Wana jf naomba niseme siungi mkono watu kuvamia mgodini,lakini serikali ya ccm iltegemea nini inapowafanya wanatarime kuwa watumwa kwenye ardhi yao?haijifunzi migogoro mingi africa inatokana na unyonyaji wanaofanyiwa wazawa ilipo rasilimali kama vile madini yaliyopo tarime?hivi watu wanapoona wanaumizwa wanahitaji kuhamasishwa na nani kama sio ugumu wa maisha ndio umewafikisha hapo?nataka serakali ya ccm ijifunze kuwa migogoro mingi inakuja kwa sababu ukisikia kuna waasi ujue kuna dhuluma inafanyika,wanatarime wameona mgodi huo hauna faida zaidi ya kuwafanya watumwa kwenye nchi yao, kwanza nimesikitishwa kauli ya kagasheki kuwa wananchi wale wamehamasishwa na wanasiasa wa chama fulani cha upinzani,sio kweli hawanufaiki na mgodi na wamekata tamaa,"can't u imagine mtu anakwenda kupambana na mtu mwenye silaha ya moto akiwa amebeba panga?"hamuoni kuwa wamechoshwa?leo mmeu tarime mkimaliza hapo mtaenda wapi tunaomba ratiba,lakini hii hali itaendelea kama watu wanaozungukwa na rasilimali muhimu hawanufaiki "mungu azilaze mahali pema peponi roho za marehemu ambao walikuwa wakipigana kupinga utumwa kwenye ardhi yao lakini wakauwawa kama wanyang'anyi" naamini ndio kwanza wamepanda mbegu ya ukombozi katika ardhi yao kwa kuwawa kwa risasi za serikali ya ccm .