Fredrick Lowassa afunguka mgogoro wa Ngorongoro, asema “Wamasai wana haki”

Fredrick Lowassa afunguka mgogoro wa Ngorongoro, asema “Wamasai wana haki”

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
1645091308848.png

Picha: Fredrick Lowassa

Mbunge wa Jimbo la Monduli, Fredrick Lowassa kupitia mtandao wake wa Instagram, ameandika kuwa jamii ya Wamasai kutoka Ngorongoro ni Watanzania na wana haki sawa Kama Watanzania wengine.

“Wamasai wa Ngorongoro ni Watanzania na wana HAKI sawa kama Watanzania wengine. Tofauti kubwa ni kabila letu kulinda utamaduni wetu ambao pia umekuwa kivutio kikubwa cha utalii ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro.

“Naamini Watanzania wote tunafahamu heshima hii ya Ngorongoro Crater kama moja ya maajabu ya dunia na mtaji mkubwa sana kiuchumi kwa Nchi yetu.

“Nadhani ni muda sahihi sasa kwa Serikali KUIWEZESHA Mamlaka ya Hifadhi ya NgoroNgoro ili kulinda hifadhi yetu na kurejesha mahusiano mazuri ya wanyama na binadamu kama ambavyo imekuwa tangu kuanzishwa kwa hifadhi hii mwaka 1959.

“Hoja ya wingi wa mifugo na zozote zingine zinajadilika kukiwa na mahusiano mazuri na wananchi. Tunaiamini Serikali ya Mama Samia Saluhu Hassan ni sikivu,” ✍🏽 - Fred Lowassa.
 
Wanyama waliachiwa Serengeti ,. Wamasai wapewe kipaumbele ngorongoro
Kwa hiyo wanyama wa Ngorongoro wauwawe au wahamishiwe Serengeti ? Na wakifa/kuhamishwa, unafikiri Ngorongoro itaendelea kuwa kivutio cha watalii?
 
Waamue idadi ya watu wanaoweza kuishi humo wapewe passi za kuishi humo. Na pia kiweke kiwango cha wanyama kila boma wanaweza kufuga.

Watakaokosa pasi ya kuishi ngorongoro itabidi wahame na mifugo yao na kupelekwa sehemu nyingine yoyote inayofaa ya nchi wakaendelee na maisha yao ya kifugaji.

Mojawapo ya njia ya mchujo ili kuondoa upendeleo au kutoelewana ni kutumika bahati nasibu 'lottery'. Bila hivyo siasa itafanya kushindwa kufanyika uamuzi wowote.
 
Hpn wasijenge nyumba za kudumu inaondoa uhalisia asili ya eneo husika ifanyike namna Ila siyo kutokomeza wamasai wote pale itakuwa tumearibu zaid
 
Ishu ya Ngorongoro imekaa kimaslai zaidi walioanzisha hiyo hifadhi walikuwa na uelewa na Akili nyingi kuliko wachumia tumbo wetu hawa, kama ni idadi ya watu uwekwe utaratibu, mifugo, mazingira na kila kitu Kitungiwe sheria.

Kwa mfano uwekwe utaratibu wa mifugo, idadi ya watu na uifadhi wa mazingira yote yanawezekana, na kwa ufupi kuna watalii wanakuja kushangaa hao masai, kwa hiyo kila kitu kinawezekana, ngorongoro ni siasa na maslahi.
 
hii issue ya wamasaai na Ngorongoro yao haiitaji mihemko wala siasa, au mahaba ya aina yoyote. technical personnel wakae waje na suluhisho la hii kitu kama kama walivyo fanya wakoloni mwaka1958!
 
Kuna aliyesema hawana Haki kama Mtanzania yoyote ?

Hivyo basi tatizo sio Wamasai tatizo ni numbers..., hata mimi au wewe mfano hapa tulipo tukiwa wengi sana hadi kuanza kuleta mmomonyoko wa udongo tutahamishwa..., au kwa busara kabla ya kuhamishwa wengine tutajipunguza na kwenda kwingine
 
Huyu mshenzi asiye hata na haiba ya ubunge alibahatika kuwa mbunge kwa uchaguzi uliochafuliwa na shetani jiwe bora akaye kimya tu.

Asilete ukabila, azingatie maslahi ya taifa.

Ndiyo amezeeka kuliko umri wake
 
Wanyama waliachiwa Serengeti ,. Wamasai wapewe kipaumbele ngorongoro
yaani tuuwe ngorongoro kwasababu ya masai? seriouly? mwambieni lowasa hao wamejengewa majengo kule tanga na shule, havitabomolewa hadi wakakae na kusoma huko.
 
Back
Top Bottom