Filamu ya Royal Tour Ingezinduliwa Tanzania Badala ya Marekani kuepuka gharama

Filamu ya Royal Tour Ingezinduliwa Tanzania Badala ya Marekani kuepuka gharama

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Tunaambiwa kwamba filamu ya Royal Tour yenye kupromote Utalii imegharimu Shilingi za Kitanzania Bilioni tisa. (9).

Leo tunaambiwa Rais ana safari ya kikazi yeye na delegation yake marekani na moja wapo ya mambo atayoyafanya ni kuzindua filamu ya Roya Tour.

Kwakua hizo kazi nyingine atazofanya hatujaambiwa ni zipi hivyo main task inakuwa ni Kuzindua filamu yake.

Ukiachana na matumizi ya Bilioni Tisa kwenye maandalizi ya filamu bado tunatumia tena mapesa mengine kwenye Uzinduzi na badala ya kuufanya hapa nyumbani tunaufanyia Marekani.

Matumizi ya mapesa haya yanafanyika kipindi tukiwa kwenye wave ya Corona maana tumeambiwa ipo na Vita Vya Ukraine.

Ukiachana na uwepo wa korona na vita ya Ukraine , Uchumi wetu umekumbwa na pigo la kupanda kwa bei za bidhaa muhimu jambo linaloongeza ukali wa Maisha kwa wananchi wa kawaida.

Inaleta ukakasi wa matumizi ya aina hii ya mapesa wakati Taifa likipitia kipindi kigumu namna hii.

Sijui viongozi wetu wanafikiria nini ila haipendezi kuzindua Filamu huko ughaibuni kwa mapesa mengi wakati kuna mtanzania hapa hata mlo wake tu unakua wa kuvizia na wakati juzi tu hapa Waziri Ummy anatuletea takwimu kwamba bado kuna idadi ya watanzania wanaojisaidia maporini(hawana vyoo)

Ningeiomba tu Serikali ijaribu kubana matumizi hasa kipindi hiki badala ya kuendelea kutumia fedha ambazo hatuna kwa mambo ambayo yanaonekana kabisa yasingefaa kufanyika kwa kipindi hiki.

Vile vile timing ya uzinduzi nayo sio nzuri maana jumuia za kimataifa zinahangaika na vita vya Urusi na Ukraine hivyo mwamko wa filamu hiyo utakua mdogo.

Wangesubiri mambo yatulie kidogo kama kweli tunataka kuipromote hiyo video.

Asanteni.



On top of that,

Uzinduzi unafanyika Marekani kuvutia watalii wakati Taifa la Marekani limekataza Raia wake kuja Tanzania kutokana na uwepo wa Korona.

Screenshot_20220413-232427.png
 
kubana matumizi ya serikali ni jambo la msingi sana, ukiruhusu hela zitumbuliwe tu kisa unaziingiza zingine sio kweli hakuna biashara ya hivyo. Kuna mahali lazima tujisahihishe
 
Watu njaa zimesharuhusiwa panda vichwani.

Hapa issue siyo Samia kwenda US, issue Ni mleta mada kutupwa NJE YA SYSTEM.

Anabweka bweka kila sekunde.
Kwahiyo unaona sawa kabisa mapesa tunavyoyamwaga kisa filamu tu.
 
Kwahiyo unaona sawa kabisa mapesa tunavyoyamwaga kisa filamu tu.
Badili hata ID maana kwa ID hi, kila utakachoongea utaonekana Ni njaa inakusumbua.

Bora hata huyo Samia anapambania kutafuta watalii, Kibwengo magufuli aliyekuwa anatumia mabilioni ya walipa Kodi kufurahisha nafsi yake tu.

Budget ya NEC kwa Jimbo moja la uchaguzi Ni Milioni 300.

Tulifanya CHAGUZI karibu 30 za kijuha juha tu eti watu wanting mkono Juhudi.

Leo, kina Mnyeti, Sabaya, Bashite, Kalemani na Genge lote la Magu Ni MATAJIRI wa KUTISHA kabisa.
 
Kwa akili ya Haraka haraka hizi Royal Tours walizofanya kina Kagame et al lengo kuu ni Ku-promote mtu na sio necessarily Taifa wala Utalii...

It just a Campaign sidhani kama hii kiti itaishi for the next 20 years..., nikitaka kujua kuhusu vivutio vya Tanzania nitawasikiliza ma-guides wenye kufanya hio kazi day in day out na sio rehearsal ya mwana-siasa
 
Badili hata ID maana kwa ID hi, kila utakachoongea utaonekana Ni njaa inakusumbua.

Bora hata huyo Samia anapambania kutafuta watalii, Kibwengo magufuli aliyekuwa anatumia mabilioni ya walipa Kodi kufurahisha nafsi yake tu.

Budget ya NEC kwa Jimbo moja la uchaguzi Ni Milioni 300.

Tulifanya CHAGUZI karibu 30 za kijuha juha tu eti watu wanting mkono Juhudi.

Leo, kina Mnyeti, Sabaya, Bashite, Kalemani na Genge lote la Magu Ni MATAJIRI wa KUTISHA kabisa.
Mkuu inaonekana unapata tabu sana na mimi.

Nikushauri tu uniignore.

Kwakua huna mamlaka ya kunipangia cha kufanya zaidi sana utaendelea kuumia tu.

Nizoee au nipotezee.
 
Mkuu inaonekana unapata tabu sana na mimi.

Nikushauri tu uniignore.

Kwakua huna mamlaka ya kunipangia cha kufanya zaidi sana utaendelea kuumia tu.

Nizoee au nipotezee.
Anyway, Magufuli alishakufa.

Tafuta njia nyingine ya kuishi Kama watanzania wengine

20220216_225742.jpg
 
Kwa akili ya Haraka haraka hizi Royal Tours walizofanya kina Kagame et al lengo kuu ni Ku-promote mtu na sio necessarily Taifa wala Utalii...

It just a Campaign sidhani kama hii kiti itaishi for the next 20 years..., nikitaka kujua kuhusu vivutio vya Tanzania nitawasikiliza ma-guides wenye kufanya hio kazi day in day out na sio rehearsal ya mwana-siasa
Mapesa meengi yameungua ila kwakweli sidhani kama tutafanikiwa kwa lolote.

Filamu inazinduliwa kwa ajili ya utalii wakati walengwa wenyewe mamefocus kwenye vita muda huu.

Pia inashangaza tunasema kuna korona halafu tunatengeneza video na kuizindua wakati wa korona.
 
Mleta uzi haelewi hata dhumuni la filamu iyo anabwabwaja tu
Dhumuni ni kupromote utalii.

Inashangaza unapromote vipi utalii watu wakiwa busy kwenye vita??

Hao watalii watapigana vita au kuja kutalii.
 
Mapesa meengi yameungua ila kwakweli sidhani kama tutafanikiwa kwa lolote.

Filamu inazinduliwa kwa ajili ya utalii wakati walengwa wenyewe mamefocus kwenye vita muda huu.

Pia inashangaza tunasema kuna korona halafu tunatengeneza video na kuizindua wakati wa korona.
Mimi naona hapo ni lengo la hao watawala kujitangaza wenyewe na sio necessarily utalii uliopo hii ni list ya wote duniani waliyofanya hii kitu

It has featured a number of world leaders including New Zealand's Helen Clark, Israel's Benjamin Netanyahu, Abdullah II of Jordan, Peru's Alejandro Toledo, Mexico's Felipe Calderón, Rwanda's Paul Kagame and Poland's Mateusz Morawiecki.

Common denominator inaweza kuwa hao watawala kuji-promote zaidi kuliko hata chochote kilichopo kwao...., Kwahio huenda kwao politically its money well spent (ukizingatia sio their hard earned cash)
 
Back
Top Bottom