dawa yenu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 2,825
- 3,675
Unaweza ukahisi utani ila hii kitu nishafanya sana. Nikatega alarm kama dakika tano mbele nilijua ndani ya muda huo lazima nitakuwa nimefika usawa wa yule binti, naam nilipofika tu hata sekunde thelathin hazikupita kudadeki kitu griiiiii.... griiiii... hapo kilikuwa kinaning'inia shingoni, nikakivua nikakata alarm halafu nikapeleka sikioni...Enzi za vimobitel. Unategesha alarm ukiwa kwenye kadamnasi ya watu halafu unapokea haloo kwa sauti kubwa.
"Hallow... eeh nimetoka kidogo... narudi sasa hivi... haya nakuja" halafu nikafanya kama nakata kisha nikairudisha Simens mayai shingoni. Nikamcheki binti nikiwa serious sana..
"Mambo..."
"Poaaaa" huku anatabasamu... hahahaha alikuwa anaitwa Prisca Mbilinyi