Freemasons ndani ya Makanisa

Freemasons ndani ya Makanisa

Digrii ya 18 inayoitwa ‘Knight of Rose Croix’ hushughulika na elimu ya aina za misalaba na jinsi ya kufanikisha kuziingiza ndani ya taasisi na madhehebu mbalimbali kwa imani ya Illuminati na freemason na kwa kweli freemason wa digrii hiyo wamefanikiwa kwa kiwango cha juu kabisa kuingiza aina nyingi za misalaba ndani ya makanisa na taasisi bila ya waumini kujua maana ya misalaba hiyo
View attachment 2105765
Alama ya msalaba ni alama ya kipagani tunaona kuwa kanisa la waadventista wasabato sasa wameingiza misalaba katika nembo ya kanisa. Hii inaonesha wazi kuwa Kanisa lipo katika Uvuguvugu na sio moto tena.
Kitu Golden Ratio kabisa
 
LUKA 4

5 Kisha shetani akamchukua hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha kwa mara moja milki zote za dunia.

6-7 Akamwambia, “Ukipiga magoti na kuniabudu, nitakupa uwezo juu ya milki zote hizi na fahari yake; maana ni zangu na ninaweza kumpa ye yote yule nimtakaye.”

8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia yeye peke yake.’

Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
So shetani amesha mchukua Elon Musk? Na kampa mauwezo yote si ndio? Ndio maana ana mapesa? Space X? Safari za mwezini? Mars? Tesla? Milki milki
 
 
Kwa bahati mbaya huyo Mungu wa dini zote ni Mmoja, na ndiye huyo huyo aliamua kuleta tofauti hizi za dini kwa madhumuni yake mwenyewe.

Muumba wa kweli Alishasahaulika zamani sana ,pale taifa lake la watu halali(black people) ktk dunia hii walipomuhasi na kukumbatia tamaduni za wapagani(white people).

Hicho kitabu chenu muitacho biblia mbona mnatumia ile ile waliyokuwa wakiiitumia wakatoric pia kama hayo madhehebu yalijiona yako sahihi basi yasingeishia tu kuhariri mifumo ya kanisa, bali walitakiwa kufumua mpaka maandiko ktk biblia ambayo baadhi hayakuwa halali maana yaliandikwa kwa kupotosha na uongo mwingi, hivyo basi ingehitajika wao Kama wanae Roho mtakatifu awaongoze walete maandiko yasiyo na makosa, pia kurudisha baazi ya vitabu vilivyofutwa kwa makusudi.

Shetan ndye anaeabudiwa na Dini zote na makanisa yote.
Hakuna nabii,mchungaji, askofu, mtume ama mwinjilisti wa kwel nyakati hizi, kwakuwa nyote mnafundisha uongo ule ule uliowekwa na mrumi.

Hivyo basi ili kumtambua mtumishi wa kweli nyakati hizi ni lazima akanushe uongo wa mafundisho ya dini zote, pia aoneshe madhaifu ya misahafu yote, pia kufunua mikanganyiko ya vitabu hivi vya dini bila kumuonea aibu mtu yeyote kuwa atachukia ama atakuwaje.

Shetan tangu afukuzwe ktk imaya ya viumbe wa roho(mbingu) aliamua kujimilikisha hii dunia, kwanzia kujipa cheo cha Umungu, pia kuchukuwa mamlaka ya urithi wa mtu mweusi kwa kuukabizi kwa taifa feki la hao watu weupe,ili aitawale dunia atakavyo.

Nowadays shetan ni huyo aitwae kwa majina tofaut tofaut ktk dini, mfano Allah, Jesus, Jehovah, elishadai,elohim, alpha and Omega, Mwenyezi Mungu, bwana, haya yote ni majina yake ktk uhusika tofaut kulingana na mazingira,tamaduni na jamii husika hapo ndipo chanzo cha dini zote.

Hakuna ukweli wowote ktk biblia&quran mnapoteza muda wenu buree kuviabudu viumbe visivyo halali.

mkoloni si mjinga kukupa biblia eti akusaidie ww kwenda mbingun kwa upendo gani kwako?, kwanza hizo mbingu zao hazipo na hazijawai kuwapo, bali kuna ulimwengu wa viumbe wa kiroho ambao ni tofaut na hayo mastor yenu ya uongo eti kuna malaika, sjui kuna wazee24 na Mungu akizungukwa huo ni uongo mkubwa.

Ulimwengu wa Roho ambao viumbe wa Muumba wanaishi unajumuishwa na viumbe halali ambao wao wana asili sawa na mtu wa kwanza kuumbwa, ambae ni mweusi, ktk dini zenu hawawez kuwaambia haya mambo, ila ukwel ni kwamba malaika,maserafi& makerubi mionekano yao wote ni mfano wa mtu mweusi aliyeumbwa kutoka ktk materials za udongo, pia spiritual DNA zao ni sawa na mtu mweusi ambaye ndie mtu Original tofaut na hizo rangi zingine za laana ambazo zlkuja dunian kwa bahat mbaya kwa malengo ya kumtawala mtu mweusi,kumtumikisha na kuiharibu asili ya dunia kama vile baba yao shetan(jesus/azazel,Allah,yehova) apendavyo kuiharibu dunia.

Kuna mengi ya kujifunza, next time nitawawekea referencesView attachment 2104578
Kwahio wewe hio reference unatoa wapi Mana hapa duniani umesema kila jina la anaeabudiwa ni shetani ilhali naww upo hapa hapa duniani inamana hata ww hayo uyasemayo ni shetani tu ndio kakutuma usituhangaishe.ww mwenyewe ndio wale wale
 
Kazi kweli kweli, Kanisa ni moja, Takatifu , la Mitume, nalo ni Katoliki tu. Hiyo bibilia unayoisoma na ku quote wamekuandalia wao na wanaijua kuliko wewe. Hao vichaa kina Hellen G white, Smith ambaye alikuwa ni freemason kabisa yani wamekuja juzi tu na wamebeba mabumunda kama wewe.
Roma Cathoric 😳😳😳
 
Ndugu mimi ni mu SDA, nalijua kanisa langu in and out, SDA toka wafariki waanzilishi kina E.G wHITE, freemason waliliingilia, na E.G.WHITE alioneshwa maono ,

je unajua FREEMASON hutumia viongoz wa juu kuingiza mafundisho kwenye makanisa? je unajua kina E.G.WHITE walipinga kanisa kuwa na kiongoz mmoja juu ,anayeunda mfumo wa pyramid, ambaye kwasasa ni raisi wa kanisa, au kwa roma ni papa, huu ni mfumo ambao ma freemason wameuingiza kwenye makanisa yote,

E.G.WHITE alipofariki , ndipo kanisa la SDA, likaunda huo mfumo wa pyramid ambao kunakuwa na kiongoz wa juu, anaitwa RAISI, kwa roma huitwa papa,

"Makanisa mengi ya kiprotestant yanafuata uovu wa Roma,wakiungana na wafalme wa dunia,makanisa ya nchi;kwa uhusiano wake na serikali za dunia na madhehebu mengine kwa kutafuta ukubali.Neno Babeli,machafuko laweza kufaa kutumika kwa makanisa haya,WOTE WANAKIRI KUTOA MAFUNDISHO KUTOKA KWENYE BIBLIA,BADO WAKIWA WAMEGAWANYIKA KARIBIA VIKUNDI VISIVYOHESABIKA,KWA UPANA WAKIWA NA KANUNI NA NADHARIA ZINAZOPINGANA

ALIPOKUFA TU E.G.WHITE SDA ikaanza kutumia Kijitabu kiitwacho KANUNI ZA KANISA, kupitia humo ndipo mafundisho kutoka ROMA hupitishwa, na huwa kinafanyiwa marekebisho kila baada ya miaka mitano na viongozi wa juu tu,

Haya waadventista wasabato,leo ndani ya kanisa kuna kitabu cha kanuni na tunakitumia,lakn wasabato wa awali hawakuwa na kanuni.1930 ndipo kanuni inayoyotumika sasa ilibuniwa,na inabadilika au kuletwa mpya baada ya miaka mitano.

Roho ya unabii inaonya kuwa ,kanisa kuwa na kanuni iliyoundwa na mwanadamu ni uasi,na Kanisa la SDA linatumia Kitabu cha Kanuni,manake limeasi? NAKUACHIA SWALI

Lakini cha ajabu zamani hiki kitabu kiliitwa "Kanuni za kanisa" baada ya baadhi ya watu wachache kukitilia mashaka kwa kutumia Roho ya unabii ,viongozi wakakibadilisha jina wakakiita"Mwongozo wa Kanisa" wakasahau msemo usemao "Nyani wapya msitu wa zamani"
Nini maana ya ROHO YA UNABII?
 
Ndugu mimi ni mu SDA, nalijua kanisa langu in and out, SDA toka wafariki waanzilishi kina E.G wHITE, freemason waliliingilia, na E.G.WHITE alioneshwa maono ,

je unajua FREEMASON hutumia viongoz wa juu kuingiza mafundisho kwenye makanisa? je unajua kina E.G.WHITE walipinga kanisa kuwa na kiongoz mmoja juu ,anayeunda mfumo wa pyramid, ambaye kwasasa ni raisi wa kanisa, au kwa roma ni papa, huu ni mfumo ambao ma freemason wameuingiza kwenye makanisa yote,

E.G.WHITE alipofariki , ndipo kanisa la SDA, likaunda huo mfumo wa pyramid ambao kunakuwa na kiongoz wa juu, anaitwa RAISI, kwa roma huitwa papa,

"Makanisa mengi ya kiprotestant yanafuata uovu wa Roma,wakiungana na wafalme wa dunia,makanisa ya nchi;kwa uhusiano wake na serikali za dunia na madhehebu mengine kwa kutafuta ukubali.Neno Babeli,machafuko laweza kufaa kutumika kwa makanisa haya,WOTE WANAKIRI KUTOA MAFUNDISHO KUTOKA KWENYE BIBLIA,BADO WAKIWA WAMEGAWANYIKA KARIBIA VIKUNDI VISIVYOHESABIKA,KWA UPANA WAKIWA NA KANUNI NA NADHARIA ZINAZOPINGANA

ALIPOKUFA TU E.G.WHITE SDA ikaanza kutumia Kijitabu kiitwacho KANUNI ZA KANISA, kupitia humo ndipo mafundisho kutoka ROMA hupitishwa, na huwa kinafanyiwa marekebisho kila baada ya miaka mitano na viongozi wa juu tu,

Haya waadventista wasabato,leo ndani ya kanisa kuna kitabu cha kanuni na tunakitumia,lakn wasabato wa awali hawakuwa na kanuni.1930 ndipo kanuni inayoyotumika sasa ilibuniwa,na inabadilika au kuletwa mpya baada ya miaka mitano.

Roho ya unabii inaonya kuwa ,kanisa kuwa na kanuni iliyoundwa na mwanadamu ni uasi,na Kanisa la SDA linatumia Kitabu cha Kanuni,manake limeasi? NAKUACHIA SWALI

Lakini cha ajabu zamani hiki kitabu kiliitwa "Kanuni za kanisa" baada ya baadhi ya watu wachache kukitilia mashaka kwa kutumia Roho ya unabii ,viongozi wakakibadilisha jina wakakiita"Mwongozo wa Kanisa" wakasahau msemo usemao "Nyani wapya msitu wa zamani"
Kwa mujibu wa uzi wako, Makanisa mengi yanafuata uovu. Je! Unaweza kuyataja machache yanafuata Kweli?
 
Unajua ukisoma Biblia hutakiwi kukurupuka unachukua tu mstari mmoja unakimbia nao na unakazana kupotosha watu. Ukisoma Biblia kwanza unatakiwa utafakari na ujiulize maswali, kwanza jiulize Je Paulo kila waraka alikuwa anataka watu wanaonena kwa lugha wasizidi watatu tu au ni kwa wakorintho peke yake, na kama ni kwa wakorintho peke yao kwanini basi aliamua kuwaambia hivyo.

Kwanza kabisa wakorintho walifanya sifa kunena kwa lugha, kwahiyo unakuta hata salamu zao ni kunena kwa lugha tu, hata mahubiri yao ni kunena kwa lugha kiasi kwamba akija mgeni asiyejua kuhusu Roho Mtakatifu hakuna atakachoambulia sanasana ataona hawa wamechanganyikiwa. Na ndipo Paulo akaamua kuwawekea hiyo sheria.

Jiulize tena, Je, Paulo ndiye aliyeahidi ujio wa Roho Mtakatifu, jibu ni hapana.

Yesu Kristo ndiye aliahidi ujio wa Roho Mtakatifu kama msaidizi wetu yeye atakapokuwa amepaa kurudi kwa Baba, Je, uliwahi kumsikia Yesu akiwaambia wanafunzi wake kwamba kati yenu nyie ni watatu tu ndio watakaompokea Roho Mtakatifu na ninyi wengine mtafsiri? Jibu ni Hapana. Ila aliwaagiza wasitoke Yerusalemu hata atakapokuja yule msaidizi ambaye ni Roho Mtakatifu.

Siku ya pentekoste walikuwa watu 120 kule Yerusalemu wakisubiri ujio wa Roho Mtakatifu na maandiko yanasema wote walijazwa Roho Mtakatifu wakaanza kunena kwa lugha mpya kwa kadri Roho alivyowajalia kunena. Ikumbukwe hawakunena watu watatu tu hapo. Soma Matendo Ya Mitume Sura yote ya pili inaelezea hicho kisa. Au soma sura yote ya kwanza na ya pili ili uielewe kiundani zaidi.

Nakaribisha swali kwako mtoa mada au kama una hoja karibu.
 
Wakati huo huo uzingatie kuwa wanafunzi wa Yesu wakati wananena kwa lugha mpya katika siku ya Pentekoste, wale ambao hawakuwa wanafunzi wa Yesu(Wayahudi wa ugenini) waliweza kuelewa kila mtu kwa lugha yake. Je mbona kunena kwa lugha kwa siku hizi si kama si kama siku ya Pentekoste?

TAFAKARI MASWALI YAFUATAYO:-

1)Kama lugha iliyonenwa siku ya pentekoste ndiyo ya sasa mbona tunaponena wenzetu hawatuelewi?
2)Kama lugha iliyonenwa siku ya pentekoste ndio lugha tunayonena leo mbona ni baadhi ya makanisa na ni baadhi ya Wakristo ndio wananena kwa lugha badala ya makanisa yote na wakristo wote kama walivyonena wote siku ya pentekoste?
3) Kama lugha ya pentekoste ndiyo ya nyakati za leo mbona hatuoni ndimi kama za moto?
4) Siku ya pentekoste hawakuwekewa mikono ila Roho aliwashukia tu na wakajawa na Roho na kuanza kunena kwa lugha mpya, baada ya kipindi cha pentekoste kupita waliofuatia kama KORNERIO, WASAMARIA, AKIDA WA ETHIOPIA nk wao waliwekewa mikono na mitume na walipoombewa tu lugha ikaanza ndani yao. Je nyakati za leo ndivyo tunavyoombea watu? Nyakati za leo badala ya kuwaombea wakristo ujazo wa Roho Mtakatifu tunawaombea ili wanene kwa lugha.
1. Na wewe huwa unaponena kwa lugha wengine wanakuelewa?

2. Ni Makanisa yapi yanayonena kwa lugha na yapi yasiyonena? Nini ushauri wako, yanayonena waache au yasiyonena nayo yaanze kunena?

3. Kuna utofauti gani kati ya kujazwa Roho Mtakatifu na kunena kwa lugha?
 
SIO KILA ANAYEJAZWA ROHO ANANENA KWA LUGHA


UNAELEWA HILO?

Matendo 7:55 NEN - Bible.com​



Lakini yeye Stefano, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alikaza macho mbinguni, akaona utukufu wa Mungu, na Yesu akiwa amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
Utajuaje kuwa mtu kajazwa Roho Mtakatifu?
 
UNADOKOA KAMSTARI EE, SIO KILA MWENYE ROHO MTAKATIFU LAZIMA ANENE KWA LUGHA, HIYO NI MOJA TU YA KARAMA , NDIO MAANA TUNASHANGAA NINYI WOTE MNASEMA MNANENA,

Roho Mtakatifu hugawa karama kwa kila mtu kama apendavyo yeye, lakini hawapatii watu wote karama moja, zinatofautiana.

TWENDE KWENYE MAANDIKO

Lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.” “Je! wote ni mitume? wote ni manabii? wote ni waalimu? wote wanatenda miujiza? wote wana karama za kuponya wagonjwa? wote wanena kwa lugha? wote wafasiri? Takeni sana karama zilizo kuu. Hata hivyo nawaonyesha njia iliyo bora.” “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.” 1 Kor. 12:11, 29-31; 13:1-3.
Mtaje alau mtu mmoja wa zama hizi unayeamini ana karama ya kunena kwa lugha.
 
UTANGULIZI

ISAYA 14
12 Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe uliyewaangusha mataifa!

13 Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini.
14 Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.
15 Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo


Hapo tunaona Shetani akiapa kwa MUNGU akisema"Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za kaskazini."

UKISOMA

Zaburi 48​

1 Bwana ndiye aliye mkuu, Na mwenye kusifiwa sana. Katika mji wa Mungu wetu, Katika mlima wake mtakatifu.

2 Kuinuka kwake ni mzuri sana, Ni furaha ya dunia yote. Mlima Sayuni pande za kaskazini, Mji wa Mfalme mkuu.

UTAONA PANDE ZA KASKAZI NDIPO LILIPOKUWEPO HEKALU PALE MLIMA SAYUNI NA NDIPO MAHALI PALIPOKUWA NA UWEPO WA MUNGU , HIVO SHETANI ALIAPA KUKAA NADNI YA MAKANISA KWA SIKU ZETU AMBAPO TUNAKUSANYIKA TUKIAMINI TUNAMUABUDU MUNGU

Tuanze mada yetu sasa, fatana nami....


Katika FREEMASON Degree ya 33 ( hii ndio hatua ya juu ya Fremason kwa ujumla Duniani, huitwa"Degree of the Craft", na mwanachama mwenye Degree 3, anaitwa Mastermasonry/Grand master, hawa ndio wapangaji wa mipango, hawa ndio wanao jua siri ya free masoni na hii degree unaipatia katika Blue Lodge.

Freemason, imegawanyika katika Vyama mbali mbali lakini vyote hujulikana kwa jina la freemason, na kila chama kina jiendesha kwa misingi yake, mfano York rite na scottish rite.

York rite, hii inapatikana marekani katika lodge za huko, na katika york rite , wao waliongeza degree 10, za ziada, lakini huwezi kupata hizi degree bila kuwa na degree tatu , ambazo ndio msingi wa freemason Duniani kwote..na katika York rite degree ya 10, na maanisha ya 13, ukijumlisha na zile degree tatu za msingi, hiyo ni hatua ya juu ambayo inaitwa the Order of the Temple, na mwanachama mwenye degree hizi anaitwa "Knight templar".

Katika Scottish rite, katika chama cha scotiland, kupitia Lodge zao, wao waliongeza Degree 30, na kuzifanya ziwe 33, na huwezi kupata hizi degree bila kuwa na degree 3, za msingi. katika hizi degre, degree ya 32, ndio degree ya juu kabisa ambayo mwana chama mwenye hatua hii anakuwa Master of the royal secreat, siri zote za freemason unapewa.

Japo katika scottish rite , kuna jumla ya degree 33, lakini freemason wana amini degree ya 33, haipo, kwasababu ni adimu sana , labda mtu mwenye IQ, kubwa kama 160, na kama wapo basi wana fahamika na freemasoni wenye degree za juu kabisa.

wapo watu wanao amini labda hii degree ya 33, hii ndio degree inayo muhusu Lucifer.. pia baadhi wana amini Albert pike, mwandishi wa kitabu cha "Morals and dogma" alikuwa na degree 33, lakini wapo ambao wana amini hakufikia hatua hiyo.

Freemason ni chama ambacho kina daiwa kuwa na mambo ya siri mengi, na hawa inasemekana wanachama wake wengi wenye degree za juu , wapo katika chama cha Illuminat.

Unaweza kuona aina za digrii hizo; kwa mfano digrii ya 18 inayoitwa ‘Knight of Rose Croix’ hushughulika na elimu ya aina za misalaba na jinsi ya kufanisha kuziingiza ndani ya taasisi na madhehebu mbalimbali kwa imani ya Illuminati na freemason na kwa kweli freemason wa digrii hiyo wamefanikiwa kwa kiwango cha juu kabisa kuingiza aina nyingizi za misalaba ndani ya makanisa na taasisi bila ya waumini kujua maana ya misalaba hiyo.

NAKUPA MFANO HAPA CHINI
View attachment 2104330

NI chama cha Prieure de Sion (Priory de Sion) kilichoanzishwa na familia ya 11 ya Illuminati inayoitwa Freeman Illuminati bloodlines ndicho kilichosababisha kuanzishwa kwa ‘Uprotestant’ au ‘Upinzani’ ndani ya dini. Wakainuka mashujaa wengi waliopinga mafundisho machafu yaliyoingizwa ndani ya imani ya kweli ili kutetea neno la Mungu litawale tofauti na mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu. Miongoni mwa mashujaa walioinuka kupingana na mafundisho ya chama cha Prieure de Sion alikuwa Martin Luther.

Kumbuka kwamba wapinzani ‘Protestants’hawa walikuwa wanapinga mafundisho wakiwa ndani ya mifumo ya dini zao. Hata hivyo hawakufanikiwa kuleta matokeo mazuri ya upinzani wao na hivyo wakaamua kutoka na kujitenga na dini wakiwa na baadhi ya mafundisho machafu waliyoyarithi kutoka kwenye mifumo potofu ya kidini. Wakiwa wamejitenga, sasa waliamua kufanya ‘matengenezo’ kwa lengo la kuondoa mafundisho machafu na kubaki na mafundisho safi kama ilivyoagizwa na Mungu. Hivyo jina lao wakaitwa‘Reformers’ au ‘Wanamatengenezo’ badala ya ‘Protestants’ au ‘wapinzani’.‘Waprotestants’ wa awali walijua maana ya kanisa na ndio maana hawakuona shida kujitenga na mifumo iliyokuwa inadhaniwa kuwa ndiyo kanisa.Lakini je, nani aliyeanzisha ‘Uprotestant’na ‘matengenezo’? Ellen White anasema: “Christ was a protestant...TheReformersdate back to Christ and the apostles. They came out and separated themselves from a religion of forms and ceremonies. Lutherand his followers did not invent the reformed religion. They simply accepted it as presented by Christ and the apostles." E.G. White, Review and Herald, vol. 2, 48, col. 2.

Hapo anamaanisha kwamba ‘Kristo (Yesu) alikuwa ni Mprotestant….wanamatengenezo waliiga kutoka kwa Kristo na mitume. Walijitenga na dini ya desturi na sherehe. Luther na wafuasi wake hawakuanzisha dini ya matengenezo. Waliikubali kama ilivyoonyeshwa na Kristo na mitume’ [rejea: R&H, Vol. 2, 48, col.2].

Ni kwa namna gani Kristo alijitenga? E. White anaendelea kusema: “Pharisees and Sadducees were alike silenced.Jesus summoned His disciples, and prepared to leave the temple, not as one defeated and forced from the presence of his adversaries, but as one whose work was accomplished. He retired a victor from the contest”. {DA 620.2}

‘Mafarisayo na masadukayo walinyamazishwa. Yesu aliwakusanya wanafunzi wake, na akawaandaa kuliacha hekalu, sio kama aliyeshindwa na kulazimishwa kuondoka kwa maadui zake, bali kama ambaye kazi yake ilikuwa imekamilika. Alikuwa ni mshindi katika mashindano”. {DA 620.2}

Biblia inasema kwamba Yesu alijitahidi kupingana na mafarisayo na masadukayo akiwa ndani ya mfumo wa dini ya kiyahudi na sasa alikuwa amefikia mwisho wa upinzani wake na akaamua kujitenga moja kwa moja na mfumo wa dini hiyo ili awafundishe vizuri wanafunzi wake ambao walikuwa tayari kukubali mafundisho safi.

E.G. White anasema:" Hitherto He had called the temple His Father's house; but now, as the Son of God should pass out from those walls, God's presence would be withdrawn forever from the temple built to His glory. Henceforth its ceremonies would be meaningless, its services a mockery. {DA 620.4}Hatimaye Yesu na wanafunzi wake walijitenga na hekalu lililokuwa mpendwa wao. Lakini kwa sababu viongozi wa hekalu walikataa kufuata mafundisho ya neno la Mungu peke yake, Mwana wa Mungu hakuona sababu ya kuendelea kubaki ndani ya hekalu ingawa “Alikuwa akiliita hekalu kuwa ni nyumba ya Baba yake; lakini sasa, kama Mwana wa Mungu ambavyo akipita kutoka katika kuta hizo, uwepo wa Mungu ungeondolewa milele usionekane ndani ya hekalu lililojengwa kwa utukufu Wake. Hivyo sherehe zilizofanyika ndani ya hekalu hazikuwa na maana, huduma zake zikawa dhihaka”. {DA 620.4}. Hivyo ndivyo alivyofanya Martin Luther na wafuasi wake.

Baada ya kifo cha Martin Luther, wafuasi wake waliendelea katika kufanya matengenezo. Hata hivyo kwa sababu freemasons hawakati tamaa, matengenezo yalikoma na kuanza kurudi nyuma taratibu ambapo leo hii wale wanaoitwa ‘Walutheri’ wameungana tena na mfumo ambao mwanzilishi wao, Martin Luther, aliuiita ‘mfumo mchafu’.

Wakati matengenezo yanaendelea, ulikuwa ni wakati wa kutimizwa kwa unabii wa siku 1260 sawa na miaka 1260 kama ilivyotabiriwa na nabii Yohana. Wakati huo kulianzishwa matengenezo mengi na kupelekea kuanzishwa kwa mifumo mingine ya makanisa. Baadhi ya makanisa yaliyoanzishwa yalikuwa haya:

Anglican: Lilianzishwa huko England na mfalme wa Uingereza ili kupinga kanisa la Roma. Kiongozi mkuu wa kanisa hilo ni Malkia wa Uingereza. Hata hivyo wachunguzi wa dini ya freemasons wanasema kwamba familia ya Malkia ni familia mojawapo kati ya familia 13 za waumini wa Freemasons.

Presbyterian: Mwanzilishi ni John Calvin mwaka 1509 – 1564 na John Knox 1505 – 1572. Kanisa hili lilijitenga na Roma likiwa na motto “Chunguza maandiko” maana liliona kwamba kanisa la Roma linakwenda kinyume na maandiko. Hata hivyo wafuasi wa John Calvin na John Knox wameshindwa kufikia malengo ya kuyachunguza maandiko na kufuata kile asemacho Mungu na badala yake wamekubali kurudi walikotoka!

MENNONITE: Lilizaliwa rasmi mwaka 1525 – 1530 na Conrad Grebel na wenzake akiwemo Zwingli Ulrich aliyetofautiana na Martin Luther juu ya somo la pasaka. Hawa walikataa ubatizo wa Roma wa kunyunyizia maji na jina jingine wanaitwa “Meno Knights” majina ambayo yanafanana na vikundi vya Freemason kama vile “The knights of Eulogia”(Skull and Bones), “The knights of Malta”. Ingawa lengo la Zwingli Ulrich lilikuwa zuri, baada ya kifo chake wafuasi wake walikubali kuingiliwa na freemasons na hivyo kushindwa kufikia lengo lililokusudiwa.

LUTHERAN: Mwanzilishi ni Martin Luther mwaka 1517. Alikuwa ni Mjerumani aliyesomea ukasisi wa kanisa la Roma na mwaka 1511 akapata Phd katika chuo kikuu cha Wattenberg. Alipingana na kanisa lake la Roma na kuandika sababu 95 zinazopinga mafundisho ya Roma ndipo akajitenga na Roma na hivyo wafuasi wake wakaendelea kutumia jina la Lutheran, yaani wafuasi wa Luther. Wafuasi wa Luther hawakuendelea mbele na sasa wamerudi kwenye makosa aliyokuwa akiyapinga Luther. Je, Lutheran wa leo wanafuata kweli nyayo za Martin Luther? Au wametekwa kwa matumizi ya njama ya “Following Gurus”yaani kufuata kila wasemacho viongozi? Tafakari!

Moravian: Mwanzilishi ni John Huss aliyezaliwa mwaka 1366 na kuchomwa moto na papa hadi kufa mwaka 1416 baada ya kulipinga kanisa la Roma. Wafuasi wake hadi leo wanaitwa kanisa la Moravian. Kwa bahati mbaya wafuasi wa John Huss hawakuendelea kufanya matengezo ili kusonga mbele zaidi ya Huss na kibaya zaidi ni kwamba wanarudi nyuma badala ya kusonga mbele. Leo Huss akifufuka atashangaa kuona jinsi wafuasi wake walivyoacha kanuni alizozianzisha. Je, wamoravian wa leo wako tayari kuchomwa moto kwa kutetea ukweli kama John Huss? Tafakari!

Baptist: Ni kanisa lililoanzishwa na wafuasi wa Martin Luther ambao walijitenga na Lutheran mwaka 1600 huko Uholanzi na Uingereza baada ya kuona kwamba wafuasi wenzao wameacha kanuni alizoziweka Martin Luther. Hata hivyo kanisa la Baptist la leo haliendeleza jitihada za Luther na sasa badala ya kusonga mbele linapiga ‘marktime’ likiwa limegeuka nyuma.

Salvation Army (Jeshi la Wokovu): Mwanzilishi ni Booth mwaka 1878. Kanisa hili lilianzishwa na wafuasi wa freemasons kwa lengo la kuchafua matengenezo ya kweli. Kumbuka kwamba Shetani hutumia fursa inayotolewa na Mungu akiwa na lengo la kuwafanya watu washindwe kujua kipi ni cha kweli na kipi sio. Katika kila matengenezo ya kweli, pamekuwepo na matengenezo bandia.

Marmon church: Mwanzilishi ni Joseph Smith (1805 – 1844). Kanisa hili linajulikana pia kama The church of Jesus Christ of later day saints. Kanisa la Mormon lilianzishwa na wafuasi wa freemason wakiwa na lengo la kuchafua matengenezo ya kweli. Mitt Romney ni muumini wa kanisa la Mormon.

Methodist: Kiongozi Mwanzilishi ni John Wesley. Lilianzishwa na watu 17 wa familia moja mwaka 1738 likiwa na lengo la kupinga mafundisho ya freemasons. Kanisa hilo halijakamilisha lengo la matengenezo kutokana na ukweli kwamba wafuasi wake hawana mwamko aliokuwa nao John Wesley.

Watch Tower/Mashahidi wa YEHOVA : Mwanzilishi ni Charles T. Russel 1852 – 1916 na mwenzake J. Lutheford 1869 – 1942. Baba yake Charles T. Russel alikuwa ni mchungaji wa Prebyterian. Mnamo mwaka 1932 huko Marekani jina la kanisa hilo lilibadilishwa na kuitwa Mashahidi wa Yehova. Markus Mpangala ameelezea kwa kirefu chanzo cha dhehebu hili akiainisha kwamba waanzilishi walikuwa ni Freemasons kutoka kwenye familia ya Illuminati inayoitwa Russel illuminati bloodline ambayo nimeshaielezea kwenye makala zilizopita.

Brethen Assemblies: Mwanzilishi ni ndg. Dabi 1800 – 1882 ambaye alikuwa ni muumini wa Anglican na akajitenga na kanisa hilo na kuanzisha kanisa lake. Dabi aliamua kujitenga na Anglican kutokana na kanisa hilo kutawaliwa na familia ya freemasons.

Makanisa ya Kipentekoste au kilokole: Ni makanisa yaliyoanzishwa miaka ya hivi karibuni. Makanisa haya yalianzishwa huko Kansas City Marekani mwaka 1901kwa lengo la kupata nguvu ya kile kinachoaminiwa kuwa roho mtakatifu. Je, unajua uhusiano uliopo kati ya muziki wa‘rap’ au ‘kufoka’ na uvuvio wa kunena kwa lugha kutoka kwa kile kinachoaminiwa kuwa ni nguvu za roho mtakatifu wakati waumini wa kilokole wanapokuwa wakiomba? Kumbuka kwamba Muziki wa rap ulianzia huko Kansas City Marekani, mahali ambako makanisa ya kipentekoste yalianzishwa. Panapo majaaliwa, nitakuwa na makala ndefu kuhusu asili, lengo na nguvu inayoonekana kwa viongozi wa makanisa ya kilokole kama kina mwamposa. Kwa wakati huu nasema,‘Soma Biblia na Tafakari’!

Gospel terbenacle: Mwanzilishi ni Pastor A.B. Simpson mwaka 1881 akitokea Presybiterian.

Christian Churches: Mwanzilishi ni Thomas Chapel mwaka 1807 akitokea Presybiterian.


Seventh –Day Advetist Church: Mwaka 1844 baada ya kutokurejea kwa Yesu duniani kama ilivyohubiriwa na muhubiri mashuhuri aitwaye William Miller, watu wengi walivunjika moyo isipokuwa watu 50 tu ndio walioendelea kujifunza Biblia miongoni mwao akiwa ni Ellen G. White. Watu hao waliendelea kuchunguza makosa yaliyofanywa na William Miller maana wao pia waliamini juu ya marejeo ya Yesu tarehe 22/10/1844. Hatimaye mwaka 1863 kanisa hilo likapewa jina la Seventh –Day Adventists Church huku likiwa na motto au kauli mbiu ya “Amri za Mungu na imani ya Yesu na Ujumbe wa malaika watatu” na baadaye kanisa hilo likawa chini ya rais wa General Conference ya SDA makao makuu yake yakiwa huko Marekani. Rais huyo ndiye kiongozi (kichwa) mkuu wa kanisa hilo duniani na huchaguliwa kila baada ya miaka mitano. Wakati viongozi wa kanisa walipokutana ili kujadili mambo ya kanisa, palikuwa na ‘Mwenyekiti’(Chairman of General Conference) ambaye aliongoza kikao hadi mwisho. Baada ya kikao kumalizika, mwenyekiti huyo alimaliza muda na kazi yake.

Hata hivyo kulitokea mabadiliko kutoka mwenyekiti wa baraza kuu hadi na rais wa kanisa ulimwenguni. Kila baada ya miaka mitano hufanyika uchaguzi wa kumpata rais wa kanisa hilo. Tofauti na makanisa mengine, kanisa hili linaabudu siku ya Jumamosi wakati makanisa mengine yanaabudu siku ya jumapili. Sasa hivi kuna makanisa mengi ya SDA ambayo yametoka ndani ya kanisa la ‘General conference of Seventh-Day Adventists’(GCSDA) kwa madai kwamba kanisa hilo limeingiliwa na freemasons.

Wengi wa waumini wa SDA waliojitenga na GCSDA wanasema kwamba walikuwa wakipinga‘protest’ mafundisho machafu huku wakiendelea kuwa ndani ya GCSDA lakini hawakuweza kuleta mabadiliko yoyote maana hali ilikuwa inazidi kuwa mbaya. Hatimaye waumini hao waliamua kufuata nyayo za akina Luther za kujitenga na sasa wanafanya ‘reformation’ au ‘matengenezo’ hatua kwa hatua maana walitoka na mafundisho machafu ambayo waliyapokea kama kweli wakiwa ndani ya GCSDA.Waumini hao wanadai kwamba walijitenga na GCSDA kwa sababu,

tukio kubwa ikiwa ni freemason kuingiza nembo yao,huku wakiiondoa ile nembo ya UJUMBE WA MALAIKA WATATU,Freemeson huingiza mafundisho, au alama zao kupitia viongozi wa juu wa kanisa kama ilivyo kawaida ya makanisa yote uyajuayo.

NEMBO YA AWALI YA SDA
View attachment 2104350
NEMBO YA SASA YA SDA
View attachment 2104361
View attachment 2104363
Je, madai hayo ni kweli? Tafakari!


Msingi wa kanisa la SDA au ‘Wasabato’ kama inavyojulikana kwa wengi,kuabudu siku ya jumamosi, ni kile kilichoandikwa na Mungu wakati wa uumbaji, kwamba aliumba kwa siku 6 na siku ya 7 akastarehe, akaibariki na akapumzika kisha akawaambia waisraeli: “Ikumbuke siku ya Sabatou itakase….” Kutoka 20:8.


Kutokana na kazi ya chama cha Priory de Sion kwa kuingiza mafundisho machafu ndani ya imani safi, kulitokea utitiri wa makanisa mengi ambayo yanadai kupinga uchafu huo. Hata hivyo wengi wa waumini wa madhehebu hayo ama hawajui asili ya dhehebu lao au hawajui asili ya kile wanachokiabudu. Wengi wamefundishwa na waalimu wa dini na kuwaamini bila hata ya kutaka kuhakikisha kwa akili zao kile wanachofundhishwa. Mungu ametoa nafasi ya kufahamu ukweli kwa kila mmoja wetu bila ya kutegemea viongozi wa dini. Umewahi kufikiri kwamba kama ungekuwa unaishi duniani wewe peke yako, ungemtegemea nani? Tafakari!
Napenda sana kunena kwa lugha, na ninampenda sana ROHO MTAKATIFU.
 
Back
Top Bottom