundi laki 3 na ushee!

Umeona analalamika? Hapana! Kwa sababu amesaini mwenyewe mkataba wa kujiunga na klabu hiyo kwa malipo hayo. Muda wake na yeye wa kupandishiwa mshahara ukifika, atafanyiwa hivyo.

Hivyo mnatakiwa muwashauri na akina Fei Toto kuwa wavumikivu, na pia kufuata utaratibu kama hawaridhiki na mishahara wanayolipwa. Siyo mnakubali tu akina Yusuph Bakhressa kutumia hela zao kutuharibia mpira wetu kwa kuwarubuni wachezaji kuvunja mikataba kienyeji, kwa kisingizio cha malipo kiduchu.

Au unataka uniambie na yeye kwenye timu yake ya Azam, anawalipa wachezaji wake wote (na hasa wazawa) mshahara sawa wa milioni 17 kwa mwezi? Nongwa iko wapi kwa Fei Toto kulipwa milioni 4 alizo ridhia mwenyewe kwenye mkataba?
 
Hapana mkuu kwa mujibu wa vipengele vya mkataba wa fei unaruhusu kufanya alicho kifanya sema hili jambo hina amuliwa kisiasa ila fei yuko sawa.

Kipengele cha mkataba kinasema iwapo fei toto atataka kuvunja mkataba bila sababu za msingi atatakiwa kuilipa yanga sh million 100 na mishahara yake ya miezi mitatu na tiyari amesha fanya hivyo.

Hili jambo lina amuliwa kisiasa kwa sababu ndani ya hizo kamati za maamuzi wamejaa mashabiki wa Yanga na Simba ila Fei yuko sawa.
Hakuna kipengele cha kuvunja mkataba bila sababu za msingi kwenye mpira lazma kuwe na Sababu.
 
Muongeze wewe kama unaona anaonewa, maana alikubali mwenyewe hicho kiasi
Roho mbaya ya viongozi iliyomfikisha hapo Feisal.

Morrison naskia anapokea 23M halafu kwa mwezi anacheza mechi mbili nazo hizo anatokea sub hachezi dakika 60

Aziz Ki inadaiwa anapokea 26M ila at least huyu anacheza mechi nyingi japokuwa kihalisia yeye na Feisal kwenye ubora sioni utofauti.

Hao wote wamemzidi Feisal mara 7 mshahara, is that fair?
 
Back
Top Bottom