For the sake of National Unity, Je tumshauri Dkt. Magufuli aahidi kumteua Tundu Lissu kuwa Mbunge?

Mkuu , Lisu ni mtu wa kawaida kabisa akishindwa akatafute kazi nyingine ya kufanya.
 
Tunawasihi watanzania kufuata sheria, kutofanya fujo wala kuharibu mali. Tuwe watulivu muda wote huku tukisimamia haki zetu. Tupige na kulinda kura zetu bila hofu wala woga wowote hii ni Haki zetu kisheria. Ukipiga kura kaa umbali wa mita 200 kutoka kituo cha kura. TUTASHINDA!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bila kupinga mawazo yako yote, kwanza Lisu hataki vyeo vya kubebwa maana ana ushawishi wa kutosha, hivyo vyeo vya mbeleko Magufuli awape wale wanaojipendekeza kwake kama kina Makonda, ww mwenyewe Paskali, Kabudi, Mrema nk lakini sio Lisu. Sisi tunataka kutoka kwenye nchi ya kumnyenyekea rais kama Mungu, ww unatujia na wazo la kuendeleza uungu mtu kwa watu wasio waadilifu!

Nilipojiunga hapa jukwaani 2011, na wakati wa maoni ya katiba mpya, baadhi ya maoni niliyotoa nilitaka kila mgombea wa nafasi ya urais atakayepata 5%+ awe mbunge automatically. Nilikwenda mbali zaidi kwa kusema na iwapo atapata kura nyingi kuliko mbunge yoyote atakayekuwa bungeni, na kuwa wa pili nyuma ya atakayeshinda urais, basi automatically awe kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni. Huu mchezo wa rais kupewa nguvu za kikatiba kuchagua kila mtu, ndio unazaa watu wanaojipendekeza kwa rais na kutii kila atakacho, badala ya kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria. Wote tumeshuhudia marais wetu kukosa uadilifu hasa kuanzia awamu ya pili, toka wakati huo nchi hii imekuwa na marais wasio waadilifu au wenye uadilifu wenye kutia shaka, na hii ndio sababu ya nchi hii kuendeshwa kwa mitazamo binafsi ya rais aliye madarakani, na sio sheria na katiba zitakavyo.

Sisi kura zetu tutampa kiongozi anayejali haki, na sio kiongozi anayetaka kuabudiwa kwa kutekeleza wajibu wake ambao analipwa mshahara. Tunachotaka ni uchaguzi wa haki, ila huu uchaguzi ambao rais anaamua ashinde kwa kiasi gani, ni kutaka kuingiza nchi yetu kwenye machafuko na kupoteza imani ya wapiga kura. Hali hii ya rais aliye madarakani kuchezea mifumo ya taasisi za kimamlaka ili zimpendelee, ndio zimechangia watu kutokupiga kura, na hata uchaguzi huu utakuwa ma wapiga kura wachache sana, huku kukiwa na mazingira ya machafuko. Napenda nikuhakikishie Magufuli hata akitangazwa mshindi sio kwa kuwa kweli atakuwa ameshinda kwa kura, bali katiba dhaifu ndio itakiwa imempa urais. Na nitamdharau sana Lisu iwapo atapewa cheo chochote na Magufuli kisha akakikubali. Iwapo cheo hicho kitatokana na katiba kama pendekezo hilo la 10% kwenye uchaguzi hapo sawa.
 
Hapana, kutopiga kabisa kura, ni kushindwa kuitumia yako ya kidemokrasia kuwachagua viongozi unaowataka, ikimpigia kura mgombea wa kushindwa, unapoteza kura yako, hivyo badala ya kumpigia mgombea kushindwa, kura yako mpe mgombea wa kushinda.
P
Na mgombea wa kushinda ni yule atakayekupa kula baada ya kushinda.
 
Hahaha Lisu ndiye rais, ubunge wa taifa.

Magufuli akuteuwe ndiyo ATAKUTUKANA kila siku na akiona umechoka kutukanwa, anakufukuza.
 
Umoja wa kitaifa tulioachiwa na waasisi wetu unazidi kudorora kwa kiwango kikubwa sana kutoa "offer" ya position ndani ya uongozi kwa mliotofautiana misingi ya kiitikadi wala haitoleta suluhu bali namna watu wanavyofanyiwa na viongozi ndio mbegu ya chuki ilipopandwa!


Chukulia mfano useme Lissu apewe positiob ndani ya Serikali ya Jiwe halafu Jiwe anafika Jimboni kwa Mpinzani anasema sijaleta na sitoleta maendeleo sababu hamjanichagulia wa ccm je hapa si sawa na kuhesabu Moja hadi 1-10 na kuanza tena kurudia kuhesabu?


Suluhu ya yote ni kubadili katiba iwe na maslahi ya wananchi wao ndio wawe na uwezo wa kumuweka kiongozi madarakani na hata kumtoa! Ila kwa katiba yetu hii kila kitu kapewa jiwe au rais yoyote ajaye kujiamulia bila kuulizwa sijui fulani anateuliwa na rais na uteuzi wake kutenguliwa na rais je huyu rais si binadamu akimisbehave nani wakumhoji? Ni ushahidi tosha nashuhudia huku nchi za watu walishaamka elimu ya uraia inaekeweka na wapi wanajua haya ni maslahi ya taifa na hapa ni ya binafsi na hapa ni pa kusema ndio na hapa hapana kitu ambacho bongo hakuna zaidi mtabaki kujidanganya miaka nenda rudi huku mkipandikiza chuki itakayokuja kukomaa na kuleta shida baadae
 
Umeshapata matokeo kwamba Magufuli atashinda? Kabla uchaguzi haujafanyika?
 
Ccm inapigwa saa 3 asubui mapema asubui sababu wamekiuka zindiko la mwenge kutokana na maagano yaliyofanyika mapangoni bagamoyo Ina maana forozo ganze alishindwa kuona kiashiria Cha uwepo wa corona ili awaambie wazee wafanyeje ili zindiko lisikiukwe? Ona sasa akili za watz zimefunguka haijawahi tokea ccm kukataliwa Hadi vijijini, tumeona ngome zao zote chali si Kanda ya ziwa si dodoma kusini ndo awatakiwi kabisa Hadi wanapiga mabomu kwa wivu Hadi mgombea wao amekacha kwenda kusini kuomba kura akitegemea miujiza.
 
CCM sera yao kubwa nikutesa watu. (Kwa maana teka, piga, filisi,ua, bambikia kesi, fukuza kazi, wafungwa walime kwameno, hapa kazi tu nk.nk)
CHADEMA sera yao kubwa ni uhuru, haki na maendeleo ya watu.
Hawa hawatakaa pamoja never, never, never
 
Maneno yako yanakatisha tamaa daaa😂😂😂😂 ko matokeo kumbe yapo kitambo mnasubiria siku ya mwisho mtangazie uma! Hahaha

Tanzania nakupenda kwa moyo wangu wote
 
Wacha bange zako wewe,Lissu levo yake ni rais
 
Unakuja na hoja mfu kwa kudhania wote ni mburura wa CCM. Tutampigia kura Lissu wewe na msukuma mwenzio mkaziibe...
 
Acha matusi kwa mheshimiwa Tundu Lissu. Kwa mtu mbovu kama magu utapata uteuzi tu Mayalla usiwe na hofu kwani anateua anavyojisikia na anaangalia kanda unayotoka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…