Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue!

Status
Not open for further replies.
Benki zote zenye visa au mastercard. Au benk zote zinazo support online payment!!

Siyp benki zote zenye visa unaweza kuzitumia kupokelea malipo toka nje ya nchi kwa njia ya VISA/Master. Kuna benki nyingine ni vimeo haswa, wakiongozwa na NBC.
 
m

msaada wako mkuu,nimefungua demo account kupitia XM na nikapata ID no ila kila nikijaribu kulog in inashindikana,naomba kujua sehemu nyingine ambayo naweza kufungua demo account bila usumbufu...nataka ni practice niliyokwisha yasoma.
Forex demo account inahitaki email tuu na password
 
Siyp benki zote zenye visa unaweza kuzitumia kupokelea malipo toka nje ya nchi kwa njia ya VISA/Master. Kuna benki nyingine ni vimeo haswa, wakiongozwa na NBC.


Theoretically inatakiwa ziwe na huo uwezo. Ila baadhi ni kweli zinazingua na zina usumbufu!! Mfano mzuri ni hizi benki kongwe!!
 
Theoretically inatakiwa ziwe na huo uwezo. Ila baadhi ni kweli zinazingua na zina usumbufu!! Mfano mzuri ni hizi benki kongwe!!
Hii ni kwa ajili yako mkuu sana Lodrick Thomas pamoja na infant traders wengine.

Naona umeingia live, hongera sana kwa uthubutu uliochukua, so impressing. Lakini nashangaa unafanya makosa ambayo ni very obvious hutakiwa kufanya. As I said earlier, There's a very thin line separating forex and gambling, mstari unaotenganisha FX na betting ni mwembamba sana. Kuna picha (screen shot) ulishare, 1 kwa 1 niseme unachokifanya si financial trading bali ni gambling.

Edited: screen shot ya Lodrick

Kwenye fx, Ukifanya analysis unatoka na conclusion 1 tu; Either to buy or to sell or to stay away from the market... and the most important thing is ni kuanalyse entry point and exit point. Lazima utambue kuwa it takes the same skills and efforts to realise there isn't a trade as it takes to find a trade

Ulichokifanya kwenye hiyo screen shot ni indiscipline, utovu wa nidhamu. Haiwezekani same currency EURUSD ukasell na ukaBuy [emoji23] [emoji23] . Yani ni utovu wa hali ya juu sana in forex. Yani hapo maana yake ni liwalo na liwe - cha kufia nini (kama ulipita jeshi). Hapo ulipaswa ufunge trades za sell na kuacha za buy zirun or vise versa. Na kama haukua na uhakika bora ungelikimbia soko hadi opportunity ije.

FX ni kama biashara zingine boss, kama hakuna fursa basi hakuna haja ya kufanya biashara. Ni jambo la ajabu sana mtu akaenda Rorya vijijini huko kisha akafungua massage parlour, sawa na FX yani hauoni fursa lkn unalazimisha kutrade.

Kuuza na kununua currency pair 1 boss ni kosa litakuja kuunguza a/c yako kama ukiliendekeza. Yani ni jambo la ajabu sana unakuta mtu yupo kwenye Buy ya XAU/USD at the same time yupo kwenye sell ya AUDUSD. Au unakuta mtu anauza Aussie (AUDUSD) na muda huo huo ananunua kiwi (NZDUSD). Yani ni nidhamu ya kiwango cha standard gauge. Au unakuta mtu amebuy Brent oil (USOIL) at the same time yupo ktk buy ya USDCAD.

●●But usiwe na presha ndipo tulipotoka bro... Tutaelezeana mdogo mdogo - lkn ukiwa na haraka haraka, unaeza kujifunza kwa njia ngumu na ndefu sn.

Wiki iliyopita currencies zilikua hazijakaa poa sana, hasa pairs za USD. Kuna yule Kijana wangu mmoja akaingia buy USDCAD alivyonitumia screen shot, nikashtuka sana maana tyr alikua ana loss ya -60 USD. Nikamwambia funga positions zote, kisha nikamwambia nunua mafuta chap chap - Dogo akaingia sokoni akanunua mafuta, ndani ya muda wa km siku 2 akagonga zake $140 tukaifunga wiki kwa amani.

Edited: screen shot ya jamaa'ngu.


==============================

Edited:

Pia kwa lot size unayotumia eeishhh. Itakuchukua muda mfupi sana kutia kiberiti account yako. Kijana wangu alianza $150 (though sikukubaliana naye - hakukua na jinsi) mpk leo account yake ina balance ya 437... lkn anatumia lot za 0.01 mwisho kbs ni 0.02 kama nikimruhusu. Unachokifanya wewe kwa account ya $70 kutumia lot ya 0.23 ni uncalculated risk ama uroho. Boss forex ukiiletea uhoro inakuchambua kama karanga.
 
m

Mkuu huyo ni broker gani aiseee!! huyo anyetoa 25% bonus ya pesa uliyoweka.. Maana hata mimi nilikuwa na mpango wa kujiunga na XM Broker nimemsoma na kumwelewa vizuri sana maana yeye ukianaza ana trading bonus ya $30. Niambie huyo broker mkuu na mimi nimjue.. Do the needful please Mr. Ontalio
 
Kwanza nimpe mkuu Lodrick Thomas Hongera kwa uthubutu kwan kupitia makosa yake madogo madogo tunajifunza mengi lakini Pia nizilete shukrani zangu kwako mkuu ONTARIO kwa kuendelea kua na sisi vijana wako wasumbufu kwa muda wote bila kuchoka ni moyo wakipekee sana ambao wengi wetu tunapaswa kujifunza kutoka kwako, Zaidi nakuombea kwa Mungu Lengo lako litimie na soon as possible Utualike Darasani, haya makosa madogo madogo yakina Lodrick Thomas na wengi huko utayamaliza. Thank you Much na Mungu awe pamoja nasi.
 
Good and brotherly advise, Nahitaji mentorship yako mkuu, niko mwanza or you can direct me, tell me the price.

 
Hahahaha.. Nimecheka kwa sauti eti kufungua massage parlour rorya mfano halisi sana huu.. Me ndomana nahangaika sana kujua kufanya analysis maana kweli ctaki mambo yakuingia nakufanya gambling pair moja ioio una sell na kubuy ili ukikosa upande huu upate mwingne.. Kwangu naona kujua kufanya analysis is everything!! And am here patiently waitn for your class mkuu ONTARIO i believe in learning from the pro's!!
 
Kweli Kabisa....forex ni kitu ingine inaweza kukuvua nguo sekunde kadhaaa...mwanaume ukajikuta unachutama ghafla na kilio juu..

Nakumbuka nilianza demo last week...kwa margin ya 5k ila nikaweka leverage Kubwa sana 500:1 (sio uroho hii kitu ya leverage ilikuwa haijaclick vzuri kichwani) siku ya kwanza nikapiga profit ya 2k+...nikacheka nikaendelea na book...j3 soko lilikuwa Nzuri sana nikaaza saa saba alfajiri kutrade...mpaka kunakucha nilikuwa na balance ya 10k+...nilitrade EURGBP pamoja na XAUUSD..mpaka inafika j3 jioni balance yangu ilikuwa 18k+.

Kimbembe kikaanza j4..nilifwekwa mapema mapema nikabakiza kama 12+ balance...nikawa mbishi nikaendelea kutrade nikapigwa tena mpaka balance ikawa 720....nikapigwa tena nikabaki na balance ya 33. Nikakubali matokeo...nikaendelea kusoma...Jana nikaanza tena na ka 33 kangu...naingia kwa lot ya 0.01 nafungua positions si zaidi ya NNE...nikaenda nako Mdogo Mdogo mpaka soko linafungwa nina balance ya 140..

Hii kitu inahitaji discipline ya hali ya juu sana.
 
Wakuu hiyo ni li trade Jana so ya hapo juu ndo profit Au vp lkn bado Niko demo account naomba ufafanuzi
 

Attachments

  • Screenshot_20170701-174029.png
    44 KB · Views: 63
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…