Hakuna mchezaji ambaye hataki kupata pesa, ukiona team inamtaka mchezaji mwenye mkataba means ipo tayari kumlipa zaidi ya kule alipokua, kwani hujawahi kusikia Team zikifungua Mashauri kulalamika team nyingine kuongea na mchezaji wao ingali akiwa na mkataba?
Team zinaweza kufungua majadiliano na mchezaji akibakisha miezi 6 ya mkataba wake.
Ndo nasema ingekua rahisi hivyo team zote kubwa zingekua zinavunja tu mikataba!
Mf. Mchezaji kama Mmakonde yupo Simba kwa mshahara wa 10 millions, Signing fee ya 200 millions, Al ahly wanaenda Simba kuulizia bei ya Mmakonde wanaambiwa anauzwa kwa 600 millions, ya nini walipe 600 millions kumbe wanaweza kumshawishi mchezaji avunje Mkataba kwa 300 millions na ahadi ya mshahara wa 50 millions ambayo hakuna mchezaji Bongo atakataa!
Ndo nasema ingekua rahisi hivyo, tusingesikia Club kubwa zikifata taratibu kununua Wachezaji, zingekua tu zinavunja mikataba kama ilivyo kwa Feisal.
Fifa sio Wajinga, wapo 50% kwa club na kwa Player.
Kuna ukweli ambao Yanga wanausema, na baadhi ya watu hawataki kuusikia.