Fixed account za benki na utajiri wa haraka haraka

Fixed account za benki na utajiri wa haraka haraka

Niliwahi kusoma humu JF kuwa kwenye saccos ukiweka 2.5m baada ya miezi mitatu wanakukopesha 10m. Hii naona imekaa vizuri zaidi kuliko fixed account. Naomba wenye uelewa na hii issue watudadavulie kwa niaba ya wote.
Kuna ukweli mkuu,ila sio utoe million 2.5 then upate millioni 10 labda, ngoja nitoe mfano, kwa mfano ngoja niwape somo kwenye hii saccos,kuna kkkt dayosisi ya kaskazini saccos, hawa ni saccos ambayo ilinivutia utendaji na uwekezaji wake, wame invest sana kwa mfano wana mashamba mbalimbali eg la miti nk na wana bank yao binafsi wana mifugo nk, wao wana masharti simple sana, kujiunga yani kufanya registration ni laki 250000TSH na fomu ni Tsh 50 elfu tu hapo unakuwa mwanachama utafungua account chini wa umiliki wako,

baada ya usajili utakuwa mwanachama na ukikaa miezi mitatu unaruhusiwa kuomba mkopo kwa sharti dogo kabisa kumuomba mwanachama mwenzako wa hiyo hiyo saccos ili akudhamini ukopaji ule na utakopeshwa kulingana na account yako ina kiasi gani lakini wata double mkopo kutokana account yako inasoma kiasi gani, mfano kama una million 5 kwenye account yako basi utapewa MKOPO wa MILION 10 ,kama kwenye account yako una MILION 10 basi utapewa MKOPO wa MILLION 20 kama una MILLION 30 basi utapewa MILLION 60 na riba ni ndogo sanaaa kwa kuwa ni mwana chama, halafu kila vikao mtakavyo kaa kujadili miradi ya saccos na shughuli nyingine basi huwa mnalipwa sitting allowance, pia huwa kuna gawio la faida la mwaka yani kila mwisho wa mwaka dividend inatolewa according to what is read in your account...
43521b146637a515b28c561f039cb5e8.jpg
 
Nimejifunza vitu hapa nilitaka nikafungue hiyo akaunti ya principle ya 10m kumbe haina faida
 
Wakuu wana JF,

Kuna tetesi kuwa ukifungua fixed account ya 10Million ktk benk za Exim, CRDB, Posta bank , NBC limited au NMB , kwa kila baada ya miezi mitatu - inazaa faidi kati ya sh. 1.8 mill up to 2.1 mil.

Hii ina maana kuwa kwa muda wa mwaka 1, yaani 12 months unakuwa umepata faida ya sh.7.2 million up to 8.4 milion,

Je hizo habari zina ukweli wowote? kwa anayefahamu plse naomba tufahamishe na sisi ili tuweze invest soon ktk hiyo fixed account.

NB: Nimeuliza hilo coz nipo mbali kidogo, huku madongo kuinama ningekuwa jirani ningefanya follow up nije na data kamili


Asanteni,

Nawasilisha
Think Big brother. 8.4 millions per year ni hela kidogo sana. Hiyo unatakiwa uipate ndani ya mwezi mmoja au chini ya hapo.
 
dah! sio kweli, kila mtu angeziweka benki maana tunavyoogopa risks za biashara ndo mambo yangekuwa murua huko
 
Ukiwekeza kwangu kila mwezi nitakupatia TShs laki 6 monthly. so kwa miezi mitatu ni million 1 na laki nane, kwa mwaka ni million 7 na laki mbili.......but tunaingia mkataba wa miezi mitatu mitatu renewable.......................

If you ARE interested ni PM for More clarifications
Una biashara gani?
 
I know bank huwa interest rate hazitofautiani sana not sure if its BOT regulating it or not.
Ila EXIM interest rate ya fixed & deposit A/C rate ni 6% kwa miezi mitatu so sijui hizo bank nyingine ulizotaja.

SO 10 million +6% = tshs 600,000 kwa miezi mitatu.

Hizo no data za ukweli toka Exim hata mimi ninayo hiyo account
mkuu mbona mi hesabu nimepata 150,000 badala ya 600,000 ?
 
I know bank huwa interest rate hazitofautiani sana not sure if its BOT regulating it or not.
Ila EXIM interest rate ya fixed & deposit A/C rate ni 6% kwa miezi mitatu so sijui hizo bank nyingine ulizotaja.

SO 10 million +6% = tshs 600,000 kwa miezi mitatu.

Hizo no data za ukweli toka Exim hata mimi ninayo hiyo account

Mkuu unafanyeje hesabu without considering period of time?
 
Mkuu utajiri wa haraka haraka uonaoutaka hauuwezi kupatikana kwa njia ya kuhifadhi Fedha kwenye akaunti za muda maalum bali akaunti ya muda maalum inaweza kukusaidia kutunza fedha kwa muda ili kufikia malengo yako, kwa mfano umepokea malipo ya nyumba yenu ya ukoo mliyoiuza na ww hautaki kuzitawanya fedha zako kwa anasa mara moja basi unaweza kuzihifadhi kwenye akaunti ya muda maalum ukitafakari nini cha kufanya.
Kwa sasa Benki ambayo inatoa riba kubwa kwenye akaunti za muda maalum ni Access Bank wao kwa kiwango cha hiyo Tshs 10,000,000/= kwa miezi 6 wanatoa 9.5%, na hesabu zinakuwa kama ifuatavyo:
Mtaji wako ni Mill 10 na faida ni 9.5% kwa miezi 6
Fanya hivi 9.5% ÷ 100 = 0.095
Kwa kuwa faida inapatikana kwa miezi 6, kinachofuata ni
Miezi 6 ÷ miezi 12= 0.5 hichi ulichokipata
0.5 × 0.095 = 0.0475 sasa hii ni factor utakayoizidisha kwa Tshs Mill 10 ili kujua utapata Tshs ngapi?
0.0475 × 10,000,000 = Tshs 475,000/= hii fedha hauichukui yote kuna kodi ya Serikali inaitwa "with holding tax" yaaani kodi ya zuio ambayo ni 10% ya Hiyo faida utakayo pata, hivyo basi
Tshs 475,000 × 0.1 = 47,500/= kiwango halisi cha kwako ni
Tshs 475,000 - 47,500 = 427,500 hizo ndo fedha zako ww.

Ukiwa na fedha nyingi kwa mfano Billioni 5 akaunti ya muda maalum inaweza kukupa fedha angalau lakini si kwa fedha kiduchu kama hizo ulizokuwa nazo.


Nawasilisha.
 
Kwa wenzetu wenye pesa ya Ukweli wanapata faida mfano umeweka Mil 50
Kwa mwaka unapata faida ya Mil 4.
Aisee lakini ni kwa sababu tu wengi hatujaona fursa..ila kweli niweke ml50 kwa mwaka mzima nipate faida ml4 tuu???nitakua namkosea mungu
 
Aisee lakini ni kwa sababu tu wengi hatujaona fursa..ila kweli niweke ml50 kwa mwaka mzima nipate faida ml4 tuu???nitakua namkosea mungu
Unajua bank [emoji542] nyingi zinaletwa kwa ajili ya watu tofauti tofauti kama mtu ana uwezo wa kufanya biashara ndio anaweka katika fixed deposit. Izi bank account [emoji542] na zenyewe zinafanya biashara. Watu wengi tunakosa elimu ya biashara ndio maana tunalalamika na hata kama unaenda bank unatakiwa kuuliza sana maana wanaweza wanakudanganya ukaweka mkwanja wako kwa muda mwingi kwa faida kidunchu
 
Ndio maana mfanyabiashara kuweka pesa katika fixed deposit uwezi kumkuta anaweka huko kwa sababu anayo elimu ya pesa ni bora akanunua hisa katika soko la hisa (mitaji) la DSE kuliko kuweka katika bank account [emoji542]
 
The only way utakapofaidi fixed account ni kama una bulk money meaning 50m+ but if u have lower than that nenda kanunue hisa DSM stock exchange.
 
The only way utakapofaidi fixed account ni kama una bulk money meaning 50m+ but if u have lower than that nenda kanunue hisa DSM stock exchange.
Ni kweli kabisa mkuu
Sema tatizo lililopo mkuu watu wengi wanachambua kisiasa siasa tuuu. Sisi watanzania tunajua sana siasa kuliko mambo ya siasa. Angalia Uzi kama huu unakuta unachangiwa na watu wachache sana
 
Wapendwa I have a certain sum of money ambayo sitarajii kuitumia soon na nimefikiria kufungua fixed account niweke angalau kwa mwaka mmoja ila sijawahi fungua hiyo account before kwa hiyo kwa wale wanaojua rate of interest ya fixed account especially kwa CRDB wanieleze tafadhali

Nenda CRDB Bank wana akaunti ya Thamani na Dhahabu ambazo zinatoa riba kubwa ya 13% ukiwa na Thamani au 10% ukiwa na Dhahabu pia unauwezo wakupata makopo hadi asilimia 80% ya amana zako.

Wasiliana nao upate maelezo zaidi.
 
Nenda CRDB Bank wana akaunti ya Thamani na Dhahabu ambazo zinatoa riba kubwa ya 13% ukiwa na Thamani au 10% ukiwa na Dhahabu pia unauwezo wakupata makopo hadi asilimia 80% ya amana zako.

Wasiliana nao upate maelezo zaidi.
Ni kweli mkuu kuna FD nzuri tu kwa uwekezaji ambao hautokuumiza kichwa kwa riba hiyo ya 13% crdb ukiweka 20ml kila mwezi unakunja 216,000 kama riba yako na unawekewa moja kwa moja katika ac yako ya kawaida
 
Habari kwako pia mkuu,ngoja nikupe faida za fixed account,faida moja wapo katika fixed account at maturity time huwa kuna riba(interest rate) ila rate zinatofautiana kati ya bank na bank,faida nyingine pia huwa hakuna ada ama makato ya mwezi maana siku ikiwa matured utapewa pesa yako kama ililivyo na faida ya riba juu,na pia riba huwa ina ongezeka kutokana na unataraji kuchukuwa kwa muda gani yani muda wa ku-mature,huwa kuna miezi 3,6,12,24...Mimi binafsi napenda kuweka kwa miezi 3 na kwanini fixed account ni kwa kuwa unakuta nina jambo natarajia kulifanya kama baada ya miezi kadhaa nichukuwe pesa yangu hasa nikiwa na malengo ya kujenga nyumba ama kuwekeza kwenye shamba, ama kama nataka gari na hela haijatoshelea huwa naweka kwenye fixed account kwa kuwa hela ya kwenye fixed account masharti yake haruhusiwi kifanya withdraw mpaka time of maturity,mimi huwa sipendi kuweka hela kwenye fixed account kwa muda mrefu huwa sizidi miezi mitatu kwa kuwa kuna emergency ya mahitaji huwa katika hali ya kawaida hutokea na unahitaji pesa kwahiyo sishauri kuweka hela kwenye fixed account mwaka mzima, ni heri uweke miezi mitatu ama miezi sita then una renew kuna unafuu, ila yote kwa yote kuweka fedha kwenye fixed account ni kamchezo kazuri sana na hela inakuwa at safe side kuepuka matumizi ya kiholela na pesa utaichukuwa kama ilivyo na faida juu....mimi huwa napenda kuwekeza kiasi kikubwa kwenye fixed account ndo faida yake utaona kuanzia milioni kumi na kupanda juu ila pia kwa miezi michache
Nikiweka milioni 21 NMB Kwa miezi 3 nitapata riba Tsh. Ngapi?
 
Kwa wenzetu wenye pesa ya Ukweli wanapata faida mfano umeweka Mil 50
Kwa mwaka unapata faida ya Mil 4.
Huu ni uvivu wa hali ya juu, uweke bank milioni 50 kwa mwaka faida ya milion 4, wakati unauwezo wa kuweka kwenye biashara milion 5 ukapata kila mwezi milioni 1 sehe ambayo hata haijachangamka, kweli tuna mawazo tofauti, mimi leo unipe milion 20 baada ya mwaka utanishangaa
 
Back
Top Bottom