Freeman Mbowe kapaki basi, kaamua kuwa mlinzi zaidi ya mshambuliaji

Freeman Mbowe kapaki basi, kaamua kuwa mlinzi zaidi ya mshambuliaji

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Baada ya kuondolewa zuio haramu la mikutano ya kisiasa, alichokifanya Mbowe katika ufunguzi kwa kumsifia Rais Samia badala ya kujikita katika hoja za kushambulia ni mkakati wa kisiasa wa aina yake.

Ukitizama vizuri baada ya mkutano wa kwanza wa CHADEMA Mwanza, MATAGA ndilo kundi linaloonekana kuchukizwa zaidi kuliko watu wengine katika hizi hatua za awali.

Nawaelewa mataga, kwamba walitaka Mbowe na CHADEMA wafanye kazi ya mashambulizi ya jukwaani kwa Samia na CCM asilia, Mbowe kajiepusha na hilo na sasa wamefura.

Sababu kubwa ya kufura kwa MATAGA ni kwa kuwa wao MATAGA hawana jukwaa la wazi la kuelekeza mashambulizi kwa CCM asilia na hasa Rais Samia. Jukwaa walilo nalo ni mitandao ya kijamii tu wakiwa katika ID za kujificha na hivyo kubaki kuwa "keyboard warriors". Walitegemea kazi hiyo kufanywa na Mbowe zaidi hivyo amewaangusha sana.

Mbowe inawezekana kang'amua shauku ya MATAGA, wote wasiopenda maridhiano na wanafuika wa siasa za uhasana na hivyo kawaacha CCM wacheze wenyewe katika nusu yao ya kiwanja huku yeye "akipaki bus" kwa matumaini watafanya makosa wenyewe wajifunge au CDM watafanya shambulizi la kushitukiza na kuwafunga.
 
Baada ya kuondolewa zuio haramu la mikutano ya kisiasa, alichokifanya Mbowe katika ufunguzi kwa kumsifia Rais Samia badala ya kujikita katika hoja za kushambulia ni mkakati wa kisiasa wa aina yake.
Asante kwa uzi huu, huu ni mwanzo wa politics of reconciliation badala ya politics of confrontations. Mtu ukabiliwe na kesi mbaya, mahakama isikilize preliminary hearing, ukutwe na prima facie, ila mara DPP aifute kwa Nolle!. Unatoka gerezani a free man unakwenda Ikulu kushukuru!. Huko Ikulu unaulizwa unashida gani?

Unalia shida, fedha za uendeshaji, fedha za vikao, fedha za trips za mamtoni na mambo mengine madogo madogo, unapewa!. Vikao vinafanyika, unapiga trips, usikute hata gharama za kuanza upya mikutano ya hadhara umelipiwa!. Kwanini usipaki gari?
P
 
Busara inatuma watu makini kufikiri kila jambo kwa kina na upana zaidi unaostahili. Kuna msemo unasema ukitaka kumua kobe, ni lazima mfanyie "timing" pale anapotoa kichwa chake, hali kadhalika ukitaka kumchinja kuku wa kienyeji kama CCM, siyo sawa na kutaka kumchinja kuku wa kisasa kama ACT Wazalendo, kuku wa kienyeji inakupasa umbembeleze kwa punje kadhaa, naye atakufuata tu mpaka kwenye eneo lililo sahihi la kumkamata na hatimaye kufanikiwa kumchinja.

Hatuwezi kumkebehi na kumhukumu Mh. Mbowe kwa kauli yake yenye nia ya kuponya majeraha na madonda ya kisiasa ambayo CDM imeyapitia. Huwezi kupata matokeo makubwa kwa mikakati ya muda mfupi, bali hupatikana kwa ile mikakati ya muda wa kati na mrefu.

Ni lazima tuwe wavumilivu wakati mbinu za mchezo zikiwa zimebalika kuendana na mazingira. Kabla ya kuanza kumshutumu kocha ni vyema tujielekeze katika mbinu bora za kumfanya kutafuta ushindi wa timu zinavyotumika.
 
Kawa pakia bus CCM manguli wa kila aina ya mtindo wa siasa hapa nchini ili awa funge kwa kushitukiza😀.

Kichekesho bora cha kisiasa kwa mwaka 2023😆.
 
Asante kwa uzi huu, huu ni mwanzo wa politics of reconciliation badala ya politics of confrontations. Mtu ukabiliwe na kesi mbaya, mahakama isikilize preliminary hearing, ukutwe na prima facie, ila mara DPP aifute kwa Nolle!. Unatoka gerezani a free man unakwenda Ikulu kushukuru!. Huko Ikulu unaulizwa unashida gani?, unalia shida, fedha za uendeshaji, fedha za vikao, fedha za trips za mamtoni na mambo mengine madogo madogo, unapewa!. Vikao vinafanyika, unapiga trips, usikute hata gharama za kuanza upya mikutano ya hadhara umelipiwa!. Kwanini usipaki gari?.
P
Haya ni mawazo yako binafsi, yaheshimiwe, japo yamejaa hisia zaidi ya uhalisia..!!

Mbowe kumsifia Samia kutaonekana jambo la ajabu kwa walio waoga, wale wachanga wa siasa, wanaodhani umaarufu wa Chadema uliojengwa kwa miaka mingi, unaweza kufutwa kwa tukio moja la Mbowe kumsifia Samia..

Hapa naomba pia niruhusu nikuite mnafiki, kwasababu pale juu umeandika siasa za confrontation hazina maana, pengine kwenye uzi mwingine ukaandika; "Samia akifanya jema asifiwe", sasa hapa iweje kwako Mbowe kumsifia Samia ionekane ni asante ya kutolewa gerezani, na sababu nyingine nyingi ulizoandika zisizo na maana kama michango kwa chama?
 
Yoda unaposema Mbowe kapaki basi una maana gani? kwako mbinu ya kushambulia kwenye siasa ni ipi?
 
Haya ni mawazo yako binafsi, yaheshimiwe, japo yamejaa hisia zaidi ya uhalisia..!!

Mbowe kumsifia Samia kutaonekana jambo la ajabu kwa walio waoga, wale wachanga wa siasa, wanaodhani umaarufu wa Chadema uliojengwa kwa miaka mingi, unaweza kufutwa kwa tukio moja la Mbowe kumsifia Samia..

Hapa naomba pia niruhusu nikuite mnafiki, kwasababu pale juu umeandika siasa za confrontation hazina maana, pengine kwenye uzi mwingine ukaandika; "Samia akifanya jema asifiwe", sasa hapa iweje kwako Mbowe kumsifia Samia ionekane ni asante ya kutolewa gerezani, na sababu nyingine nyingi ulizoandika zisizo na maana kama michango kwa chama?
Kama ulivyo heshimu mawazo yangu, nami naomba niheshimu mawazo yako.
P
 
Ukiitwa pale ikulu na ukapewa kahawa hata ungekua mtu wa misimamo kiasi gani utalegea tu. Mwenyekiti alipita kipindi kigumu sana, alikaribia kufirisika mnadhani angefanyaje?

Tukumbuke mwenyekiti ana familia ya kuilisha na sio watu wa kuwafurahisha, maisha ndio haya haya fainali uzeeni.
 
Huko Ikulu unaulizwa unashida gani?, unalia shida, fedha za uendeshaji, fedha za vikao, fedha za trips za mamtoni na mambo mengine madogo madogo, unapewa!.
Huu ni uwongo kiwango cha sgr. Ndiyo maana siku zote nasema huyu mwandishi/mwasheria uchwara ni mnafiki wa kutupwa.
 
Ukiitwa pale ikulu na ukapewa kahawa hata ungekua mtu wa misimamo kiasi gani utalegea tu. Mwenyekiti alipita kipindi kigumu sana, alikaribia kufirisika mnadhani angefanyaje?

Tukumbuke mwenyekiti ana familia ya kuilisha na sio watu wa kuwafurahisha, maisha ndio haya haya fainali uzeeni.
Ule msemo kuwa hakuna mkate mgumu mbele ya chai, ni kweli!. Mkate hata uwe mgumu vipi, mbele ya chai, unalainika!.
P
 
The biggest looser ni common Mwananchi.

Hizi mechi / maigizo yanayochukua miaka mitano kila mwaka na kuwa na hitimisho lile lile ni muendelezo wa the Mass kupata Opium yao.

Anyway if it makes / give people Hope from their miserable lives, so be it.
 
Back
Top Bottom