For 1500 years .... Hakuna Jambo La Kushtua Dunia

Mbona miujiza IPO inafanywa Na akina mbonke Leonard, kakobe, mwingira, Mzee wa yesu, Mzee wa upako nabii flora? Ina maana hujapata wasikia hawa?
Miujiza Si kama ya Mitume bali wanafanya Miujiza yao Binafsi
 
Mbona miujiza kibao tuu, Akina Kakobe c naskia wanafufua watu
 
Hivi Babu wa Loliondo na Kibwetele hamkuwaona?
 
Swala la msingi hapo nilipi ?? Nikutokea kWa maajabu au Ni kushtuka kWa watu ??
 
SI UMESIKIA PLANET X MAARUFU KAMA NIBIRU ITAIGONGA DUNIA AU KUPITA KARIBU NA DUNIA NA KUSABABISHA MAJANGA YA ASILI (HUJASHTUKA?)
 
maajabu yapo mengi tu lkn hatuamini km ni ya Mungu, hebu fikiria inatokea ajali halafu watu wote wanakufa anapona mtoto ambaye hata mkanda hakufungwa nk
 
Humuoni magufuli au macho huna una matobo
 
wewe unataka nini mitume na manabii wako wengi sana kuliko hicho kipndi zamani
 
We sema unampa promo huyo kakobe
 
Soma maandiko vizuri.Yesu alishasema nyakati za ishara na miujiza zimeshapita wakati wake.Ishara na miujiza ilikuwa ni njiia mojawapo ya kutuonyesha uwepo wake na ukuu wake.Darasa la kwanza au chekechea ulijifunza kwa kuhesabu vijiti je baada ya kujua kuhesabu bado uliendelea kuvihitaji katika kujielemisha kwako?

Mungu anaendelea hadi sasa kutuonyesha ukuu na uwezo wake kwa kupitia Roho Mtakatifu ambaye yuko mioyoni mwetu na anatujalia vipaji mbalimbali.
Unataka miujiza na ishara zipi? Vyombo vinaenda anga za mbali sio muujiza?Magonjwa yaliyokuwa hayana tiba sasa wataalamu wamepata tiba.Nini tena?

Mungu wetu sio static.Hawezi kuendelea kufanya yale yale kwa njia zile zile na kwa utaratibu ule ule.Ikiwa hivyo dhana ya uungu haipo tena.
 
Miujiza na ishara mbalimbali ni sehemu ndogo sana ya uwezo na ukuu wa Mungu.Yeye ni zaidi ya hayo.Roho Mtakatifu kwa mapaji yake saba ameendelea kutufunulia juu ya nguvu za Mungu.Na hata Yesu aliweka wazi hilo kuwa miujiza ile aliyokuwa anafanya kilikuwa kitu kidogo sana kwake na ndiyo maana akasema mtu akiwa hata imani kidogo kama punje ya haradali basi anaweza kuhamisha mlima au hata kukausha bahari.Kumbe tusifikirie miujiza isipokuwepo basi Mungu hayupo.Hayo ni mambo tunaweza kuendelea kuyafanya sisi leo na infact qatu wengine wanafanya.Leo wewe unaandika kwa keyboard na kila mtu anasoma mawazo yako popote duniani instantly! Leo unaongea na mtu aliyeko maelfu ya kilomita duniani.Je,unataka tena muujiza gani?Mrusi kwa sasa anahangaika ili uwe na uhai milele. Je, huo sio muujiza?
 
watu wamegundua computer+cellphone, huoni kuwa ni maajabu, unaongea na mtu ambaye yupo EUROPE through watsap/cellphone sio jipya hilo???
 
-kutokana na maelezo yako inaelekea una base sana kwenye mono-religion na si poly-religion theology kama ungekuwa unasoma dini zaidi ya moja ungeelewa ni kwa 7babu gani haitokei tena kama zamani kwa hiyo kama utaendea kukaa na uelewa wako wa dini moja hautaelewa ni kwa nn haitokei tena cha msingi ni kuitafuta elimu na kuielewa basi...sijakukosoa ni challenge ndogo ndogo 2
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…