Flaviana Matata amjia juu anayedai kumfikisha alipo

Flaviana Matata amjia juu anayedai kumfikisha alipo

Binti Maringo

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
2,804
Reaction score
96

Haya ma-celeb wetu wa kibongo hawa...Inabidi wafundiswe PR......



flaviana matata amjia juu anayedai kumfikisha alipo
Dear Ankal Michuzi,
Nimesoma nukuu inayosema kwamba binadamu siku zote tunapenda kupata sifa isiyo stahili kwa mazuri tu lakini mabaya tunasingizia bahati mbaya.
We always take credit for the good and attribute the bad to fortune. Maneno haya yamenichoma moyoni kwani nimeona kuwa yana ukweli katika maisha yetu ya kila siku. Nimefanya kazi siku zote bila kujali mwenzangu au wenzangu wanafanya nini, na sipendi kutangaza mafanikio yangu yote.
Ila kuna watu maishani ambao wamenisaidia kufika hapanilipo na hata wao huwa wanaishi kwa kufuata msingi wa kuwa “tendawema uende zako”, na hawajawahi kukaa na kujitangazia kuwa wao ndo wamenifikisha hapa nilipo ingawa ni kweli.
Cha ajabu ni pale kuona kuwa kuna mtu ambaye namfahamu kawaida tu na hatuna mazoea wala hajuiniishivyona nimefika vipi hapa nlipo inasemekaana kuwa yeye ndo kanifikisha hapa nilipo. Kibaya zaidi si kuwa kaongea hadharani na marafiki zake bali ni kuiweka bayana katika gazeti.
Kitendo hiki kimenishtua na kunisikitisha kwanimimi binfasi sijawahi kuongea katika magazeti kuhusu maisha ya mtuwala kudai kuwa mi ndo nimemfikisha mahala fulani. Lakini chakusikitisha zaidi, watu ambao kweli wamenisaidia katika maisha yanguhawajawahi kukaa na ‘kuuza sura’ kwa kutumia jina langu.
Mafanikio yangu madogo nilonayo sasa ndani na nje ya nchi yamefikiwa kwa juhudi zangu na zawatu wachache, hii ni pamoja na kupatikana kwa mkataba wangu wa nje(Afrika Kusini) na mkataba na maelewano yote ni kati yangu mimi,kampuni yangu ya Afrika Kusini na kampuni yangu mama ya CompassCommunications.
Hatua zozote zilizochukuliwa hazikumhusisha mtanzaniamwingine. Na hata katika siku zijazo, itaendelea kuwa hivyo. Kwaheshima na taadhima naomba mhusika na wahusika, waache kuongeleamaisha yangu, mafanikio yangu, kwani haiwahusu.
Pia naomba wanajamii wenzangu mkisikia kitu kinazungumzwa ambacho hakijatoka kwangu au kampuni yangu mama, basi wajue atakuwa ni binadamu mwingine ambaye ametetereka na kuingia katika mtego ule wakutaka kupata sifa asizostahili.
Mwisho kabisa napenda kuwashukuru wote ambao wapo sambamba na watanzania wote kwa ujumla
Regards,
Flaviana Matata
 
Haya ma-celeb wetu wa kibongo hawa...Inabidi wafundiswe PR......



flaviana matata amjia juu anayedai kumfikisha alipo


Dear Ankal Michuzi,



Nimesoma nukuu inayosema kwamba binadamu siku zote tunapenda kupata sifa isiyo stahili kwa mazuri tu lakini mabaya tunasingizia bahati mbaya.



We always take credit for the good and attribute the bad to fortune. Maneno haya yamenichoma moyoni kwani nimeona kuwa yana ukweli katika maisha yetu ya kila siku. Nimefanya kazi siku zote bila kujali mwenzangu au wenzangu wanafanya nini, na sipendi kutangaza mafanikio yangu yote.



Ila kuna watu maishani ambao wamenisaidia kufika hapanilipo na hata wao huwa wanaishi kwa kufuata msingi wa kuwa "tendawema uende zako", na hawajawahi kukaa na kujitangazia kuwa wao ndo wamenifikisha hapa nilipo ingawa ni kweli.



Cha ajabu ni pale kuona kuwa kuna mtu ambaye namfahamu kawaida tu na hatuna mazoea wala hajuiniishivyona nimefika vipi hapa nlipo inasemekaana kuwa yeye ndo kanifikisha hapa nilipo. Kibaya zaidi si kuwa kaongea hadharani na marafiki zake bali ni kuiweka bayana katika gazeti.



Kitendo hiki kimenishtua na kunisikitisha kwanimimi binfasi sijawahi kuongea katika magazeti kuhusu maisha ya mtuwala kudai kuwa mi ndo nimemfikisha mahala fulani. Lakini chakusikitisha zaidi, watu ambao kweli wamenisaidia katika maisha yanguhawajawahi kukaa na ‘kuuza sura' kwa kutumia jina langu.



Mafanikio yangu madogo nilonayo sasa ndani na nje ya nchi yamefikiwa kwa juhudi zangu na zawatu wachache, hii ni pamoja na kupatikana kwa mkataba wangu wa nje(Afrika Kusini) na mkataba na maelewano yote ni kati yangu mimi,kampuni yangu ya Afrika Kusini na kampuni yangu mama ya CompassCommunications.



Hatua zozote zilizochukuliwa hazikumhusisha mtanzaniamwingine. Na hata katika siku zijazo, itaendelea kuwa hivyo. Kwaheshima na taadhima naomba mhusika na wahusika, waache kuongeleamaisha yangu, mafanikio yangu, kwani haiwahusu.




Pia naomba wanajamii wenzangu mkisikia kitu kinazungumzwa ambacho hakijatoka kwangu au kampuni yangu mama, basi wajue atakuwa ni binadamu mwingine ambaye ametetereka na kuingia katika mtego ule wakutaka kupata sifa asizostahili.


Mwisho kabisa napenda kuwashukuru wote ambao wapo sambamba na watanzania wote kwa ujumla




Regards,


Flaviana Matata


Ya. Namuuunga mkono sana. Aliyemfikisha hapo kishamaliza kazi yake na achuke time. Huyo jamaa aliyemfikisha hapo aliona kipaji cha huyo binti ndiyo maana akajitahidi kumleta hapo alipo. Mbona wengine hakuwatafuta ili kuwafisha hapo alipo Flaviana? Katika life, siku zote haimaanishi kwamba kwa kuwa umepitia hatua fulani kimaendeleo, basi ni lazima urudi huko kusalimia au kunyenyekea. Labda niulize shwali: ni wangapi waliojaribu kuulizia au kutafuta waalimu wao wa chekechea, primary na secondary school ili waende wakawape shukrani kwa mafanikio yao ya sasa? Kama wapo baso ni asilimia 0.0009! Flaviana keep it up na songa mbele. Achana na vijilawama vya kidwanzi vya kibongo.
 
Niimeona mtu kaweka coment kwenye blog ya Uturn na eti huyo Millen hakumsaidia kitu chochote, naona mwanzo wa mabifu unanukia
 
Kosa ni kutangaza Hadharani au kusema kwake Ukweli ? Mti unapo zaa matunda tusisahau kwamba una shina na mizizi..!! Big mistake kwa dada yangu..

Asinge pungukiwa kitu kama angeamua kukaa kimya kwani mwenye kudai ndiye aliyemfikisha hapo angeji chokea na kujikalia kimya baada ya muda...!!
 
Niimeona mtu kaweka coment kwenye blog ya Uturn na eti huyo Millen hakumsaidia kitu chochote, naona mwanzo wa mabifu unanukia


LOL!...Mimi nilidhani anaoongelea hapa ni modeling agency fulani kuwa inamsema kuwa hana fadhila kumbe ni beef za BFF's?.....sasa si waambiane wenyewe kwa wenyewe kuna sababu gani ya kuanza kuingia kwenye blog?.....
 
Kuna tofauti kubwa kati ya walioenda shule na wasioenda!

Mama Subi...Kama shule Flaviana ameenda i think ana degree ya Engineering from UDSM!.....Kama sikosei nilimsikia katika interview yake aliyofanya alivyokwenda kwenye ile big brother Africa-Revolution......

Oh well pia kuna shule za aina mbili unaweza ukaenda shule just because or ukaenda shule kupata education ili uweze kuwa somebody..... career wise....
 
LOL!...Mimi nilidhani anaoongelea hapa ni modeling agency fulani kuwa inamsema kuwa hana fadhila kumbe ni beef za BFF's?.....sasa si waambiane wenyewe kwa wenyewe kuna sababu gani ya kuanza kuingia kwenye blog?.....

Yani hata mie nilidhani ni Agency wake, mhh mambo kweli yeye Lavvy anadai kuwa hajawahi msaidia kwa lolote wala huyo Millen hapajui nyumbani kwa Lavvy jamni haya tutafika tu wadada wanamambo!


Binti maringo hiyo avatar yako balaaa nipunguzie kidogo plz!!!!!
 
Yani hata mie nilidhani ni Agency wake, mhh mambo kweli yeye Lavvy anadai kuwa hajawahi msaidia kwa lolote wala huyo Millen hapajui nyumbani kwa Lavvy jamni haya tutafika tu wadada wanamambo!


Binti maringo hiyo avatar yako balaaa nipunguzie kidogo plz!!!!!


Kama ndiyo hivyo yeye Millen si a-move on tuu...Wanasema "Tenda wema uende zako usingoje shukurani"...Au yeye Millen alitegemea 10%?...kama hamkuandikiana mein! forget about it!....

Besides Millen si yupo na contact na Ford USA?.....Kwa maana hiyo yupo juu zaidi sasa si asonge mbele tuu kuliko kukaa na kupigiana makelele jamani eeh!......

Haya Maria Roza nitakupunguzia lakini how?
 
[/FONT]

Kama ndiyo hivyo yeye Millen si a-move on tuu...Wanasema "Tenda wema uende zako usingoje shukurani"...Au yeye Millen alitegemea 10%?...kama hamkuandikiana mein! forget about it!....

Besides Millen si yupo na contact na Ford USA?.....Kwa maana hiyo yupo juu zaidi sasa si asonge mbele tuu kuliko kukaa na kupigiana makelele jamani eeh!......

Haya Maria Roza nitakupunguzia lakini how?

mhh hii ishu naona wanajuana wenywe kiundani maana duh! nanukuu kutoka kwenye coment za wadau wa Uturn


Happyness Magese ama Millen ambae pia ni model huko sauz amehojiwa na gazeti
jana na akadai kwamba yeye ndie haswa aliempokea flaviana huko south africa na
ndie aliemfikia alipo kwa kumsaidia hapa na pale.
 
facesFlaviana.jpg
 
Ok, not that I care, but since a name has been dropped, i just read a link from Haki blog and found the article "Meteoric rise of Tanzanian beauty..."

Assuming Millen Magesse is the concerned culprit, could the misleading part be this paragraph;

The 179cm tall model was the first Tanzanian model to be signed by Ice Models in South Africa. She later paved the way for former Miss Universe Tanzania Flaviana Matata.

I think it is a language problem by the accusser and Millen Magesse has done nothing wrong. Infact, if you read the article well, it is not an interview, and Millen is not quoted at all.
 
Mama Subi...Kama shule Flaviana ameenda i think ana degree ya Engineering from UDSM!.....Kama sikosei nilimsikia katika interview yake aliyofanya alivyokwenda kwenye ile big brother Africa-Revolution......

Sidhani kama taarifa hizi ni sahihi maana wakati anachipukia na kwenda sijui kwenye miss universe ile alikuwa hajaenda hata college na baada ya hapo ndio akatoka, sikuwahi kusikia kuwa anasoma au amesoma UDSM na by that time mimi mwenyewe nilikuwa nasoma pale, kwa umaarufu alioupata ghafla hata kama si kumuona ningeshasikia uwepo wake pale..otherwise it is very simple kwa mtu aliyezaliwa 1987 na kusomea katika system hii ya kitanzania si rahisi awe ameshasoma na kumaliza University tena 4 years course, sana sana labda sasa ndio angekuwa anamaliza.
 
...lakini baadhi ya masuper stars wabongo huwa wana kasumba ya kukataa ukweli,kama mtu ni kweli amekusaidia hata kama ni kwa kiasi kidogo kwanini umkatae,inawezekana ni juhudi zake ndizo zilizomfikisha hapo lakini huwa tunasahau ku-appreciate hata support ndogondogo tunazopata toka kwa watu wengine.,inawezekana ndiye aliyemsaidia kusettle huko bondeni hata kama kipaji alikuwa nacho tayari lakini huo nao ni msaada lazima uheshimiwe.
 

Mmh kwa kubong'oa nusu uchi ndio amefanya kazi ya ziada,hivi baba,mama,kaka,dada na ndugu wengine kweli wanafurahia binti wao kuwa yuko kazini kwa kuwabong'olea hivyo jamani,hivi kwanini mtu usiende shule ukasome na upate kazi ya heshima,kazi zingine zinadharirisha ingawa wengine wanaona ndio u celeb hadi wanaanzisha malumbano,hiyo picha haina tofauti na wale wa Ambiance na wa Ohio tena hata hao wanastaha kidogo sababu wanafanya kwa kujificha usiku na si kwa kujianika mwaaa
 
mhhh wabongo bana,
tunafurahiiiiisha.kwa kweli.
 
Back
Top Bottom