For how long should we....?

mengi umenionea kubwa zaidi ndio hilo....jamani jamani Fidel mbona hivyo? nikueleze mara ngapo? ""namsaidia pale panapostaili na icwe mazoea"..au unataka kujua namsaidia nini au kipi?

haya mama lakini simu alias kimeo usishangae sana hata kama unakuwa na blackberry uswazi tunaita kimeo hata kama una philips savy sisi uswazi tunaita kimeo. Haya mama nimekupata sema tu unamsaidia kutokana na uwezo wa kipato chako hapo sawaaaaaa. Nenda katulize roho mi nawahi saba saba
 

Fidel usisahau pia kuna kitu kinaitwa makubaliano ambayo yanawezafanyika kutokana na upendo wa mtu kwa mwenzake. Sasa kama Mr. wa nyamayao anampenda sana mkewe kiasi cha kulichukulia hilo kama jukumu lake besides pengine tangu wanachumbiana alilikubali hilo sidhani kama kuna shida. Wapo watu wakubwa wengi tu ambao wanafanya hivyo pesa ya mke wala hawaiulizi.

Ila kumbuka kuwa kuna emergencies nyingi tu ambazo baba huwa hazikavi hivyo sidhani kama ni sahihi kusema pesa za mama zinatumika kwa mama peke yake. Mf. wanaweza kuja ndugu za mume ambao wanashida na kujikuta wewe kama mke unawasaidia na wala bamsap haulizi.

Oh temea mate chini kwani utajajuta kwa kumwachisha wifi kazi !!
 

I tell you my friend mtimizie wifi mambo makubwa uone kama atakuja kukudharau hata siku moja!! Madharau haya ya kijinga eti umeongea amekung'ong'a mbele ya watu thubutu! Piga picha mbaba na heshima zake anahudumia kila kitu nyumbani kwake na (hafail anahakikisha kila kitu kiko on time at the time it is needed) then libaba hilo hilo likawa na nyumba ndogo somewhere reaction ya mama akijua ni tofauti na ya yule mmama ambaye mumewe ni mwanaume suruali na asiyejali nyumbani halafu anajitutumua kutafuta nyumba ndogo... utasikia nyoo mwanaume mwenyewe hana kitu hata huko nyumba ndogo sijui anakopesha!! au nyumbani tunalala njaa yeye anafuja tu pesa huko kwa vichangu vyake!! Kuna tofauti I guess

Angalia nidhamu kati ya wamama wa nyumbani (ambao hawana kazi) wanaowategemea waume zao asilimia 100, na wale ambao wanajitegemea na kucover mahitaji ya familia badala ya mume. Wengi wao hawa wenye uwezo wana kaelement ka kuzoeana zaidi kuliko nidhamu kwa waume zao.

(Ni mtazamo na mawazo yangu)

Kwenye Red: nafikiri ni suala la mapokeo, tumezaliwa tukakuta babu, baba wanachukuliwa hivyo kuwa ni vichwa wa familia, tumekuzwa na kulelewa kufuata hayo na hata mafundisho tunayoyapata katika dini zetu, familia zetu tunafunzwa kumheshimu mume kama mkuu wa familia- vichen party, mafundisho ya ndoa. In short jamii inayotuzunguka imetulea hivyo.
 
Oh temea mate chini kwani utajajuta kwa kumwachisha wifi kazi !!

hahahaha Mwanajamii mimi natema mate juu kisha nayadaka kwa mdomo. Kuna akina mama ni mbogo we acha tu umesema hapo kwenye ndugu wa mwanaume wengine tunaona kituo cha polisi kwenda kwa shemeji zetu akina mama mna vituko eti amekuja kunywa juice na soda za watoto hapa...mmh kama wewe umeenda kwa wifi yako umesikia kauli hiyo akiongea wifi yako sidhani kama utakuwa unaenda kusalimia pale kwa kaka ako. Mwanajamii tema mate juu.....kwi kwi kwi kuna wanawake wengi wanaroho za......yamenikuta na yananikuta najuuuta. Sasa chukulia hapo wifi anakipato kizuri kuliko kaka ako hehehe ndugu wote mnapigwa kufuri kung'aa pale mnafilisi mama yeye na maisha yake na mmewe ndugu hana nafasi mambo haya yapo kama unabisha tema mate juu ...Nyamayao atakuja kuthibitisha hili roho mbaya za akina mama wanao chukua kipato kikubwa kuliko waume zao.
 
Ni kweli unayosema Fidel na nakubaliana nawe kabisa ila kumbuka kuwa si wote wenye tabia ya kuchuna, wala si wote wenye kuwanyanyapaa ndugu za mume. Mie ninaye mke mwenzangu mtarajiwa yeye ukienda kusalimia kwake atakukarimu sana majuice, soda, maziwa mpaka kuku utachinjiwa ila ndo akirudi mume ah anamdebt. Anapigiwa mahesabu kaja nduguyo hapa amekula a, be, na che ni kiasi kadhaa na baba analipa.

Ila bado nasisitiza ni makubaliano kati yao.
 

Kweli kuna akina baba ni characters za aina yake, kwa hiyo hao wanaokaa nyumbani wanavishwa na nani? Matokeo yake bila kujijua, wanatengeneza gap kubwa kati yao na familia zao, kiasi kwamba anakuwa hata mzito kunyoosha mkono kumtambulisha mkewe kwa watu.....si tayari hata madaraja yanaonekana tofauti? La kwake analipandisha kwa 'image' anayojitengenezea!
 
Na ndo urudi hivyo!!

hahah nimerudi, nimeipenda iyo!!


Apo tupo sawa my dear...lakini pia sio sawa kwa mwanamke kufanya hivyo eti kwa vile mwanaume hawezi kuwa kichwa cha nyumba kutokana na kutokuwa na uwezo...hilo la kuwa kichwa cha nyumba limaanishe ile jinsia yake, majukumu anaweza kutekeleza yasiyohitaji pesa kama hana kwa wakati huo (sio wanaume wote wana kipato kikubwa au sawa na wake zao)


nidhamu ya ivo mmmh siipendi/sio nzuri, ni vema mwanamke akaendelea kuwa mwanamke, na sio kwa vile eti hana kipato kikubwa ndo anyenyekee......hehehhe


ni kweli kabisa, lakini ni nini zaidi ya haya kinachomfanya mwanaume akubalike, hasa na mkewe, kuwa ni kichwa cha nyumba? manake haya mafundisho ndo naona wengine wala hawayajali wakipata kipato kidogo tu hao, utajuuuuuuuuuuuta kuwafaham..wanakuwa gafla wao ndo 'kichwa cha nyumba'.....πŸ˜•

MwanajamiiOne, angalia PM yako......πŸ™‚
 


ndo hapo nikakuambia swity mie kimeo changu nakihudumia mwenyewe....MASA kapotelea wapi?...nipe michapo ya 77 , kuna beer za promotion?
 



MJO umenielewa vya kutosha kabisa, kuna ile kama mama yake anashida hawezi kumwambia mwanae atanieleza mie na nitamtatulia na mr atakuja kuckia baadae nimesha solve, na mambo mengine kama hayo.....
 



sio wote, kuna wengine wana roho nzuri na wengine kweli wapo hivyo, nina best frnd wangu mume wake alipata matatizo kazini so kwasasa yupo nyumbani tu kila kitu anafanyiwa na mkewe na ana watoto wake wawili aliwazaa ujanani wote mke ana watunza, na wao wana mmoja so ni wa3....anawasomesha watoto skul nzuri , wanavaa vizuri etc na ni wote bila kubagua huyu ni wangu hawa sio wangu, na baba anawekewa gari mafuta na pesa za mfukoni, jmoc ma frnd kanical ananiambia gari yake imetelekezwa nyumbani mwanaume katoroka, alifumaniwa na mke wa jirani yao kumbe bwana aliwafatilia muda mrefu mpaka kawafumania, kavunja vunja vioo vya gari halitazamiki, mr alipo mpaka leo hapajulikani na wanae bado wapo na wanaenda skul kama kawaida, sasa MJO/Fidel mtu kama huyu umsaidie vipi jamani? anapewa kila kitu na mkewe na matokeo yake ndio haya....so sio wote wananyanyasa waume zao kwa kuwa na kipato kikubwa zaidi yake/akipata tatizo kama la mr niliemzungumzia.
 

Masikini I feel for that friend of your nyamayao. Yaani somettimes hawa wenzetu jamani wana mambo. Sasa wewe badala ya kushukuru umempata mke mvumilivu anayeelewa maana ya maisha unamchezea. Tena si ajabu unahongea pesa anayoihangaikia na kukupa ikufute aibu. Wanaume!!

Yaani hapa ndipo mnaponichosha kabisa ninyi viumbe!!πŸ˜•
 

Nyamayao, huyo ndo mwanamke sasa..that man is a crap.....nimeona tangazo hapa la huduma ya maombezi mchungaji nani sijui davie from Arusha, huenda akahitaji huduma😑
 
Nyamayao, huyo ndo mwanamke sasa..that man is a crap.....nimeona tangazo hapa la huduma ya maombezi mchungaji nani sijui davie from Arusha, huenda akahitaji huduma😑


imani yake ni kiislamu, jana huko aliko ka2mia mke wake msg ya kumuomba samahani, hapo hapo akazima cmu, mke kamcal weee mpaka kachoka mpaka asubuhi hii hapatikani, nyie nyie wanaume cc wamama/ wadada 2nawavumilia kwa mengi.
 

MJO mwanaume yeye ni kwenda tu kuwapeleka watoto skul na kwenda kuwachukua, gari full tank, na pesa za mfukoni juu, credoo! yaani huduma zote, sasa umfanyaje mwanaume kama huyu? na walikutwa hotel! mke anajitahidi mume acjickie vibaya/mpweke baada ya kukosa kazi matokeo yake hela ya mke unaenda kufanyia haya yote.
 
imani yake ni kiislamu, jana huko aliko ka2mia mke wake msg ya kumuomba samahani, hapo hapo akazima cmu, mke kamcal weee mpaka kachoka mpaka asubuhi hii hapatikani, nyie nyie wanaume cc wamama/ wadada 2nawavumilia kwa mengi.

Mradi ni mzima asihangaike naye atarudi tu kama ameweza kumsms. Aibu ikimtoka atarudi mwambie shost wako atulie na kuomba MUNGU atamsaidia.
 
imani yake ni kiislamu, jana huko aliko ka2mia mke wake msg ya kumuomba samahani, hapo hapo akazima cmu, mke kamcal weee mpaka kachoka mpaka asubuhi hii hapatikani, nyie nyie wanaume cc wamama/ wadada 2nawavumilia kwa mengi.

Sasa kwa nini huyo mama asimpige chini huyo mwanaume? Amemng'ang'ania wanini kama anaona anafanyiwa vitu ambavyo sivyo? Mwambie aachane nae.
 
Sasa kwa nini huyo mama asimpige chini huyo mwanaume? Amemng'ang'ania wanini kama anaona anafanyiwa vitu ambavyo sivyo? Mwambie aachane nae.

nakuonyesha jinsi gani tulivyo wavumilivu kwenu, bado haja2lia kwanza anataka ajue kama mume huko alikojifichia/kimbilia ni kwema/mzima? then amtaarifu mamake kuwa mwanao yupo mahali fulani hivi na vile halafu ndio atajua uamuzi atakaouchukua.
 
Mradi ni mzima asihangaike naye atarudi tu kama ameweza kumsms. Aibu ikimtoka atarudi mwambie shost wako atulie na kuomba MUNGU atamsaidia.

Mwambie ampe talaka kabisa mwanaume huyo anatuaibisha kabisa.
 
Mradi ni mzima asihangaike naye atarudi tu kama ameweza kumsms. Aibu ikimtoka atarudi mwambie shost wako atulie na kuomba MUNGU atamsaidia.

anawafikiria hao watoto wa mume wawili alionao hapo nyumbani awapeleke kwa mamake na mume, na mambo ya ada na mengineyo anayakatisha, ni kitendo cha jmoc kuwapeleka huko....hebu ona mwanaume amewakosesha watoto masomo yao kisa tamaa za kipumbavu, yaani inatia uchungu sana.
 

Mwambie watoto hawana kosa Nyamayao mwenye kosa ni baba watoto aawaache ila libabalao alitimue akae na huyo mama mwenza wajue watafanyaje kuwasaidia watoto hao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…