Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue!

Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue!

Status
Not open for further replies.
Wakuu naomben iyo forex for dummies na naked forex mwenye nayo aipandishe APA tupakue aseh naomba ukiweka uniatag pls
 
Ila inafaida nzur sana mfano leverage ya broker ni 100:1 mfano ume deposit $1000 .... kwa leverage una 100,000$ kwa volume hii unapata faida kubwa sana uki trade... the higher the volume the higher the profit.. so hii leverage n nzur sana...! Kama mkopo tu....
Leverage ni double-edged sword mzee,hapo umetazama upande mmoja lakini ikitokea trade imekuendea vibaya hasara inakua maradufu pia.
 
Ontario tafadhali Kama unaweza kutupia hivyo vitabu viwili humu ndani itakuwa vyema, iwapo tu unavyo kimtandao Na Nafasi yako inaruhusu. Asante.
Vitabu vipo post no. 441 na 663[/QUOTE]
on point
 
Bro nimekuwa nafwatilia huu uzi kwa makini sana ningependa niwe miongoni mwa hyo first batch ili nipate nafasi ya kujifunza zaidi na kuielewa forex .
 
Kiongozi ONTARIO plz usiniache kwenye iyo namba ya 150.
 
NA MIE NATAKA MKUU,USINIKOSEEEE!DAH NIMEGUNDUA RAIA TUNA UCHU SANA NA PESA AISEE
 
NA MIE NATAKA MKUU,USINIKOSEEEE!DAH NIMEGUNDUA RAIA TUNA UCHU SANA NA PESA AISEE
 
Update ya kwanza

Kwanza kabisa niseme mimi na team yangu tumekuwa tukipambana sana kuhakikisha operation inaanza ASAP, lakini kiukweli mambo ni mengi sana, tofauti na nilivyotegemea.

Mpaka sasa naeza sema tupo almost half way katika kupata documents za kiserikali, vikwazo ni vingi sana sana, kila mtu anakwambia hiki, lkn tangu J5 tumekutana na watu wa ndani zaidi wa CMSA, hivyo nategemea week ijayo itakuwa smooth-tunaweza kukamilisha japo 90% ama kila kitu.

Kuhusu office yani hapa kichwa cha motooo si mchezo. Bajeti ya awali na hali halisi ni tofauti kabisa, kila unachogusa bei utakayotajiwa unatamani uwatukane wauzaji. But mwisho wa siku kwasababu maji tumeshayavulia nguo lazima tuyaoge.
e8a396d8ef8067c2ccd10f3f5f6be338.jpg
Reception kwajili ya maulizo nk
234b7fdb146208206d15915d4c6b9d82.jpg
1 ya office za mentors

Pia niseme nimesikitishwa sana na baadhi ya watu either kwa kutokua na uelewa wa forex ama kwa maksudi kuanzisha thread za kunichafua mimi pa1 na hii programme. Kwanini mtu asije kuniattack hapa, ananiattack kwenye uzi ambayo siwezi kuuona ama naweza kuuona baada ya siku kadhaa. Kama mtu ana strong argument aje kwa huu uzi, sio kusambaza chuki kwenye nyuzi ambazo siwezi kutoa clarification. Nimeona wanavyonizungumzia in negativities, sijataka kuwajibu hata neno - kwasababu binafsi naamini muda ndio hakimu makini zaidi. Nataka results za wanafunzi wangu ndio ziongee si maneno yangu, tayari nimeongea sana.

Zaidi ya yote, niwaombe tuwe wavumilivu... vitu vizuri havihitaji haraka. Nahisi Mungu akijalia tunaweza kuanza kabla ya tarehe 15 June - mambo si marahisi kama nilivyotegemea, but nusu mwezi utatosha. Na ninapromise, this is gonna be a financial breakthrough kwa wale waliodhamiria, naongea kwa kile ninachokifahamu, kamwe katika maisha yako hautajilaumu kuifahamu forex.

Pia, baada ya kufanya tathmini kwa kina pamoja na team yangu nimegundua kua watu 300 ni wengi mno. Darasa litakuwa na watu 50 tu, ili interaction kati ya mwanafunzi na mwalimu iwe ya juu zaidi, pamoja na kuongeza concentration. Kutakuwa na maximum 3 sessions kwa siku. Hivyo nitaanza na watu 150 maximum. Kwa wale ambao hamtabahatika kua katika hawa 150 msiwe na presha, mtapata hii fursa mbeleni bila upendeleo, though charges may apply.

Kwasasa mtu anaweza asione umuhimu wa kulipia hii training, lkn nikitoa batch ya kwanza ya wanafunzi wangu, najua kila mtu atapanda dau kwajili ya kupata mafunzo. Moja ya aspect ya msingi kabisa ktk training tutafanya "Live trading" kwa pamoja. Yani tutatrade live kila mtu aone na aelewe nini ni nini, kwa wale ambao watakua na account wataweza kupiga mpunga jicho kwa jicho na mentors wetu. Yani mf kama una $300, pale pale live tutafungua trades tugonge $100 ya chap chap.

Wakati tunasubiri update ya mwisho, naomba tuendelee kusoma kitabu cha Forex for dummies. Baada ya kumaliza hicho kitabu tuanze kitabu kingine kiitwacho Naked Forex - High-Probability Techniques for Trading Without Indicators >>Kimeandikwa na Alex Nekritin. Please soma kuelewa, si kusoma kumaliza pages ama kumfurahisha Ontario. Your knowledge is the best weapon to beat the market.

Ontario.

Ontario Mkuu niko na kampun ya kuandaa Events,Naomba Nitumie fursa hii kuomba kazi ya kuandaa hyo Event,Kama hutojali ni PM mail nikutumie Company Profile
 
  • Thanks
Reactions: MC7
Ontario asante sana. Nasubiri hiyo opportunity ya kujifunza. Hata kama isingekuwa free I would be willing to pay. Again thanks. Waiting for more information.
 
Salute bosses

Utangulizi

Wengi mmesikia sikia sana kuhusu Forex trading, mmepata kujua taarifa kadhaa kuhusu hii biashara lakini mmeshindwa kufahamu nini kinaendelea. This is the perfect thread, tutaelewa kila kitu hapa na hakuna atakayebaki na swali kichwani - we have to leave this thing completely naked. Nakuhakikishia (mimi Ontario) kupitia hii thread sitamwacha mtu yeyote nyuma. Naomba twende pa1, tufahamu, tujifunze, tuelimike, tuhamasike na tujichallenge.

Kwanza nitoe shout out na credits kwa member mmoja hapa JF anaitwa Davion Delmonte Jr. Aliwahi kupost uzi educative sana kuhusu forex, ni moja ya uzi wa forex uliopata hamasa kubwa hapa JF ndio maana nikauchagua kama sample -lkn kuna nyuzi zingine nyingu tu, nakushauri unaweza kuupitia kidogo Fahamu utajiri kwenye biashara ya fedha za kigeni (FOREX TRADING)

Tuendelee
Katika tembea tembea zangu, mwaka 2016 mwanzoni nilikuwa Durban, nikakutana na dogo mmoja anaitwa Mike Lungu, ye mwenyewe anajiita MLU. Kukutana kwetu kulikuwa very coincidentally, mimi nilikua naishi Garden Court hotel, asubuhi muda wa breakfast tukajikuta tumekaa meza moja. Baada ya Kusalimiana tukajikuta story haziishi, nikazungumza mengi sana kwa upande wangu, baadae nikataka kujua na yeye upande wake.

Mike akanieleza kuwa alidrop out of college akiwa mwaka wa kwanza, na kwa kile kipindi alisafiri kutoka kwao Mpumalanga sasa amekuja Durban kukutana na mentor wake. Nikataka kujua zaidi kuhusu hiyo mentorship inayomfanya atoke Mpumalanga (ambapo ni mbali sana na Durban). Mike akaniambia kwamba ni Forex.

Kipindi hiko nilikua sielewi chochote kuhusu forex, yani sina clue kabisa. Mike Akaanza kuniambia kuhusu watu waliofanikiwa sana ktk forex, akanitajia kijana mmoja ambae siku kama 3 zilizopita nilimuona anafanya interview kwa TV lkn nikashindwa kabisa kumwelewa anachokisema. Huyo dogo aliyenitajia ni celeb wa forex SA na anaitwa Sandile Shezi, ni dogo mwenye utajiri mkubwa sana kupitia forex, nae aliacha chuo mwanzoni kbs mwa masomo.
6784542861cf86e42eed93dd8361df54.jpg
Sandile Shezi anaemiliki Global Forex Institute.

Kama ilivyo kawaida ya wabongo wengi, nikambishia sana Mike, nikamwambia hiyo kitu ni utapeli na wizi ambao hauwezi ukamtajirisha mtu wa kawaida. Nilikua sina knowledge kbs lakini nilikomaa kusema kua forex nayo ni kama forever living (networking marketing). Hata nilivyosoma kwenye mitandao, bado nilimbishia sana Mike kuhusu hiyo forex nikidai kuwa kamwe siwezi poteza muda wangu na pesa katika huo upvmbavu, nikafika hatua ya kumDiss kua anapoteza mufa wake bure.

Basi, tukawa tunapiga story zingine, namweleza kuhusu Bongo nk. Yani tulitokea kuwa marafiki ndani ya muda mfupi sana, nilikaa pale kwa siku 8 nikaondoka kurudi Bongo. Lakini Tuliendelea kuwa in touch, hasa kupitia WhatsApp, tunajuliana hali na maendeleo kimaisha. Mimi nampa updates za kilimo na ufugaji na yeye ananipa updates za Forex kwa upande wake.

Sept 2016 nikaendaga USA, basi nikawa namsumbua sana MLU kwamba kilimo ni kitamu sana bora aache hizo forex yake afanye kilimo. MLU akanambia sasa Octario kwenda US unaona ni mafanikio makubwa? Tukabishana mwishoni akasema nimpe mwezi mmoja anishangaze - mimi nikawa namcheka, na kumwambia kua yupo ndotoni.

Mara ghafla siku 1 October 2016, Mike akanitumia text, hey Ontario nimevuta BMW mpya 0 km. Wabongo kwenye situation kama hizi hua ni wabishi sana, nami kama kawa nikabishana nae Asubuhi, mchana na usiku (kama dozi ya mseto). Jamaa akanambia subiri nikikamilisha paper works nakutumia picha. Ndani ya siku 4 tu, Mike akanitumia hii picha.
6ccbe86153d474187c32b8a2c8f65d68.jpg


Hapa nikawa mpole - ukweli ambao hakuna binadamu atakubali ni kuwa "Kila binadamu hapa duniani ana chembe chembe ndogo za wivu endapo mtu baki akifanikiwa kumzidi". Huu ni ukweli mchungu, ambao mimi nimeuprove katika situation kadhaa. Lakini watu wanaoweza 'kudeal' na hizo chembe chembe za wivu positively ni rahisi na wao kufanikiwa.

Kama hauwezi kupambana nao ungana nao
Baada ya hile hali nikawa motivated mno. Nikajipiga juu chini Nov 2016 nikarudi SA, nia ni kuonana na Mike. Nafahamu kabisa huyu jamaa hakuna kitu anachofanya hapa duniani zaidi ya hii Forex, leo kanunua gari KALI kupitia hiyo forex, lazima nami niingie humo. Nikajipa moyo kua I am never late.

Safari hii nilivyokutana nae sikuishi hotel, Mike alinifata Airport tukaenda kwake. Nyumba ambayo alikua anaishi ni sawa ama zaidi ya hizi ambazo mawaziri hapa Bongo wanazitumia. I was over shocked. Nikasema afe simba afe mmasai lazima hii kitu niijue. Hapa ndipo Mike alipoanza kunizingua, utani mwingi wa kunicheka kua mimi najifanya mjanja kumbe ni mshamba tu, akawa anasema hawezi kunielekeza hadi nipige magoti nimshike miguu nimuome msamaa. Haha haha!!

Akanipa tips zote kuhusu forex, akafungua book store yake akanipa vitabu 6 nivisome kwa makini sana. Nikavisoma haraka haraka kwa pupa, ili mradi nivimalize then Mike anipe mbinu nami nianze kupiga hela. Nilivyomaliza kusoma ki1 nikamtaarifu Mike, akanichapa swali 1 nikajibu pumba na mashudu. Jamaa akaniambia nisome upya letter by letter. Nikapunguza jazba, nikaweka concentrate ya kutosha, nikaanza kuelewa.

Sikukaa muda mrefu sana nikarudi Bongo. Nikawa naendelea kusoma vitabu alivyonipa kwa umakini sana na akawa ananiuliza maswali ya hapa na pale.

Nilivyoanza Forex trading

Mpaka hapa bado wengi hamuelewi nini maana ya Forex, bado hamfahamu hata nazungumzia nini, usiwe na pupa na jazba kama nilivyokuwa nazo. Twendeni pole pole, mpk hii thread inaisha hakuna atakayetoka mtupu.

Wiki kadhaa baada ya mwaka mpya 2017 nikaanza forex rasmi. Mike alinipa mwongozo wa awali akaniomba nifungue 'demo account'. hii ni account ambayo imewekwa virtual money, unaitumia kwa ajili ya kujifunza kutrade. Ukijiona umeiva unahamia kwenye real account ambayo unaweka pesa yako na kuanza kutrade kiuhalisia.

Nikapiga hii demo account, kwa kuwa sikua na msimamizi (mentor) karibu yangu ikanichukua mwezi mzima kumaster hii trading. Nikaanza kuona mwanga, nagonga profits, naelewa nini kinaendelea, nikaanza kujua basics za market analysis - fundamental na analytical. Baadae nikapata picha kubwa zaidi kuhusu hii kitu. Kwakweli nikajidharau sana sana kwanini nilikua namcheka Mike hapo awali, nikajiona Baxhite wa kiwango cha standard gauge.

Nikajiridhisha kuwa I am good to go. Na Mike rafiki yangu wa faida akanipa go ahead. Nikaanza kwanza na $700, nikakimbiza kimbiza nikaona nagonga profits za ajabu mpk nikawa naanza kuogopa. Kuna ile kasumba fulani wabongo tunayo kama unahisi unatapeliwa hivi, nami nikaanza kua na hiyo feeling. Nikawa kama vile nachallenge ubongo wangu, kusema hii haiwezi ikawa real, yani capital ndogo na bado napiga profits za ajabu hivi.

Nikakimbiza hadi kufika $2000 ndani ya wiki 2, nikasema nijaribu kuichomoa ile pesa kidogo nione kama ni real. Nikawithdraw $500, kudadeki kitu kikakubali, nikaenda CRDB nikavuta kamilioni kangu na tuchenji kadhaa. Sasa nikasema hapa ni kupiga pesa mpk mnikome. Mambo yakawa matamu sana, nikipata shida kwenye kuku na mashamba yangu nachomoa pesa kutoka kwenye trading account ndani ya siku 2 au 3 ninayo mkononi nafanya mambo mengine. Na kadri nilivyozidi kuchomoa pesa na kuwa nayo mkononi ndio nilikua napata morali ya kufanya forex.

Siku nikachomoa $1500 kwaajili ya mdogo wangu ambae ndio alikua anaenda kuanza form 1 huko Moshi. Hapa account yangu ilikua imefika kama $11,000. Nikasema hii pesa ($1500) niliyoichomoa lazima niirudishe ndani ya siku ile ile ili kubalance mahesabu.

Kuna kitu kinaitwa Psychology of trading and Over Trading. Hivi vitu nilikua naviona tu kwenye vitabu lkn naviruka kwa kuvipuuza, hii siku wakati nipo aggressive kurudisha pesa niliyochomoa ndio nikavunja hizo kanuni. Aisee nikaingia kwenye trades, nikawa nimeovertrade, nikaacha trades zinarun usingizi ukanipitia. Sikukumbuka kuweka stop loss (SL) wala take profit (TP) [hivi vitu tutavielewa baadae], aisee kumbe hiyo siku kulikuwa na economic news release. Baada ya kushtuka kutoka usingizini nilichokiona sikuamini macho yangu.

Nasema kama ile siku sijafa kwa presha siwezi tena kufa kwa presha siku za usoni. Yani nilikuta account yangu yote imepukutika kama mvuke. Sikuamini, nilipoteza karibia pesa zote zote ndani ya muda mfupi, sisi tunaita kuBlow ama kuchoma/kuunguza account. Kuna feeling fulani ukipoteza kitu cha thamani unaipata, yani unahisi kama unajikojolea. Sijui kama mnanielewa. Yani sielewi kilichonitokea, ni km nilipigwa ganzi ya ubongo

Nikamshtua Mike kuhusu msala wangu, akacheka sana sana akaniambia, nilijua tu lazima uunguze account, speed yangu ilikua ya mwanga wa radi. Zaidi sana anakambia kuchoma account ndio kukomaa na kuwa mtaalamu ama guru wa trading. Nikapiga moyo konde, nikajipa muda wa kupumzika na kusikilizia machungu yaishe.

Baada ya muda kama week 1 nikaanza upya kama kawa. Nikaweka $3000 nikaanza kukimbiza upya. Mambo yakawa matamu, yani nashukuru baada ya kupoteza ile pesa akili ikawa imenikaa vzr sana ktk kitu kimoja tunaita trading risk management. Nikawa makini kuliko kiasi, nikawa ninatrade pale tu ninapoona kuna opportunity, nikawa very strategic huku nikiamini kuwa bado mimi ni mwanafunzi na nahitaji kujifunza zaidi na zaidi kuhusu financial markets. Mpaka sasa ninavyoongea najiamini ktk trades zng vibaya mno kuliko kipindi chochote kile.

--Sasa twende kwenye maana ya Forex trading.

Forex trading ni nini hasa?

Waliosoma uchumi na masomo ya business chuoni najua tangu naanza uzi wanaelewa nini naongelea kijuu juu. Lkn wenzangu na mimi tuliosoma Sciences, technology, engineering na humanities hatuelewi hata punje.

Forex ama wengine hufupisha kwa kusema FX ni kufupi cha maneno Foreign Currency Exchange. Basically Ni biashara inayosisha kuuza na kununua fedha za kigeni. (Najua wengi hapa akili imegonga kwenye bureau exchange). Yes! Ni kitu kile kile lkn sasa hii Forex ni baba lao, tuwashukuru sana (wazungu) walioleta technology ya computer na Internet. Sasa kiuhalisia tukizungumzia Forex trading ni kubadilisha fedha za kigeni electronically and at real time. (Sijui kama unanielewa?). Ni wewe na computer ama smartphone yako pamoja na bundle lako.

Kinachotokea ni kwamba unaspeculate utendaji ama tuseme performance ya fedha fulani labda Dollar ama Yen ama Pound kisha ukifahamu uelekeo wake either utainunua ama kuiuza, kupitia huo mzunguko utatengemeza pesa kubwa sana ama kama ukijichanganya unapoteza vile vile. Hapa unahitaji uwe na uelewa mpana sana wa kufanya analysis ya soko la dunia (global currency market).

Hii ndio biashara yenye utajiri mkubwa kuliko biashara yoyote ile hapa duniani. Huwezi kuamini kwa siku katika forex trading kuna mzunguko wa $5 trillion (dola trillion tano), naomba hapa tusiiweke in Tsh maana tutaishia kuongea herufi za ajabu mara hexa trillion mara hepta trillion, lkn ni mkwanja mrefu sana. Kiasi kwamba itaihitaji New York Stock Exchange ifanye biashara siku 30 ili kupata pesa za siku 1 zilizopo kwenye forex market. Ndio maana sisi traders hua tunasema "kudownload pesa" yani kwenye forex ni kupakua tu pesa, kama vile upo uTorrent

Central banks zote zinafanya forex trading, financial institutions karibia zote duniani zinafanya forex, wafanyabiashara wakubwa karibu wote wanafanya forex (tena huyu bilionea wetu ambae alibahatika kufanya kazi Wall street atakua ni trader mzuri sana wa forex na stock), Donald Trump ndio hata usimzungumzie - huyu kashindikana, leo hii trump anasukuma tweets ambazo zinabadilisha upepo wa dollar katika soko ili yeye na team yake wagonge pesa, mpk anatoka madarakani atakua kazidisha utajiri wake hata mara 5.

Ukweli uliofichwa kuhusu forex

Sijui nisemaje, lkn ukweli ni kwamba kuna nguvu kubwa sana sana sana inatumika na mabenki kuwafanya watu wasiitambue forex. Wenzetu Ulaya na Marekani walishtuka mapema sana, kwao forex si kitu kipya sana japo bado kuna wingu kubwa hapo kati. Huku Afrika ndio usiseme, wenzetu SA kidogo wamewahi kushtuka kutokana na muingiliano mkubwa kati yao na mataifa ya Magharibi.

Utamu upo hivi - Leo hii ukichukua mil 10 na kuiweka benki katika fixed account, utapewa interest ya 7-10% kwa mwaka, hiyo miezi yote 12 unasubiria milioni 1. Lakini kwa forex ukiwa unajitambua ukaweka mil10 ukatrade, kama ww ni average trader ndani ya siku 2 utakua umepiga faida ya milioni 1. Sasa hapa benki zinapambana juu chini ili watu wasitambue forex ili wasije kupoteza wateja wa fixed accounts. Na ukweli ni kwamba pesa zinazowekwa fixed account bank hua wanazitumia kufanya forex trading, hii kuwapa watu mikopo hua ni kiini macho tu.

1 ya changamoto niliyokumbana nayo ni hii ya bank. Wakati nachomoa pesa ndogo ndogo ilikua ni faster tu, ndani ya siku 3 pesa iko mkononi. Lkn siku niliyojaribu kuchomoa pesa ndefu ndipo nilipoelewa nguvu inayotumika na mabenki. Sitataja jina la benki niliyokuwa natumia, ni bank ya kibongo (local bank), lkn kiukweli walinizungusha sana, wamenisumbua vibaya mno, wananisainisha makaratasi kila siku, kila siku naambiwa nikutane na XX, mara wananiambia nithibitishe kua ile pesa si "money laundering" "kutakatisha pesa". Hii yote ilikua ni mbinu ya kunidiscourage nisiendelee na forex, kumbe hawajui mtu wanaeshindana nae. Hayo yote nilikua nishayasoma kwenye vitabu siku nyiiingi, ni kama nilikua nina theory sasa nimeeingia kwenye practical. Mwishoe wakanipa changu!!

Hakuna bank yoyote ingependa ujue kuhusu forex, yani hata humo kwenye mabenki wafanyakazi wa humo humo benki hawatambui kabisa kuhusu forex. Ni wajanja tu ndio wanaweza wakaelewa nini kinaendelea huko duniani. Nguvu inayotumika si ya nchi hii.

Hata juzi nilimpa jukumu member m1 hapa JF ambae alinisaidia kusajili kampuni yangu mwanzo kbs, nilimuomba afatilie ishu ya forex BRELA, wizara ya fedha na BOT. Yani kuna blah blah vibaya mno, watu hawataki kufunguka kabisa. Lakini tutafika tu, dunia haiwezi ikatuacha just kwasababu ya manufaa ya wachache, sio fair.

Way forward

9899c7dad05c1ace817ac027eb891b45.jpg
Hii picha niliichukua kwa bahati mbaya nikiwa mile 60,000 angani lkn hapa iko relevant.
Hivi nazungumza sina muda mrefu tangu nitoke Afrika Kusini, na nilichokifuata naweza kusema kwa asilimia 99% kimefanikiwa. Nimetumia gharama nyingi sana kufanikisha dhumuni langu but it's worth it. Naamini hivyo.

Naangalia fedheha na dhihaka tunayopata wasomi, it's too much. (Nikisema wasomi simaanishi kama unavyodhani bana hahahaaa, no disrespect hata mwenye form 4 nae ni msomi). Jamii imekua na expectation kubwa mtu akifika form 4, form 6, degree namasters, watu wanategemea uwe mtu fulani hivi, mwenye maisha fulani hivi. Lkn kwa system ya nchi zetu hizi , inakua tofauti, inafika kipindi huwezi kumtofautisha graduate na mtu kama msaga sumu ama man Fongo.

Kwa experience niliyonayo nikaona Forex is the BEST way forward kuepuka hizi fedheha za ajabu. Unakuta mtu hata wazazi wako wanajilaumu kwanini walitumia nguvu kukupeleka shule, walikua wanategemea a lot kutoka kwako, lkn hadi leo unakuta graduate ana miaka 26 anagombania kipande cha nyama na mdogo wake. Lol.

Iko hivi wakuuu:-

●●Nimefanikiwa kuAttract mentors watatu akiwemo mentor wng binafsi, kuja Bongo kwaajili ya kutoa training, coaching na mentorship kuhusu forex. Nimeona niwatumie waafrika kusini kutokana na uzoefu mpana walionao na uwelewa katika forex kwa hapa Afrika.

●●kwa usumbufu wa Local banks nimeweza kuongea na FNB bank, hii ni bank makini na maarufu sana SA ambao wana experience kubwa ktk kudeal na transactions za forex. Wamekubali partnership na uzuri Bongo wana branches kadhaa so ni rahisi zaidi.

●●Nimeweza kuAttract forex broker kuja Bongo. Hapa kidogo nikupe uelewa - Broker ni financial institute inayokuwezesha wewe kuingia global market na kufanya trades zako. Wanakupa platform ya wewe kuweza kutrade katika soko la kimataifa. Fedha zote sasa zinapitia kwa broker wako, ukitaka kupokea pesa zako zinapita kwa broker, huwezi ukatrade bila kua na broker.
Sasa kwenye forex kuna aina 2 ya brokers, niseme kuna aina nyingi lkn hizi mbili ndio common zaidi.

1. Market makers: hawa ni broker wanaeshindana na wewe retail trader. Hawa ni hatari sana kwa afya yako. Huyu broker yupo against na wewe, yeye anapambana wewe upoteze pesa, na hiyo unayopoteza inakua faida yake. Anaweza kufanya hujuma za kila aina ili upoteze pesa yako kwa kutrade, yeye ndio apate faida.

2. ECN forex broker: Huyu ndie broker safi kwaajili ya afya yako. Huyu atahakikisha kufa kupona wewe uwe unapiga faida, anataka wewe milele daima uendelee kupiga pesa kupitia forex, muda wote yupo na wewe benet ili usianguke. Why?! Huyu ni broker ambae anapata commission ndogo sana kwa kila unapoexecute trade, sasa ili yeye apate faida inabidi wewe trader uwe unaweza kutrade zaidi na zaidi, na ili wewe uweze kutrade zaidi inabidi uwe unawin ili uzidi kuwa na account kubwa ya ww kuendelea kutrade zaidi.

Sasa broker ninayemtumia mimi ni huyu ECN, nimefanya juhudi kubwa sana kuweza kumshawishi aje afungue branch Bongo. Na as planned amekubali, uzuri ni kua vibali vyake vinamruhusu aingie nchi yoyote ile Duniani. Na kwasasa tayari wana branch kwa jirani zetu hapo Kenya. na hivi naongea tayari wameshafungua account ya FNB Tanzania ili kusudi kutuwezesha kuweza kufanya one day deposit/withdraw. Yani ukitaka kuchomoa pesa yako kutoka trading account zoezi hilo litakamilika ndani ya siku 1 tu.

Na tayari nimewapa ushauri ambao wanaufanyia kazi - waweze kuleta broker visa card. Yani kunakuwepo na card ambayo itatuwezesha kuchomoa pesa 1 kwa 1 kupitia ATM yoyote ile duniani.
Kitu kama hiki:-
8a8a1308766b3617cf78b85a6bdffc57.jpg


Nini tutegemee

Mpaka sasa ninavyozungumza team yangu tunafanya kazi, kazi kweli kweli kuhakikisha haya yote ninayoyazungumza hayaishii kwenye papers ama JF. I want to get this thing done, come rain or shine, ije jua ama inyeshe mvua.

Hapa naandika huu uzi nahisi nakula muda wangu - but it's worth it. Napambana kupata papers zote, ili operations ziwe legalised kwa sheria na utaratibu wa nchi. It's hard but it will be done.

Jana nimetoka kucheki office na nitailipia soon. Tumependezwa sana na Jangid plaza ipo pale mataa karibu na Dar Free Market. Nimeshaonana na mmiliki, badp kukamilisha paper works tu.
c7d5df684fb732908483b161556f0399.jpg
44dea36bd9ac6e051cd9403b75aa76c9.jpg


Let's get started

Any time niko tayari kuanza, soon indeed!! Tunataka watu wawe financial independent, watu waweze kucontrol uchumi wao pasipo kuinyenyekea/kuililia serikali. We must move forward with the rest of the world, same time same speed bado hatujachelewa.

Am young but very motivated. Sijui niseme nini, but hivi naongea nimereject mwaliko kutoka World Bank ambapo nimealikwa kushiriki ktk Global Youth Symposium for SDGs, nimewaambia nimebanwa. Just nipate muda na space ya kupush hii kitu ianze. Na itaanza tu inshaallah.

Tutatoa kila kitu unachohitaji ili uwe profitable forex trader. Kadri tunavyokuwa ndivyo tutazidi kupanuka, kuwafikia watu wa mikoani mpk hii kitu ieleweke. Najua it's not easy, but it's possible.

Only Special for JF
Since day 1 JF is my family, tunakutana majukwaa mbali mbali tunataniana, kukwaruzana, kupishana mitazamo, lkn sisi ni ndugu. Thanks kwa team nzima kupambana effortlessly kuhakikisha hii kitu (JamiiForums) inadumu, najua wanapitia mengi ili JF iwe shut down lkn wameendelea kuwa strong forever. Na Alaaniwe hayawani yule anayetaka kuizima JF, na mwingine anataka kuzima mtandao. Shame!! - no politics am real.

Mimi nikikwambia nimelipa Rand 14,000 (ni kama mil 2.5) kwaajili ya 1 to 1 mentorship huwezi kuamini. But wanaoelewa forex wanajua nini namaanisha. Vijana makini sana ambao pia nina malengo ya kumeet nao mwakani wanaitwa AstroFX wana charge $7500 kwaajili ya 1 week training na 6 months guidance ktk forex.

Mimi nimekaa na kuwaza sana, nimefikiria nitoe offer ya watu wa mwanzo kabisa kutoka JF. It's gonna be FREE! namaanisha 100% FREE. Watu 300 wa mwanzo nitakaoanza nao hii safari nitatoa learning materials, trainings, mentorship, na 3 months guidance for free. I am blessed to bless others - Don't misquote me.

Kwanini nafanya free?! Bado forex haijulikani TZ, na ni ngumu sana kubadili mind set ya watanzania wengi - ambao mara nyingi hua hawapendi kujifunza. So, natoa hii kitu for free kwa watu wa mwanzo, ili wapige pesa na wabadili financial status zao. Then hawa watu watakua ambassadors wangu, namaanisha hawa ndio watatutangaza pande zote za TZ. Watu wakimake consistent profits, wakaelewa how it works basi kama watu hawa si wachoyo wa mafanikio wataenda kuwashtua wenzao - ndugu, jamaa na marafiki. Hapo tutaanza na reasonable fees mpk tutakapoona ni muda sasa wa sisi nasi kula jasho letu, ndio tutaanza kuweka bei za faida.

Again I salute all you bosses

ONTARIO.
Niweke kwenye Orodha mkuu
 
Yani nasoma wee nakua kama naelewa vile...kuna muda nahisi kama mambo ya mkeka flani hv...ila ngoja
 
Ina maana hii kitu hata wafanyakazi wa mabenki hawajui huu mchezo kweli? very interesting.
 
FOREX IS HALAL IF
Forex is Halal if you are not gambling and have your end goals clearly distinguished.
1- As a Forex trader you need to have a reason to take that action (sell or buy)
2- Not gamble on the trend direction but analyze the market
3- Not trade for the sake of excitement but trade for the potential income and to make a living
4- Not to approach it as a game but as a job
5- Have a mindset to win or to protect your equity rather than telling yourself “if I win I win, if not next time”
6- You learn from your losses and move on with the decision taken by yourself rather than blaming the market or blaming the situation
7- You have a SWAP free account or trade avoiding SWAP
FOREX IS HALAL OR HARAM?
There is a thin line between trading and gambling, we all must admit it. But the good news is that you can avoid being a gambler.
1- Only take trades with a high probability of making profit based on your analysis
2- Exiting a trade is as just important as entering one, have a trade plan
3- Define your stop levels
4- Choose the right entry size, if you are risking all to double it its is called gambling
5- Know what you are trading
6- Understand the time frames, do not be addicted it is a sign of gambling
7- Back test your strategy and aim to develop it
8- Constantly review your historical performance and try to understand why you made loss and profit
9- Be disciplined, trading is a job not a game
10- Focus
11- Trade with an Islamic account providing Forex Broker
Note: The above is a part of my 1 week research with 3 Islamic scholars from Azerbaijan, 1 from Irag, 1 from UAE, 1 from Indonesia and 1 from Egypt. Since this subject is debatable please feel free to comment your thoughts below in the comments section
Hii ni kwa wale ndugu zangu katika iman yaan waislam.
Mkuu ONTARIO nimekutana na kitu Swap-free Forex islamic account.
Kuna tofauti gani kati ya ma broker wengine na hawa wa Swap free Forex islamic acount
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom