Fixed account za benki na utajiri wa haraka haraka

Fixed account za benki na utajiri wa haraka haraka

Since UTT zinakua categorized kama low risks investment, usishangae return yake ni ndogo zaidi au Sawasawa na hio ya fixed account. The lower the risk, the lower the returns.
UTT wana product 5..
zisomeni hapa HOME trust me ni nzuri zaidi ya hayo MAFIX-DEPOSIT
 
Since UTT zinakua categorized kama low risks investment, usishangae return yake ni ndogo zaidi au Sawasawa na hio ya fixed account. The lower the risk, the lower the returns.
Uwekezaji katika UTT upoje mkuu, ni kununua share ama?kama una ufahamu huo tupe mwangaza kidogo,lakin nacho juwa KAMA ni ununuaji wa share basi kama kutakuwa na hasara mtagawana hasara kama kuna faida mtagawana faida according to what percent umewekeza
 
Uwekezaji katika UTT upoje mkuu, ni kununua share ama?kama una ufahamu huo tupe mwangaza kidogo,lakin nacho juwa KAMA ni ununuaji wa share basi kama kutakuwa na hasara mtagawana hasara kama kuna faida mtagawana faida according to what percent umewekeza
SOMA HAPA HOME
 
Mtui, ulishawahi kuwekeza katika UTT? Hebu tupe mwangaza,tupe experience yako faida na hasara, uliwekeza kwa kiasi gani ulipataje faida, tupe taratibu zao, usije kuta unaelewa UTT kwa story tupe experience tufungue mind zetu, tupe agreenlight,na kwanini uwekezaji UTT ni better than kufungua FIXED ACCOUNT nishawishi kwa facts

Ndo raha jf, share ur experience here with us..
 
Hili swala la kuweka pesa kwenye fixed account unategemea kupata faida unajidanganya. Ki maerufi ndyo pesa itaongezeka ila kihesabu unaweza kujikuta unahasara hasa kwa pesa ya Tz ambayp dhaman yake inashuka kila siku. Never do such kind of investment. Invest kwenye asset na sio liabilities au assets ambazo value yake inadepreciate. Goo deal ni kama unapesa kama m80 waweza nunua asset kama gold na ikatunza bank. In years value yake itakuwa imepngezeka ukilinganisha na kutunza pesa za value yake.
 
Asee Mkuu hesabu yako haiko Sawa kabisaaa, kama kwa mwaka riba ya access bank ni 15% then kwa miezi 3 riba utayopata ni 3/12×15%=3.75%, hio 3.75% ndio rates utayolipwa Mkuu, hio 13.8% ni impossible kabisa Mkuu.
Ni kweli kabisa bwana Mng'ato
 
Naomba kujua jamani ukiweka pesa fixed unaweza kuongeza? Na je ukiongeza inakuwa calculated vipi?
 
Uwekezaji katika UTT upoje mkuu, ni kununua share ama?kama una ufahamu huo tupe mwangaza kidogo,lakin nacho juwa KAMA ni ununuaji wa share basi kama kutakuwa na hasara mtagawana hasara kama kuna faida mtagawana faida according to what percent umewekeza
Mkuu naweza nikakueleza hapa lkn labda lugha yangu isiwe nyepesi, ngoja nimualike Mkuu @Sunctus Mtsimbe Naona anaweza kutuelezelea vizuri Mkuu
 
Check na BOT pia. Mtu binafsi waweza weka kuanzia 5m
 
Website za taasisi za kifedha zimelala awajaeleza kuhusu bidhaa zao kama za mikopo, malipo ya kadi, huduma za mobile money
 
Asee Mkuu hesabu yako haiko Sawa kabisaaa, kama kwa mwaka riba ya access bank ni 15% then kwa miezi 3 riba utayopata ni 3/12×15%=3.75%, hio 3.75% ndio rates utayolipwa Mkuu, hio 13.8% ni impossible kabisa Mkuu.
Correct, but still 13%per annum ni nzuri sana
 
kwanini usiwekeze UTT..ambao hutoa riba hadi 16%
Wacha wee,hawa nishasikia wako vzuri sana, japo sijaelewa je ni lazma kununua vipande au inakua ni unadeposit tu unasubiria riba regardless hali ya soko ilivo
Mana mtindo wa dividends soko likiwa baya inakula kwako
 
Wacha wee,hawa nishasikia wako vzuri sana, japo sijaelewa je ni lazma kununua vipande au inakua ni unadeposit tu unasubiria riba regardless hali ya soko ilivo
Mana mtindo wa dividends soko likiwa baya inakula kwako

Sijapata doc. ambayo ni current sana but nahisi hii itawapa mwanga.... mengine someni kwenye website yao

MAMBO MUHIMU KUHUSU MFUKO WA KUJIKIMU

• Madhumuni: Mfuko huu ni mpango ulio wazi wenye lengo la kukuza na kutoa gawio kutokana
na mapato ya ziada katika vipindi tofauti na pia kukuza mtaji kwa mwekezaji wa muda mrefu.
• Chaguo la Mpango wa Uwekezaji : Mfuko unatoa fursa mbili za uwekezaji - (a) Mapato ya robo mwaka (b) Mapato ya mwaka yaliyoambatanishwa na ukuaji wa vipande (growth option)
• Nani anaruhusiwa kuwekeza:
Mfuko uko wazi kwa watanzania walio ndani na nje ya nchi, watu binafsi, makampuni/taasisi, mabenki, asasi za kiraia (NGO) n.k. kama inavyoonyeshwa kwenye waraka huu.
• Thamani ya Mwanzo ya Kipande:
Thamani ya mwanzo ya kipande (face value) ni Sh. 100.
• Bei ya Kipande (Issue Price):
Vipande vitauzwa kwa bei ya Sh. 100 kwa kila kipande wakati ya mauzo ya awali (kuanzia 3 Novemba 2008 hadi 29 Novemba, 2008) na baada ya hapo kipande kitauzwa kulingana na thamani halisi.
• Mipango ya mgao wa Mapato:
Mpango wa mapato kila robo mwaka na mpango wa mara moja kwa mwaka wenye gawio na ukuaji.
• Kiwango cha Chini cha Kuwekeza:
Ni Sh. milioni 2 kwa mpango wa mapato ya robo mwaka, na Sh. milioni moja kwa mpango wa gawio kwa mwaka na Sh. 5,000 kwa mpango wa ukuaji wa mtaji kwa mwaka.
• Uwekezaji wa Nyongeza:
Kiwango cha chini cha uwekezaji wa nyongeza/unaofuata
(additional investment) ni Sh.15,000 kwa mpango wowote wa gawio na Sh. 5,000 kwa mpango wa ukuaji wa mtaji kwa mwaka, hakuna ukomo wa kiwango cha kuwekeza
• Ukwasi:
Ununuzi na Uuzaji wa vipande utafanyika kila siku ya kazi kuanzia tarehe 16 Aprili, 2009 yaani miezi minne na nusu baada ya kufungwa kwa kipindi cha mauzo ya awali.
Dhamana ya Uwekezaji Tanzania (UTT) itatuma malipo ya mauzo ya vipande ndani ya siku 10 za kazi tangu kuwasilishwa kwa maombi ya mauzo.
• Uwazi:
Dhamana ya Uwekezaji Tanzania (UTT) itafanya tathmini na kutangaza thamani halisi ya kwanza ya mfuko (Net Asset Value) katika kipindi kisichozidi siku 60 tangu kufungwa kwa mauzo ya awali na baadaye itatathmini na kutangaza kila siku ya kazi. Hali kadhalika
Dhamana ya Uwekezaji Tanzania (UTT) itatoa mgawanyo wa uwekezaji (Investment portfolio) kwa kila robo mwaka.
• Uhamishaji wa Vipande:
Uhamishaji wa vipande kutoka kwenye mfuko mmoja kwenda mwingine kati ya mifuko inayoendeshwa na Dhamana ya Uwekezaji Tanzania unaruhusiwa.
Uhamishaji huu utatumia thamani halisi ya kipande kwa wakati huo bila gharama yoyote.
Uhamishaji huo utafanywa kwa mauzo ya vipande kutoka kwenye mfuko mmoja na
kuviwekeza kwa kununua vipande kwenye mfuko mwingine, ilimradi sifa za kuwekeza kwenye mfuko mwingine zimezingatiwa.
• Makato ya Kodi:
Kulingana na sheria za sasa, kodi ya mapato haitotozwa kwenye gawio litokanalo na uwekezaji kwenye mfuko huu.
• Kuorodheshwa:
Kwa sababu ni mfuko uliowazi ambapo manunuzi na mauzo ya vipande yatafanywa wakati wote na Dhamana ya Uwekezaji Tanzania (UTT), vipande vya mfuko
havitapendekezwa kuorodheshwa kwenye soko lolote la hisa. Hata hivyo, hapo baadaye
Meneja wa mfuko, baada ya kushauriana na Mwangalizi wa Mfuko na maombi yake kupitishwa na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, ana uwezo wa kuamua kuorodhesha vipande vya mfuko kwenye masoko ya hisa.
 

Attachments

Interest= Capital*Rate*Time
Ndio unapata iyo faida ukiweka pesa yako. Nimefanya Research yangu ktk izi bank apa Tanzania. Wanayotoa Riba kubwa ni Exim bank account. Wanatoa Riba ya 8%. Kama umeweka 1 milioni unapata 80,000 kwa mwaka.
 
Asisahau na kutoa tax charges wakati anapokea faida yake.
fixed account huwa ni kiasi ulichoweka x muda x rate/100
mfano unataka kuweka mil 100 fixed account kwa mwaka (miezi 12) kwa rate say 8%
calculations inakua 100,000,000 x 12/12 x 8/100 = 1,000,000/= hii uliyoipata toa 10% yake kama kodi inaenda serikalini.
10/100 x 1000000=100,000/= utabakiwa na laki tisa.

kwa hiyo baada ya mwaka utapewa zile mil100 zako pamoja na laki tisa. hivyo utaondoka na Tsh 100,900,000/= tu.

kama mlikubaliana iwe miezi 6 yaani nusu mwaka calculations zitakua zilezile isipokuwa badala ya kuzidisha kwa 12/12 itqzidishwa na 6/12 utapata kilo 5 ukiondoa kodi 10% ya hiyo unaondoka na kilo nne na nusu tu + ile mil 100 zako hayo tu ndio inavyokua na si vinginevyo. ahsante
 
Back
Top Bottom