KERO Foleni Mbagala Rangi 3-Kongowe

KERO Foleni Mbagala Rangi 3-Kongowe

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Unapanda juu kama mnalani au ukifika kwenye pacha unakata kulia inayoshuka chini?
Wewe nadhani ulikua unakaa upande uliojengwa kituo cha mwendo kasi sisi kanisani ukivuka mtaa wa kina samatta kama unaelekea Natal.
 
Mbagala nadhani hadi askari wa usalama wamepasusa. Sio asubuhi sio jioni. Watu wengi, magari mengi, na biashara pembeni ya barabara ni nyingi. Ni vurugu tu
Kuanzia Mbagala kwenda wilaya za mkoa wa Pwani mpaka mikoa ya Kusini hizo Barabara zinahitaji matengenezo ya haraka.
 
Wewe nadhani ulikua unakaa upande uliojengwa kituo cha mwendo kasi sisi kanisani ukivuka mtaa wa kina samatta kama unaelekea Natal.
Hahaha dah sijaja muda sana huko kusema kweli.
 
Naam kama ilivyokua utaratibu wa hii njia kila siku foleni kutokana na ubovu na ufinyu wa njia lakini leo nimeinyooshea mikono juu.

Saa 10:31 jioni ya leo nikiwa kwenye pikipiki na ndugu yangu pale kokoto nakutana na basi la superfeo linaloenda songea ambao hutoka stendi ya rangi 3 saa 10:00 jioni. Basi tukaliacha pale limekwama kwenye foleni mimi na ndugu yangu tumefika mzinga tukanunua mahitaji ili tukapike gheto. Tumefika gheto saa 11:17 jioni tumepika tumekula tumezungumza sasa tukapata simu tunahitajika Kongowe mwisho.

Nikaona tutembee maana si mbali ebwana enhee saa 1:48 usiku huu basi ile bado haijavuka kongowe ndo kwanza ipo bakwata. Nimewaza sana jinsi serikali hii isi yoithamini njia ya kusini na watu wake na sijui lini watasikiliza vilio vya watu yaan kipande cha kutembea dk 10 mtu anamaliza masaa 4 kweli na hajavuka si aibu hii. Miaka na miaka shida ile ile na serikali ipo inakusanya kodi na tozo🚮.
Dah umeongea kwa hisia sana
 
Nimepita hapo leo mkuu nilikua kijijini MKUI. Sio poa.police na traffic wako bize na MBOE/CHADEMA.
All the best.
 
Nitakujulisha mkuu ila hili sitanii niko serious.
Mkuu, Mimi nitakuunga mkono, achana na thread za humu ndani wanapondea wanawake wa kingoni. Mimi ni rafiki/jirani zangu. Ni wife material sana.
 
Nimepita hapo leo mkuu nilikua kijijini MKUI. Sio poa.police na traffic wako bize na MBOE/CHADEMA.
All the best.
Leo polisi karibu nusu nchi nzima walijikusanya mjini huku wameacha kusimamia vitu vya maana.
 
Mkuu, Mimi nitakuunga mkono, achana na thread za humu ndani wanapondea wanawake wa kingoni. Mimi ni rafiki/jirani zangu. Ni wife material sana.
Wengi hear say ila mimi nimekaa songea na nimefanya nao biashara nawajau vizuri.
 
Kuanzia Mbagala kwenda wilaya za mkoa wa Pwani mpaka mikoa ya Kusini hizo Barabara zinahitaji matengenezo ya haraka.
Kwani wana habari... Miaka zaidi ya 60 toka tupate uhuru, ukiambiwa hii ni barabara inayounganisha mikoa utakataa. Mikoa ya kusini kuna rasilimali nyingi ila haiwezi kufunguka wala kuvutia wawekezaji kutokana na uduni wa miundombinu. Tusubiri miujiza, maana huruma ilishakosekana.
 
Ule mlima wa kutoka Kongowe kuja Rangi 3. Maroli mengi yanakwama wakati wa kupanda na njia ni 1. Watu wa gari ndogo bora upite diversion kuliko kukaa nyuma ya roli
 
Hiyo njia mpaka mkuranga miaka inavyoongezeka foleni inazidi kukua, maana viwanda, yard za maroli, container freight stations (CFS) vipo ukanda huo. Suluhisho ni kupanua barabara, hasara ya hiyo njia haina Service road yenye muunganiko hata ukitanua unatembea umbali mfupi inakubidi urudi highway tena
 
Back
Top Bottom