Freeman Mbowe umeacha alama. Wewe si mnyonge bali ni Shujaa

Freeman Mbowe umeacha alama. Wewe si mnyonge bali ni Shujaa

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Leo umehitimishwa uongoze wa Freeman Mbowe, baada ya kukaa kwenye nafasi ya juu ya chama kwa takribani miaka 21.

Miaka 21 ndani ya uongozi wa chama cha siasa cha upinzani, si jambo rahisi. Hiyo ni miaka ya mara jela, mara mahakamani, mara kuharibiwa biashara, mara kufungiwa account, na mengine mengi magumu.

Kwa kazi kubwa aliyoifanya Mbowe, na baadhi ya wanaCHADEMA ambao wengine wamepoteza mpaka maisha yao, michango yao haiwezi kutwezwa wala kudhihakiwa, bali itakuwa msingi imara wa kuendeleza mapambano ya kuitafuta haki na demokrasia ya kweli kwa nchi yetu.

Uongozi mpya, uboreshe na ulete matumaini mapya, bila ya kuyapiga teke mazuri ya msingi yaliyofanywa na watangulizi hawa.

Mbowe anatoka kwenye nafasi ya uongozi wa chama akihitimisha kwa kutoa elimu ya bure ya demokrasia kwa CCM ambayo haijawahi kuwa na uchaguzi, zaidi ya maigizo ya uchaguzi ambayo huitikiwa na wajumbe wa mkutano mkuu, kwa kusema tu NDIYO, bila ya ushindani.

CCM imepelekwa darasani, kufundishwa maana ya uchaguzi. Je, wana akili ya kufundishika au ni mbumbumbu wa kudumu, tusubiri kuona watafanya nini juu ya maamuzi yao waliyoyafanya siku za karibuni DODOMA yanayokiuka hata kanuni zao wenyewe.

WanaCCM walioudhiwa na mambo yasiyo ya kidemokrasia ndani ya CCM yaliyofanyika pale Dodoma, nendeni CHADEMA mkaifaidi demokrasia ya kweli.

Hongera sana Lisu, Hongera sana Heche, mmebeba matumaini ya watanzania wengi wenye dhamira njema na Taifa hili.

CHADEMA MOJA, TAIFA MOJA, LENGO MOJA DHIDI YA WALIOPORA MAMLAKA YA UMMA.
 
Umeongea vizuri sana. Kipimo cha kwanza cha uongozi mpya ni watawafanyia nini wale ambao waliomuunga mkono Mbowe. Watalipa visasi? Watawabeza? Au watawapa heshima wanayostahili?
Kwa yale ambayo nimeyaona kutoka kwa wafuasi wa Lissu ni kuwa wanataka damu lazima imwagike.
Mimi naamini bado kuwa haya ndio matokeo ambayo CCM waliyataka. Watakuwa wamefurahi sana.

Amandla...
 
Leo umehitimishwa uongoze wa Freeman Mbowe, baada ya kukaa kwenye nafasi ya juu ya chama kwa takribani miaka 21.

Miaka 21 ndani ya uongozi wa chama cha siasa cha upinzani, si jambo rahisi. Hiyo ni miaka ya mara jela, mara mahakamani, mara kuharibiwa biashara, mara kufungiwa account, na mengine mengi magumu.

Kwa kazi kubwa aliyoifanya Mbowe, na baadhi ya wanaCHADEMA ambao wengine wamepoteza mpaka maisha yao, michango yao haiwezi kutwezwa wala kudhihakiwa, bali itakuwa msingi imara wa kuendeleza mapambano ya kuitafuta haki na demokrasia ya kweli kwa nchi yetu.

Uongozi mpya, uboreshe na ulete matumaini mapya, bila ya kuyapiga teke mazuri ya msingi yaliyofanywa na watangulizi hawa.

Mbowe anatoka kwenye nafasi ya uongozi wa chama akihitimisha kwa kutoa elimu ya bure ya demokrasia kwa CCM ambayo haijawahi kuwa na uchaguzi, zaidi ya maigizo ya uchaguzi ambayo huitikiwa na wajumbe wa mkutano mkuu, kwa kusema tu NDIYO, bila ya ushindani.

CCM imepelekwa darasani, kufundishwa maana ya uchaguzi. Je, wana akili ya kufundishika au ni mbumbumbu wa kudumu, tusubiri kuona watafanya nini juu ya maamuzi yao waliyoyafanya siku za karibuni DODOMA yanayokiuka hata kanuni zao wenyewe.

WanaCCM walioudhiwa na mambo yasiyo ya kidemokrasia ndani ya CCM yaliyofanyika pale Dodoma, nendeni CHADEMA mkaifaidi demokrasia ya kweli.

Hongera sana Lisu, Hongera sana Heche, mmebeba matumaini ya watanzania wengi wenye dhamira njema na Taifa hili.

CHADEMA MOJA, TAIFA MOJA, LENGO MOJA DHIDI YA WALIOPORA MAMLAKA YA UMMA.
Kumpongeza Mbowe ni ujinga mkubwa.

Angejiweka pembeni kwa heshima tungeamini haya unayoyasema ni adili.

Amepoteza kila kitu mpaka heshima yake
 
Leo umehitimishwa uongoze wa Freeman Mbowe, baada ya kukaa kwenye nafasi ya juu ya chama kwa takribani miaka 21.

Miaka 21 ndani ya uongozi wa chama cha siasa cha upinzani, si jambo rahisi. Hiyo ni miaka ya mara jela, mara mahakamani, mara kuharibiwa biashara, mara kufungiwa account, na mengine mengi magumu.

Kwa kazi kubwa aliyoifanya Mbowe, na baadhi ya wanaCHADEMA ambao wengine wamepoteza mpaka maisha yao, michango yao haiwezi kutwezwa wala kudhihakiwa, bali itakuwa msingi imara wa kuendeleza mapambano ya kuitafuta haki na demokrasia ya kweli kwa nchi yetu.

Uongozi mpya, uboreshe na ulete matumaini mapya, bila ya kuyapiga teke mazuri ya msingi yaliyofanywa na watangulizi hawa.

Mbowe anatoka kwenye nafasi ya uongozi wa chama akihitimisha kwa kutoa elimu ya bure ya demokrasia kwa CCM ambayo haijawahi kuwa na uchaguzi, zaidi ya maigizo ya uchaguzi ambayo huitikiwa na wajumbe wa mkutano mkuu, kwa kusema tu NDIYO, bila ya ushindani.

CCM imepelekwa darasani, kufundishwa maana ya uchaguzi. Je, wana akili ya kufundishika au ni mbumbumbu wa kudumu, tusubiri kuona watafanya nini juu ya maamuzi yao waliyoyafanya siku za karibuni DODOMA yanayokiuka hata kanuni zao wenyewe.

WanaCCM walioudhiwa na mambo yasiyo ya kidemokrasia ndani ya CCM yaliyofanyika pale Dodoma, nendeni CHADEMA mkaifaidi demokrasia ya kweli.

Hongera sana Lisu, Hongera sana Heche, mmebeba matumaini ya watanzania wengi wenye dhamira njema na Taifa hili.

CHADEMA MOJA, TAIFA MOJA, LENGO MOJA DHIDI YA WALIOPORA MAMLAKA YA UMMA.
This is maturity na siyo ushabiki wa 'Oya Oya'. Wangekuwa wale wengine zngeogozana nyuzi za matusi na kebehi.
Baada ya ushindi wa Lissu ukiona nyuzi za kumkebehi Mbowe, ujue huyo aliyeanzisha ni mpinzani wa CHADEMA au ni Mwana CCM,
 
WanaCCM walioudhiwa na mambo yasiyo ya kidemokrasia ndani ya CCM yaliyofanyika pale Dodoma, nendeni CHADEMA mkaifaidi demokrasia ya kweli.
Chanzo cha yote ni Mwasi Kitoko akamuingiza Chaka yule Mzee na Mzeenae kajaa likaundwa azimio la Dodoma, Nyerere angekuepo wote wangechapwa bakora
 
Umeongea vizuri sana. Kipimo cha kwanza cha uongozi mpya ni watawafanyia nini wale ambao waliomuunga mkono Mbowe. Watalipa visasi? Watawabeza? Au watawapa heshima wanayostahili?
Kwa yale ambayo nimeyaona kutoka kwa wafuasi wa Lissu ni kuwa wanataka damu lazima imwagike.
Mimi naamini bado kuwa haya ndio matokeo ambayo CCM waliyataka. Watakuwa wamefurahi sana.

Amandla...
Muhimu Uchaguzi umekwisha Lissu ilete CDM pamoja na ongoza kwa team spirit usilipe kisasi kabisa. Sana sana wote mnategemeana nenda na kanuni ya complementarity
 
Umeongea vizuri sana. Kipimo cha kwanza cha uongozi mpya ni watawafanyia nini wale ambao waliomuunga mkono Mbowe. Watalipa visasi? Watawabeza? Au watawapa heshima wanayostahili?
Kwa yale ambayo nimeyaona kutoka kwa wafuasi wa Lissu ni kuwa wanataka damu lazima imwagike.
Mimi naamini bado kuwa haya ndio matokeo ambayo CCM waliyataka. Watakuwa wamefurahi sana.

Amandla...
😂😂😂
 
Leo umehitimishwa uongoze wa Freeman Mbowe, baada ya kukaa kwenye nafasi ya juu ya chama kwa takribani miaka 21.

Miaka 21 ndani ya uongozi wa chama cha siasa cha upinzani, si jambo rahisi. Hiyo ni miaka ya mara jela, mara mahakamani, mara kuharibiwa biashara, mara kufungiwa account, na mengine mengi magumu.

Kwa kazi kubwa aliyoifanya Mbowe, na baadhi ya wanaCHADEMA ambao wengine wamepoteza mpaka maisha yao, michango yao haiwezi kutwezwa wala kudhihakiwa, bali itakuwa msingi imara wa kuendeleza mapambano ya kuitafuta haki na demokrasia ya kweli kwa nchi yetu.

Uongozi mpya, uboreshe na ulete matumaini mapya, bila ya kuyapiga teke mazuri ya msingi yaliyofanywa na watangulizi hawa.

Mbowe anatoka kwenye nafasi ya uongozi wa chama akihitimisha kwa kutoa elimu ya bure ya demokrasia kwa CCM ambayo haijawahi kuwa na uchaguzi, zaidi ya maigizo ya uchaguzi ambayo huitikiwa na wajumbe wa mkutano mkuu, kwa kusema tu NDIYO, bila ya ushindani.

CCM imepelekwa darasani, kufundishwa maana ya uchaguzi. Je, wana akili ya kufundishika au ni mbumbumbu wa kudumu, tusubiri kuona watafanya nini juu ya maamuzi yao waliyoyafanya siku za karibuni DODOMA yanayokiuka hata kanuni zao wenyewe.

WanaCCM walioudhiwa na mambo yasiyo ya kidemokrasia ndani ya CCM yaliyofanyika pale Dodoma, nendeni CHADEMA mkaifaidi demokrasia ya kweli.

Hongera sana Lisu, Hongera sana Heche, mmebeba matumaini ya watanzania wengi wenye dhamira njema na Taifa hili.

CHADEMA MOJA, TAIFA MOJA, LENGO MOJA DHIDI YA WALIOPORA MAMLAKA YA UMMA.
FREEMAN MBOWE NI PROFESSOR WA DEMOCRASIA NA MAGEUZI WA TZ. AHESHIMIWE.🖖🏽🖖🏽🖖🏽🖖🏽
 
Kumpongeza Mbowe ni ujinga mkubwa.

Angejiweka pembeni kwa heshima tungeamini haya unayoyasema ni adili.

Amepoteza kila kitu mpaka heshima yake
Si kweli. Alichokifanya ndio sahihi. Ndio maana wengine tulitoa maoni sanduku la kura ndio liamue n si vinginevyo. Kujitoa kwake na kumuachia Lisu ilikuwa ni pigo kubwa toka kwa washindani wao. Kungekuwa na maswali mengi kuhusu demokrasia inayonadiwa.
 
Hongera sana kwa Mh Lissu. Watanzania tulio wengi tunatambua jinsi alivyo mpenda haki, mkweli na mfatiliaji wa mambo. Hivyo tumefurahi sana yeye kushinda hiyo nafasi. Sasa kutakuwa na upinzani nchini.
 
Well said Kiongozi..Mh Mbowe anastahili taji..kila la kheri Lissu et al, ustaafu mwema Kamanda Mbowe
 
FAM mhuni tu, kashapiga hela za CCM kaja kushindwa uchaguzi jamaa (CCM) hawana cha kumfanya.

Tuachane na FAM, tukae sasa tuanze kuipiga mawe CCM na kumpambania TAL ikiwezekana 2025 CCM itoke na tuache siasa za busara NAA hekima dhidi ya CCM.
 
Nashangaa kuona watu wanaoimba demokrasia kila siku kuja na hoja ya MBOWA KAAIBIKA. Nonsense kabisa, Trump aligombea 2020 akapigwa chini, leo amerudi tena kama POTUS, unataka demikrasia na hutaki ushindani, utakuwa mwehu usiyejielewa kabisa. Mbowe alikuwa sahihi kugombea as katiba ilimpa ruhusa kufanya hivyo, wajumbe wamemkataa kwenye sanduku la kura, amekubali kidemokrasia kuwa ameshindwa. What's wrong with that?

Seems wajongolala wanaimba demokrasia ila bado wanataka mambo ya sisiem kuleta jina moja, kulipitisha na kuimba mapambio ya kumpongeza mwenyekiti.

Hongera FAM, hongera TAL na hongereni CDM, mmetufundisha nini maana ya demokrasia.
 
Back
Top Bottom