Ushindi wa Tunzo ya msanii bora wa Hip Hop wa Fid Q kiuhalisia umetokana na yeye kufanyiwa campaign kubwa na marafiki wasanii, watu wa media na mashabiki walioona Fid Q hakushinda Tunzo miaka ya nyuma lakini si kwamba yeye ndio mwanaHip Hop bora wa mwaka 2013 may be ya mtunzi bora. Ngoja nikupe sababu kwa mtizamo wangu lakini. Ili ushinde Tuzo hiyo inabidi uwe umefanya ngoma ambazo ni heats zaidi ya wenzako. Kushirikishwa katika ngoma mbali mbali ambazo ni heats, kufanya shows nyingi zaidi ya wenzako n.k hayo yote kwa ujumla ndo kigezo kikubwa cha mtu kuweza kushinda. Kwa mwaka 2013 Fid Q ametoa ngoma moja tu ya siri ya mtungi ft Juma Nature, ambayo pia ilikua katika category ya nyimbo bora ya Hip na haikushinda. Kwa wafuatiliaji wa Hip Hop hamtabisha kua ngoma hiyo haikupata airtime ya kutosha. Kosa ambalo KTMA walifanya sijui kwa nini ni kutomuweka Joh Makini in nomination ya msanii bora wa Hip Hop. Haijalishi wanaosema Joh hafanyi Hip Hop lakini mziki anaofanya according to KTMA ni Hip Hop(not according to Hardcore Hip Hop lovers). Kwangu Joh Makini ndo msanii bora wa Hip Hop 2013 kwa nini? According to Dj Choka ni kua Joh Makini ni msanii wa Hip Hop aliefanya show nyingi zaidi kwa mwaka 2013 kuliko mwanaHipHop yoyote. Joh Makini kwa mwaka 2013 amefanya ngoma kali kama Sijutii na Nikumbatie pia amefanya ngoma ambazo zimeingia kwenye nominations KTMA ambazo ni Bei ya mkaa na Nje ya Box(imeshinda nyimbo bora ya Hip Hop), pia kundi lake la WEUSI lilikua kwenye nomination za kundi bora la mwaka-kizazi kipya (likashinda). Kwa sababu za Hapo juu Joh Makini ndo alistahili kuwa msanii bora wa Hip Hop 2013. Fid Q alishinda kwa huruma tu za mashabiki tu