Festo Dugange: Serikali inajenga vituo vya Kusubiria wagonjwa Kwenye Hospitali ili kuondoa kero kwa ndugu

Festo Dugange: Serikali inajenga vituo vya Kusubiria wagonjwa Kwenye Hospitali ili kuondoa kero kwa ndugu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Fuatilia yanayojiri Bungeni leo tarehe 31 Januari, 2023 kwenye Mkutano wa Kumi, kikao cha kwanza.



HOJA YA SEHEMU ZA KUSUBIRI KUWAONA WAGONJWA
Mbunge wa Viti Maalum, Mariam Nassor Kisangi ameuliza kuhusu mpango wa Serikali katika kujenga na kuongeza maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika hospitali Nchini.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt Festo Dugange alisema Serikali inaendelea na ujenzi wa hospitali katika halmashauri ambazo hazikuwa na huduma hiyo na kuwa tayari kuna hospitali 127 zinaendelea na ujenzi.

Amesema “Kumekuwa na changamoto ya maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika hospitali nyingi, ili kutatua changamoto hiyo Serikali katika mwaka wa fedha 2023/24 imetenga bajeti ya Tsh. Bilioni 2.04 kwa ajili ya ujenzi wa sehemu za kusubiria wagonjwa katika zaidi ya hospitaili 100.

“Changamoto hiyo inazikumba Hospitali za Temeke, Amana na Mwananyamala Mkoani Dar es Salaam.”

MGAMBO KUSUMBUA WATU MUHIMBILI
Aidha, Mbunge huyo alihoji kuhusu tamko la Serikali kuhusu mgambo kufukuza wanaosubiri kuwaona wagonjwa katika Hospitali ya Muhimbili.

Naibu Waziri wa Afya, Naibu Waziri wa Afya Dr Godwin Mollel akajibu kuwa upande wa Hospitali ya Mwananyamala na Temeke kuna bajeti imetengwa kwa ajili ya ujenzi huo, kuhusu Muhimbili ujenzi unaendelea na ndani ya miezi mitatu kila kitu kitareje kama kawaida.


TATIZO MKOANI IRINGA
Mbunge wa Viti Maalumu, Rita Kabati amesema tatizo hilo ni kubwa Mkoani Iringa hasa katika Hospitali ya Mkoa, amedai kuwa wananchi wanalazimika kusubiri kuwaona wagonjwa kwenye maeneo ya magereza.

Akaongeza kuwa hata katika Wilaya ya Kilolo na Mufindi napo kuna changamoto hiyo, akaongeza “Kuna haja ya kuwepo kwa hosteli, wale wanaosubiri wagonjwa wawe wanalala nje ili kusubiri kuwaona wagonjwa.

Naibu Waziri wa Afya, Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Mollel amesema kweli kuna changamoto hiyo na kumekuwa na hoja kuhusu kuihamisha hospitali hiyo lakini hilo halitawezekana kwa sasa kutokana na aina ya uwekezaji uliofanyika.

“Kuna mambo ya muhimu yanafikiriwa katiya TAMISEMI na Wizara ya Afya kabla ya kufanya maamuzi.”
 
Hivi kuna watu huwa wanasikiliza bunge leo hii.mm nakumbuka bunge langu la mwisho kulisikiliza ni lile la enzi ya akina kafulila, zitto, Antipas Lisu, Sugu, Prof J, Mkosamali,nk .bunge la ndiyooo lisilojali maslahi ya watz ni la nn.

tuombeane uzima nadhani 2025 itakuwa ya kihistoria maana hawa tulionao kwa sasa wanakusanya kilicho chao wakijua mziki mtamu uko 2025.
 
Fuatilia yanayojiri Bungeni leo tarehe 31 Januari, 2023 kwenye Mkutano wa Kumi, kikao cha kwanza.
HAKUNA BUNGE tuna Vikao vya CCM ndani ya JENGO LA BUNGE
NCHI ni ya Mfumo wa Vyama Vingi lakini ina BUNGE la Chama Kimoja
Bunge halina KAMBI RASMI ya UPINZANI
Bunge halina KIONGOZI wa KAMBI la UPINZANI
Bunge halina MNADHIMU MKUU wa KAMBI ya UPINZANI
Bunge halina MAWAZIRI VIVULI wa UPINZANI
Bunge halina HOTUBA ya KAMBI RASMI ya UPINZANI
Bunge halina HOTUBA za MAWAZIRI Vivuli
Yote hayo ni UKIUKWAJI wa KATIBA ya NCHI
Huwezi kusema una BUNGE kwa KUKIUKA KATIBA
Hiyo ndiyo TANZANIA ya Toka Awamu ya 5 na 6
 
Fuatilia yanayojiri Bungeni leo tarehe 31 Januari, 2023 kwenye Mkutano wa Kumi, kikao cha kwanza.



HOJA YA SEHEMU ZA KUSUBIRI KUWAONA WAGONJWA
Mbunge wa Viti Maalum, Mariam Nassor Kisangi ameuliza kuhusu mpango wa Serikali katika kujenga na kuongeza maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika hospitali Nchini.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt Festo Dugange alisema Serikali inaendelea na ujenzi wa hospitali katika halmashauri ambazo hazikuwa na huduma hiyo na kuwa tayari kuna hospitali 127 zinaendelea na ujenzi.

Amesema “Kumekuwa na changamoto ya maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika hospitali nyingi, ili kutatua changamoto hiyo Serikali katika mwaka wa fedha 2023/24 imetenga bajeti ya Tsh. Bilioni 2.04 kwa ajili ya ujenzi wa sehemu za kusubiria wagonjwa katika zaidi ya hospitaili 100.

“Changamoto hiyo inazikumba Hospitali za Temeke, Amana na Mwananyamala Mkoani Dar es Salaam.”

MGAMBO KUSUMBUA WATU MUHIMBILI
Aidha, Mbunge huyo alihoji kuhusu tamko la Serikali kuhusu mgambo kufukuza wanaosubiri kuwaona wagonjwa katika Hospitali ya Muhimbili.

Naibu Waziri wa Afya, Naibu Waziri wa Afya Dr Godwin Mollel akajibu kuwa upande wa Hospitali ya Mwananyamala na Temeke kuna bajeti imetengwa kwa ajili ya ujenzi huo, kuhusu Muhimbili ujenzi unaendelea na ndani ya miezi mitatu kila kitu kitareje kama kawaida.


TATIZO MKOANI IRINGA
Mbunge wa Viti Maalumu, Rita Kabati amesema tatizo hilo ni kubwa Mkoani Iringa hasa katika Hospitali ya Mkoa, amedai kuwa wananchi wanalazimika kusubiri kuwaona wagonjwa kwenye maeneo ya magereza.

Akaongeza kuwa hata katika Wilaya ya Kilolo na Mufindi napo kuna changamoto hiyo, akaongeza “Kuna haja ya kuwepo kwa hosteli, wale wanaosubiri wagonjwa wawe wanalala nje ili kusubiri kuwaona wagonjwa.

Naibu Waziri wa Afya, Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Mollel amesema kweli kuna changamoto hiyo na kumekuwa na hoja kuhusu kuihamisha hospitali hiyo lakini hilo halitawezekana kwa sasa kutokana na aina ya uwekezaji uliofanyika.

“Kuna mambo ya muhimu yanafikiriwa katiya TAMISEMI na Wizara ya Afya kabla ya kufanya maamuzi.”

Bunge la sasa halina mvuto. Mtu mwenye akili huwezi kupoteza mda wako kuangalia/kusikiliza bunge la machawa
 
Kati ya maybe yaliyokosa hamasa nadhani hili linaongoza
Kweli Mkuu, enzi za Bunge la Mzee Sitta watu tulikuwa tunazingatia ratiba ya Bunge kwasababu Wabunge walikuwa wanachambua hoja kwa kina, hapa Dkt.Slaa,kule Freeman Mbowe, John Heche, Msigwa, Halima Mdee, nk,CCM walikuwa wanapumulia mashine pamoja na kwamba Spika ni wao.

Sasa ili Bunge la kusifu na kuabudu wapi na wapi!
 
Fuatilia yanayojiri Bungeni leo tarehe 31 Januari, 2023 kwenye Mkutano wa Kumi, kikao cha kwanza.



HOJA YA SEHEMU ZA KUSUBIRI KUWAONA WAGONJWA
Mbunge wa Viti Maalum, Mariam Nassor Kisangi ameuliza kuhusu mpango wa Serikali katika kujenga na kuongeza maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika hospitali Nchini.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt Festo Dugange alisema Serikali inaendelea na ujenzi wa hospitali katika halmashauri ambazo hazikuwa na huduma hiyo na kuwa tayari kuna hospitali 127 zinaendelea na ujenzi.

Amesema “Kumekuwa na changamoto ya maeneo ya kusubiri kuona wagonjwa katika hospitali nyingi, ili kutatua changamoto hiyo Serikali katika mwaka wa fedha 2023/24 imetenga bajeti ya Tsh. Bilioni 2.04 kwa ajili ya ujenzi wa sehemu za kusubiria wagonjwa katika zaidi ya hospitaili 100.

“Changamoto hiyo inazikumba Hospitali za Temeke, Amana na Mwananyamala Mkoani Dar es Salaam.”

MGAMBO KUSUMBUA WATU MUHIMBILI
Aidha, Mbunge huyo alihoji kuhusu tamko la Serikali kuhusu mgambo kufukuza wanaosubiri kuwaona wagonjwa katika Hospitali ya Muhimbili.

Naibu Waziri wa Afya, Naibu Waziri wa Afya Dr Godwin Mollel akajibu kuwa upande wa Hospitali ya Mwananyamala na Temeke kuna bajeti imetengwa kwa ajili ya ujenzi huo, kuhusu Muhimbili ujenzi unaendelea na ndani ya miezi mitatu kila kitu kitareje kama kawaida.


TATIZO MKOANI IRINGA
Mbunge wa Viti Maalumu, Rita Kabati amesema tatizo hilo ni kubwa Mkoani Iringa hasa katika Hospitali ya Mkoa, amedai kuwa wananchi wanalazimika kusubiri kuwaona wagonjwa kwenye maeneo ya magereza.

Akaongeza kuwa hata katika Wilaya ya Kilolo na Mufindi napo kuna changamoto hiyo, akaongeza “Kuna haja ya kuwepo kwa hosteli, wale wanaosubiri wagonjwa wawe wanalala nje ili kusubiri kuwaona wagonjwa.

Naibu Waziri wa Afya, Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Mollel amesema kweli kuna changamoto hiyo na kumekuwa na hoja kuhusu kuihamisha hospitali hiyo lakini hilo halitawezekana kwa sasa kutokana na aina ya uwekezaji uliofanyika.

“Kuna mambo ya muhimu yanafikiriwa katiya TAMISEMI na Wizara ya Afya kabla ya kufanya maamuzi.”

Wanaosubiri kuona wagonjwa wajengewe Hostel? Nadhani hili si sahihi. Kwa ufahamu wangu mdogo ambao Mungu amenijalia, hostel ni mahali ambapo hutoa huduma ya chakula na malazi kwa kikundi cha watu, kama vile wanafunzi, wafanyakazi au wasafiri.

Sasa kama mtu anatoka umbali wa Kilomita chache kutoka kutoka Hospitali ilipo kwa lengo la kuja kumuona mgonjwa pamoja na kumpelekea chakula, kweli ni sahihi huyo mtu kujengewa Hostel ili wakati anasubiri kumuona mgonjwa akauchape usingizi kidogo?
 
Bunge la hovyo kabisa kupata kutokea, Ee Mungu tujalie tupate KATIBA MPYA NA TUME HURU YA UCHAGUZI ili ujinga huu UKOMESHWE

Bajeti.PNG

Uongozi.jpg
 
Yaani sijui mpk ukae kufuatilia bunge labda umelewa chakali - Bunge magudo kbs hili
Lazima uwe mtu wa hovyo kabisa, zaidi ya asilimia 90 ya bajeti inapelekwa kwenye matumizi binafsi (ANASA) na asilimia chache tu ndio inaenda kwenye maendeleo. Tuna serikali au GENGE la wahalifu na walafi tu?
 
Bora nisikilize clip za Mh. Lissu walau sintaujutia muda wangu.
 
Bunge la hovyo kabisa kupata kutokea, Ee Mungu tujalie tupate KATIBA MPYA NA TUME HURU YA UCHAGUZI ili ujinga huu UKOMESHWE

View attachment 2501304
View attachment 2501308
Hivi haya matumizi ya kawaida huwaga ni nini? maana Bil 93 afu ya maendeleo ya wananchi inakuwa 23bil - mbona huu ni uonevu mkubwa. yaani unatumia alimost 90% afu 10 ndiyo ya maendeleo - haya maendeleo utayapata lini sasa?
 
Back
Top Bottom