Forex ni scam au real?

Forex ni scam au real?

Mimi huwa najikusanyia peaa ya vocha huku nikijifunza taratibu kwa siku sikosi 1 usd profit... I will do anything to learn this
Screenshot_20210803-180539.jpg
 
Nimeandika mada ndefu kiasi, so tenga muda kiasi , wale mtakaopita na kusema nimeandika pumba mna nafasi pia ya kucomment karibuni.

wakuu habari zenu, hongereni kwa wale mnaonufaika na hii kitu ya kuitwa Forex, kwanza kabisa lengo la kuwa mention hapa ni baadhi yenu ambao mpo kwenye huu mjadala, napenda na mimi nizungumze machache juu ya hii biashara, japo ni mada ya muda lakini mniwie radhi, naweza sema nimechelewa kuona huu mjadala.

Huu mjadala unatokea kwenye huu uzi (Siri kubwa kuhusu Forex hakuna Mentor anaetaka uijue) ambapo aliandika TEAM 666

Kwanza kabisa biashara hii wengi wetu humu tumekuwa tukisema ni utapeli na n.k kikubwa kuna watu hawaamini kabisa katika hii biashara na wao wanasema ni betting na kuna ambao wanasema hii biashara ni halali na imewatoa kimaisha, mvutano huu utakuwepo mpaka kesho na kesho kutwa, nizungumze machache ninayofahamu kuhusu hii biashara.

Katika research yangu nimegundua ni kweli watu wanatengeneza pesa kupitia hii biashara na kweli wanatengeneza pesa si mchezo na pia wapo wanapoteza pesa na hawana tena matumaini.

Forex ukitazama graph zake zinapanda na kushuka na pia mtaji wako utapanda na kushuka kama graph zinavyoonyesha.
Watanzania wengi ni masikini hivyo wana ndoto za kugeuza $100 kuwa $200 kwa siku 2.

Hebu tujiulize akitokea mtu ana uwezo na strategy ya kupata profit 100% within 2-3 days au niseme wiki ina maana baada ya muda fulani hata Elon Musk atakusikia na atakufahamu.
Mathematically.
tufanye una strategy yenye accuracy ya hatari yaani within a week una 100% profit.
so.
100 x 2 = 200 1st week
200 x 2 = 400 2nd week
400 x 2 = 800 3rd week
800 x 2 = 1600 4th week
1600 x 2 = 3200 5th week
3200 x 2 =6400 6th week
6400 x 2 = 12800 7th week
25600 8th week
51200 9th week
102,400 10th week
204,800 11th week
409,600 12th week
819,200 13th week
1,638,400 14th week
3,276,800 15th week
6,553,600 16th week
13,107,200 17th week
26,214,400 18th week
52,428,800 19th week
104,857,600 20th week (Hapa Ushakuwa zaidi ya Ginimbi bongo, celebrity wa kike wanakugombania) wiki ya 20 tu 🙂
209,715,200 21th week
419,430,400 22th week
838,860,800 23th week
1,677,721,600 24 th week
3,355,443,200 -------------------------(Hapa moo anakusikia kwenye redio na ni wiki ya 25)
6,710,886,400 26th week
13,421,772,800 27th week
26,843,545,600 28th week
53,687,091,200 29th week
107,374,182,400 30th week
214,748,364,800 31st week----------------(Hapa Vladimir Putin na Elon Musk wameshakufahamu na ni wiki ya 31 hata mwaka hujaisha) You are the 1st billionare in the world na kila mtu duniani hata Biden anakufahamu.

Huo mtiririko hapo juu wa earnings na time ndio mawazo ya vijana wengi wadogo wanaongia kwenye hii biashara.

Hayo ndio mawazo ya watanzania wengi kuhusu Forex kwamba kuwa bilionea wa kwanza duniani kabla ya mwaka kuisha kwa maana kuwaza utaingiza 100% profit ya capital ndani ya wiki 1 au 2, ni sawa na kuwaza kuwa bilionea wa kwanza duniani kabla ya mwaka kitu ambacho haiwezekani... at all haiwezekani.

Acha we mwenye $100 kuna ambao wana $1m na kungekuwa kuna urahisi huo na kuna trader ana strategy na uwezo wa maajabu kama huo wa ku trade basi tajiri wa kwanza duniani angekuwa trader.

Lakini professional trader wote kwa nini huwasikii kwenye list ya matajiri wakubwa mfano 5 bora, utakuta Musk, Jeff Bezos, Bill Gates, Bernard Anault , Mark n.k... ni kwa sababu Forex ni risk niseme ni very risk.

Wewe unaweka $100 unachukua very high leverage mfano 1:500 hapo una $50000, which means ukitrade kwa units zote unaingiza 5$/pip which means market ikiwa kwenye favor yako unahitaji only 20 pips kuwa na profit ya 100 usd, na hapo ume double, but leverage ya 500 ina hitaji -20 pips tu ikaushe na mtaji wako na hapa ndipo sekeseke linaanzia.

Ukweli ni kwamba kuwaza mafanikio kama hayo ni sawa na kuwaza utachukua sport car uikanyage tuseme unatoka Dar unakwenda Mwanza na speed yako ni 180km/hr haushushi, umbali km 1200, kwa maana utumie saa 7 tu kufika mwanza, hujawaza kuna bumps,kona, kuna gari njiani but ukijaribu nini kinatokea? ni kifo... same na Forex.. kweli kuna sehemu itafika utakanyaga hadi 200km/hr lakini itakuwa ni kwa umbali mchache.

Thats why wengi wanaanza vizuri in long run wanafeli vibaya.

Kuna dada namfahamu ni kamanzi fulani ni kapisi kinoma age kwa makadirio 23yrs back in 2018 kalinionyeshaga chart zake asee alikuwa ana trade alikuwa anaishi kwa Madiba Cape Town yule manzi alitrade from $10 mpaka akafikisha $5400 within 3 monthes, si unajua tena wabongo kwa connection sikuwahi kumuona face to face baadae kalisafiri kwenda ughaibuni, nilirushaga ndoano ikarudi na chambo... samaki sikumkamata ... 🙂 nilimuuliza amefanyaje ? alinambia bahati imechukua nafasi kubwa pia ni katika kukuza mtaji tu lakini sio namna bora ya trading kwa muda mrefu, nilitazama anavyotrade ni kawaida mnoo.

Pia nimefatilia na kuwauliza hao wanajiita professional traders, nikachukua nasaha 1,2...3, kikubwa wanachozungumza karibu wote ni kwamba forex kwa asilimia kubwa ni psychology,money management, risk management na strategy ina asilimia ndogo.

Kuna traders wana strategy zina accuracy ya 40% winning, which means within 10 trades ana loose trades 6 na 4 pekee ndio wanashinda, and wanakuambia wapo profitable na wameridhika na forex kwao ni ajira na kila kitu.
Kama huamini nifanya hesabu hapa uone jamaa wapo profitable kabisa.

Tuseme ana $50000 ana leverage ya 5, kwa hio hapo ana $250,000, akiweka units zote ni sawa na $25/pip anaingia kwenye soko anataka kufanya target afunge na 40 pips which means profit itakuwa $1000, kila siku ana trade 1, so within 10 days na strategy yake ya ku loose 6 na kupata 4 akiwa na risk reward ratio ya 1:2,atapata kama kama ifuatavyo.

ana risk $500 na target 1000. risk 20 pips na target 40 pips.
4 x 1000 = $4000 profit.
6 x 500 = $3000 loose.
4000 - 3000 = 1000,
ametengeneza $1000 profit within 10 trades which took 10 days, so within a month ana $3000.

Hapo nimetolea mfano na ndivyo uhalisia wa Forex ulivyo, kuna watu wanajenga nyumba ya Mil 50 anapangisha 7 mil/yr mfano.
Huyu wa Fx ana milioni 100 anatengeneza 6 million per month na 72 million per year.
Fx katengeneza 72% as profit/yr na huyu ni trader ana trade kwa adabu anahitaji mwaka na miezi arudishe pesa na ana double mtaji, so soon anaanza kuingiza $6000/month, na ile ile style yake ya ku loose trade 6 na ku win 4.
Hapo anatumia leverage ya 5, vipi akiweka ya 15, so Forex ni very profitable sema unahitaji maarifa.


Real Estate amepata 14% as profit kwa mwaka, anahitaji miaka 7 na miezi arudishe pesa yake.

Na hapo ndipo unapoamini kwamba Forex ni biashara kama zilivyo biashara zingine japo kwa namna moja ama nyingine inaweza kuwa na faida nzuri, kuna hasara na faida na mengineyo.

Nmefanya reserach ya kutosha, nimefuatilia hawa guru wa ku trade wengine hata nimeonana nao pitia skype n.k lakini watakuambia kitu kimoja cha kuzingatia discipline, pyschology..and all that...blah blah blah.....

Sasa basi hatupo kwenye darasa mimi Forex najua wengi hapa mnanizidi maarifa lakini najaribu kuwasilisha tu mawazo yangu na uzoefu mdogo nilionao juu ya hii biashara. Thanks......

Sasa basi niseme tu... ni metrade kama hobby na nimeingiza tu hela twa vocha n.k lakini kwangu ni kama side hustle, nawaza siku 1 may be nikiwa comfortable ku invest at least $10000 kwa kuanza then taratibu naweza kuwa full time trader kama nikipata profit nzuri.

So issue ni kwamba Forex inapaswa uwe na mtaji, uifikirie kama biashara ya real estate au biashara ya duka or any kind of legal business, si unaona mtu ananunua costa ya Mil 50 au 70 na anapewa profit ya 80k tshs kwa siku, so same na Forex.

Kuna traders professional na wapo comfortable kabisa wanatengeneza good 10% per month kwa hii biashara kwa sababu wametrade for years, wana mitaji minono,wana ile kitu wenyewe wanaita 6th sense baada ya kutrade kwa muda mrefu wamenunua gari za kifahari, wamenunua majumba ya kifahari wana mamanzi wakali kinoma noma and all that. lakini it takes time kufika hapo.

Hata hivyo hawa jamaa baada ya kulizoea soko kwa muda wanaweza kukuza mitaji yao kwa muda mfupi sana wanaacha ghafla hio tabia mbaya na kuanza ku trade kwa adabu...so huwa wanaweza kujitune kuwa agressive kwenye market n.k...kikubwa tayari wana 6th sense kwenye market yaani... ukichukua sample ya damu yake ukaweka kwenye microscope unaona candlestick tayari ana coonnection na Fx market 🙂 ...j*k*

Sasa sisi tukiona zile picha na traders instagram tunaona this is it... unaingia na $1000 zako unapigwa kipigo cha mbwa koko, kama yule dogo naonaga anaitwa FBK yule ni gambler sio trader....beleive it kuna gambler wengi tu casino na wametajirika kupitia gambling.....🙂 Kuna wengine wameathirika na gambling kabisa, ukikutana na gambler wamekubuhu wanaweza wakawa wanatembea wakaona jogoo zinapigana hapo hapo wanaweka pesa kubet nani anashinda.

So forex sio gambling wala betting, kwenye kubet hakuna risk management lakini kwenye forex ipo, so ndugu zangu tuelewe hivyo wanaokula hela ya hili soko ni wale wana mitaji minono na pia wamepata hiyo kitu inaitwa 6th sense, yaani ipo hivi....

Ukijua kuendesha baiskeli, hata ujue vipi na uwe bora kiasi gani huwezi kumfundisha mtu ambae hajui akajua siku hiyo ghafla akaanza kuendesha kama wewe... utamwambia usitazame tyre tazama mbele... kanyaga pedali na uende mbele... n.k
Kweli kuendesha kuna mambo ya msingi machache tu... tazama mbele.... kanyaga pedali... songa mbele thats it na simple kabisa...
Lakini kwa sababu wewe ni mwl na una uzoefu kwa siku unaendesha km 10/ siku unaweza hata kuendesha unaangalia juu, umeshika mkono mmoja, umekaa kiti cha nyuma n.k.

Sasa hiyo hali ya wewe kushindwa kumuelezea mwanafunzi jinsi gani una balance hiyo baiskeli hauanguki ndio tunasema 6th sense, hiyo huwezi elezea... na haifundishiki bali inapatikana kwa kufanya mazoezi ya kutosha na kwa sababu mwanadamu tuna software kichwani ya ku adapt vitu basi uta adapt.

Lakini huwezi kumuelezea mwanafunzi wewe una balance vipi hauanguki na hio baiskeli kwa nini yeye anaanguka, wakati huo atajua una siri na kuna jambo una mficha lakini anafikiria wrong, anahitaji aendeshe aanguke, afanye mazoezi ya kutosha, baadae baada ya muda atakuwa na yeye anaendesha huku anatazama juu kama wewe.

Thats why professional trader anaweza kuanza na $100 akafika $5000 akaanza kutrade kwa risk ndogo akiwa bara bara ya kuelekea $10000, ukabaki mdomo wazi japo it takes time... which means wana connection na market tayari...

Thanks...

Nseme tu ahsanteni sana ndugu zangu kwa kusikiliza mawazo yangu na kutenga muda wako...nisiwachoshe sana naweza andika mengi ni ka wa bore... kikubwa loose what you can afford, Forex ni risk kama zilivyo biashara zingine,Forex ina faida kama zilivyo biashara zingine.

Thanks for your time...

TEAM 666
RRONDO
ONTARIO
gfsonwin
Nyani Ngabu
Upepo wa Pesa
prospilla
Grahnman
Na wengineo...itoshe kwa kusema tu...itifaki imezingatiwa 🙂
Uchambuzi mzuri sana huu
 
Ukiniambia neno moja lakukushauri kufanya, hiyo hela kampe mama ntilie kama huna chakufanyia.

Forex ni mchezo mchafu, usidanganyike kuwa odds zipo upande wako, unapigwa na market, na broker, cfd yaani unapigwa kote kote mbaya zaidi ukiwa na nyota nzuri ukapiga hela, my dear hupati hela broker anakupiga na huna pakushitaki, njoo kwenye serikali yetu unawekwa ndani 😁😅 sasa wewe jifanye una tafuta odds

Market yoyote ina circle, ikiwa katika circle nzuri, hata mbumbumbu anaweza kupata profit FX lakini soko likigeuka ni wanao elewa tu, economic, business, stocks, futures etc ndio wanao piga hela.

Wapo wanao fanya hicho kitu, na broker wao sio hawa mnao wajua, kwanza kufungua account tu si mchezo, hebu wewe mwenyewe fikiria yaani kitu chakukuingizia mahela unafungua leo unaanza kutrade eti leo au kesho, kichwa chako kinachaji kweli 😕🙌 wakati kuchukua mkopo mkubwa benki sio siku mbili. Broker hawa ni wawatu wachache, tena entry zao si chini ya $ 50,000 na kuendelea.

FX ni gamble, ila Stock market ni investment, vyote hivi ni lazima ujuwe who are your enemies. Kwenye hela hakuna urafiki ila kuna maadaui.

Kama wewe unapenda ku take risk, fanya hivi kama unataka kufanya FX;
  • Soma chimbuko la FX na uhalisia wote unaozunguka FX.
  • Soma wanaoshikilia FX, na kuelewa structure nzima ya FX marketing.
  • Soma about currency and little bit of economic related to currency exchange, etc.
  • Soma stocks, future and correlation between them and FX.
  • Fahamu pillar za economic.
Na mengineyo utajua ukiwa uasoma hayo, then fanya hivi;

• fungua account ya FX demo, trade efficiently and effectively with resonable strategy kwa 6 mnths hata year. Then ukiweza kutengeneza pesa, win to loose ratio. Then fungua really account na anza kutrade.

Ila nafahamu ukifwata hatua hizo zote hapo utanambia, mwishoni huta trade FX na kama uta trade itakuwa kwa mwezi unatrade mara moja hadi mara tatu nawe utakuwa ni long time trade, wa ku buy and hold kwa miezi kadha, kama Stock investor.

Kama wewe ni forex trade hafu hujaelewa nilicho kisema, ndugu unahatari sana. 😅😅😅🙌🙌🔥
Ukiniambia neno moja lakukushauri kufanya, hiyo hela kampe mama ntilie kama huna chakufanyia.

Forex ni mchezo mchafu, usidanganyike kuwa odds zipo upande wako, unapigwa na market, na broker, cfd yaani unapigwa kote kote mbaya zaidi ukiwa na nyota nzuri ukapiga hela, my dear hupati hela broker anakupiga na huna pakushitaki, njoo kwenye serikali yetu unawekwa ndani 😁😅 sasa wewe jifanye una tafuta odds

Market yoyote ina circle, ikiwa katika circle nzuri, hata mbumbumbu anaweza kupata profit FX lakini soko likigeuka ni wanao elewa tu, economic, business, stocks, futures etc ndio wanao piga hela.

Wapo wanao fanya hicho kitu, na broker wao sio hawa mnao wajua, kwanza kufungua account tu si mchezo, hebu wewe mwenyewe fikiria yaani kitu chakukuingizia mahela unafungua leo unaanza kutrade eti leo au kesho, kichwa chako kinachaji kweli 😕🙌 wakati kuchukua mkopo mkubwa benki sio siku mbili. Broker hawa ni wawatu wachache, tena entry zao si chini ya $ 50,000 na kuendelea.

FX ni gamble, ila Stock market ni investment, vyote hivi ni lazima ujuwe who are your enemies. Kwenye hela hakuna urafiki ila kuna maadaui.

Kama wewe unapenda ku take risk, fanya hivi kama unataka kufanya FX;
  • Soma chimbuko la FX na uhalisia wote unaozunguka FX.
  • Soma wanaoshikilia FX, na kuelewa structure nzima ya FX marketing.
  • Soma about currency and little bit of economic related to currency exchange, etc.
  • Soma stocks, future and correlation between them and FX.
  • Fahamu pillar za economic.
Na mengineyo utajua ukiwa uasoma hayo, then fanya hivi;

• fungua account ya FX demo, trade efficiently and effectively with resonable strategy kwa 6 mnths hata year. Then ukiweza kutengeneza pesa, win to loose ratio. Then fungua really account na anza kutrade.

Ila nafahamu ukifwata hatua hizo zote hapo utanambia, mwishoni huta trade FX na kama uta trade itakuwa kwa mwezi unatrade mara moja hadi mara tatu nawe utakuwa ni long time trade, wa ku buy and hold kwa miezi kadha, kama Stock investor.

Kama wewe ni forex trade hafu hujaelewa nilicho kisema, ndugu unahatari sana. 😅😅😅🙌🙌🔥
We jamaa unaongea utadhani wewe ndo kipimo ambacho watu wengine wanatakiwa kujipima.

Ukishindwa kitu Fulani haimaanishi wengine watashindwa kama wewe.
 
fOREX sio scam ila hawa traders wa instagram na twitter ndio wanaofanya hii biashara ionekane kama ni utapeli huwa wanawaaminisha watu utajiri uliopo kwenye forex kiasi kwamba forex ni mgodi wa dhahabu yani ukiingia tu after few days/weeks/months we tayali ushakuwa tajiri na soon utaanza kumiliki BMW mpyaa na hanasa nyingine.

Tukumbuke suala la biashara sio kitu cha kukikurupukia tu.Kiufupi ukitanguliza suala la PESA mbele ktk biashara yeyote ile wakati mwingine unaweza usikutane kabisa na hizo PESA...Maarifa juu ya biashara unayotaka kuifanya ni muhimu sana.
 
470d9e1c-25c9-4a19-9a00-c8cbea993a3a.jpg

a6329ecc-ddbf-43c8-a4e3-d53fdeab7533.jpg

00fa8f9a-8656-40d8-806f-58cec5a07f4c.jpg

Mmeongea sanaaaa ila forex sio wizi ni ww tu usipo kuwa na elimu ya kutosha utapigwa sana sokoni utaona ni wizi nimetrade fx kitambo ila sikuwa na elimu ya kutosha mwaka huu ndio naona matunda kwenye fx baada ya kupata elimu ya kutosha

Cha msingi wekeza kwanza kwenye maarifa mtaji sio tatizo kabisa unaweza anaza hata na 10$
IMG_2484.png

Kamaa hapaaa iyo ni 9$ inakupa 50000/= kwaiyo ni swala la elimu

Pia watu tunajisahau kuwa forex ni biashara manake kuna faida na hasara piaa. Hata uwe na strategy bora kiasi gan lazima upate hasara coz hii ni biashara chamsingi ni kusimamia mtaji wako vizuri mwisho wasiku ufunge na faidaa tu unaeeza win 70$ leo kesho ukapoteza 20$ ila badae ukawin 80$ kwaiyo mwisho wa siku hakikisha una faida nzuri

Note: kikubwa ukitradae hakikisha una chomoa faida kuna raha yake asee
 
View attachment 1968833
View attachment 1968835
View attachment 1968834
Mmeongea sanaaaa ila forex sio wizi ni ww tu usipo kuwa na elimu ya kutosha utapigwa sana sokoni utaona ni wizi nimetrade fx kitambo ila sikuwa na elimu ya kutosha mwaka huu ndio naona matunda kwenye fx baada ya kupata elimu ya kutosha

Cha msingi wekeza kwanza kwenye maarifa mtaji sio tatizo kabisa unaweza anaza hata na 10$
View attachment 1968836
Kamaa hapaaa iyo ni 9$ inakupa 50000/= kwaiyo ni swala la elimu

Pia watu tunajisahau kuwa forex ni biashara manake kuna faida na hasara piaa. Hata uwe na strategy bora kiasi gan lazima upate hasara coz hii ni biashara chamsingi ni kusimamia mtaji wako vizuri mwisho wasiku ufunge na faidaa tu unaeeza win 70$ leo kesho ukapoteza 20$ ila badae ukawin 80$ kwaiyo mwisho wa siku hakikisha una faida nzuri

Note: kikubwa ukitradae hakikisha una chomoa faida kuna raha yake asee
Mt4 za iPhone zinapendeza Sana ngoja nivute iphone
 
Wakubwa hivi hii forex ilianzishwaje af kwa nini itawale sana kwenye mitandao
 
Duh sijajua why imekuja kama notification maana hata sijatagiwa ila uko nondo mkuu af suala la mtaji ni muhim ila sio muhim saaana
 
Mwaka 2008 wakati bitcoin inaanzishwa, ilijitokeza fursa ya kujipatia sarafu kwa kuchimba (mining) kupitia computer bure. Wachache waliamini wakachimba ila wengi walipuuzia kwa kuwa hazikuwa na thamani ya pesa (monetary value) kwa wakati huo. Wale waliochimba wamenufaika kwa kuuza sarafu walizochimba.

Miaka 14 baadaye imejitokeza tena fursa ya kujipatia coin za RENEC kwa kufanya mining.

1. Kujisajili na kuchimba ni bure.
2. Hakuna ulazima wa kumuunga mwenzako.
3. Coin ikizinduliwa waweza kutoa pesa kwa njia ya simu au benki.

Kama upo willing, nicheki DM kwa maelezo zaidi na jinsi ya kujiunga njoo DM ni buure bila hata 50

Pia waweza kutembelea ukurasa wa instagram Heisslyman Msaba
 
Kuna msemo unasema hivi,,, Anguka nyanyuka, anguka nyanyuka kunasiku utanyanyuka Moja Kwa Moja,,,, kun baadhi ya watu kipengere cha kuanguka kwenye biashara biashara hawataki hapo ndipo sekeseke linapoanza kuwa forex trading is betting km betting zingine, hawataki kujifunza kwa walio fanikiwa wao wanataka chap kwa harakat kulala maskini kuamka na V8 GXR ndani ya usiku mmoja ni kitu kwamwe hakiwezi tokea kupiti forex.....!!! Pmj cn wadau wa Forex tujaze buti wakubet waendere kubet simple
 
Back
Top Bottom