Pre GE2025 Freeman Mbowe: Sina tabia ya kumshambulia kiongozi mwenzangu hata napokuwa siridhiki, Katiba kumbana Lissu

Pre GE2025 Freeman Mbowe: Sina tabia ya kumshambulia kiongozi mwenzangu hata napokuwa siridhiki, Katiba kumbana Lissu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Akijibu swali la Salim Kikeke Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe amekiri kuwa mara kadhaa amekuwa akikaa na Makamu wake, Tundu Lissu na kujadili mambo yanayohusu Chama na baadae anakuja kuzisikia taarifa hizo zimetoka nje.



Soma, Pia: Freeman Mbowe: Shutma za Lissu dhidi yangu ni za uongo
 
Lissu Mwanaharakati..., Mbowe Mwanasiasa; Tatizo siamini wanasiasa na sio kila wakati ni wakati wa harakati...

Kama ningeweza kuchagua ningesema wapunguze nguvu za Mwenyekiti yaani mtu mmoja asiwe na nguvu za kufanya maamuzi yoyote makubwa
 
Hatutaki SIRI za kuficha wizi na ufisadi kisa eti umefanywa na kiongozi mwenzako hivyo mtajadiliana kwenye vikao sijui kamati kuu...upuuzi!
Lissu anatosha.
Ufisadi umeliwa hela za kwako?unajifanya una uchungu kwenye pesa husizozijua
 
Lissu Mwanaharakati..., Mbowe Mwanasiasa; Tatizo siamini wanasiasa na sio kila wakati ni wakati wa harakati...

Kama ningeweza kuchagua ningesema wapunguze nguvu za Mwenyekiti yaani mtu mmoja asiwe na nguvu za kufanya maamuzi yoyote makubwa

Ndivyo ilivyo maana kamati kuu ndiyo decision maker
 
Ndivyo ilivyo maana kamati kuu ndiyo decision maker
Sasa hizo lawama za Mbowe alifanya hiki au kile zinatoka wapi Kama decision maker sio yeye ? Na hio Kamati inakaa muda gani ? Yaani akatwe meno kabisa hata day to day decisions ziwe kwa mujibu wa Katiba abakie tu kuwa symbolically (Mwenyekiti Kibogoyo)
 
1. Nimemsikiliza mwamba kwa hizo dakika 20 za mahojiano yake. Sijaona hoja yoyote ya maana aliyotoa zaidi kutetea kutokuwa na umuhimu wa ukomo wa madaraka ya uongozi ndani ya CHADEMA...

2. Kingine ambacho ni very funny ni kuwa, katinga kwenye mahojiano na katiba ya chama. Lakini mpaka anamaliza mazungumzo yake ameishia kuonesha gamba la katiba hiyo tu badala ya kuitumia kujengea hoja....

3. Mimi nikafikiri kuwa angetoa mifano ya hoja za Tundu Lissu ambazo zinavunja/kiuka ibara au kipengere chochote cha katiba. Hakufanya hivyo na badala yake kaishia kumshambulia tu mpinzani wake na kumtishia na kauli ya "mwisho wa siku tutarudi na kuangalia katiba inasemaje!"

4. Kingine ktk mantiki ya majibu yake ktk interview hii cha kushangaza ni kuwa, ni kama kwamba Freeman Mbowe hajui kuwa wako kwenye kipindi cha uchaguzi wa kidemokrasia huku yeye akiwa mgombea pia. Na ni kama hatambui kuwa ana wapinzani wanaokitaka kiti chake cha uenyekiti wake aliokaa hapo miaka 21. Najiuliza tu, kuwa, kwanini anafikiri hawa wapinzani wake watafanya kampeni zao kwa kumsifia yeye badala ya kueleza udhaifu na mapungufu yake binafsi na ya uongozi wake wa miaka 21 ndani ya chama? Mbowe hajui hili kweli? Je, huku ndo kuvunja au kukiuka katiba ya chama kunakosemwa? Mimi simuelewi kabisa huyu mzee..!!

5. Kwa nilivyomtazama, kumuona na kumsikiliza Mwamba, haina shaka kuwa jamaa ana hofu kubwa sana na uchaguzi ndani ya chama chake anachokiongoza. Na kusema ukweli ana haki ya kuwa na hofu kwa sababu ni yeye mwenyewe kufanya fyongo kwa kushindwa kuzitambua ishara za nyakati na majira kuwa haziko upande wake. AMECHELEWA KUCHUKUA MAAMUZI SAHIHI, YA HEKIMA NA BUSARA ya kupumzika na kulea chama...!

6. Hivi Freeman Mbowe anadhani anaweza kumtoa Tundu Lissu katika mstari kirahisi tu kama alivowahi kufanya kwa Chacha Wangwe, Zito Kabwe na wenzake, Cecil Mwambe kila walipojaribu kuutaka uenyekiti?

7. Au anadhani anaweza kumfukuza Tundu Lissu chamani kirahisi tu kama alivyofanya kwa wengine? Kwa hoja na sababu zipi hasa? Aisee wafanye kazi ya ziada sana ambayo Mimi sioni hiyo ziada...!

I don't see that possibility at least for now.....
 
Lissu kwa maisha ya huku kitaa wahuni "tunawaita mdomo wazi"...
Maana yake mtu asie na siri wala kifua cha kuchagua kipi azungumze kipi aache.
Erythrocyte Muiteni Lisu mmkanye, to the worst side msimamishe uanachama for say 6 months, the mpate muda wa kutafakari naye!
 
Busara kwa sasa Mhe Mbowe amuschie Lissu kijiti, wala wadigikiri kama kuna mwingine pale wa kuendeleza mapambano
 
Akijibu swali la Salim Kikeke Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe amekiri kuwa mara kadhaa amekuwa akikaa na Makamu wake, Tundu Lissu na kujadili mambo yanayohusu Chama na baadae anakuja kuzisikia taarifa hizo zimetoka nje.
View attachment 3191703


Soma, Pia: Freeman Mbowe: Shutma za Lissu dhidi yangu ni za uongo
Sijawahi ona au sikia lissu akimshambulia moja kwa moja mbowe, mara nyingi.Viongozi wa chadema akiwemo mbowe wanaoingia kwenye mtego kwa maswali ya kijanja ya waandishi wa habari, lissu katoa hoja sio kumshambulia mtu.Ukimsikiliza vizuri mbowe, anajifanya kuishabikia demokrasia lakini sio mwanademokrasia.Nimemfuatilia kwa umakini
 
Ha
A very good observation.
1. Muiteni Lisu kwenye vikao vyenu.....displinary platform ya chama
2. To the worst side,unlikely one though, fukuza takataka
Hakuna kosa la kumuita lissu kwa chama now, lipi? Mbowe kaingia kwenye mtego wa like jana
 
Back
Top Bottom