Formula; 'Ondoka' 'Acha' ndio maana halisi ya kupata Mafanikio

Formula; 'Ondoka' 'Acha' ndio maana halisi ya kupata Mafanikio

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Formula; "ONDOKA" 'ACHA' NDIO MAANA HALISI YA KUPATA MAFANIKIO.

Anaandika, Robert Heriel
Mwanafalsafa

Nitakuambia ukweli na siri wala sitakuchaji hata sumni wala shilingi yoyote. Vitu tulivyopewa bure tunavitoa Bure. Wala usinipe sifa yoyote Kwa maana sistahili sifa. Wala usinishukuru Bali mshukuru Mungu wako aliyekuumba.

Niite Taikon Master, Mwalimu asiye wa Mshahara lakini asiyepungukiwa na chochote.

Kila mtu hupenda kufanikiwa Kwa kila Jambo alifanyalo. Binadamu wengi Kama sio wote hupenda mambo mazuri. Kwayo huyaita mafanikio. Hata hivyo kila mtu anamafanikio yake kulingana na Yale ayapendayo,

Lakini mafanikio ili kuyafikia kunahitaji mchakato Fulani. Leo Taikon atajadili Jambo moja nyeti katika Mafanikio ambalo ni kanuni ya "ONDOKA" au "ACHA" na ili uondoke au uache itakupasa usiwe na UOGA. Ukiwa muoga huwezi kuondoka au kuacha baadhi ya vitu au mambo. Utaishi Kwa mazoea na kuogopa vitu ambavyo havipo.

Huwezi kufanikiwa katika Jambo lolote Kama hujaitumia kanuni hiyo. Kanuni hiyo ni moja ya nguzo muhimu ya mafanikio.

Kuondoka au kuacha ni Kama kanuni moja niliyowahi kuielezea iitwayo kujipachua, hata hivyo katika kanuni ya kujipachua nilijikita zaidi katika kuelezea mfumo mzima wa kuunda Uhusika bandia Kwa kuji-matrix(kujipachua). Kujipachua kunamaanisha huwezi kufanikiwa katika maisha ukiwa na uhusika mmoja(uleule) lazima uwe na uhusika mbalimbali.

Mfano, Mimi Taikon halisi nijipachue mara tatu. T¹, T², T³ na kila uhusika uwe na roles zake. Maadui zangu nihakikishe wanapambana na wahusika bandia niliowaunda huku Mimi mhusika OG nikiwa naendelea na mambo yangu. Hata hivyo hiyo sio mada ya Leo.

Kuondoka au kuacha ni kitendo cha kutoka au kubadilisha kitu au Hali au Jambo au Mazingira kwenda katika kitu au Hali au Jambo au Mazingira mapya.

Kwenye maisha hiyo ni kanuni namba moja ya mafanikio.

Aina za kuondoka au kuacha;
1. Kuondoka Kiakili
2. Kuondoka kimazingira
3. Kuondoka kimahusiano
4. Kuondoka Kiroho

1. Kuondoka Kiakili.
Hii ni Ile hali unaifanya akili yako isifikiri Kwa namna uliyozoea, Kwa kuwaza vitu vipya na kuvifanya Kwa vitendo.

Huwezi kufanikiwa kwa akili ya zamani uliyonayo hivi leo.
Lazima akili yako uweze kuifanya ifikiri vitu vipya kisha uvitekeleze.

2. Kuondoka kimazingira.
Huwezi fanikiwa katika Mazingira yaleyale uliyozaliwa, ni ngumu Sana.
Mafanikio ya watu wengi huchipuka pale wanapoondoka sehemu zao za Asili na kwenda Maeneo mageni.

Wazungu na mataifa ya Ulaya yalifanikiwa Kwa namna hii kipindi cha Mercantilism, ukoloni na sasa ukoloni mamboleo.

Wahindi, waarabu na sasa Wachina wote wanatumia kanuni hiyohiyo.
Kwa hapa Tanzania, Makabila kama Wachagga, wakinga, Wabaya, Waha na kidogo Wasukuma pia wanatumia kanuni hiyo.

Kidini, Biblia inatuambia Mungu alipomuumba Mtu Kwa mfano wake, alimpeleka katika Bustani ya edeni(yaani alimuondoa sehemu yake ya Asili alipomuumbia) kwa Adamu hayo yalikuwa mafanikio.
Lakini alipoasi alimrudisha Sehemu yake ya Asili Kwa kumfukuza kwenye Bustani ya Edeni.

Abrahamu pia aliambiwa aondoke kwenye Ardhi ya Asili yake,
Genesis 12:1
The LORD had said to Abram, “Leave your native country, your relatives, and your father’s family, and go to the land that I will show you.
Kwa wale wapenzi wa kiswahili,
Mwanzo 12:1
BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

Tafsiri ya kingereza imekaa Fresh mwakemwake kuliko ya Kiswahili.
Yaani hapo Abrahamu anaambiwa aondoke na kuiacha nchi yake ya Asili, ndugu na jamaa zake na Baba yake yaani awaache. Mpaka nchi atakayoonyeshwa na Mungu.

Aya hiyo lazima kabla haujaifanyie uchambuzi au ufafanuzi wowote lazima nchi anayoambiwa aiache ni nchi ipi na ilikuwaje, ujue jamaa na ndugu zake Abrahamu anaoambiwa awaache ni kina Nani na walikuwaje, huyo Baba yake Abrahamu ni Nani na Kwa nini Abrahamu anaambiwa amuache.
Ukishajua hayo sasa uje kwenye uchambuzi na ufafanuzi kadiri utakavyobarikiwa.

Nchi ya Uhuru wa ukaldayo ilikuwa ya waabudu sanamu, Baba yake Abrahamu aliyeitwa Tera alikuwa fundi wa kuchonga miungu ya sanamu. Ambaye kwenye Uislam alitambulika kama "Azar"
Quran inamtambua Baba yake Abrahamu kwa jina la kazi yake na sio jina lake halisi ambalo ni Tera ndio maana ameitwa "Azar" ambapo Kwa lugha ya Kiswahili humaanisha mchonga vinyago au masanamu.

Vitabu vyote viwili Biblia na Quran vinamtambua Baba wa Abrahamu kama mchonga vinyago vya sanamu na muabudu sanamu.

Hiyo ndio sababu ya Ibrahimu kuambiwa aachane na Baba yake na ndugu zake na Nchi hiyo ya waabudu miungu na masanamu.

Kisha aende katika nchi atakayoagizwa.

Kitu pekee cha Muhimu kuzingatia hapa ni sababu za kuondoka, kuacha au kuhama.
Unaweza ishi Eneo ambalo ni Asili yenu ambalo wazazi wako hawakukuwekea mifumo na eneo hilo unaweza ukahama kwani ni ngumu kufanya vizuri au kufanikiwa.

Lakini kama ni eneo ambalo wazazi wako walihamia na wakakuwekea mifumo yaani mifumo umeikuta basi unaweza endelea kupambana hapohapo na ukafanikiwa.

Eneo ambalo unatakiwa kuhamia linatakiwa Liwe na sifa zifuatazo;
1. Rasilimali za muhimu kama Ardhi yenye rutuba, maji ya kutosha, Hali na tabia ya nchi nzuri, sio Mkondo wa Maji kupita au kutuama(mafuriko), sio Mkondo wa upepo mkali.
Hizo ni Rasilimali muhimu.

2. Mila na desturi ikiwemo miungu na mambo ya kishirikina.
Lazima uishi sehemu ambayo Mila na desturi zake sio za kipuuzi au kishetani.
Na Kama itakuwa sehemu yenye tija na unaihitaji Sana lakini kuna watu wa Aina hiyo. Fanya njama au hila watu HAO wahame au waue. Au tengeneza mazingira ambayo mfumo hautawasapoti kuishi pamoja nao, wao ndio wahame.

Kama mtaishi pamoja basi hakikisha watoto wako unawajengea misingi ya kuwaona jamii hiyo sio watu Bali ni mfano wa watu. Hivyo ndivyo wafanyavyo Wazungu, waarabu, wahindi, na Wayahudi na jamii zote zenye hadhi ya juu.

Kwa Mazingira ya sasa, Kijana ukitaka kufanikiwa kanuni hiyo ni muhimu na nyeti ambayo hutaambiwa na yeyote zaidi ya akili yako ndio itakuwa inakushauri uondoke kwenye mji wenu uende miji ya mbali.
Ni rahisi wageni kuja kuwatawala kama ninyi ni jamii isiyosambaa.

Yaani kama kwenye jamii yako ninyi sio watu wa kusambaa kwenda kwenye jamii zingine ni rahisi jamii zingine kuja kuwatawala karibu Kwa kila kitu katika Ardhi yenu.

Mfano, ni ngumu Kwa muafrika kutoboa kwenye nchi za Wazungu au waarabu Kwa sababu jamii hizo zilitangulia kusambaa Afrika kabla Sisi hatujaanza kwenda kwao.

Au hata hapahapa Bongo ni ngumu Kwa mtu kutoka Dar au Morogoro kutoboa akifika Moshi au Arusha, au akifika Mwanza au Iringa Ila ni rahisi Kwa watu wa Moshi au Arusha au Mwanza au Iringa kutoboa wakiwa DAR au Morogoro.

Unajua ni kwanini? Wengi watajibu kuwa ni ubaguzi, nop! Jibu lake nitatoa siku nyingine na tayari nimeshaligusia.

Chakuzingatia zaidi, unapoondoka na kuacha asili au kwenu basi kuwa Makini na huko uendako, lazima uchague mahali pazuri na sahihi pakwenda.

3. Kuondoka kimahusiano.
Ili ufanikiwe katika mahusiano yoyote Yale lazima uwe mahiri katika kuondoka na kuacha.
Biblia inasema;
Mwanzo 2:24
Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.

Uwezo wa kuacha na kuondoka ndio utaamua mahusiano ya wanandoa kuwa mazuri na thabiti au laa.
Ili ufanikiwe kwenye ndoa au mapenzi lazima uwe na uwezo wa kuacha baadhi ya mambo na vijitabia ambavyo havina Afya katika mahusiano yenu. Lazima ukubali kuacha watu wasio na tija katika mahusiano na mwenzi wako.

Kuacha wazazi sio Jambo Dogo, ingawaje ndio kafara juu ya ndoa. Hiyo ndio maana halisi ya Upendo. Kuacha wazazi wako kwaajili ya mwenza wako. Na hicho ndicho Adamu alifanya.

Aliamua kumuacha Mungu(mzazi na Baba yake) sababu ya Hawa Mkewe. Alikubali kubeba madhaifu ya mkewe na kukubali lawama za Mungu, ingawaje. Wengi wanamlaumu lakini Hakuwa na Option zaidi ya hiyo.

Kwenye upendo hakuna options mbili zaidi ya Moja tuu kujitoa kwaajili ya mtu umpendaye.
Uwe tayari kufa Kwa ajili ya mwenza wako. Ndio maana Mungu hakumlaumu Adamu hata hivyo haikumzuia kumpa adhabu Kwa kuasi kwake.

Umeoa alafu unaleta mambo ya Wazazi wako kwenye Familia yako, hiyo ni Dalili ya kushindwa.
Umeolewa unaleta mambo ya wazazi wako, huko ni kuteteresha ndoa. Na kutotambua maana ya familia.

Familia yako ni Ile ya wewe na Mumeo tuu, hata hao watoto wakikua wataondoka na kuanzisha familia zao na wengine kuolewa.

Yote hayo yanawezekana palipo na upendo WA kweli. Pasipo Upendo WA kweli hii itakuwa ni nadharia isiyowezekana kutekelezeka, lakini penye upendo hii ni nadharia halisi.

Watu wanashindwa kuacha Ma-Ex wao, wanaachana kimwili lakini kiroho bado wanapendana matokeo yake ni kupashana viporo.

Ndio maana inashauriwa Vijana waoe wanawake Bikra ili Kupunguza na wala sio kuondoa kabisa mambo ya Ma-ex.

4. Kuondoka Kiroho.
Huwezi kufanikiwa kiroho kama utashikilia kile tuu unachokiamini pasipo kuchunguza na kujifunza Imani zingine.

Imani sio kuwa na msimamo pekee yake pasipo kujifunza,
Imani ni kujifunza kila iitwapo leo habari za kiroho na ili kujua ukweli na uthabiti wa kike unachokiamini.
Kujifanya unamisimamo ya kijinga katika Imani ndio imepelekea mpaka hivi leo wapo wanaamini vitu visivyoeleweka ati kisa amekuta wazazi wanaamini katika Imani hiyo.

Kumbuka Ibrahimu mpaka anaitwa Baba WA mataifa au Baba wa Imani ni kutokana alizaliwa na kukulia Kwa jamii na wazazi wanaoabudu masanamu kama miungu yao, lakini Ibrahimu akajiongeza Kwa kuchunguza na kujifunza kuwa kile anachokiamini ni sahihi.

Lazima ufanye uhakiki wa kile unachokiamini. Jambo lolote ambalo utashikilia msimamo bila kufanya uhakiki litakutambulisha Kama mtu mjinga usiyejitambua.
Kufanya uhakiki sio dhambi, sio kosa. Bali ni kujithibitishia kuwa upo Njia sahihi.
Lazima ufanye utafiti, lazima ulinganishe ubora wa Imani utakazozikuta katika jamii yako.

Usipende kupelekwa pelekwa na wanadamu wenzako pasipo kutumia Akili yako vizuri kisa tuu labda hao binadamu wanamaneno matamu, au wanavaa au majoho, au kanzu, au sifa yoyote Ile.
Tumia akili, huwezi fanikiwa bila kutumia Akili yako vizuri.
Kisha uombe msaada Kwa Mungu aliyekuumba.

Lazima ujifunze kuacha na kuondoka katika tabia au mazoea ambayo yanakufanya usifanikiwe ili uweze kufanikiwa.

Nipumzike Sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Moshi,
 
Taikon embu ongea na mwanamke aliejeruhiwa sana kihisia kutokana na infidelity ndani ya ndoa...meaning mume kachepuja na kazaa nje ya ndoa..kaletewa mtoto na mume anamuacknowledge mama wa mtoto kama mke wa pili....kwamba she has to accept it...and the fact kuwa mke halali was a good woman isipokuwa na vijiudhaifu vinavyorekebishika. She feels lost...ana uchungu sana.

Ana fedha na maisha mazuri na she vmcan manage bila huyo mwanaume ila ndo saivi jambo liko hot...limetokea currently.

Wana watoto wanne actually...je aondoke kimazingira, kihisia na kiakili..atapona?? Au afanyaje???? Nitamsomea utakachoandika. Kumbuka tayari ana uchungu sana.
 
Taikon embu ongea na mwanamke aliejeruhiwa sana kihisia kutokana na infidelity ndani ya ndoa...meaning mume kachepuja na kazaa nje ya ndoa..kaletewa mtoto na mume anamuacknowledge mama wa mtoto kama mke wa pili....kwamba she has to accept it...and the fact kuwa mke halali was a good woman isipokuwa na vijiudhaifu vinavyorekebishika. She feels lost...ana uchungu sana.

Ana fedha na maisha mazuri na she vmcan manage bila huyo mwanaume ila ndo saivi jambo liko hot...limetokea currently.

Wana watoto wanne actually...je aondoke kimazingira, kihisia na kiakili..atapona?? Au afanyaje???? Nitamsomea utakachoandika. Kumbuka tayari ana uchungu sana.
duuh! Methali 6:32
jamaa atajiua kwa mikono yake mwenyewe "kiroho ameshakufa."
hakutakiwa kumleta mtoto mwngine kwenye ndoa yake/ktk nyumba ya mkewe.
huyo mama awe mpole atengeneze afya ya akili, kimwili na kiroho.
asizungumzie huu mgogoro kwa yeyote maana utazidi kumharibu kiakili/kiroho(akae kimya)
ampende mume wake kama hakijatokea kitu yaan ndyo awe km ametoka kwa kungwi jana(ASIONDOKE)
 
Taikon embu ongea na mwanamke aliejeruhiwa sana kihisia kutokana na infidelity ndani ya ndoa...meaning mume kachepuja na kazaa nje ya ndoa..kaletewa mtoto na mume anamuacknowledge mama wa mtoto kama mke wa pili....kwamba she has to accept it...and the fact kuwa mke halali was a good woman isipokuwa na vijiudhaifu vinavyorekebishika. She feels lost...ana uchungu sana.

Ana fedha na maisha mazuri na she vmcan manage bila huyo mwanaume ila ndo saivi jambo liko hot...limetokea currently.

Wana watoto wanne actually...je aondoke kimazingira, kihisia na kiakili..atapona?? Au afanyaje???? Nitamsomea utakachoandika. Kumbuka tayari ana uchungu sana.


1. Mke anayohaki ya kukubali au kukataa mtoto wa nje WA mumewe. Hilo suala lipo chini ya maamuzi ya Mke na sio maamuzi ya mume.
Kama mume analazimisha watoto wake aliowazaa nje ya ndoa(na hapa namaanisha akiwa ndani ya ndoa) tafsiri yake ameamua kuvunja ndoa kimakusudi.
Mwanaume huelwezi ukawa umeoa alafu ukafanya uhuni wako nje ya ndoa akapatikana mtoto alafu umlazimishe hiyo mtoto she aishi hapo nyumbani, huo ni uhuni na ubabe wa kipumbavu.
Kama Mwanaume atashindwa kumshawishi Mkewe basi mtoto huyo atakaa nje ya nyumba hiyo atalelewa na Mama yake.
Lakini kama Mke atakubali Kwa moyo mmoja alee mtoto.
Ila Kidini na kisheria Mwanamke ndiye anajukumu la kukubali au kukataa watoto ambao hajawazaa yeye, hilo wala sio kosa. Hiyo ni nature na ndio sheria ipo hivyo.
Halikadhalika na watoto wa nje WA mke/mwanamke ni hivyohivyo. Mume anaweza kukataa kuwalea na hapaswi kulazimishwa kuwalea labda Kwa ridhaa yake mwenyewe.

Ni vile tuu Dunia watu wanajitungia sheria kujipendelea au Kwa ubabe.

2. Mke wa pili, nature haitambui mke wa pili. Hivyo mwanamke yoyote anayohaki kukataa na kupinga Kwa nguvu zote. Bahati nzuri mambo huja automatically, yaani upende usipende lazima mwanamke usikie wivu na uchungu pale unapoongezewa mke mwingine.
Ingawaje zipo sababu ambazo mwanamke anaweza kuridhia aongezwe mke wa pili aweze kumsaidia majukumu, kama vile,
i. Ugonjwa,
Ugonjwa ambao unamfanya ashindwe kumhudumia Mume wake kwenye Faragha.

ii. Utasa.
Mwanamke anayoruhusa Kwa upendo Kuruhusu mumewe aweze kujipatia mtoto Kwa mwanamke mwingine ikiwa yeye ni Tasa.
Mwanamke kama anakupenda Kwa dhati Hilo lazima alifanye ili kukuibulia ukoo. Hivyo ndivyo alifanya Sarah Kwa Ibrahimu.
Lakini kuzaa na Mwanaume haimaanishi huyo ni mumeo. Hivyo mke atabaki kuwa Mke na huyo aliyezaa hatahesabika kuwa Mke isipokuwa Kwa amri ya Mke Mkubwa

iii. Watoto wakiume.
Ni kweli ni ndoto ya kila Mwanaume kuwa na mtoto wa kiume atakayeendeleza Ukoo wake. Mke WA ndoa anayoruhusa ya Kuruhusu mumewe alale na Mwanamke mwingine ili ajipatie mtoto wa kiume. Hiyo Inategemea na Mapenzi baina yao(mke na mume).
Zingatia Mwanamke hatoi ukoo au kizazi, isipokuwa mwanaume ndiye anatoa kizazi au ukoo.

Amuombe mumewe ampa sababu zenye mashiko ambazo zinamfanya amuongezee mke mwenza Kama hamna sababu ya maana ni wazi ameamua kumdhalilisha tuu.
Ni Bora amfanye huyo mwingine mchepuko lakini hata hiyo haifai kwani tayari mkewe ashajua.
Ni kweli wanaume hatuwezi kuwa na Mwanamke mmoja Ila haimaanishi hatuwezi kuwafanya wake zetu wajione wapo wenyewe tuu.
Inawezekana na mbona wengi wameweza.

3. Kuhusu kuondoka,
Kama mumewe hatatoa sababu za maana za kuongeza mke WA pili, ambazo nishazitaja hapo juu na pia hizo sababu nilizozitaja sio Kwa kuongeza mke Bali Msaidizi wa kumsaidia mke Mkubwa(mjakazi au kibarua)
Basi wahesabu kila mmoja haki yake inayomuangukia katika hiyo Ndoa.
Wagawane Mali wala asimchukie, wafanye Kwa haki, kuhusu Watoto jukumu la kutunza watoto nila Baba, Baba atoe matumizi Kama ilivyokuwa awali, sema atapunguza matumizi ya Mke(huyo Rafiki yako) Ila matumizi ya watoto yabaki kama yalivyo.

Mwanamke WA hadhi ya juu na mwenye thamani hawezi kukubali kuolewa Mke Mwenza au kukubali ndoa za mitala.

Asiliendee Jambo hili Kwa hisia Kali, atatue Kwa utulivu Mkubwa, huku akimuomba Mungu.

Ila awe na msimamo kuwa haitowezekana kamwe kukubali kuwa Mke wa Pili hata angepewa amri na Nani, na aseme yupo tayari Kwa matokeo ya uamuzi wake na hatojutia kukubali kushushwa hadhi na thamani, labda ingekuwa ni ridhaa yake.

Mwisho, Rafiki yako ni Dini gani?
Mumewe ni Dini gani?
Elimu zao ni muhimu pia,

Mbali na hivyo, je anafanya majukumu yake ya kindoa?
Je anapendeza na kujiweka kama Mwanamke mwenye thamani?

Msisitizo; asikubali mtu awaye yeyote achezee furaha yake, mwishowe aone maisha hayana maana kisa mpuuzi mmoja.
Shukrani,
 
duuh! Methali 6:32
jamaa atajiua kwa mikono yake mwenyewe "kiroho ameshakufa."
hakutakiwa kumleta mtoto mwngine kwenye ndoa yake/ktk nyumba ya mkewe.
huyo mama awe mpole atengeneze afya ya akili, kimwili na kiroho.
asizungumzie huu mgogoro kwa yeyote maana utazidi kumharibu kiakili/kiroho(akae kimya)
ampende mume wake kama hakijatokea kitu yaan ndyo awe km ametoka kwa kungwi jana(ASIONDOKE)
Ushauri mzuri lakini naomba kaa katika reality kidogo. Unamuona aliekuletea maumivu mbele yako afu anakwambia inabidi ukubali uke wenza. Na mbaya jamaa kashamtangaza mke mdogo publically na anajisifu am a man and am responsible so i wont deny my second family. Yani ni kama kamtemea.mate mke mkubwa usoni
 
Ushauri mzuri lakini naomba kaa katika reality kidogo. Unamuona aliekuletea maumivu mbele yako afu anakwambia inabidi ukubali uke wenza. Na mbaya jamaa kashamtangaza mke mdogo publically na anajisifu am a man and am responsible so i wont deny my second family. Yani ni kama kamtemea.mate mke mkubwa usoni

Ni Dini gani hao?
Madhehebu Yao?
Na elimu zao pia?

Tuanzie hapo,
 
Wakristo pure
Madhehebu sifahamu
Wana elimu nzuri tu..degree holders. Elimu inamatter??

Hapo hakuna ndoa itakayofungwa,
Muambie aendelee na mambo yake, ajiweke nadhifu, awe mrembo,
Apunguze bajeti yake ya nyumbani(yaani pesa anayoitumia kuchangia hapo nyumbani aiondoe) amuache Mumewe ndiye awe anatoa matumizi yote hapo nyumbani.
Maana kuna wanaume wakiwa na pesa zisizo na kazi wanakosa Akili.
Aongeze gharama za maisha hapo nyumbani ili kuibana kila senti ya Mumewe itumike hapo ndani.

Zakwake atumie kujiremba na kununua Mafuta mazuri ili apendeze,
Mumewe akisuasua ampeleke Ustawi WA jamii akatwe pesa za kutunza familia kadiri itakavyowezekana bahati nzuri ni mke WA Ndoa hivyo haitosumbua.
Na Kama wameajiriwa itasaidia kumdhibiti.

Elimu inachangia Kwa kiasi kikubwa,
Nasisitiza, amuwekee Sanctions za kutosha katika uchumi,
Kisha apunguze kumlisha vyakula vyenye kumuongezea nyege mshindo,
Huku akimuongezea mzigo wa gharama za maisha hii itamfanya aanze kuwa na Stress,

Mara nyingi Sisi wanaume tunachepuka tukiwa hatuna Stress za kiuchumi au tukiwa tunakosa utulivu nyumbani Kwa wake zetu.

Aanzishe programs za maombi usiku Kama kusoma Biblia kujadili Biblia na familia, hata mama mumewe hatakuwa na time asijali Sana wala asionyeshe makasiriko wala asimsemeshe Kwa ulimi mbaya.

Akishagundua mzigo ni mzito WA kutunza familia mbili lazima achague Mavi ya kale yasiyonuka, au Ganda la Jana la muwa Chungu kaona kivuno.

Hizo ni mbinu Kwa uchache
 
Hapo hakuna ndoa itakayofungwa,
Muambie aendelee na mambo yake, ajiweke nadhifu, awe mrembo,
Apunguze bajeti yake ya nyumbani(yaani pesa anayoitumia kuchangia hapo nyumbani aiondoe) amuache Mumewe ndiye awe anatoa matumizi yote hapo nyumbani.
Maana kuna wanaume wakiwa na pesa zisizo na kazi wanakosa Akili.
Aongeze gharama za maisha hapo nyumbani ili kuibana kila senti ya Mumewe itumike hapo ndani.

Zakwake atumie kujiremba na kununua Mafuta mazuri ili apendeze,
Mumewe akisuasua ampeleke Ustawi WA jamii akatwe pesa za kutunza familia kadiri itakavyowezekana bahati nzuri ni mke WA Ndoa hivyo haitosumbua.
Na Kama wameajiriwa itasaidia kumdhibiti.

Elimu inachangia Kwa kiasi kikubwa,
Nasisitiza, amuwekee Sanctions za kutosha katika uchumi,
Kisha apunguze kumlisha vyakula vyenye kumuongezea nyege mshindo,
Huku akimuongezea mzigo wa gharama za maisha hii itamfanya aanze kuwa na Stress,

Mara nyingi Sisi wanaume tunachepuka tukiwa hatuna Stress za kiuchumi au tukiwa tunakosa utulivu nyumbani Kwa wake zetu.

Aanzishe programs za maombi usiku Kama kusoma Biblia kujadili Biblia na familia, hata mama mumewe hatakuwa na time asijali Sana wala asionyeshe makasiriko wala asimsemeshe Kwa ulimi mbaya.

Akishagundua mzigo ni mzito WA kutunza familia mbili lazima achague Mavi ya kale yasiyonuka, au Ganda la Jana la muwa Chungu kaona kivuno.

Hizo ni mbinu Kwa uchache
Mademoiselle bila shaka umeipenda hii
😆😆
 
Iko vizuri....and thats what she decided sema tu kakataa uke wenza kamwambie mme aende kwa mke wake mwingine. Kakataa kuitwa mke wa kwanza. Kamwambia jamaa alikochagua ndo huko aende. Yeye anabaki na familia..watoto. atawalea atawatunza. Kasema imani yake hairuhusu ndoa ya watu wengi so she.let the man go. Niliwaambia she is financially stable. Sema tu saivi mke mdogo anamchokoa chokoa na vijipost mtandaoni insta huko ili tu ajibu. Yeye yuko busy na maisha yake she launched a foundation recently. Yuko so composed ila ndo ivo
 
Back
Top Bottom