FMEs!: Msiba Clouds Radio & Kusaga!

FMEs!: Msiba Clouds Radio & Kusaga!

Joined
Apr 27, 2006
Posts
26,584
Reaction score
10,400
- Habari zilizopatikana hivi punde toka South Africa, ni kwamba Baba wa The Greatest promoter and entertainer nchini Ndugu yetu Joe Kusaga, yaani Mzee Kusaga, amefariki leo huko South Africa, alikokuwa akishikiri katika matibabu ya ugonnjwa mbaya sana wa kansa, ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda sasa.

- Hizi ni habari za majonzi sana wapenda michezo wote nchini, kwani Joe na Marehemu, wameshiriki sana tena kwa kiwango kikubwa sana kuu-create na kuuinua mziki wa kizazi kipya nchini yaani Bongo-Flava. Ninakumbuka Clouds Disco, toka in the 80s ilipoanzishwa rasmi na Kaka yake Joe, Mkulu Justin Kusaga na in the the 90s, ikachukuliwa na kufufuliwa upya na Joe, ambaye kwa kushirikiana na Marehemu ambaye siku zote alikuwa behind the scene hasa ofisini, wameiwezesha Clouds leo kuwa ni the Giant entertainment wa muziki nchini, na hasa jiji la Dar.

- Ninatoa pole kwa moyo mzito sana, kwa Brother Joe Kusaga, Bro Gody, Bro Andy na familia nzima ya Kusaga, Mungu awape nguvu, ujasiri na busara katika kipindi hiki kigumu sana cha majonzi ya kuondokewa na mzee.

- Bwana ametoa na Bwana ametwaa, lihimidiwe jina la Bwana Mungu. tutaendelea kufahamishana maendeleo ya matayarisho ya mazishi ya Marehemu Mzee Kusaga, ambaye mwili wake unatarajiwa kurejeshwa siku ya Alhamis.

Mungu Awabariki Familia Nzima ya Kusaga!

Respect.


Field Marshall Es
 
RIP mr Alex Kusaga poleni akina Joseph,Andrew
Bwana ametwa na bwana ametoa jina la bwana lihimidiwe.

Nimeona hili tangazo James Malongo ametangaza kwenye his Blog this afternoon.

Amen
 
Hii ni habari ya kusikitisha lakini tumshukuru Mungu kwani alitoa na ametwaa.

Natoa salamu zangu za pole kwa familia ya akina Kusaga. Nakumbuka miaka ya 80s jina hili lilikuwa maarufu sana hasa kwa tulosoma maeneo ya mjini Dar-es-Salaam hasa Forodhani na nakumbuka hata dada yao Judith alisoma hapo.

RIP Mzee Kusaga.
 
rip mzee kusaga!
THE WORLD IS MISSING YOU
 
Poleni sana wana familia hii, na Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu.
 
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi.Ameni
 
Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi zinahesabiwa
rip mzee wetu
amen
 
nawapa pole wadau wote wa muziki na clouds fm wote,kipekee familia nzima ya Ndugu yetu J.Kusaga.

Mungu awatie nguvu hasa wakati wa majonzi na mgumu kwenu.

tupo pamoja nanyi kisala,mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi.amen
 
Poleni sana familia yote ya Kussaga kwa kuondokewa na baba mpenzi.

Mungu awape faraja katika kipindi hiki kigumu.
 
- Wakulu salam kwa wananchi wote, leo jioni Marehemu Mzee Wetu Kusaga, Alex ndio amezikwa rasmi kwenye viwanja vya Kinondoni. Ni muda mchache sana uliopita nimemaliza kuongea na Brother Joe, kuhusu shughuli nzima ya mazishi a very sad day kwa wapenzi wote wa muziki wa kizazi kipya.

- Ninaomba kukumbuka tulikotoka kidogo, unajua mzazi wangu at onetime alikuwa RC Mwanza, na Mzee Alex Kusaga, alikuwa msaidizi wake kama assistant Administrator pale ofisini hii ni longtime ago, and then tukakutana tena Dar na mashirikiano makubwa sana na Joe ya binafsi na hasa kwenye Muziki, then wote tulikuwa tunapiga ma-Disco, mimi kwenye maharusi na ma-party na yeye kwenye Disco la Big Brother Justin, yaani Disco Clouds, mpaka wakati mmoja Disco RSVP Mbowe Club, ambalo ndilo lililokuwa the power House mjini lilipofungwa kwa big renovations, ndipo Joe akawa creative na kukusanya vyombo hapa na pale tena vya Domestic na kuanza kupiga disco pale Motel Afrique, nakumbuka jinsi ambavyo ilikuwa kila baada ya muziki kuisha usiku ilikuwa lazima tusaidane kurudisha meza na viti vya hotel ili asubuhi iweze kutumika tena kama Restaurant ambalo lilikuwa ni sharti kubwa la kupewa pale kupiga Disco!

- Ninakumbuka kumpokea safari ya kwanza ya Bro Joe, NYC kutafuta vyombo vya kurekodia na Disco, akiwa njiani kuhamia Leaders Club hii in the 90s, tukaishia kukodi gari pale NYC na kuendesha kwenda kuvinunua DC Washington, ninakumbuka DC tumefikia kwenye Apartment ya Waziri Masha then akiwa mwanafunzi wa MBA pale Georgetown, pia tuliwakuta washikaji kama Lukuba, Adriani, Chitumbi, Simbo na Bandawe, baadaye tukarudi tena NYC, ambapo we were able to work together on Brother Joe's first produced album nafikiri wapenzi wengi wa Bongo-flava mtaikumbuka kwa jina la "Hoya! Msela" na all this time we always had to report back maendeleo kwa Marehemu, ambaye mwanzoni alisita sana kuafiki Joe kupiga Disco pale Motel, lakini at this point tulipokuwa tunatengenza hii album ya kwanza ya muziki wa kizazi kipa Tanzania, alikuwa in full support.

- Since then Brother Joe hajawahi kuangalia nyuma amekua akisonga mbele tu, ikaja Radio, na sasa TV ikiwa ni pamoja ofisi yake binafsi tena kubwa sana, bravo Joe maana huu wako ni mfano wa kuigwa, again salaam kwa familia as we celebrate the lifes of Marehemu Mzee Kusaga, ambaye ameacha mfano mkubwa sana wa kuigwa kwamba kumbe marehemu Mkewe alipofariki, Mzee Kusaga was smart enough kununua kaburi next to his wife kwa siri na hii ni in the 1983, Brother Joe ananiambia kwamba kumbe hata suti ya kuvaa siku ya kuzikwa Marehemu alishaitayarisha siku nyingi sana tena mwenyewe, woow this is wasup! yaani hata mimi nimeguswa sana, sasa tuwahimize wazee wetu jamani kununua makaburi mapema yaani kuwa tayari wakati wowote na hasa sisi wenyewe pia!

- Again, Mungu awabarikie familia ya Kusaga na poleni sana na huu msiba mzito sana, na Brother Joe heshima zangu bro maana ulioyafanya kwenye hiki kipindi ni uwezo mkubwa sana wa uongozi kwa familia, sina wasi wasi kabisa na wewe kuiongoza hii familia.

Mungu Ambariki Marehemu na Familia Nzima ya Kusaga, Bwana ametoa na Bwana Ametwaa lihimidiwe jina la Bwana wa Majeshi.

Respect.


Field Marshall Es!
 
Nawapa pole wanafamilia wote na Dr. Shangali bwana akutie nguvu.

Naakagone!
 
RIP Mzee Kusaga..
Pole Dr (Mrs) Hellen Shangali - Kusaga kwa kuondokewa na mumeo.
Mungu akupe nguvu kustahimili msiba mzito huu.
 
Back
Top Bottom